Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi - 27/09/2021

Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi - 27/09/2021

Si tu hlo , limeibuka lingine kuwa shahidi adamoo alikubali na kusaini kuwa aliachishwa kazi kwa utovu wa nidhamu, na kwa mujibu wa maelekezo yake aliachishwa kwa sababu ya battle confusion na si utovu wa nidhamu!
Kwa maelezo yake mashitaka yote ya awali aliyakana - alisanishwa na Kingai bila kujua nini kilichomo ndani baada ya mateso makali ya kufungwa ka mshikaki .
 
Jaji: Wakili wa Serikali

Wakili Kidando: anatambulisha Jopo lake
1. Robert Kidando​
2. Nassoro Katuga​
3. Ignas Mwanuka​
4. Esther Martin​
5. Tulumanywa Majigo​

Wakili Kibatala: anatambulisha Jopo lake
Adv Peter Kibatala​
Adv Sisty Aloyce​
Adv Gaston Garubindi​
Adv Idd Msawanga​
Adv Alex Massaba​
Adv Evaresta Kisanga​
Adv Hadija Aron​
Adv Michael Mwangasa​
Adv Faraji Mangula​
Adv Fredrick Kiwhelo​
Adv Nashon Nkungu​
Adv Jonathan Mndeme​
Adv John Mallya​
Kibatala: Kwa Mshitakiwa wa Kwanza Nashon Nkungu Mshitakiwa wa Pili John malya Mshitakiwa wa tatu Fredrick Kiwhelo Wengine wote ni Kwa mshitakiwa wa Nne

Jaji: Siku ya Ijumaa shahidi( Mshtakiwa wa pili) alikuwa hajakamilisha Utetezi wake

Jaji: arejee kwenye Kizimba tuweze Kuendelea

Shahidianaenda

Jaji: Wakili wa Serikali mpo tayari..?

Jaji: Upande wa Utetezi Mmpo tayari

Wote: wapo tayari

Jaji: Shahidi bado upo chini ya Kiapo kama tulivyokuapisha Siku ya Ijumaa Unaweza kuchagua Kukaa au Kusimama..... Mawakili wa Serikali watakuhoji Maswali na Baadae Upande wa Utetezi hususani Wakili waKo anaweza Kuja Kukuongoza tena Kwa Kukuuliza Maswali.

Shahidi: Nitakaa Mheshimiwa Jaji, nakaa Chini Mahakama Kimya Kidogo, Jaji anaandika

Jaji: bila shaka Wakili wa Serikali Chavula unaendelea

Wakili wa Serikali: Naam Mheshimiwa

Jaji: tafadhali endelea

Wakili wa Serikali: Awali siku ya Ijumaa kabla hatujahairisha nilikuuuliza kuhusiana na wale waliokuvamia maeneo ya Rau hawakupata kujitambulisha,Kweli au Si Kweli

Shahidi: Kweli

WS: wale watu Mlivyotoka pale kwenda Kituo cha Polisi hawakukueleza Majina yao akina nani.? kweli au Si Kweli

Shahidi: Kweli

WS: walivyokutoa Moshi kukuleta Dar es salaam hawakukueleza wao Majina yao ni Akina nani

Shahidi: niliwafahamu kwa wao alipokuwa wanaitana Majina yao na Nikaja kuthibitisha Majina yao hapa Mahakamani walipo Jitambulisha

WS: Wakati wa Kukusafirisha Moshi Kuja Dar es salaam Watu wale walikufunga Kitambaa Usoni

Shahidi: ni Sahihi

WS: ni Jacket,Si Ndiyo

Shahidi: ni Jacket ndiyo

WS: Hukujua ni akina nani unasafiri nao

Shahidi: Kweli

WS: na hata Ulipofika Dar es salaam ukafikishwa Kituo cha Kwanza cha Polisi hukujua upo wapi

Shahidi: kama nilivyoeleza

WS: We Jibu swali langu Kweli au si Kweli

Shahidi: Kweli

WS: Umedai ulipokuwa unasafirishwa Ulikalishwa Chini kwenye gari,Kweli au si kweli

Shahidi: ni kweli

WS: Uliweza Kujua ni sehemu gani ya gari ..?

Shahidi: nilipotoa Upande wa Kulia Kwa Uelewa wangu siyo Kwa Kuona, Nikafahamu nimekaa nyuma ya gari

WS: Ulikaa nyuma ya gari

Shahidi: ndani ya gari,Sehemu ya Nyuma

WS: Bila shaka ilikuwa ni haya Magari Madogo

Shahidi: Siwezi Kujua ni gati gani

WS: unakubaliana na Mimi ukiwa Umefungwa Machoni uwezi Kuona .?

Shahidi: Ndiyo uwezi Kuona,ila ukiwa unatendewa unahisi

WS: ukiwa umefungwa Macho uwezi Kuona hata Kile kifaa wanachokusababishia Maumivu

Shahidi: kweli

WS: nakurudisha Moshi,umesema walipokuwa wanakutesa Moshi walikuwa wabakuuliza Umekuja Moshi Kufanya nini

Shahidi: ni sahihi

WS: Wewe Ukajibu umekuja Moshi Kufanya VIP protection ni Sahihi

Shahidi: ni sahihi

WS: Ulisema ulipofika Dar es salaam kituo cha kwanza cha Polisi walikupa Chakula .?

Shahidi: ni sahihi

WS: Ni Chakula gani

Shahidi: Ugali na Mboga za Majani

WS: na wakati wote ulipokuwa pale hukufanyiwa Mateso

Shahidi: Sahihi

WS: na hata ulipokuwa Mbweni hakuna aliyekuja Kukupiga..?

Shahidi: ni sahihi

WS: Alipokuja Ramadhani Kingai alipokutaka Uthibitishe Maelezo yako na Kutia Sahihi alikupa Vitisho wala hakukupiga.?

Shahidi: ni sahihi

WS: ni Lipi Mahakama ichukue kati ya haya Mawili, Ulieleza Mahakama kwamba Wakati unatoa Maelezo hapa Mahakamani, kwamba ulitoa Maelezo kwa sababu ulikuwa unateswa, Sasa unasema kwamba Kingai na wenzake hawakukupatia Mateso isipokuwa Walipa Vitisho tuh

Shahidi: Rudia swali lako

WS: Wakati wa Kesi Kubwa Umesema Kuwa Kingai wenzake walichukua Maelezo yangu baada ya Mateso,Leo unasema Alikuja Bwana Kingai kunitishia

Shahidi: umeuliza wakati wa Kuchukuliwa Maelezo, Mimi wakati wote nilikuwa Chini ya Mateso

Mallya: OBJECTION Naomba Shahidi akiwa anatoa Maelezo yake apewe nafasi ya Kumaliza Kujibu Maswali

WS: Ulipokuwa Dar es salaam hukuteswa isipokuwa Bwana Kingai alikutishia.?

Shahidi: Wakili anauliza na Kunilisha maneno ambayo mimi Mwanzo sikujibu hivyo.... Aliniuliza kuhusu Kupigwa siyo Kuhusu mateso,kwa sababu, Mimi nilikuwa Chini yao na Nimefungwa pingu, Bado hayo kwangu ni Mateso

Jaji: Shahidi nafikiri ungejibu sasa hilo unalotaka wala hakuna tatizo kwamba uliteswa au lah

Jaji: naweza kukusomea

Shahidi: ningependa unisomee Mheshimiwa Jaji

Jaji: Kingai "Hakunipiga tulipokuwa Mbweni,alinipiga na Kunitishia" Sasa tuambie nini kilichokuwa kimetokea

WS: sasa nafikiri umeelewa, Kwamba Ulitoa Maelezo Yako baada ya Kuteswa na Sasa unasema baada ya kuteswa

Shahidi: miye ananihoji Machaguo ambayo mimi sikuyasema

Jaji: nafikiri Wakili sasa unaweza Kubadirisha swali

Jaji: Mallya tusaidie hapo tafsiri yake ni nini

Mallya: Kupiga ni Kitu Kidogo katika Jambo Kubwa Mateso,Unaweza Usipigwe na Ukawa upo wenye Mateso

Jaji: Mawakili wa pande zote Mbili nisaidieni hapo

WS: Mahakama ichukue kwamba Dar es salaam Hakupigwa

Kibatala: Siyo kwa Nia mbaya lakini wakili Mwenzangu Kakosa mbinu na ulewa

Jaji: Sitaki Muingie Kwenye Malumbano

Jaji: nitamuhoji Shahidi Mwenyewe, Je ungependa tuandike Kuwa Dar es salaam hukupigwa.?

