Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu - Januari 19, 2022

Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake watatu - Januari 19, 2022

Ndugu kama hujaelewa husilazimishe acha sio pumzi hiyo kusema utakufa.

Make Your Investigations Smarter, Faster and More Efficient​

Cellebrite's end-to-end Digital Intelligence Investigative Platform and Services are trusted by over 6,700 federal, state and local public safety agencies and enterprises in over 140 countries and is used in millions of cases each year.
 
Kamanda wa Polisi hajui kirefu cha DCI mpaka akumbushwe na bosi wake! Hajui vyeo vya jeshi la polisi! Ndiyo maana muda wote anakwenda chooni kujikumbusha kwenye kikaratasi alichowekewa.

Jeshi la polisi mnaowaita wajinga wako na CELLEBRITE​

Make Your Investigations Smarter, Faster and More Efficient​

Cellebrite's end-to-end Digital Intelligence Investigative Platform and Services are trusted by over 6,700 federal, state and local public safety agencies and enterprises in over 140 countries and is used in millions of cases each year.
 
Mwongo Mwongoze akudanganye harafu mbanie humo humo-By Sukuma Ndani (Aggrey Mwanri)!
Unabanwa mpaka unaomba kwenda chooni?
 
Kibatala: Kwa uchunguzi wako wewe ungekuta taarifa za kupanga uhalifu, ungeacha kuandika kwenye report yako kwa sababu haujaambiwa kwenye terms of reference?

Shahidi: Mimi ni Askari Polisi, kama ningekuta meseji za kupanga uhalifu ningeweka kwenye report yangu..

Hakuna kesi Tena hapa
 
Kibatala: Kwa uchunguzi wako wewe ungekuta taarifa za kupanga uhalifu, ungeacha kuandika kwenye report yako kwa sababu haujaambiwa kwenye terms of reference?

Shahidi: Mimi ni Askari Polisi, kama ningekuta meseji za kupanga uhalifu ningeweka kwenye report yangu..

Hakuna kesi Tena hapa

Hongera Jeshi la polisi kwa kwenda na wakati wa kidigital- watu kama Mbowe wamesumbua sana nchi hii sasa wanashikwa kirahisi​

Accelerate Justice​

From the field to the lab and the courtroom… solve cases faster.

CELLEBRITE
 

Hongera Jeshi la polisi kwa kwenda na wakati wa kidigital- watu kama Mbowe wamesumbua sana nchi hii sasa wanashikwa kirahisi​

Accelerate Justice​

From the field to the lab and the courtroom… solve cases faster.

CELLEBRITE

utakuwa hupo saloon za wanawake unasuka maana hata nchi ufahamu
 

Jeshi la polisi mnaowaita wajinga wako na CELLEBRITE​

Make Your Investigations Smarter, Faster and More Efficient​

Cellebrite's end-to-end Digital Intelligence Investigative Platform and Services are trusted by over 6,700 federal, state and local public safety agencies and enterprises in over 140 countries and is used in millions of cases each year.
Mbona wapo wengi wanasimu kali sana lakini hawajui kuzitumia zaidi ya kupiga! Hata huko Cellebrite wanaweza kuwa wanatumia kiwango cha chini sana cha programu kwani kuna baadhi ya mambo amesema hayajui.
 
Salaam Wakuu,

Leo tarehe 10/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea.

Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=======


Kufahamu ilipoishia, soma hapa:Yaliyojiri mahakamani kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Kesi imeahirishwa hadi 19/01/2022

Jaji ameingia, kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa.

Jaji: Shahidi Nakukumbusha Upo Chini ya Kiapo Bado na Wakili wa Mshtakiwa Namba Mbili Ilikuwa Unaendelea, Karibu

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba nikumbushwe niliishia wapi

Jaji: Uliishia Wakati anakusomea Kielelezo H



Mallya: Shahidi tusomee hii ni Tarehe

Shahidi: Imeandikwa 05 August 2020

Mallya: Kuna Entry imeandikwa Owner of Article, Kwenye PF Je imeandikwa Jina gani?

Shahidi: Nashindwa Kusemea Sana Mheshimiwa Jaji sababu Siyo Mimi Niliyeandaa

Jaji: Hujaambiwa Uisemee Umeambiwa Usome

Shahidi: Imeandikwa Mohammed Abdallah Ling'wenya.. Lakini sijaandaa mimi

Mallya: Kwa Hiyo nani kaleta Mahakamani

Shahidi: Ni Mimi

Mallya: Kwa hiyo tuiondoe Mahakamani?

Shahidi: Hapana

MALLYA: Soma Sasa

Shahidi: Mwisho Imeandikwa DOYI

Mallya: Kutoka Tarehe 05 August 2020 Mpaka Tarehe Uliyo letewa Kwenye Ofisi yako Kuna Interval ya Siku Ngapi

Shahidi: Kuna Interval Ya Siku 08

Mallya: Na wewe Ulifanyia Kazi Tarehe Ngapi

Shahidi: Mwezi Wa July 2021

Mallya: Tarehe Ngapi

Shahidi: Sikumbuki Tarehe

Mallya: Kutoka Muda Umeletewa Mpaka Unafanya Uchunguzi Kuna Muda gani

Shahidi: Angalau Miezi 10

Mallya: aliyekuletea hiyo Item "H" alikwambia alikamata katika Physical Condition gani

Shahidi: Hakuniambia

Mallya: Alikwambia alikuwa Amehifadhi Siku gani

Shahidi: Hakuniambia

Mallya: alikwambia Kwamba aliondoa au Kutumbukiza Physically Kitu gani

Shahidi: Hakuna Kitu kama hicho Unachosema, kuwa alitoa chochote, Utaratibu Wa Kutunza Kielelezo Unajulikana, Kwa Utaratibu Wa Polisi Kielelezo Umapo Ki Seize unapaswa Umantain Kilivyo

Mallya: aliyekuletea alikwambia alifuata Utaratibu au Haku fuata Utaratibu huo

Shahidi: Ni Askari Polisi ni Imani yangu alifuata

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu Swali Langu

Shahidi: Mheshimiwa Jaji swali linahitaji Maelezo,

Jaji: Nani sasa, Maelezo ya Wakili au Ya Kwako?

Shahidi: Mimi Naamini Kuwa Utaratibu ulifuatwa

Jaji: Swali lake Halipo Huko kama Utaratibu ulifuatwa au Lah Bali Je alikueleza

Shahidi: Mheshimiwa Jaji hakunieleza

Mallya: Ndiyo Jibu ndiyo Nilikuwa nayafuata

Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Physical Damage inaonekana hapa, Kuna gaps, Je Macho yangu ya naona sawasawa

Shahidi: Condition Siwezi Kuzungumzia hapa

Mallya: Hilo Sijakuuliza, Nauliza Kuna Damage hapa Inaonekana, Je Kinachoonekana ni nini

Shahidi: Kinachoonekana ni Simu

Mallya: Siulizi simu hapa Mahakamani, usilete mahakamani michezo yako..

Mallya: Unachokiona ni Kitu gani

Shahidi: Ninachokiona ni Simu Mheshimiwa Jaji

Mallya: Ngoja Nichukue Simu F tulinganishe na H, Zote Umeleta Wewe, Swali langu hii yenye haya Ma gaps unahitaji?

Shahidi: Mhe Jaji Hizi ni simu Mbili tofauti, Siyo lazima zifanane..

Wakili wa Serikali: Mhe Jaji Wakili amebakia Muda Mrefu na Majibu yameshatolewa, Swali lake limeshajibiwa

Mallya: Mheshimiwa Jaji Swali langu halijajibiwa bado

Jaji: Muulize swali tena

Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Ma' gaps, Je kitaalamu Unayaitaje?

