Wakuu kumekucha tena, na kwa kweli muda ni mfupi mno, tuendelee kuvumiliana kwa kero zetu za kampeni. Leo tena kipenzi cha Watanzania Rais mtarajiwa Mh Tundu Lissu anawasili Mkoani Njombe kwa lengo la kueneza sera nzuri mno za CHADEMA , ikiwa ni pamoja na kuomba kura kwa mabosi wake ambao ni wananchi , basi kwa heshima na taadhima nakuombeni tuendelee kubaki hapa hapa kwa taarifa zaidi.
=========
LISSU: Naomba nizungumze habari ambayo leo Rais wetu ameizungumza pale kijijini kwake Chato. Amesema kwamba huyo mtu aliokula ugali akashiba anachikiona ni Chato tu, kwanini hahoji viwanja vingine ambavyo tumevijenga akataja Singida, Songea, Shinyanga, Dodoma na vingine vingi.
Nimezungumza Chato sana, naomba nifafanue kwanini Chato lazima iwe kelele.
Uwanja wa Chato ni tofauti na viwanja vingine vyote, tofauti yake ni hii, Chato ni kijiji wala sio mji. Karibu na Chato kuna kamji kakubwa kanaitwa Katoro hakana uwanja wa ndege, mbele kuna mji mkubwa wa Geita, hakuna uwanja wa ndege.
Sasa kwanini Chato? Ni kwa sababu mija tu, Magufuli ni Rais ndio maana kuna uwanja wa ndege Chato. Mwaka 97 wakati Mkapa akiwa Rais ilitungwa sheria ya maadili ya viongozi wa umma, inasema kiongozi wa umma hapaswi kutumia mamlaka yake ya umma kwa manufaa yake binafsi.
Kiongozi wa umma wa kwanza ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, tujiulize manufaa ya umma ya uwanja wa ndege wa Chato ni yepi?
Hizi ndege nyingi alizonunua anazotutambia nazo hakuna hata moja inayokwenda Chato. Hakuna abiria hata mmoja anaekwenda Chato, mtu pekee anaekwenda Chato ni Rais Magufuli na nimesema na mama yake wala sio uongo, na ndugu zake.
Uwanja wa Chato umeharibu mabilioni ya shilingi za kitanzania, ni mfano wa kwanza wa jinsi ambavyo watu wenye mamlaka ya umma wanaweza kutumia mamlaka yao vibaya.
=======
UPDATES
Hapa ni jimbo la Makambako Mkoa wa Njombe
View attachment 1569763
View attachment 1569768