Shahidi: ndiyo Dar es salaam Sikupigwa

WS: shahidi kwahiyo tuchukue kuwa Maelezo ulichukuliwa baada ya Mateso, Chini ya Kingai na Leo unatuambia ulitishwa..?

Shahidi: sijaelewa Swali

Jaji: Maelezo yanayobishaniwa,Maelezo yalichukuliwa Nje ya Muda,Je ulitoa hayo Maelezo lakini kwa mateso.?

Jaji: Picha ninayopata leo hukutoa Maelezo ila ulisaini tuh

Shahidi: sahihi ninazungumzia kuwa niliteswa na Kuning'inizwa kama Popo au Mshikaki

WS: Shahidi ulieza Mahakama Bw Kingai Alikutesa na Kutokana na Mateso hayo ulilazimika Kutoa Maelezo, Sasa unasema Bw Kingai sikutia Maelezo kwake alikuja na karatasi yake akanitaka nisaini na kujaza sehemu ya Kuthibitisha,Kipi unachoeleza sahihi.

Shahidi: Vyote ichukue

WS: Kwa hiyo Mahakama ichukue Vyote

Jaji: sasa niandike Vipi Hukutoa Maelezo na Ulitoa Maelezo .?

Shahidi: Ananiuliza Mambo Mawili tofauti ambayo ajayatenganisha, Mimi nilitoa Maelezo Moshi Chini ya Mateso,nalisaini bila Mateso

Jaji: Nilisaini Maelezo bila Mateso lakini nisaini baada ya Vitisho

WS: ni sahihi Mheshimiwa Jaji

Mahakama Kichekooooooo


WS: Kabla ya Kuletwa Dar es salaam tarehe 07,Kabla ya siku hiyo uliwahi Kufika Dar es salaam.?

Shahidi: ndiyo

WS: Makazi yako yapo Dar es salaam.?

Shahidi: Hapana

WS: unafahamu wapi

Shahidi: Kambi ya Jeshi Twalipo na Maeneo ya Uwanja wa Taifa

WS: Ujawahi Kufika Tazara.?

Shahidi: ndiyo

WS: Ulishawahi Kufika Mbweni

Shahidi: Hapana

Jaji: kwa hiyo Kabla ya kesi hujawahi kufika Tazara wala Mbweni

Shahidi: Ndiyo

WWSS: Hakuna Wakati ,unafikishwa Kituo cha Polisi wakakuacha wazi.?

Shahidi: sijawahi Kutolewa nje ya kituo cha Polisi

Jaji: Mnaeleeana kweli..? Kutoka Tazara kwenda Mbweni ulifungwa Jacket.?

Shahidi: nilifungwa Jacket Usoni Mheshimiwa

Jaji: wakili ulimaanisha hivyo.?

WS: Ndiyo Mheshimiwa

Jaji: sasa nitaomba Mnapomtajia Vituo vya Polisi Mtaje na Majina


WS: Naanza Upya Ulitolewa kitambaa ama Jacket lako ulipofilishwa ndani ya Kituo cha Tazara

Shahidi: Ndiyo

WS: Wakili wa Serikali Mpaka Unaingia Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa umefungwa Usoni

Shahidi: Ndiyo

WS: Moshi Mlikamatwa wangapi

Shahidi: tulikamatwa wawili

WS: na nani.?

Shahidi: na Mohammed Abdilah Ling'wenya

WS: wakati wote unasafirishwa hukujua yupo wapi

Shahidi: Ndiyo

WS: Kingai na Mwenzake Mahita,walieleza Mahakama kwamba waliwasafirisha wewe na Ling'wenya Kwenye gari moja

Shahidi: kweli walitoa Ushahidi huo

WS: Hakuna Mtu aliyewaambia Mashahidi wale kuwa Si kweli Nyie hamkusafirishwa pamoja.?

Shahidi: sasaaaaa

WS: Jibu swali langu

Jaji: Je ulisikia au Hukusikia.?

Shahidi: Sikusikia

WS: Kama wakati wote unasafirishwa Mpaka unafikishwa Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa hufahamu Mohammed Abdilah Ling'wenya yupo wapi,Kweli au si Kweli

Shahidi: Sahihi

WS: Ulikuwa peke yako Kwenye mahabusu

Shahidi: nilikuwa peke yangu kwenye Chumba Changu,ila Mahabusu wengine walikuwa Kwenye Vyumba vyao

Jaji: kwa hiyo ulikuwa Mwenyewe Kwenye Chumba cha Mahabusu..?

Shahidi: Ndiyo

Jaji: hapakuwa na Mahabusu wengine..?

Shahidi: Walikwepo kwenye Vyumba vyao

Jaji: hapa naona tusingeelewana

Mallya: Shahidi alitupa Picha Kuwa kuna mahabusu Yenye Vyumba Vidogo Vidogo na yeye alikuwa kwenye kichumba Chake ndani ya mahabusu

Jaji: naomba Kusoma "Nilifunguliwa Jacket nikawa naona Sasa,nikajivuta hadi Mlangoni nikaanza kuona Mahabusu wengine wakiwa kwenye Vyumba Vyao" nafikiri ndicho nilicho andika

Jaji: sasa tujielekeze Hapo

WS: Umesema ulikuwa Peke yako Kwenye Chumba

Shahidi: Ndiyo

WS: Kushoto na Kulia palikuwa na Ukuta

Shahidi: ni sahihi Kabisa

WS: Ulikuwa kwenye tafakari kwanini haya yananiyokea,nimekosa nini.?

Shahidi: ni Ukweli

WS: Ulikuwa unaugulia Maumivu huku ukitafakari,Kweli au si kweli

Shahidi: Kweli

WS: Nikujeresha Moshi,Unasema walikuning'iniza Kama Mishikaki Kwenye Bomba

Shahidi: Kweli

WS: Ulikuwa unaeleaelea ukiwa Juu

Shahidi: Kweli

WS: Walikuwa wanakupiga Maeneo gani ya Mwili wako

Shahidi: Kwenye Magoti na Kwenye Unyayo

WS: Mara ngapi.?

Shahidi: Mara nyingi

WS: alikuwa anatumia Nguvu kubwa sana

Shahidi: kweli

WS: Walikuwa wanakupiga kwa Kutumia nini.?

Shahidi: Rungu la Chuma

WS: walikuvunjavunja magoti.?