Shahidi: Miye siwezi Kuongelea chochote

Mallya: Hii difference ya Kuwa hii ina button Kwenye simu na hii haina, unasemaje?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji siwezi Kuzungumzia kuhusu tofauti

Mallya: Kwenye Riport yako Kwenye Kielelezo F Je aina Positive Results..?

Shahidi: Ndiyo Ilikuwa na Positive Results

Mallya: Kuna Simu Ulizo letewa ukakuta Hazina Positive Results Kama Ulivyoletewa kwenye Terms of reference

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Kwa Mujibu wa Sheria Askari Polisi anaruhusiwa Kukamata simu.?

Shahidi: ndiyo Kwa Mujibu wa Sheria

Mallya: Kama Askari Polisi anataka Kujiridhisha Juu ya Kitu anachotafuta analeta Forensic?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Unafahamu Simu ni Personal Property ya Mtu?

Shahidi: Inaweza Kuwa Simu ya Ofisi

Mallya: Yapo Mazingira Mtu anaweza Kuwa na Simu Kama Mali yake Binafsi.?

Shahidi: Kama amenunua ni Mali yake Binafsi

Mallya: Je Yule ambaye amekamata kama Hajakuta Kitu anatakiwa kumrudishia Simu yake..?

Shahidi: Sifahamu

Mallya: Unafahamu Kwenye Simu ya Mtu Binafsi ambayo kanunua Kwa Pesa Yake, Inaweza Kuwa na Taarifa zake Binafsi?

Shahidi: Simu ya Mtu anaweza Kuweka Taarifa ambazo anahisi anaweza Kuhifadhi

Mallya: Kuna uwezekano Kuwa Mtu akahifadhi Taarifa au Nyaraka ya Utetezi kwenye Simu?

Shahidi: Sifahamu

Mallya: Taarifa Uliyompelekea huyo aliyekuomba Umfanyie Uchunguzi, Je akipokea Kwa Mkono au Kwa Email?

Shahidi akipokea Kwa Mkono

Mallya: Je alisoma hiyo Taarifa Yako ya Uchunguzi

Shahidi: Naamini alisoma

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 23 Samahani

Mallya: Shahidi Interest yangu Katika Riport Yako ni Ukurasa Wa Sita Unapozumgumzia Kuhusu Kielelezo A, B, C, D

Shahidi: Vielelezo Tajwa A, B, C, D hazina Taarifa Zenye Maudhui

Mallya: Kwenye Hicho Kielelezo namba C ulikuta ni Cha Nani

Shahidi: Ni Cha Khalfani Bwire

Mallya: Kwa hiyo Katika simu ya Khalfani Bwire hukukuta Jambo Lolote?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Ulifanya Uchunguzi Wako Lini

Shahidi: July 2021

Mallya: Ulikuja Kutoa Ushahidi wako lini

Shahidi: Juzi January 2022

Mallya: Kuna Interval ya Muda gani kati ya Wewe Kufanyia Uchunguzi Mpaka Kutoa Ushahidi

Shahidi: Usio Pungia Miezi Mitano

Mallya: Hiyo Content ambayo ulikuta negative Results upo wapi

Shahidi: Sikuona Haja ya Kuweka Kwa sababu sikukuta Kitu

Mallya: Bwana Bwire alikuwa anataka Negative Results ambayo Ingekuja Mahakamani Kuonyesha Kuwa Hakuna Maswala ya Ugaidi

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Nilipewa Terms of Reference, Kwa Hiyo Kama Haipo siwezi Kutoa

Mallya: Shahidi Umesha wahi Kupima Malaria

Shahidi: Hilo swali Limeingiaje hapa

Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory?

Shahidi: Sioni likihusiana

Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory

Shahidi: Sioni likihusiana

Mallya: Lina husiana Kwa Sababu Malaria Ukipimwa Wakikuta Negative Results wanakupa Majibu Yako

Shahidi: Kuna Baadhi ya Simu Zina Taarifa zaidi ya GB 20 huwezi Ku Print zote

Mallya: Je ulitoa taarifa Kwamba hukukuta kwa sababu ni Kubwa

Shahidi: Kwa sababu ni Out of Context

Mallya: Ulishajibu Kuwa Hukuona Haja

Shahidi: Siku Jibu hivyo

Jaji: Hapo Ndipo Mr. Malya Unapotuchanganya, Ni wapi Tutaona Huku uliza

Mallya: Nilikuwa namkumbusha Majibu Yake

Jaji: Basi Kama Unaulizwa Swali Hakuna Haja ya Kuongea Yote hayo

Mallya: Shahidi Nilisikia Unasema Mnatumia Legitimate Software Ku Updates yenu, Je Ulizungumzia Mnapewaje

Shahidi: Hapana Sikuzungumzia

Mallya: Mheshimiwa Jaji Naomba Barua ya Airtel na Ya Tigo

Mallya: Nakuonyesha Kielelezo P15 na Interest yangu ni Mtu aliyepewa hii Barua

Shahidi: Barua hii Imeelekezwa Kwa Kamishina wa Uchunguzi wa Kisayansi

Mallya: wewe sasa hivi ni Inspector Wa Polisi, Je Mwaka 2021 uliwahi Kuwa Kamishina wa Polisi

Shahidi: Mimi Sijawahi Kuwa Kamishina

Mallya: Kwenye hii Barua wapi Umekuwa Adressed.?

Shahidi: imekuwa Adressed Kwa Kamishina wa Uchunguzi Wa Kisayansi

Mallya: Naomba na ya Tigo

Mallya: Umesema Ofisini Kwenu Mkubwa wa Command ni Nani

Shahidi: Anaitwa CP SHABANI

Mallya: Kuna Departments Ngapi katika Forensic Beaural

Shahidi: Tuna Units Mbalimbali Ka Cyber crime ambayo Natoka Mimi, Toxicology, DNA, Pathology, Fingerprints, Ballistic, Documents, Crime scenes

Mallya: Kwa Mahesabu yangu ni Nane, Kwa Kiswahili zinaitwaje?

Shahidi: Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi

Mallya: Zote hizi Ukubwa Wake Kwa Maana ya Commanding Ofisa wake ni CP SHABANI.?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Naomba uniseme Adress ambayo Tigo Wameitumia

Shahidi: UCHUNGUZI WA KISAYANSI
S. L. P 9094
DAR ES SALAAM
TANZANIA

Malya: naomba Mwenzangu Wakili Faraji Mangula aendelee

Mangula: Shahidi Pole na kuuguq Kichwa Siku ya Kwanza

Mangula: Ni sahihi ulisema Kuwa umesema Advanced Diploma ya Computer Science

Shahidi: Ndiyo

Mangula: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali, Ulielezea Kuwa Baada ya Masomo Ulipata Award gani

Shahidi: Nilisema nilikuwa napata Certificate

Mangula: Wakati Unafanya Uchunguzi Ulisema Ulikuwa una cheo Gani

Shahidi: Mkaguzi Msaidizi

Mangula: kwa sasa Una cheo Gani

Shahidi: Inspector

Mangula: Wakati Mawakili Wanakuongoza Hapa Mahakamani, Je ulisema Kuwa Ulipata Mafunzo gani Mpaka Ukapanda Cheo

Shahidi: Unakuwa Awarded siyo Kwa Kwenda Kozi

Mangula: Cheo chako umekipata wakati awamu ya 5 au ya 6?

Shahidi: Sijaelewa logic ya swali lako

Jaji: Swali la nani alikuwa Rais, unataka kujenga nini

Mangula: Mhe Jaji kuna premise nataka kutengeneza

Jaji: hiyo premises ndiyo utengeneze kupitia Rais aliye madarakani?

