Nashangaa TBC imekwenda kurusha kampeni lakini badala ya kurusha hotuba za watu haswa zile zinazochallenge namna Magufuli anavyoendesha nchi wao wanakatakata.
TBC wajue kuwa kampeni ni pamoja na kujinadi na kukosoa namna nchi inavyoendeshwa na utawala uliopo. Sasa TBC yenyewe ndo wamegeuka wahutubiaji kila mtu huko kwenye kampeni anapopiga nyundo kali!
TBC kama mmegeuka nyie ndo wahutubiaji basi rudini studio mkatengeneze documentary.
Yaani hakuna matusi, wala kitu kibaya lakini kwa sababu wanachallenge namna serikali ya Magufuli ilivyoshindwa katika angle mbalimbali wanakata!
Mnaboa sana!