Shahidi: hapana

WS: Eeenhee wewe si Komandooo Bwana awawezi Kukuvunja,Umefuzu sana Bwana

Jaji:Naomba Mawakili kama kuna lolote msinong'one tufuate utamaduni wetu Jaji nafikiri Wakili wa Serikali Umeelewa swala la wakili Mwenzako

WS: ni swali tuh Mheshimiwa Jaji

Jaji: ulikuwa uulizi Swali ulikuwa unaweka Maoni yako

WS: sawa Mheshimiwa Jaji

WS: Kutokuvunjika kwako ni kwa sababu umefuzu Mafunzo ya Ukomando

Shahidi: Sahihi

WS: kutokana na Ukomandoo wako na Kufuzu kwako hukuona haja ya kwenda Hospitali

Shahidi: siyo sahihi

WS: Umeeleza walikuwa wanakupiga kwa kutumia nini

Shahidi: nishaeleza ni Rungu la Chuma

WS: alikupiga mara ngapi

Shahidi: Sikumbuki

WS: Zaidi ya amara 10

Shahidi: Ndiyo

WS: Walikutesa kwa muda gani

Shahidi: sikumbuki,maana walikuwa wananipiga na Kuniacha wakipumzika wanarudi tena

WS: nyayo zilivunjika.?

Shahidi: Hapana

WS: Baada ya Kukupofa kwenye Nyayo ulimba

Shahidi: Ndiyo

WS: ulipatwa na lengelenge

Shahidi: lengelenge na Kuvilia ni Kitu gani

WS: yote ni hayohayo, Ulipofika Tazara uliweza kutembea..?

Shahidi: Kwa tabu sana

WS: anawafuata wenzie wananong'ona

WS: ulieleza Mahakama kuna Ugonjwa uliupata Ulipokuwa Jeshini,ni Ugonjwa gani

Shahidi: Battle Confusion

WS: Ulisema ulitibiwa Lugalo ukapata nafuu

Shahidi: kiasi chake

WS: Walikupa Dawa za Kuwa unameza

Shahidi: nilikuwa napewa nilipokuwa pale

WS: uliporuhusiwa ulirudi Moja kwa moja kwenye kituo chako cha Kazi

Shahidi: ni sahihi

WS: Ulirudi kwa Muda gani

Shahidi: Kwa amuda wa Miezi Miwili

Jaji: Miezi miwili ya nini​
 
Kiongozi wetu,mbona updates hakuna nini kimetokea huku?
updates mbona zipo ! JF haijawahi kushindwa

IMG_20210927_120930.jpg
IMG_20210927_120921.jpg
IMG_20210927_115922.jpg
 
Si tu hlo , limeibuka lingine kuwa shahidi adamoo alikubali na kusaini kuwa aliachishwa kazi kwa utovu wa nidhamu, na kwa mujibu wa maelekezo yake aliachishwa kwa sababu ya battle confusion na si utovu wa nidhamu!
Hapo ndio wamejichanganya,sababu Mahakama inaweza kuomba taarifa kutoka Jeshini.
 
Sidhani,ndio maana nasema jeshi watatoa taarifa ya ukweli.
1. Kwanini iwe Jeshi? Kwani aliyekuwa mwajiri wa Adamoo (JWTZ) ambayo ni taasisi ya umma yenye taratibu za kisheria za ku - HIRE, FIRE and SUSPEND ingewezaje kumsimamisha au kumfukuza kazi mwajiriwa/askari wake bila kumtaarifu kwa maandishi na sababu za kufukuzwa kwake..?

2. That means, lazima lazima Adamoo ana barua ya kuachichwa kwake kazi ya uaskari jeshini. Kwa hiyo haihitajiki hata kuomba taarifa kwa CDF kwa sbb evidence kwamba Adamoo aliachichwa kazi kwa sababu yoyote anayo yeye anayejitetea...

Kama JWTZ lilimwachisha kazi Adamoo kwa sababu yoyote ile bila ya kumwandikia suspension/dismissal letter inayoeleza sababu ya kuachichishwa kwake kazi ya uaskari, basi hilo ni tatizo jingine kabisa na tena ni kubwa linaloweza kuathiri kesi yote hii na kuipa sura nyingine kabisa...!!!
 
Leo tena kama kawaida tunakuletea moja kwa moja yanayojiri kwenye Mahakama kuu , divisheni ya Uhujumu Uchumi , ambako kesi ya ugaidi unaogharimu kitita cha tsh laki 6 inaendelea.

---
Jaji ameshaingia

Kesi inatajwa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire, Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe

Jaji: Wakili wa Serikali

Wakili Kidando anatambulisha Jopo lake....
  1. Robert Kidando
  2. Nassoro Katuga
  3. Ignas Mwanuka
  4. Esther Martin
  5. Tulumanywa Majigo

Wakili Kibatala anatambulisha Jopo lake
  1. Adv Peter Kibatala
  2. Adv Sisty Aloyce
  3. Adv Gaston Garubindi
  4. Adv Idd Msawanga
  5. Adv Alex Massaba
  6. Adv Evaresta Kisanga
  7. Adv Hadija Aron
  8. Adv Michael Mwangasa
  9. Adv Faraji Mangula
  10. Adv Fredrick Kiwhelo
  11. Adv Nashon Nkungu
  12. Adv Jonathan Mndeme
  13. Adv John Mallya
Kwa Mshtakiwa wa Kwanza - Nashon Nkungu
Mshitakiwa wa Pili - John Mallya
Mshitakiwa wa tatu - Fredrick Kiwhelo
Mawakili Wengine wote ni Kwa mshitakiwa wa Nne Freeman Mbowe

Jaji: Siku ya Ijumaa shahidi( Mshtakiwa wa pili) alikuwa hajakamilisha Utetezi wake. Arejee kwenye Kizimba tuweze Kuendelea

Shahidi anaenda

Jaji: Wakili wa Serikali mpo tayari..?

Jaji: Upande wa Utetezi mpo tayari?

Wote wapo tayari

Jaji: Shahidi bado upo chini ya Kiapo kama tulivyokuapisha Siku ya Ijumaa. Mawakili wa Serikali watakuhoji Maswali na Baadae Upande wa Utetezi hususani Wakili wako anaweza kuja kukuongoza tena Kwa Kukuuliza Maswali. Unaweza kuchagua Kukaa au Kusimama

Shahidi: Nitakaa Mheshimiwa Jaji

Jaji: Bila shaka. Wakili wa Serikali Chavula unaendelea. Tafadhali endelea

Wakili wa Serikali: Naam Mheshimiwa

Wakili wa Serikali: Awali siku ya Ijumaa kabla hatujaahirisha, nilikuuuliza kuhusiana na wale waliokuvamia maeneo ya Rau hawakupata kujitambulisha, Kweli au Si Kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Wale watu Mlivyotoka pale kwenda Kituo cha Polisi hawakulueleza Majina yao akina nani.? Kweli au Si Kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Walivyokutoa Moshi kukuleta Dar es salaam hawakukueleza wao Majina yao ni Akina nani. Walipokupeleka Mbweni hawakukueleza Majina yao akina nani?

Shahidi: Kweli hawakunieleza

Wakili wa Serikali: Haukupata Kuwafahamu amajina yao wakati wote?

Shahidi: Niliwafahamu kwa wao alipokuwa wanaitana Majina yao na Nikaja kuthibitisha Majina yao hapa Mahakamani walipojitambulisha

Wakili wa Serikali: Wakati wa Kukusafirisha Moshi Kuja Dar es salaam Watu wale walikufunga Kitambaa Usoni?

Shahidi: ni Sahihi

Wakili wa Serikali: ni Jacket, Si Ndiyo?

Shahidi: ni Jacket ndiyo

Wakili wa Serikali: Hukujua ni akina nani unasafiri nao

Shahidi: Kweli kama nilivyoeleza

Wakili wa Serikali: Na hata Ulipofika Dar es salaam ukafikishwa Kituo cha Kwanza cha Polisi hukujua upo wapi

Wakili wa Serikali: We Jibu swali langu Kweli au si Kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Umedai ulipokuwa unasafirishwa Ulikalishwa Chini kwenye gari,Kweli au si kweli

Shahidi: Ni kweli

Wakili wa Serikali: Uliweza Kujua ni sehemu gani ya gari ..?