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mahakama Ilisha wahi Kutoa Maelekezo Juu ya Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani

Jaji: nilitoa Maelezo Kuhusiana na Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani, lakini pia nataka Kujiuliza Kuhusu Kuuliza Maswali ya Rais wa Awamu ya Tano au Lah

Sasa Unachotaka hapo ni nini.?

Mangula: Ngoja Niulize Kwa Namna Nyingine

Mangula Naomba Kielelezo Namba 23,Shahidi Naomba Usome Kwa Sauti Kichwa Cha Habari cha Hicho Kielelezo

Shahidi Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi, ya Makosa ya Kimtandao Chini ya Sheria ya Mtandao namba 14

Mangula: Je ni kifungu Kipi ambacho umekitumia?

Shahidi: Mimi siyo Mtaalamu wa sheria, Ila nilifanya kwa sheria ya mtandao

Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji sasa ni kifungu kipi ulitumia

Shahidi: Mheshimiwa sikutumia kifungu

Mangula: Nikikupa hiyo sheria, unaweza Kunitajia kifungu ulichotumia

Shahidi: Mimi sina UFAHAMU WA MAMBO YA KISHERIA

Mangula: Kwa hiyo nyie Ofisini kwenye mnafanya bila ufahamu wa Sheria

Shahidi: Nishasema mheshimiwa SINA UFAHAMU WA SHERIA

Mangula: Fungua sasa Ndani, Ieleze Mahakama ni Kielelezo Kipi Ulichofanyia Kazi Ukagundua Kuna Makosa ya Ugaidi Uliyaona, Ni wapi Umeandika hivyo..

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Jibu linahitaji Maelezo, Mimi nililetewa tu Kufanya Uchunguzi.

Mangula: Kwa hiyo wewe hujui Kuwa Kuna Ugaidi au Hakuna Ugaidi kwenye hicho Kielelezo?

Shahidi: Sahihi

Mangula: bado unataka Mahakama ichukue Kielelezo Hiki Kama Kielelezo Cha Umuhimu?

Shahidi: Nimesema ni Kazi ya Mpelelezi

Mangula: Umesomeshwa na Serikali?

Shahidi: Ni Sahihi

Mangula: Na Umelipiwa Masomo Kwa Kodi ya Watanzania

Shahidi: Sahihi

Mangula: wewe Umesomea Udukuzi

Shahidi: Nimesomea Ethical Hacking

Mangula: Ulisema Mwanzo Kuwa Vifaa Vyako Vya Uchunguzi Vina Uadilifu

Shahidi: Ndiyo

Mangula: Na Kila Unachotaka Kwenye hiyo Simu, Mambo wako Unakuonyesha

Shahidi: Yes

Mangula: Kama Kuna video inakuomyesha.?

Shahidi: Inaonyesha Vile Vitu ambavyo Inaweza Ku Extract Kwenye Kielelezo

Mangula: Inakupa kila Kitu ambacho Kipo Kwenye simu?

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Mangula: Mheshimiwa Jaji Naomba Extraction Report

Mangula: Katika huo Mambo unaosema Ulikuwa upo Sawa Kukupa Kila Kitu, Ukisoma Kielelezo Cha Kwanza hicho namba 25

Mwambie Mheshimiwa Jaji kwenye hicho Kifaa Ulichofanyia Uchunguzi Kulikuwa na Content gani

Shahidi: Kukikuwa na Proxy Ya Chat ya WhatsApp

Mangula: Kulikuwa na Picha Kwa Maana Images

Shahidi: Picha Hakuna, Zipo Profile Picture

Mangula: ambazo ni za nani

Shahidi: Sijui za nani

Mangula: Katika hivyo Vielelezo ambavyo Vimepokelewa Mahakamani, Palikuwa na Mazungmzo ya Simu kati ya Watuhumiwa

Shahidi: Hakuna ila kwenye Kielelezo namba 26 zipo

Mangula: apewe Namba 26,,tuchagulie Mazungmzo Marefu Kuliko yote

Shahidi: Kuna Mazungmzo ya Dakika 9

Mangula: Bila Shaka Ndipo walikuwa wanapanga Ugaidi, Haya Mwambie Mheshimiwa Jaji Walizungumza nini hawa Watuhumiwa

Shahidi: Kuna Call Logs tu

Mangula: zile Sauti zipo wapi

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Kama Mahakama Yako itaniruhusu Kwa sababu za Ki Usalama nisijibu Hilo swali

Mangula: Swali langu ni Juu ya Watuhumiwa Ukiwa Mchunguzi wa Hizo Simu, Nauliza Mazungmzo ya Watuhumiwa Wale Wanne, Narudia Swali Sauti zao Watuhumiwa Zipo wapi ndugu shahidi?

Shahidi: Sababu za Kiusalama huwezi Kuzungumzia suala la Sauti

Mangula: Shahidi Nimesikia unasema Kuwa huwezi Kuzungumzia Kwa sababu ya Kiusalama, Je Sheria gani inakuzuia Usizungumzie hilo Suala?

Shahidi: Sijataja Sheria

Mangula: haya Sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji, Sauti za Watuhumiwa Zipo wapi????

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Hazikuwa zinahitajika katika Terms Of Reference

Mangula: Ni sahihi nikisema Kuwa Katika Extraction Uliyo fanya, Kuna Vitu Uliviondoa sababu hazikuhitajika?

Shahidi: Swali linahitaji Maelezo, Mwanzoni Nilisema Kuwa Tunafanya Kwa Hatua tatu, Aquisation, Analysis na Extraction

Mangula: Kwa hiyo ni sahihi Kuwa Kwenye Mtambo Kuna Baadhi Ya Taarifa Hukutoa Sababu Hazikuhitajika?

Shahidi Wa Jamhuri: Kimya

Mangula: Kwa Mujibu Wa Kielelezo Namba 22, Mwambie Mheshimiwa Jaji Vitu gani Viliombwa Kwa ajili ya kufanyia Uchunguzi

Shahidi: Kwa Mujibu wa Barua yako Yenye Reference........

Mangula: Hoja ya Barua Ilikuwa unahitaji Ufanyie nini

Shahidi: Pamoja na Taarifa Hii Nakuletea Uchunguzi Niliofanya .... Mimi Inspector Innocent Ndowo

Mangula: Ni wapi Walikutaka Wewe Usitoe Sauti za Watuhumiwa?

Shahidi: Mimi nilifuata Terms of reference

Mangula: Nikisema Kuwa Wewe Inspector Ndowo na Viongozi Wako wa Polisi Kwa Makusudi Mliamua kuficha Baadhi ya Taarifa katika
Kesi hii kwa Maslahi yenu Itakuwa sahihi au siyo Sahihi Ukizingatia Kuna Taarifa Hazipo hapa?

Shahidi: Siyo Sahihi, Hatufanyi Kazi kwa interest zetu

Mangula: Fungua Kielelezo H, na Umwambie Mheshimiwa Jaji IMEI namba ya hicho Kielelezo Ni namba Ngapi Kwa Mujibu wa PF 145

Shahidi: Kwa Mujibu wa PF Hakuna IMEI namba

Mangula: Soma huo Mstari Wa Pili Kwa Sauti Umeandikwaje

Shahidi: Simu TECNO IMEI imefutika

Mangula: Wakati Unaongozwa Kwenye Ushahidi Ulisema nani aliyefuta hizo IMEI namba

Shahidi: Si Kuulizwa hilo swali

Mangula: Wewe unafahamu aliye futa hiyo IMEI namba

Shahidi: Simfahamu

Mangula: Katika hicho Kikaratasi Umeeleza IMEI namba Imefutwa Wapi.?

Shahidi: Sikusema

Mangula: ukiacha Kielelezo namba 35 ambacho kimechezewa na Watu wasiojulikana , Ni Kielelezo Kipi Kingine Mlichochezea

Shahidi: Hakuna Kielelezo Kilichochezewa

Mangula: Fungua Kielelezo namba 23, Mheshimiwa Jaji Namuonyesha Kielelezo namba 23

Mangula: Nataka Majibu ya Riport Yako ya Uchunguzi

Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi Katika Report Yako ya Uchunguzi Umeandika IMEI namba Imefutika

Shahidi: Hakuna Mahala Nilipo andika

Mangula: Nilisikia Unasema Ulichukua simu Ukiweka Katika Mtambo Wa Uchunguzi, Ule Mtambo utakuonyesha Kuwa Simu ni Original au Feki

Shahidi: Mtambo hauonyeshi Kuwa Simu ni Feki au Original

Mangula: Kitu gani Kinaonyesha kuwa Simu ni Feki au Original

Shahidi: Kitu nilichosema Kuna Kama zile Simu za Kichina, Mtambo una Operate kwa OS

Mangula: Kwa hiyo nini Kina onyesha ni FEKI Au ORIGINAL?

Shahidi: Nilichosema naomba Unisikie Vizuri, Mtambo una Option ya Kufanya Kazi hata Kwa kutumia Chip

Mangula: Mheshimiwa Jaji naomba NIISHIE Hapo

Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji NAOMBA KWENDA WASHROOM (CHOONI)....

Shahidi anatoka na kuelekea katika vyoo vya nje..

Mahakama Ipo kimya inasubiri arejee kizimbani.

Shahidi amerejea kizimbani kutokea kwa fasii ya chooni.

Kihwelo: Shahidi Nilisikia Unazungumzia Kuhusu Celebrite Physical analyser Je ni Software Au.?

Shahidi: Ni software

Kiwhelo: nani alifanya Development ya Software

Shahidi: Celebrite Wenyewe

Kiwhelo: Nilisikia Umesomea Kuhusu Penetration Test

Shahidi: Ndiyo

Kihwelo: Je Penetration Testing, Ni sawa na Fazzing

Shahidi: Sifahamu

Kiwhelo: Je Wakati Unafundishwa Kuhusu Penetration Testing, Walikufundisha Kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao (High Tech Cyber Attack)

Shahidi: Sijafundishwa hiyo

Kiwhelo: kwakuwa Ujafundisshwa kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao, Ni sahihi Celebrite Ingeweza Kuingiliwa

Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa

Kiwhelo: pale Ofisini kwenu ni nani Network Provider

shahidi: ni TTCL

Kiwhelo: Ni sahihi Kuwa Network Services Provider anaweza Kuingilia Data Zako

Shahidi: Hawezi

Kiwhelo: Nyinyi Kama Jeshi la Polisi Mnatumia Nini Kujilinda na Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao

Shahidi: Naomba nisijibu sababu za Kimtandao

Kiwhelo: Nilisikia Kuwa unazungumzia kuhusu DECORDING

Shahidi: Ndiyo

Kiwhelo: Shahidi Pegasus Technology ni Moja ya Technology mnayotumia?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji naomba Nisijibu Sababu za Kiusalama

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba anijibu sababu Baadae Nitataka kujua Intergrity ya Technology Wanayotumia

Jaji: Shahidi ame raise suala la Security, Au mnasemaje Upande wa Serikali?

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi amesha Sema kuwa awezi Kusema Sababu za Kiusalama, Sisi tunaona Sababu hizo ni Valid, lakini siyo kutulazimisha

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Shahidi Wakati Shahidi anataka Ushahidi Wake Jana Alitaja Hapa Kuhusu Microsoft na Celebrite, alitaja hizo Mbili Maana yake ameshataja

Jaji: Sasa Shahidi Kaja na suala la Security kwa hii Uliyotaja

Kiwhelo: Basi Ngoja Niendelee na Kingine, Shahidi Wakati Una Extract Data Kwenye Celebrite Ulihifadhi Kwenye nini

Shahidi: Nili hifadhi Kwenye Computer

Kiwhelo: Vipi kuhusiana na Usalama wa computer yenyewe

Shahidi: Kimya

Kiwhelo: Uliandika Taarifa ya Simu Nne..?

Shahidi: Simu zote Nane

Kiwhelo: Siku ya Tarehe 09 July 2020 Uliingia Saa ngapi

Shahidi: Niliingia Saa 1 na Nusu Asubuhi

Kiwhelo: na Ulitoka Muda gani

Shahidi: Unatoka Muda wowote, hupangiwi kwa Sababu tunafanya Kazi Masaa 24

Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji ulikuwa unaandika summary kisha unafuata extraction

Shahidi: Siyo sahihi

Kiwhelo: Soma hapo kwenye report yako

Shahidi: Inaanza na summary kisha extraction

Kiwhelo: Kwa hiyo imeanza na summary

Shahidi: Ni sawa, imeanza na Summary

Kiwhelo: Tuzungumze Kidogo Kuhusu Kampuni ya CELEBRITE Ukasema Kuwa Ni Moja ya Kampuni inayodevelop Software

Je unafahamu Celebrite Ni Kampuni Ya Kijasusi wa Kidigitali ya Nchi Israel

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kiwhelo: Je Unafahamu Kuwa Hiyo Kampuni inahusishwa na Unyanyasaji wa Waandishi Wa Habari na Wana Harakati Duniani

Shahidi: Sifahamu

Kiwhelo: na Je Unafahamu Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa.?

Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa

Kiwhelo: Je Nitakuwa Sahihi Nikisema Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa na Kubadili Taarifa Zilizotamgukia na zilizopo

Shahidi: Hapana Siyo Sahihi

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba nimkabidhi Shahidi Nyaraka asome Kuhusiana na Celebrite

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba wakili azuiwe Kusoma hiyo Nyaraka

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Kwa ajili ya Muda nitaomba Kuachana na hiyo

Naomba nipatiwe P23 na P35

Naomba Sasa Nimkabidhi Shahidi

Kiwhelo: naomba Unisomee description hapo Juu

Shahidi: Imeanza Neno Station, Date 05 August 2020, CF imeandikwa. Simu Imeandikwa Tecno IMEI imefutika, Ilipatikana Maungoni (Mwilini)

Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Wewe Umetoa wapi Namba kwa Mujibu wa IMEI namba ambayo Imefutika

Shahidi: Inawezekana Physically Isionekane ila akuna Namna unaweza Kuona, au Kwenye Barua

Kiwhelo: hiyo Barua Ipo Hapa Mahakamani

Shahidi: Haipo Mahakamani

Kiwhelo: Ulizungumzia Kuwa IMEI namba ulitoa Kwenye Barua.?

Shahidi: Nili zungumza Kwa Ujumla

Adv. @FrederickWakili
: Mheshimiwa Jaji nimeishia hapo na naomba kurudisha vielelezo

Anasimama Wakili Msomi Peter Kibatala.

Kibatala: Inspector Ndowo Mambo Vipi

Shahidi: Salama

Kibatala: Siku ya Kwanza Uliomba Kusitisha Ushahidi Kwa sababu uliumwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: na Ulipitia Hospitali.?