Shahidi: Nilipita Upande wa Kulia Kwa Uelewa wangu siyo Kwa Kuona, Nikafahamu nimekaa nyuma ya gari

Wakili wa Serikali: Ulikaa nyuma ya gari

Shahidi: Ndani ya gari,Sehemu ya Nyuma

Shahidi: Siwezi Kujua ni gari gani

Wakili wa Serikali: Unakubaliana na Mimi ukiwa Umefungwa Machoni uwezi Kuona .?

Shahidi: Ndiyo uwezi Kuona, ila ukiwa unatendewa unahisi

Wakili wa Serikali: Ukiwa umefungwa macho uwezi kuona hata kile kifaa wanachokusababishia Maumivu

Shahidi: Ni sahihi

Wakili wa Serikali: Nakurudisha Moshi,umesema walipokuwa wanakutesa Moshi walikuwa wabakuuliza Umekuja Moshi Kufanya nini

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: Wewe Ukajibu umekuja Moshi Kufanya VIP protection ni Sahihi

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: Ulisema ulipofika Dar es salaam kituo cha kwanza cha Polisi walikupa Chakula .?

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: Ni Chakula gani

Shahidi: Ugali na Mboga za Majani

Wakili wa Serikali: na wakati wote ulipokuwa pale hukufanyiwa Mateso

Shahidi: Sahihi

Wakili wa Serikali: na hata ulipokuwa Mbweni hakuna aliyekuja Kukupiga..?

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: Alipokuja Ramadhani Kingai alipolutaka Uthibitishe Marlezo yako na Kutia Sahihi alikupa Vitisho wala hakukupiga.?

Shahidi: ni sahihi

Wakili wa Serikali: Ni Lipi Mahakama ichukue kati ya haya Mawili,Ulielezq Mahakama kwamba Wakati unatoa Maelezo hapa Mahakamani,kwamba ulitoa Maelezo kwa sababu ulikuwa unateswa,Sasa unasema kwamba Kingai na wenzake hawakukupatia Mateso isipokuwa Walipa Vitisho tuh

Shahidi: Rudia swali lako

Wakili wa Serikali: Wakati wa Kesi Kubwa Umesema Kuwa Kingai wenzake walichukua Maelezo yangu baada ya Mateso,Leo unasema Alikuja Bwana Kingai kunitishia

Shahidi: Umeuliza wakati wa Kuchukuliwa Maelezo, Mimi wakati wote nilikuwa Chini ya Mateso

Wakili wa Serikali: Aahaaaaaa

Wakili Mallya: OBJECTION. Naomba Shahidi akiwa anatoa Maelezo yake apewe nafasi ya Kumaliza Kujibu Maswali

Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Dar es Salaam hukuteswa isipokuwa Bwana Kingai alikutishia.?

Shahidi: Aliniuliza kuhusu Kupigwa siyo Kuhusu mateso,kwa sababu, Mimi nilikuwa Chini yao na Nimefungwa pingu, bado hayo kwangu ni Mateso

Jaji: Shahidi nafikiri ungejibu sasa hilo unalotaka wala hakuna tatizo kwamba uliteswa au lah

Jaji: Naweza kukusomea

Shahidi: Ningependa unisomee Mheshimiwa Jaji

Jaji: Kingai "Hakunipiga tulipokuwa Mbweni, alinipiga na Kunitishia" Sasa tuambie nini kilichokuwa kimetokea

Shahidi: Vyote vichukue

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Mahakama ichukue Vyote

Jaji: Sasa niandike vipi Hukutoa Maelezo na Ulitoa Maelezo ..?

Shahidi: Ananiuliza Mambo Mawili tofauti ambayo ajayatenganisha, Mimi nilitoa Maelezo Moshi Chini ya Mateso,nalisaini bila Mateso

Jaji: Nilisaini Maelezo bila Mateso lakini nisaini baada ya Vitisho

Shahidi: ni sahihi Mheshimiwa Jaji

Mahakama Kichekooooooo

Wakili wa Serikali:
Kabla ya Kuletwa Dar es salaam tarehe 07,Kabla ya siku hiyo uliwahi Kufika Dar es salaam.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Makazi yako yapo Dar es salaam.?

Shahidi: Hapana

Wakili wa Serikali: unafahamu wapi?

Shahidi: Kambi ya Jeshi Twalipo na Maeneo ya Uwanja wa Taifa

Wakili wa Serikali: Ujawahi Kufika Tazara.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Ulishawahi Kufika Mbweni

Shahidi: Hapana

Jaji: Kwa hiyo Kabla ya kesi ujawahi kufika Tazara wala Mbweni

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Hakuna Wakati ,unafikishwa Kituo cha Polisi wakakuacha wazi.?

Shahidi sijwahi Kutolewa nje ya kituo cha Polisi

Jaji Mnaeleeana kweli..?

Jaji Kutoka Tazara kwenda Mbweni ulifungwa Jacket.?

Shahidi nilifungwa Jacket Usoni Mheshimiwa

wakili ulimaanisha hivyo.?

Wakili wa Serikali Ndiyo Mheshimiwa

Jaji sasa nitaomba Mnapomtajia Vituo vya Polisi Mtaje na Majina

Wakili wa Serikali Naanza Upya Ulitolewa akitambaa ama Jacket lako ulipofilishwa ndani ya Kituo cha Tazara

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali Mpaka Unaingia Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa umefungwa Usoni

Wakili wa Serikali Moshi Mlikamatwa wangapi

Shahidi tulikamatwa wawili

Wakili wa Serikali na nani.?

Shahidi na Mohammed Abdilah Ling'wenya

Wakili wa Serikali wakati wote unasafirishwa hukujua yupo wapi

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali Kingai na Mwenzake Mahita,walieleza Mahakama kwamba waliwasafirisha wewe na Ling'wenya Kwenye gari moja

Shahidi kweli walitoa Ushahidi huo

Wakili wa Serikali Hakuna Mtu aliyewaambia Mashahidi wale kuwa Si kweli Nyie hamkusafirishwa pamoja.?

Shahidi sasaaaaa

Wakili wa Serikali Jibu swali langu

Jaji Je ulisikia au Hukusikia.?

Shahidi Sikusikia

Wakili wa Serikali Kama wakatibwote unasafirishwa Mpaka unafikishwa Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa hufahamu Mohammed Abdilah Ling'wenya yupo wapi,Kweli au si Kweli

Shahidi Sahihi

Wakili wa Serikali Ulikuwa peke yako Kwenye mahabusu

Shahidi nilikuwa peke yangu kwenye Chumba Changu,ila Mahabusu wengine walikuwa Kwenye Vyumba vyao

Jaji kwa hiyo ulikuwa Mwenyewe Kwenye Chumba cha Mahabusu..?

Shahidi Ndiyo

Jaji hapakuwa na Mahabusu wengine..?

Walikwepo kwenye Vyumba vyao

Jaji hapa naona tusingeelewana

Mallya Shahidi alitupa Picha Kuwa kuna mahabusu Yenye Vyumba Vidogo Vidogo na yeye alikuwa kwenye kichumba Chake ndani ya mahabusu

Jaji naomba Kusoma "Nilifunguliwa Jacket nikawa naona Sasa,nikajivutq hadi Mlangoni nikaanza akuona Mahabusu wengime wakiwa kwenye Vyumba Vyao" nafikiri ndicho nilicho andika

Jaji sasa tujielekeze Hapo

Wakili wa Serikali Umesema ulikuwa Peke yako Kwenye Chumba

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali Kushoto na Kulia palikuwa na Ukuta

Shahidi ni sahihi Kabisa

Wakili wa Serikali Ulikuwa kwenye tafakari kwanini haya yananiyokea,nimekosa nini.?

washitakiwa 1,2,na 3 walikubali wanafahamianina wa wakiwa wanafanya kazi Ngerengere KJ92

Wahitakiwa 1,2, na 3 Walikuwa wanafahamiana kabla ya Kesi Kuanza

Wakili wa Serikali Hukubisha kwamba kwamba hukuondolewa Jeshini kwa Maswala ya Kinidhamu, na asasa unasema Uliondolewa Jeshini kwa Maswala ya Afya

Shahidi Siwezi kulijibia

wakili wa Serikali Kwanini uwezi Kulijibia

Shahidi Documents zote sijawahi kuzitolea Maelezo, zilikuja na kuletwa na watu walioandaa

Wakili wa Serikali Documents zipi hizi

Shahidi zilioletwa Kufungulia Kesi ya Ugaidi

Wakili wa Serikali Ulisaini hukusoma.?