Shahidi: Nilienda Ofisini, nikarudisha Vielelezo

Kibatala: Kwa hiyo Baada ya Kutoka Hapa Hukwenda Hospitali Moja kwa Moja

Shahidi: Si kwenda Hospitali Moja Kwa Moja

Kibatala: Ulisema Kichwa Kilikuwa Kinafanya nini Vile

Shahidi: Kilikuwa Kinaniuma Kadri nilivyokuwa natoa Ushahidi

Kibatala: Na Kwa hiyo Ofisi Yako Ilikuwa wapi Vile

Shahidi: Posta

Kibatala: na Baada ya Hapo Ukaenda Hospitali Wapi

Shahidi: Kilwa Road

Kibatala: Twende Kwingine, Shahidi Je Uliwahi Kufanyiwa Training na Watu wa CELEBRITE

Shahidi: Yes Wawakilishi Wao

Kibatala: Unakumbuka Kozi Mbalimbali Ulizo taja Siku ya Kwanza Ukiwa unataja Mafunzo mbalimbali uliyopata.

Kibatala: Je kwa Kumbukumbu yako Ulitaja Mafunzo Yaliyo endeshwa na Celebrite au Wawakilishi wao

Shahidi: Jibu Lina hitaji Maelezo, Nilitaja Kozi Mbalimbali na Baadhi walitoka Nairobi.

Kibatala: Maelezo Ambayo Umeyatoa, Kuna Mahali Umesema Kuna watu Walitoka Nairobi Kuja Kuku train Kuhusu Celebrite.%?

Shahidi: Nilipata Kozi Mbalimbali, sikudadavua

Jaji: Swali Lake Ulisema Kuwa Kuna Wataalamu Kutoka Nairobi Kuja Kuku Fundisha Kuhusiana na Celebrite.

Shahidi: Sikutaja Mheshimiwa

Kibatala: Katika Maelezo yako, Ulisema Ulienda Training Mahala Mbalimbali, Je Ulisema Kuwa ulienda Israeli.?

Shahidi: Israel Sikutaja

Kibatala: Unafahamu Kuwa Makao Makuu ya CELEBRITE Yapo Nchini Israel

Shahidi: Nafahamu Yapo Israel

Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Israel Kwa Wivu na Technology yao Hawaja Outsource kwa Mtu Kuhusiana na Training wala Technology?

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kibatala: Unafahamu Kuwa Nairobi Hakuna Wakala Wa CELEBRITE?

Shahidi: Hapana Sifahamu

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Misamiati Migumu ya Technology shahidi anaweza asijue ni nini Kinaongelewa.

Kibatala: Mheshimiwa Jaji hakuna hoja hapo, Mbona shahidi anajibu, Eti ndugu shahidi, ni kweli huelewi Kitu?

Shahidi: Ndiyo sielewi

Kibatala Kwanini sasa ulikuwa unajibu?

Shahidi wa Jamhuri: Kimya

Kibatala: unafahamu sababu ya Wivu Wa Technology, Israel Hawana Mwakilishi wa CELEBRITE Duniani katika Nchi yoyote

Shahidi: Yupo Nairobi

Kibatala: Anaitwa Nani

Shahidi: SAM

Kibatala: Unafahamu Kuwa Technology ya Pegasus ni Technology ya Israel Pia

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kibatala: una Cornfirm kwetu bila kwenda kwenye details kuwa Jeshi la Polisi mnatumia pegasus?

Shahidi: Naomba nisijibu hilo swali kwa sababu za Kiusalama

Kibatala: Baadae Nitakuja hapo na nitakutaka kwa lazima ujibu hilo swali, kwa sasa ngoja niende kwingine.

Kibatala: Ni sahihi Kwamba Celebrite unatumia Software Mbili UFET na physical analyser?

Shahidi: Ndiyo ni baadhi ya product za kwake

Kibatala: UFEN kazi yake I naingia katika Simu au Computer kisha Inatengeneza Back up

Shahidi: Inategemea na level ya Extraction Unayofanya

Kibatala: Ni sahihi Kuwa katika kazi Uliyo kuwa unafanya unaunganisha Simu Kwa Kutumia Cable kisha Celebrite inachofanya Kwa kutumia UFEN Kutengeneza Back up

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Ni sahihi Kuwa physical analyser Inafanya kazi Kwa Ku arrange Taarifa In Chronological Order

Shahidi: Sahihi ila inategemea Level

Kibatala: Jaji akimaliza Ku Rekodi Mwambie Kuwa Kazi ya Physical Analyser Kama Software Ni kuyapanga Mafaili Kwa Mchunguzi ili Ku Make Sense na hiyo Process inaitwa PASSING

Shahidi: Naomba nijibu kwa Maelezo Kuwa Physical analyser, Inafanya kazi 3 ila Kwa Ujumla Ndiyo PASSING

Kibatala: Katika Report Yako Kuna Item Ya PASSING

Shahidi: Kama Software Include hizo Taarifa zake, Basi itaonekana

Kibatala: Basically Physical analyser haina Jipya Zaidi ya kupanga Mafaili

Shahidi: Hapana Physical analyser ni zaidi ya hapo

Kibatala: Tofauti Yake nini, Kama Unaingia Kwenye simu yangu ya Telegram na kisha unapamga Mafaili

Shahidi: Ni zaidi ya hapo kwa sababu ina Uwezo Kuwa Kufanya Back Up Kwa Vitu Vilivyofutwa

Kibatala: Physical ANALYSER inaweza za KubadiliSha Chochote

Shahidi: Hapana

Kibatala Physical analyser Ina extract

Shahidi: Hapana

Kibatala: unapokuwa na Kifaa kama Simu Kutoka Kwa DCI Nini Kilianza Kati ya kutumia UFEN Kufanya Extraction au Physical Analyser Kupamga kazi yako

Shahidi: Nilianza Kutumia UFEN

Kibatala: Wewe Umeletewa 8 applications phones, Je zile Data zilizokuwa katika Hizo phones, Je ni Software gani zilikuwezesha Kuingia Kwenye simu na Kusoma Meseji

Shahidi: Ni Physical analyser

Kibatala: Sasa Mbona Mwanzo Ulikataa, Wacha sasa Ikae Hivyo

Kibatala: Jana Ulizungumzia Kuwa huwezi Ku impose Vitu Vyako Kutoka Nje,

Shahidi: Ndiyo WRITE BLOCK

Kibatala: Unafahamu Kuhusu Software ya CELEBRITE Kuhusu Soft Write Block?

Shahidi: Hiyo sifahamu kwa kweli

Kibatala: Ni kweli au siyo Kweli Kuwa Celebrite Soft Write Block Ndiyo inayomzuia Mtu Kuingilia Mashine ya CELEBRITE

Shahidi: Hiyo sifahamu

Shahidi: Na Bado Ukitaka Kutuaminisha Kuwa Mashine zenu zina Intergrity?

Shahidi: Ndiyo Sijataja

Kibatala: Je ulitaja Jana software zaidi ya Mbili

Shahidi: Sikutaja

Kibatala: Ulizungumzia Forensic Cables,

Shahidi: Sawasawa

Kibatala: Ni Cables kama za USB tuh au Kuna tofauti

Shahidi: Ni Tofauti Kabisa

Kibatala: Inasifa gani Kitaalamu ambayo ni zaidi za USB

Shahidi: Ni Cable Zenye namba pembeni

Kibatala: Je Hapa Umetaja Namba za Cables

Shahidi: Hapana

Kibatala: Hizi Simu ambazo wewe Ulifanyia Extraction, Makers ni Tofauti

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Jana Nilisikia Unasema wewe siyo Mpelelezi ni Mchunguzi?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ni wapi au Kwenye Instrument ipi Inatofautisha Mpelelezi na Mchunguzi?

Shahidi: Ukija Ofisini Utajua

Kibatala: Mpaka Nije Ofisini kwenu, Vipi PGO Inatambua?

Shahidi: Sijui

Kibatala: PGO ya 8 Sehemu Ndogo ya 4 inasema Kuwa Ofisi Ya DCI inagawanywa katika Divisheni Nne, Mmoja wapo ndiyo hiyo ya Forensic Beaural

Shahidi: Sijui ni PGO gani

Kibatala: zote mbili

Shahidi: Mimi ninachojua Forensic Beaural ni Imtependent Beaural

Kibatala: na Ndiyo Maana ni Kuuliza Unapata wapi Mgawanyo huo

Shahidi: Ukienda Ofisini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi au Dodoma

Kibatala: Mhe Jaji naomba Kielelezo 6,7,

Kibatala: angalia Maneno ya DCI Katika hiyo Barua. Unafahamu Kirefu chake?

Shahidi: nimesahau kidogo

Kibatala: Mimi nikikwambia kwamba kirefu cha hayo maneno uliyoandika wewe kwenye barua yako ni DIRECTOR OF CRIMINAL INVESTIGATION?

Shahidi: Sijui mpaka Nipate Mwongozo Wa Wakubwa zangu

Kibatala: Juu pia maneno ya DFSI kuwa ni DIRECTORATE OF FORENSIC SCIENCE INVESTIGATION?

Shahidi: Sifahamu mpaka Nikumbushwe na wakubwa zangu

Kibatala: Na Bado wewe Unasema ni inspector wa Jeshi la polisi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala Mheshimiwa Jaji muda wetu wa kupumzika umefika, labda nipate mawazo kutoka kwa wenzetu nina maswali mengi bado

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tu' break dakika 45

Wakili Peter Kibatala Saa Saba na Dakika 45

Jaji: Tuna break kwa dakika 45 tutarudi saa saba na dakika 45
Shahidi anajibu swali halafu anasema halielewi swali alilojibu!
 
Salaam Wakuu,

Leo tarehe 10/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHEDEMA Freeman Mbowe inaendelea.

Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
=======


Kufahamu ilipoishia, soma hapa:Yaliyojiri mahakamani kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Kesi imeahirishwa hadi 19/01/2022

Jaji ameingia, kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa.

Jaji: Shahidi Nakukumbusha Upo Chini ya Kiapo Bado na Wakili wa Mshtakiwa Namba Mbili Ilikuwa Unaendelea, Karibu

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba nikumbushwe niliishia wapi

Jaji: Uliishia Wakati anakusomea Kielelezo H



Mallya: Shahidi tusomee hii ni Tarehe

Shahidi: Imeandikwa 05 August 2020

Mallya: Kuna Entry imeandikwa Owner of Article, Kwenye PF Je imeandikwa Jina gani?

Shahidi: Nashindwa Kusemea Sana Mheshimiwa Jaji sababu Siyo Mimi Niliyeandaa

Jaji: Hujaambiwa Uisemee Umeambiwa Usome

Shahidi: Imeandikwa Mohammed Abdallah Ling'wenya.. Lakini sijaandaa mimi

Mallya: Kwa Hiyo nani kaleta Mahakamani

Shahidi: Ni Mimi

Mallya: Kwa hiyo tuiondoe Mahakamani?

Shahidi: Hapana

MALLYA: Soma Sasa

Shahidi: Mwisho Imeandikwa DOYI

Mallya: Kutoka Tarehe 05 August 2020 Mpaka Tarehe Uliyo letewa Kwenye Ofisi yako Kuna Interval ya Siku Ngapi

Shahidi: Kuna Interval Ya Siku 08

Mallya: Na wewe Ulifanyia Kazi Tarehe Ngapi

Shahidi: Mwezi Wa July 2021

Mallya: Tarehe Ngapi

Shahidi: Sikumbuki Tarehe

Mallya: Kutoka Muda Umeletewa Mpaka Unafanya Uchunguzi Kuna Muda gani

Shahidi: Angalau Miezi 10

Mallya: aliyekuletea hiyo Item "H" alikwambia alikamata katika Physical Condition gani

Shahidi: Hakuniambia

Mallya: Alikwambia alikuwa Amehifadhi Siku gani

Shahidi: Hakuniambia

Mallya: alikwambia Kwamba aliondoa au Kutumbukiza Physically Kitu gani

Shahidi: Hakuna Kitu kama hicho Unachosema, kuwa alitoa chochote, Utaratibu Wa Kutunza Kielelezo Unajulikana, Kwa Utaratibu Wa Polisi Kielelezo Umapo Ki Seize unapaswa Umantain Kilivyo

Mallya: aliyekuletea alikwambia alifuata Utaratibu au Haku fuata Utaratibu huo

Shahidi: Ni Askari Polisi ni Imani yangu alifuata

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu Swali Langu

Shahidi: Mheshimiwa Jaji swali linahitaji Maelezo,

Jaji: Nani sasa, Maelezo ya Wakili au Ya Kwako?

Shahidi: Mimi Naamini Kuwa Utaratibu ulifuatwa

Jaji: Swali lake Halipo Huko kama Utaratibu ulifuatwa au Lah Bali Je alikueleza

Shahidi: Mheshimiwa Jaji hakunieleza

Mallya: Ndiyo Jibu ndiyo Nilikuwa nayafuata

Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Physical Damage inaonekana hapa, Kuna gaps, Je Macho yangu ya naona sawasawa

Shahidi: Condition Siwezi Kuzungumzia hapa

Mallya: Hilo Sijakuuliza, Nauliza Kuna Damage hapa Inaonekana, Je Kinachoonekana ni nini

Shahidi: Kinachoonekana ni Simu

Mallya: Siulizi simu hapa Mahakamani, usilete mahakamani michezo yako..

Mallya: Unachokiona ni Kitu gani

Shahidi: Ninachokiona ni Simu Mheshimiwa Jaji

Mallya: Ngoja Nichukue Simu F tulinganishe na H, Zote Umeleta Wewe, Swali langu hii yenye haya Ma gaps unahitaji?

Shahidi: Mhe Jaji Hizi ni simu Mbili tofauti, Siyo lazima zifanane..

Wakili wa Serikali: Mhe Jaji Wakili amebakia Muda Mrefu na Majibu yameshatolewa, Swali lake limeshajibiwa

Mallya: Mheshimiwa Jaji Swali langu halijajibiwa bado

Jaji: Muulize swali tena

Mallya: Kwenye Kielelezo H Kuna Ma' gaps, Je kitaalamu Unayaitaje?

Shahidi: Miye siwezi Kuongelea chochote

Mallya: Hii difference ya Kuwa hii ina button Kwenye simu na hii haina, unasemaje?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji siwezi Kuzungumzia kuhusu tofauti

Mallya: Kwenye Riport yako Kwenye Kielelezo F Je aina Positive Results..?

Shahidi: Ndiyo Ilikuwa na Positive Results

Mallya: Kuna Simu Ulizo letewa ukakuta Hazina Positive Results Kama Ulivyoletewa kwenye Terms of reference

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Kwa Mujibu wa Sheria Askari Polisi anaruhusiwa Kukamata simu.?

Shahidi: ndiyo Kwa Mujibu wa Sheria

Mallya: Kama Askari Polisi anataka Kujiridhisha Juu ya Kitu anachotafuta analeta Forensic?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Unafahamu Simu ni Personal Property ya Mtu?

Shahidi: Inaweza Kuwa Simu ya Ofisi

Mallya: Yapo Mazingira Mtu anaweza Kuwa na Simu Kama Mali yake Binafsi.?

Shahidi: Kama amenunua ni Mali yake Binafsi

Mallya: Je Yule ambaye amekamata kama Hajakuta Kitu anatakiwa kumrudishia Simu yake..?