Shahidi nilisaini

Wakili wa Serikali Na Mahakama ilikusomea.?

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali Unasema Ulikuwa kwenye Misheni Congo

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali Ulikuwa Battalion ya 3

Wakili wa Serikali wewe ulikuwa kikosi cha Mizinga

Shahidi Hapana

Wakili wa Serikali Wewe ulikuwa unafanya nini

Shahidi nilikuwa Special Force

Wakili wa Serikali Huko Special Force ulikuwa unafanya kazi gani

Shahidi Kazi zote

Wakili wa Serikali Zitaje

Shahidi zote kuanzia kupika Mpaka Kwenda Vitani

Wakili wa Serikali Huko Vitani huwa mnajihusisha na Kuteka Watu

Shahidi siyo kazi Yangu kuzungumzia Maswala ya Vita

Wakili wa Serikali lakini Vitani huwa watu wanatekwa

Shahidi Ukingalia kwenye Muvi wanatekwa ila Mimi ya Vitani siwezi kuyaeleza,Kuna watu wake Maalum wa Kuyaeleza

Wakili wa Serikali Moja ya kazi ni Kulinda Lindo,mnalinda dhidi ya nani

Shahidi dhidi ya Adui

Wakili wa Serikali unapoluwa umemkamata Mtu lindo Moja ya jambo ni Kumfunga pingu ili asitoroke

Shahidi Kweli

Wakili wa Serikali kweli kwa sababu Mmeyafanya huko Vitani

Wakili wa Serikali anaongea na Jopo lao

Wakili wa Serikali Wewe huwa unatesa watu.?

Shahidi Sijawahi

Wakili wa Serikali Ukiwa umekamata Adui ukamfunga Pingu utakuwa umemtesa

Shahidi Utakuwa hujamtesa,Ndiyo maana umemuita Adui

Wakili wa Serikali Naomba kuwaachia wenzangu

Jaji nawakumbusha tuna Fakika 20 Kabla hatuja break

Wakili wa Serikali 2 Mheshimiwa mimi ninayo Machache kati ya mengi yaliyoulizwa na Mwenzangu

Jaji labda nimuulize Shahidi Mwenyewe,Unanguvu au tunaweza kuendelea na Maswali

Shahidi Tuendelee Mheshimiwa Jaji

Wakili wa Serikali 02 Wakati umeanza kuulizwa na Wakili wa Serikali umeongea Ukweli,Tunaomba uendelee kusema Ukwei

Wakili wa Serikali 02 wakati unakamatwa Ling'wenya ,je yeye alikuwa umbali gani

Shahidi alikuwa karibu yangu,Sababu nilikuwa Pembeni naongea na Simu

Wakili wa Serikali 02 Umesema Ling'wenya alishuhudia wakati Unawekewa Madawa ya Kulevya

Shahidi siyo yeye tuh watu wote waliona kwa Sababu Jambo hilo lilifanyika hadharani mbele za watu

Wakili wa Serikali 02 kati yako wewe na Ling'wenya nani Mtaalamu wa Madawa ya Kulevya

Shahidi hakuna,Swala la Madawa walisema wao Wenyewe kuwa "Tumemkuta na Madawa ya kulevya"

Wakili wa Serikali 2 Kwenye ushahidi wako wako ulisema kuwa kuhusiana na Swala la kusaini hati yakukabidhi vitu vyako

Shahidi Siku sema

wakili wa Serikali 02 ulimuonyesha jaji Kuhusu makovu, Je unamakovu Mangapi

Shahidi Mengine yapo kichwani

Wakili wa Serikali 02 Uliiambia Mahakama kuwa makovu haya amengine yatofautishwale na Miguuni

Shahidi Mahakama haikuuliza,Kuwa hayo Mengine yametokana na nini

Wakili wa Serikali 02 amahakama itatofautishaje sasa

Shahidi hiyo ni kazi ya Mahakama siwezi kuifundisha

Wakili wa Serikali 02 Ulipokuwa Mbweni Kuna Askari alikwambai Upo Mbweni Baada ya Kuwaonea Huruma

Shahidi Ndiyo

wakili wa Serikali 02 huyo wa Pili aliyekuwa anasema huyo Askari ni nani.?

Shahidi Mohammed Abdilah Ling'wenya

Wakili wa Serikali 02 kumbe mlikuwa naye na Mkaonana Mbweni

Shahidi Kujua tupo naye nilijua nimesema,Sikuwahi Kumuona kwa macho

Wakili wa Serikali 02 Umeiambia Mahakama aliyekupiga Rungu Moshi ni nani

Shahidi Sikuwa namfahamu

Wakili wa Serikali 02 Maelezo aliyokuletea Bwana Kingai ukayasaini na Kuyathibitisha,Ukiyqona utayakumbuka.?

Shahidi Siwezi Kuyakumbuka,Kwa sababu sikuyasoma,Labda sehemu za sahihi yangu na nilipoandika

Wakili wa Serikali 02 awakati unateswa Moshi uliwajibu Kuwa umeenda kwa VIP PROTECTION ,ukawajibu upo kwenye mazungumzo

Shahidi ni Kweli

Wakili wa Serikali 02 Wakati Wakili Kibatala anakuuliza wakati wa Maelezo ulisema Ungeweza Kumuita Mwajiri wako

Shahidi Muajiri Mtarajiwa

Wakili wa Serikali 02 Kwa hiyo Mahakama iandike ujawahi na kuajiriwa na Mshitakiwa wa nne

Shahidi ni sahihi

Wakili wa Serikali 02 Kwahiyo nisahihi nikosema katika hayo Mazungumzo yenu mliwawahi Kufanyia Aishi Hotel

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali 02 Wakati mnafanya hayo Mazungumzo mlikuwa na Mshitakiwa wa 3.?

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali 02 Wakati Upo Tazara unasema uligudua kwa Vitu Viwili Kwa Honi ya Treni na Kuambiwa hiki ni kituo cha Kuhifadhia Watuhumiwa wa Ugaidi

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali 02 Ulishaiambia Mahakama Kwamba Unatuhumiwa kwa Ugaidi.?

Shahidi Hapana

Jaji Subiri Kidogo

Wakili wa Serikali 02 Ninaswali moja la Mwisho

Jaji sawa endelea

Wakili wa Serikali 02 wakati unachomwa na Bisibisi ushawahi kuiambia Mahakama walikuwa wanataka nini,kama vile Moshi walikuwa wanakuuliza Umefuata nini..?