Shahidi: Sifahamu

Mallya: Unafahamu Kwenye Simu ya Mtu Binafsi ambayo kanunua Kwa Pesa Yake, Inaweza Kuwa na Taarifa zake Binafsi?

Shahidi: Simu ya Mtu anaweza Kuweka Taarifa ambazo anahisi anaweza Kuhifadhi

Mallya: Kuna uwezekano Kuwa Mtu akahifadhi Taarifa au Nyaraka ya Utetezi kwenye Simu?

Shahidi: Sifahamu

Mallya: Taarifa Uliyompelekea huyo aliyekuomba Umfanyie Uchunguzi, Je akipokea Kwa Mkono au Kwa Email?

Shahidi akipokea Kwa Mkono

Mallya: Je alisoma hiyo Taarifa Yako ya Uchunguzi

Shahidi: Naamini alisoma

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 23 Samahani

Mallya: Shahidi Interest yangu Katika Riport Yako ni Ukurasa Wa Sita Unapozumgumzia Kuhusu Kielelezo A, B, C, D

Shahidi: Vielelezo Tajwa A, B, C, D hazina Taarifa Zenye Maudhui

Mallya: Kwenye Hicho Kielelezo namba C ulikuta ni Cha Nani

Shahidi: Ni Cha Khalfani Bwire

Mallya: Kwa hiyo Katika simu ya Khalfani Bwire hukukuta Jambo Lolote?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Ulifanya Uchunguzi Wako Lini

Shahidi: July 2021

Mallya: Ulikuja Kutoa Ushahidi wako lini

Shahidi: Juzi January 2022

Mallya: Kuna Interval ya Muda gani kati ya Wewe Kufanyia Uchunguzi Mpaka Kutoa Ushahidi

Shahidi: Usio Pungia Miezi Mitano

Mallya: Hiyo Content ambayo ulikuta negative Results upo wapi

Shahidi: Sikuona Haja ya Kuweka Kwa sababu sikukuta Kitu

Mallya: Bwana Bwire alikuwa anataka Negative Results ambayo Ingekuja Mahakamani Kuonyesha Kuwa Hakuna Maswala ya Ugaidi

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Nilipewa Terms of Reference, Kwa Hiyo Kama Haipo siwezi Kutoa

Mallya: Shahidi Umesha wahi Kupima Malaria

Shahidi: Hilo swali Limeingiaje hapa

Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory?

Shahidi: Sioni likihusiana

Mallya: Kwa Sababu Wewe ni Mtu wa Laboratory na Malaria inapimwa Laboratory

Shahidi: Sioni likihusiana

Mallya: Lina husiana Kwa Sababu Malaria Ukipimwa Wakikuta Negative Results wanakupa Majibu Yako

Shahidi: Kuna Baadhi ya Simu Zina Taarifa zaidi ya GB 20 huwezi Ku Print zote

Mallya: Je ulitoa taarifa Kwamba hukukuta kwa sababu ni Kubwa

Shahidi: Kwa sababu ni Out of Context

Mallya: Ulishajibu Kuwa Hukuona Haja

Shahidi: Siku Jibu hivyo

Jaji: Hapo Ndipo Mr. Malya Unapotuchanganya, Ni wapi Tutaona Huku uliza

Mallya: Nilikuwa namkumbusha Majibu Yake

Jaji: Basi Kama Unaulizwa Swali Hakuna Haja ya Kuongea Yote hayo

Mallya: Shahidi Nilisikia Unasema Mnatumia Legitimate Software Ku Updates yenu, Je Ulizungumzia Mnapewaje

Shahidi: Hapana Sikuzungumzia

Mallya: Mheshimiwa Jaji Naomba Barua ya Airtel na Ya Tigo

Mallya: Nakuonyesha Kielelezo P15 na Interest yangu ni Mtu aliyepewa hii Barua

Shahidi: Barua hii Imeelekezwa Kwa Kamishina wa Uchunguzi wa Kisayansi

Mallya: wewe sasa hivi ni Inspector Wa Polisi, Je Mwaka 2021 uliwahi Kuwa Kamishina wa Polisi

Shahidi: Mimi Sijawahi Kuwa Kamishina

Mallya: Kwenye hii Barua wapi Umekuwa Adressed.?

Shahidi: imekuwa Adressed Kwa Kamishina wa Uchunguzi Wa Kisayansi

Mallya: Naomba na ya Tigo

Mallya: Umesema Ofisini Kwenu Mkubwa wa Command ni Nani

Shahidi: Anaitwa CP SHABANI

Mallya: Kuna Departments Ngapi katika Forensic Beaural

Shahidi: Tuna Units Mbalimbali Ka Cyber crime ambayo Natoka Mimi, Toxicology, DNA, Pathology, Fingerprints, Ballistic, Documents, Crime scenes

Mallya: Kwa Mahesabu yangu ni Nane, Kwa Kiswahili zinaitwaje?

Shahidi: Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi

Mallya: Zote hizi Ukubwa Wake Kwa Maana ya Commanding Ofisa wake ni CP SHABANI.?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Naomba uniseme Adress ambayo Tigo Wameitumia

Shahidi: UCHUNGUZI WA KISAYANSI
S. L. P 9094
DAR ES SALAAM
TANZANIA

Malya: naomba Mwenzangu Wakili Faraji Mangula aendelee

Mangula: Shahidi Pole na kuuguq Kichwa Siku ya Kwanza

Mangula: Ni sahihi ulisema Kuwa umesema Advanced Diploma ya Computer Science

Shahidi: Ndiyo

Mangula: Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali, Ulielezea Kuwa Baada ya Masomo Ulipata Award gani

Shahidi: Nilisema nilikuwa napata Certificate

Mangula: Wakati Unafanya Uchunguzi Ulisema Ulikuwa una cheo Gani

Shahidi: Mkaguzi Msaidizi

Mangula: kwa sasa Una cheo Gani

Shahidi: Inspector

Mangula: Wakati Mawakili Wanakuongoza Hapa Mahakamani, Je ulisema Kuwa Ulipata Mafunzo gani Mpaka Ukapanda Cheo

Shahidi: Unakuwa Awarded siyo Kwa Kwenda Kozi

Mangula: Cheo chako umekipata wakati awamu ya 5 au ya 6?

Shahidi: Sijaelewa logic ya swali lako

Jaji: Swali la nani alikuwa Rais, unataka kujenga nini

Mangula: Mhe Jaji kuna premise nataka kutengeneza

Jaji: hiyo premises ndiyo utengeneze kupitia Rais aliye madarakani?

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mahakama Ilisha wahi Kutoa Maelekezo Juu ya Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani

Jaji: nilitoa Maelezo Kuhusiana na Kutaja Majina ya Watu ambao Hawapo Mahakamani, lakini pia nataka Kujiuliza Kuhusu Kuuliza Maswali ya Rais wa Awamu ya Tano au Lah

Sasa Unachotaka hapo ni nini.?

Mangula: Ngoja Niulize Kwa Namna Nyingine

Mangula Naomba Kielelezo Namba 23,Shahidi Naomba Usome Kwa Sauti Kichwa Cha Habari cha Hicho Kielelezo

Shahidi Kamisheni ya Uchunguzi Wa Kisayansi, ya Makosa ya Kimtandao Chini ya Sheria ya Mtandao namba 14

Mangula: Je ni kifungu Kipi ambacho umekitumia?