Shahidi Hapana

Jaki sawa tunapumzika kwa Muda tutarejea Baada ya Dakika 20

Jaji ananyanyuka

Mahakama imerejea

Jaji Meingia Leo Mapema sana akuliko watu wengi na Watuhumiwa

Imebidi Jaji asubiri watuhumiwa waletwe

Kesi imetajwaa

Jaji nataka kuanza Utamaduni wa Kuanza Kuzingatia amuda

Nikisema naanza Saa 3 Mtanikuta humu

Nikisema tunaanza saa 3 itakuwa Saa 3 Kamili

Na Nikisema Saa 4 itakuwa Saa 4 Kamili

Itapendeza kama Tutazingatia Muda

Na huo ndiyo Ustaarabu,Ikitokea Mtu anadharula nijulishwe

Haipendezi kesi Ikianza milango inafunguliwa kila Saa

Jaji Upande wa Jamuhuri wapo tayari Kuendele.?

Utetezi.?

Shahidi.?

Wote wapo Tayari

Wakili wa Serikali 03 Wakati tukiendelea na hii Kesi tangu Mwanzoni na kingai,Mawakili wako na Ushahidi wako ulihojiwa Mantle Status ya akili yako,Ni kweli Jambo hili limejitokeza.?

Shahidi Nikweli limejitokeza.?

Wakili wa Serikali 03 kwa usahihi ukaita Battle Confusion.?

Shahidi ni sahihi

Wakili wa Serikali 03 Kama Kweli hali hiyo imejitokeza Moja ya Jambo ambalo litakukumba ni Kupoteza kuona mambo kwa usahihi.?

Shahidi Sijui

Wakili wa Serikali 03 Ujui kwa sababu Hukumbuki wakati Ukiwa na tatizo hilo nini kilikuwa kinakutokea.?

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali 03 Umewahi Kupoteza Uwezo wa watu unaowatambua au amaeneo unayoyafahamu.?

Shahidi Sijawahi

Wakili wa Serikali VipibKuhusiana kutambua Muda na Tarehe.? umewahi Kuwa na tatizo la Kuchanganya hivi vitu.?

Shahidi Hapana sijawahi

Wakili wa Serikali 03 Vipibkwenye Kuchukua Maamuzi Sahihi, Kwamba Umempiga Mtu bila Sababu alafu baadae ukaja Kukumbuka

Shahidi Hapana sijawahi Kufanya Maamuzi ya namna hiyo

Wakili wa Serikali 03 kwa sababu ya Jambo la Battle Confusion ujaeleza Kwanini lilikukuta

Shahidi nilieleza Mahakama kuwa tatizo hilo nililipata baada ya Kutoka Vitani

Wakili wa Serikali 03 Sababu ya Battle Confusion zipo Nyingi,utakubaliana na mimi

Shahidi Mimi siyo Mtaalamu

Wakili wa Serikali 03 Moja ya Sababu ya Kupata Battle Confusion ni Matumizi ya amadawa ya kulevya yaliyo Kithiri,Ni sawa.?

Shahidi Sababu zenu hizo siwezi Kuwabishia

Wakili wa Serikali 03 Katika Kipindi cha hili tatizo ulipangiwa kazi..?

Shahidi nilipangiwa kwenda Hospitali

Wakili wa Serikali Ilikuchukua Takribani Miezi 02 baada ya Kurudi Jeshini, kabla ya Kufukuzwa kazi kwa Sababu wewe uliendelea kutumia madawa ya kulevya

Shahidi Sijawahi Kutumia Madawa ya Kulevya

Wakili wa Serikali 03 Post Dramatic Disorder ni Kitu gani.?

Shahidi Sifahamu

Wakili wa Serikali 03 Kama ufahamu kuhusiana na Ugonjwa wa Post Dramatic Disorder limefikaje hapa Mahakamani,Umewahi Kumwambia nani

Shahidi Sijawahi Kumwambia Mtu

Wakili wa Serikali 03 Uataribu baada ya Kurudi kazini ulikuwaje

Shahidi Nilitakiwa Kuendelea kuriport Hospitali

Wakili wa Serikali 03 Kwa hiyo Ugonjwa huu ,umeathiri utimamu wa akili.?

Shahidi Hapana

Wakili wa Serikali Unasema ulienda Moshi Kufanya kazi ya VIP PROTECTION, Kile Kitabu chenye Orodha ya Mashahidi na Ushahidi wote we ulikipata.?

Shahidi Ndiyo ninacho

Wakili wa Serikali 03 Kuna Chochote Mshitakiwa wa nne amesema alikuita wewe na wenzako kwa ajili ya VIP PROTECTION.?

Shahidi Sijakiona

Wakili wa Serikali 03 kwa hiyo hili swala lako la VIP PROTECTION ajalisema,hata alipopewa nafasi ya kusema hakuwahi Kulisema popote

Shahidi Sijui yeyesasa,Miye niliulizwa ndiyo Maana nikajibu

Wakili wa Serikali 03 Ulipoluwa unahojiwa na Mawakili wa Serikali ulikuwa unachukua Muda Sana Kujibu,hata Wakati Mwingine Mheshimiwa Jaji alikuwa akitoa Mwongozo,Nikisema unauwezo Mdogo au Umeathirika kiakili

Shahidi kama wewe ni Daktari siwezi Kukubishia Uchunguzi wako,ila Miye nikikiwa nshindwa akujibu kwa haraka kwa sababu Maswali yanazunguuuuuka hayajanyooka

Wakili wa Serikali 03 Nipo sahihi nikisema hali ya Akili yako ipo sawasawa.?

Shahidi Upo sahihi

Wakili wa Serikali 03 Ujatueleza Umuhimu wa Kutuleza Utimamu wa kwanini Umeieleza Mahakama Ya tatizo la Akili kwa wakati Fulani

Shahidi nimeeleza Umuhimu, kwa Kufuatia Swali nililoulizwa Mahakamani

Wakili wa Serikali 03 inahusiano gani swala la Ugonjwa wako na Makosa ya Njama za Kutenda Ugaidi

Shahidi Kwangu naona Vinauhusiano kwa Sababu nimeulizwa na Mahakama,Isingekuwa na Umuhimu nisingeulizwa

Wakili wa Serikali 03 Je unajua umuhimu wa kwamba umewahi kupata Battle Confusion ..?

Shahidi Umuhimu unajua Mahakama yenyewe iliyouliza hilo swali

Wakili wa Serikali 03 Mheshimiwa Jaji naomba tukomee Hapa hakuna Swali Lingine

Jaji: Wakili Mallya kama Unamaswali ya marejeo

Malya Mheshimiwa Jaji ninayo Machache

Mallya Swali langu la Kwanza kwamba wewe Ni Komandoo umefundishwa kukaa na Njaa na Kuhimili Mateso, JE uelewa Wako ni nini katika Swali hili

Wakili wa Serikali 03 OBJECTION hilonswalo haliruhusiwi katil Re Examination, Yeye ange recall tuh katika yale aliyojibu katika Examination

Jaji Mallya Unakubaliana na alichosema Wakili wa Serikali

Mallya sababu ya Muda naomba ni Rudie Swali tuh

Jaji Hapana,Je umekubaliana naye

Mallya Sikubaliani naye lakini sababu ya Muda Nirudi swali tuh

Jaji Sasa hapo tulimalize kwanza kabla Ujaenda Mbali,Kuliko kwenda na Mambo ambayo Mtu hajaridhika nayo

Mallya Sijaja ja Swali Jipya napitia Maswali yale yale na majibu yaleyale

Jaji sawa unaweza ukaanza na Swali Mwanzoni

Mallya Swali langu la Kwanza kwamba wewe Ni Komandoo umefundishwa kukaa na Njaa na Kuhimili Mateso, JE uelewa Wako ni nini katika Swali hili

Shahidi Katika Upande wa Mafunzo unakanuni zake na taratibu zake na kwa Uolpande wa ukamataji wa watuhumiwa kuna Kanuni zake na Taratibu zake

Wakili wa Serikali OBJECTION

Jaji Subiri kwanza Shahidi ajibu kwanza tuone kama linahusika na Mnachotaka Kufanya Objection

Wakili wa Serikali Hakuna sehemu tuliyomuuliza kuhusiana na Kuvumilia Njaa

JAJI mliuliza nini Siku hiyo.?

Wakili wa Serikali Chavula,Katika Mafunzo yenu Mnafundishwa Kuvumilia Njaa.?

Jaji Kwanini uliuliza hilo swali,Ulilenga Ku Establish kitu gani

Wakili wa Serikali Nililenga Kuwa ni Mtu ambaye ni Trained na yale ya Kukaa na Njaa si Kitu kigeni kwake

Jaji sawa kaeni Chini nafikiri hakuna Kitu Kigeni kati ya amlichouliza ,kilichoulizwa na Kinachojibiwa

Namruhusu wakili Mallya Kuendelea

Mallya kwa uelewa wako kwanini uliulizwa swali hilo

Shahidi nimeelewa Kuwa akukaa na Njaa ni Haki kwangi,Kupitia Mateso ni Haki yangu na Kwamba Kukamatwa Bila kuzingatia Sheria ni Haki yangu kwa sababu tuh ni Vitu nilivyowahi Kupitia

Mallya Kuna sehemu umesema Ulipigwa na kuna sehemu Uliteswa mgawanyiko wa hili Jambo likoje

Shahidi Kupogwa ni sehemu ya mateso,Kutishiwa ni Sehemu ya mateso,Ndiyo maana nilisema anilipofika Dar es salaam nilikuwa bado nipo Ndani ya Mateso,

Kitendo Cha Kutolewa Kwenye Chumba na akuambiwa Kitakurudia kilichokutokea Moshi ni sehemu ya mateso wakati huo Comfortability yangu Imeshapotewa kwa sababu Nilikuwa nasimamiwa na Bastola

Na Vilevile Kitendo Cha Kushinda na Njaa ni Mateso pia

Kitendo Cha Kutolewa kituo Kimoja kimoja cha Polisi na Kupelekwa Kingime na Kubadirishiwa jina unalotambulika na Ulimwengu,Kwangu iliniathiri na Nikaona bado Nipo Chini ya mateso

Mallya Umeulizwa kumjua au Kumuona Mahabusu ya Tazara na Mbweni,ulipokuwa unasema Ulijua yupo ila sikumuona

Shahidi nilikuwa nakimaanisha alipokuwa Mahabusu Nyingine tuliweza kusalimiana hata kwa sauti ya Juu,Lakini siyo Kuonana Kwa face to face

Mallya Nia ya Kuonyesha Makovu ilikuwa ni nini.?

Shahidi Kwa sababu kuonyesha Kuwa baada Matendo yale yaliacha Alama za kuumia, ndiyo maana nikaonyesha Makovu

Mallya umeulizwa Pia Kuhusiana na Kupigwa ukiwa moshi na Kuwaona waliokutesa moshi kama uliwatambua au hukuwatambua

Shahidi Kwenye kile chumba nilichokuwa nateswa palikuwa na watu wengi,Wengine nilikuja kuwatambua mbele ya Mahakama na Mtu Mwingine sikuweza Kumfahamu

Mallya Uliulizwa kuhusiana Kutobolewa na Bisibisi Kwenye Makalio,.........

Wakili wa Serikali OBJECTION aulize Yaliyojitokeza kwenye Examination ,Hii kwamba elezea hiyo,Ni Mswali ambayo hayaruhiwi

Jaji Wakili Mallya

Mallya Re examination wajibu wake ni Kufanya Explanation

Jaji Nafikiri Wakili wa Serikali yupo sahihi,Unachouliza Unaacha ywanja Mpana wa Shahidi Kueleza Jambo Jipya badala Kuziba Mwanya wa Kilichoulizwa

Mallya Wale waliokuwa wanakuchoma Bisibisi, Walikuwa wanataka nini

Shahidi Ilikuwa ni sehemu ya Mateso

walikuwa wanasema Nyinyi si mmejifanya kutisaliti,Sasa Mtaona

Jaji Nafikiri sasa tunafungu Box kwa kile nilichokuwa naeleza

Mallya Mawakili wa Serikali alikuuliza Swali kwamba waliokuwa wanakuchoma bisibisi walitaka Kujua nini.?

Jaji Naona Mawakilibwa serikali wanataka mshauriane hapo,Inaruhusiwa

Mallya nitarudi baadae kwenye swali hilo,Je hapa Kwa ufahamu wako kinachoendelea Mahakamani ni Jambo gani

Shahidi ni Shauri dogo katika Shauri Kubwa

Jaji lile swali lako umeuliza kweli

Mallya nimeliweka Akiba nitalirejea

Mallya anaenda Kushauriana na Jopo lake

Mallya wakati wanakuchoma walikuwa wanataka nini

Shahidi Muendelezo wa Mateso

Mallya nafikiri nimemaliza

Shahidi (Mshitakiwa wa pili) Anatoka Kizimbani

JAJI wakili Malya endelea Uwanja ni Wako

Mallya tunae shahidi Mwingine

Mallya Mohammed Abdilah Ling'wenya

Jaji Jitambulishe

Shahidi Mohammed Abdilah Ling'wenya

Dini Muislamu

ajibThibitisha Wallah Billah taalah Natihibitisha mbele ya Mahakama hii Ushahidi nitakaotoa utakuwa ni Kweli tupu,Eeh Mwenyezi Mungu Nisaidie

Jaji tutapisha Hadhana alafu tutaendelea

Hadhana Inaendeleeeee

Jaji Wakili Kibatala Ulitaka Kuzingumza

Kibatala naomba nimtambulishe Wakili Dickson Matata kwa ajili ya Mshitakiwa watatu

Jaji sawa nakushukuru

Jaji Hapa Kuna Maelezo

Jaji kuna Shida Kumuita Msjitakiwa watatu kuwa Shahidi ,Serikali.?

Jaji Kiwhelo Kuna tatizo kwa Mshitakiwa wako kuwa Shahidi

Wakili Kiwhelo Hapana

Mallya Makazi yako kwa sasa hivi Kimara King'ong'o

Jaji Makazi yako kwa sasa hivi

Shahidi Natolea Gereza la Ukonga

Kabla ya Kukamatwa ulikuwa wapi

Shahidi Mtwara kampuni DOT kampuni ya kusaga Kokoto

Mallya Kabla ya hapo..?

Shahidi nilikuwa Ngorongoro

Mallya Unamfahamu Mshitakiwa wa 2

Shahidi Ndiyo

Mallya umemfahamu wapi.?

Jeshini KJ 92 JWTZ Ngerengere

Mallya Umeanza Lini

Shahidi Mwaka 2008 Mpaka 2017

Mallya Kazi gani ulikuwa unafanya .?

Shahidi Komandoo,Special Force

Mallya Unamfahamu Vipi Mshtakiwa wa Pili

Shahidi nilikuwa nipo Mtwara nikapigiwa Simu na Askari Mwenzangu ambaye nilikuwa nipo naye Jeshini anaitwa Dennis Urio

Kwamba Kuna kazi ya kwenda kumlinda Mtu bila kunitajia huyo Mtu ni nani

Nikamwambia asubiri nikifika Nyumbani aongee na Baba akikubali sawa

Nilipofika Nyumbani akapiga simu nikampa akaongea na Baba

Baba akauliza si unamfahamu,nikasema Ndiyo akaniambia nakuombea Dua nenda

Mallya Siku ya tarehe 05 Mwezi 08 2021 Maeneo ya Rau Madukani kulitokea kitugani

Shahidi Nilikuwa kwa Dada yangu Mmoja anaitwa Asma,akiwa Dukani kwake mimi na Adamoo tukawa tunasubiria Chakula

Mallya kilichokupeleka Rau Moshi ni kitu gani

Shahidi Tulikuwa tunaenda kukutana na Mwajiri wetu ilikuwe kukubaliana naye

Mallya Mshitakiwa wa pili alikuwa anafanya kitu gani

Shahidi Wakati nipo Dykani Kwenye Upenyo Coridor nikasikia Kelele sana,Nikatika niende Kuona

Nikakuta Adamoo ameshanyanyuliwa na Kukabwa

Nikauliza Tatizo ni nini.?

Nikashikwa Mkono wakaniuliza wewe Unamfahamu huyu

Mallya Ulipata Kujua ni akina nani.?

Shahidi Niliwaona kwa mara ya kwanza

Wakaniuliza unamfahamu huyu.?

Akatoka mwingine akasema anapistol anapistol anapistol

Alinyofoa Kutoka amwilini Kwa Adamoo Upande wa Kulia akasema anapistol anapistol akasema na madawa ya Kulevya anayo

Mallya eleza sasa Pistol anatoa wapi.?

Wakili wa Serikali OBJECTION anamfeed Majibu

Mallya baada ya kumkuta Adamoo amenyanyuliwa Juu kitu gani kiliendelea

ukisema alimtolea unataka Mahakama ipate apicha gani

Shahidi Baada ya Kuona Wanamfanyia Adamoo yale na Adamoo na Mfahamu na nilikuwa naye muda mrefu,Nikauvuta Mkono wangu kwa aliyekuwa amenishika

Nikawaambia Kuwa adamoo hakuwa na hivyo Vitu,nikatoa Simu na wallet nikaweza Kibarazani

Jaji Ulitoa simu na nini

Shahidi Simu na wallet

Mallya Kusema walimuwekea unamanisha nini.?

Shahidi Kwa Sababu nilianza Safari ya kwenda moshi na Adamoo Kuanzia Chalinze,Nafahamu hakuwa na Vitu hivyo

Nikasema huyu Mtu kwakuwa mmemuwekea na Mimi ngoja nitoe Vitu vyangu

Mallya: wakati huo Adamoo Yupo wapi

Shahidi: Wameshusha Chini ila wanampiga pale pale chini

Mallya: uliweka vitu vyako wapi,.?

Shahidi: waliochukua walikuwa ni Polisi

Mallya Kwenye wallet Kulikuwa na nini.?

Shahidi Palikuwa na Pesa.?

Mallya Kiasi gani.?

Shahidi Laki tatu

Mallya Zipo wapi

Shahidi Haoana sielewi

Mallya Waru waliomvamia Adamoo Unaweza Kujua walikuwa ni watu wangapi.?

Shahidi Walikuwa Zaidi ya watano

Mallya baada ya Kupanda gari Mmlielekea Wapi.?

Shahidi Central Moshi

Mallya Kichofuata nini.?

Shahidi Waliotuleta wakatoka,baada ya kutuacha

Walitutenganisha,Nakumbuka Mmoja alikuwa Askari Bonge nilimueleza Kuwa Mimi nilikuwa mwanajeshi

Wakauliza Kama nawajua Komba na msellemu.?

Jaji Komba ni Mtu Mwingine na Msellemu Mtu Mwingine

Mallya nini ulishihudia Kinacho muhusu Adamoo

Shahidi nilishihudia akiwa yeye ni wa Kwanza kuinginzwa Cello yake na Mimi nikawekwa Cello Nyingine

Mallya Walipomtoa Cello Ulionaje.?

Shahidi Cello ya Kwanza Ya Kwangu na Yapili,Wakati wanamuingiza Cello yake sikumuona ila wakati wanamtoa alikuja Mtu kwenye Cello yangu akaita Ling'wenya Nyuma yake wakampitisha amtu wamemuinamisha ,

Mallya Ulimtambuaje..?

Shahidi alikuwa na Jinsi Nyeusi na Shati la amaua Maua

Mallya nini Kilifuata

Shahidi nilisikia akilio Huko alipopelekwa Kwa Sababu haikuwa mbali na Cello yangu,Nilisikia kilio akilia na nilimtambua kwa Sauti sababu namuitaga sauti ya zege

Mallya ulitambua sauti ni ya nani.?

Shahidi nilitambua ni Sauti ya Adamoo

Mallya Ilikuwa ni Sauti ya namna gani.?

Shahidi ya amtu anayepigwa ,alikuwa analia Eeeehiii Ehiiiiiii Ehiiiiiiiiiiiiiiii ya amtu anayeteswa

Mallya ilidumu kwa Muda gani

Shahidi Sina uhakika ila ni Kama Nusu saa

Mallya Umesikia Sauti ya zege analia kwa Nusu saa,Nini Kilifuata

Shahidi Baada ya amuda amfupi Kupita akapitishwa Mtu yuleyuke aliye Vaa Jinsi Nyeusi na ashati la maua akiwa awezi akutembea alishikwa huku Kushoto na kulia na kwamba wakamburuza hadi Cello inayofuata baada ya kwangu

Mallya nini Kilifuata

Shahidi nikajua anayefuata ni mimi

Mallya baada ya akujia Unayefuata ni wewe,kilifuata nini

Shahidi walinichukua Mimi wakanipeleka huko,Nikaenda anikakuta watu wamekaa na wanasimu zao wananirekodi

Wakasema taja majina Matatu

Nikawatajia

Wakaniuliza Unafanya kazi gani

nikawatajia nimetoka Mtwara

Wakanipiga Buti wakasema wanajua mimi nimefuata nini Moshi

Mallya Mahita yupi unayemzungumzia.?

Shahidi Mara ya Mwisho nilimuona hapa mahakamani akitoa Ushahidi

Mallya hapo Mlikuwa sehemu gani

Shahidi Ni ndaninya Central Police palepale,nilitolewa Cello nikapalekwa kwenye Kijumba Kidogo

Palikuwa na Bomba refu,nikiwa nimefungwa Mikono na miguu,Mimi kwa ufahamu wangu inaitwa killing zone

Mallya Killing zone ni Kitu gani

Shahidi Unakuwa Unaning'inizwa Miguu Juu Kichwa chini,

Mallya kilifuata kitu gani..?
Anilipigwa Sana kwenye Unyayo kwa sababu Zilikuwa zimekaaa Juu

Mallya wakati wanakupiga wanasemaje

Shahidi aliyenipiga ni Mahita tuh

Mallya walikuwa wanahitaji kitu gani

Shahidi niliwaambia nimekuja kwa kazi ya VIP PROTECTION Kwa Kumlinda Mwenyekiti wa Chadema

Wakasema Utasema tuh

Mallya Ilichukua Muda gani

Shahidi kama Nusu saa

Mallya ikawaje

Shahidi alikuja Mtu Mtu aliyevaa akiraia akatoa Amri "Mwacheni sasa msimpige

Wakawa wameniweka nimekaa Chini nikiwa na Pingu na Mguuni nimefungwa kamba

Jaji Miguuni Ulifungwa nini

Shahidi Miguuni nilifungwa kamba

Mallya baada ya hapo Ulipelekwa wapi

Akaniambia huku Hoi na yeye akaniambia Mimi Mwenyewe Huku Hoi

Jaji Ukisema Mimi Huku hoi unamaanisha nini.?

Shahidi yani nimeumiabsana na kuchoka sana

Mallya Mahita alikuwa anakupiga na Kitu gani

Shahidi Sijakishika Vizuri lakini kama Shaba Nzito

Mallya nini Kilifuata?
Mashaidi wa utetezi (Chadema) wanajigongagonga kweli. Yaani anasema Jaji aandike aliteswa na hakuteswa, vyote kwa pamoja!!! Wahesabu maaumivu kwa ushahidi huu
 
Back
Top Bottom