Shahidi: Mimi siyo Mtaalamu wa sheria, Ila nilifanya kwa sheria ya mtandao

Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji sasa ni kifungu kipi ulitumia

Shahidi: Mheshimiwa sikutumia kifungu

Mangula: Nikikupa hiyo sheria, unaweza Kunitajia kifungu ulichotumia

Shahidi: Mimi sina UFAHAMU WA MAMBO YA KISHERIA

Mangula: Kwa hiyo nyie Ofisini kwenye mnafanya bila ufahamu wa Sheria

Shahidi: Nishasema mheshimiwa SINA UFAHAMU WA SHERIA

Mangula: Fungua sasa Ndani, Ieleze Mahakama ni Kielelezo Kipi Ulichofanyia Kazi Ukagundua Kuna Makosa ya Ugaidi Uliyaona, Ni wapi Umeandika hivyo..

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Jibu linahitaji Maelezo, Mimi nililetewa tu Kufanya Uchunguzi.

Mangula: Kwa hiyo wewe hujui Kuwa Kuna Ugaidi au Hakuna Ugaidi kwenye hicho Kielelezo?

Shahidi: Sahihi

Mangula: bado unataka Mahakama ichukue Kielelezo Hiki Kama Kielelezo Cha Umuhimu?

Shahidi: Nimesema ni Kazi ya Mpelelezi

Mangula: Umesomeshwa na Serikali?

Shahidi: Ni Sahihi

Mangula: Na Umelipiwa Masomo Kwa Kodi ya Watanzania

Shahidi: Sahihi

Mangula: wewe Umesomea Udukuzi

Shahidi: Nimesomea Ethical Hacking

Mangula: Ulisema Mwanzo Kuwa Vifaa Vyako Vya Uchunguzi Vina Uadilifu

Shahidi: Ndiyo

Mangula: Na Kila Unachotaka Kwenye hiyo Simu, Mambo wako Unakuonyesha

Shahidi: Yes

Mangula: Kama Kuna video inakuomyesha.?

Shahidi: Inaonyesha Vile Vitu ambavyo Inaweza Ku Extract Kwenye Kielelezo

Mangula: Inakupa kila Kitu ambacho Kipo Kwenye simu?

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Mangula: Mheshimiwa Jaji Naomba Extraction Report

Mangula: Katika huo Mambo unaosema Ulikuwa upo Sawa Kukupa Kila Kitu, Ukisoma Kielelezo Cha Kwanza hicho namba 25

Mwambie Mheshimiwa Jaji kwenye hicho Kifaa Ulichofanyia Uchunguzi Kulikuwa na Content gani

Shahidi: Kukikuwa na Proxy Ya Chat ya WhatsApp

Mangula: Kulikuwa na Picha Kwa Maana Images

Shahidi: Picha Hakuna, Zipo Profile Picture

Mangula: ambazo ni za nani

Shahidi: Sijui za nani

Mangula: Katika hivyo Vielelezo ambavyo Vimepokelewa Mahakamani, Palikuwa na Mazungmzo ya Simu kati ya Watuhumiwa

Shahidi: Hakuna ila kwenye Kielelezo namba 26 zipo

Mangula: apewe Namba 26,,tuchagulie Mazungmzo Marefu Kuliko yote

Shahidi: Kuna Mazungmzo ya Dakika 9

Mangula: Bila Shaka Ndipo walikuwa wanapanga Ugaidi, Haya Mwambie Mheshimiwa Jaji Walizungumza nini hawa Watuhumiwa

Shahidi: Kuna Call Logs tu

Mangula: zile Sauti zipo wapi

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Kama Mahakama Yako itaniruhusu Kwa sababu za Ki Usalama nisijibu Hilo swali

Mangula: Swali langu ni Juu ya Watuhumiwa Ukiwa Mchunguzi wa Hizo Simu, Nauliza Mazungmzo ya Watuhumiwa Wale Wanne, Narudia Swali Sauti zao Watuhumiwa Zipo wapi ndugu shahidi?

Shahidi: Sababu za Kiusalama huwezi Kuzungumzia suala la Sauti

Mangula: Shahidi Nimesikia unasema Kuwa huwezi Kuzungumzia Kwa sababu ya Kiusalama, Je Sheria gani inakuzuia Usizungumzie hilo Suala?

Shahidi: Sijataja Sheria

Mangula: haya Sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji, Sauti za Watuhumiwa Zipo wapi????

Shahidi: Mheshimiwa Jaji Hazikuwa zinahitajika katika Terms Of Reference

Mangula: Ni sahihi nikisema Kuwa Katika Extraction Uliyo fanya, Kuna Vitu Uliviondoa sababu hazikuhitajika?

Shahidi: Swali linahitaji Maelezo, Mwanzoni Nilisema Kuwa Tunafanya Kwa Hatua tatu, Aquisation, Analysis na Extraction

Mangula: Kwa hiyo ni sahihi Kuwa Kwenye Mtambo Kuna Baadhi Ya Taarifa Hukutoa Sababu Hazikuhitajika?

Shahidi Wa Jamhuri: Kimya

Mangula: Kwa Mujibu Wa Kielelezo Namba 22, Mwambie Mheshimiwa Jaji Vitu gani Viliombwa Kwa ajili ya kufanyia Uchunguzi

Shahidi: Kwa Mujibu wa Barua yako Yenye Reference........

Mangula: Hoja ya Barua Ilikuwa unahitaji Ufanyie nini

Shahidi: Pamoja na Taarifa Hii Nakuletea Uchunguzi Niliofanya .... Mimi Inspector Innocent Ndowo

Mangula: Ni wapi Walikutaka Wewe Usitoe Sauti za Watuhumiwa?

Shahidi: Mimi nilifuata Terms of reference

Mangula: Nikisema Kuwa Wewe Inspector Ndowo na Viongozi Wako wa Polisi Kwa Makusudi Mliamua kuficha Baadhi ya Taarifa katika
Kesi hii kwa Maslahi yenu Itakuwa sahihi au siyo Sahihi Ukizingatia Kuna Taarifa Hazipo hapa?

Shahidi: Siyo Sahihi, Hatufanyi Kazi kwa interest zetu

Mangula: Fungua Kielelezo H, na Umwambie Mheshimiwa Jaji IMEI namba ya hicho Kielelezo Ni namba Ngapi Kwa Mujibu wa PF 145

Shahidi: Kwa Mujibu wa PF Hakuna IMEI namba

Mangula: Soma huo Mstari Wa Pili Kwa Sauti Umeandikwaje

Shahidi: Simu TECNO IMEI imefutika

Mangula: Wakati Unaongozwa Kwenye Ushahidi Ulisema nani aliyefuta hizo IMEI namba

Shahidi: Si Kuulizwa hilo swali

Mangula: Wewe unafahamu aliye futa hiyo IMEI namba

Shahidi: Simfahamu

Mangula: Katika hicho Kikaratasi Umeeleza IMEI namba Imefutwa Wapi.?

Shahidi: Sikusema

Mangula: ukiacha Kielelezo namba 35 ambacho kimechezewa na Watu wasiojulikana , Ni Kielelezo Kipi Kingine Mlichochezea

Shahidi: Hakuna Kielelezo Kilichochezewa

Mangula: Fungua Kielelezo namba 23, Mheshimiwa Jaji Namuonyesha Kielelezo namba 23

Mangula: Nataka Majibu ya Riport Yako ya Uchunguzi

Mangula: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi Katika Report Yako ya Uchunguzi Umeandika IMEI namba Imefutika

Shahidi: Hakuna Mahala Nilipo andika

Mangula: Nilisikia Unasema Ulichukua simu Ukiweka Katika Mtambo Wa Uchunguzi, Ule Mtambo utakuonyesha Kuwa Simu ni Original au Feki

Shahidi: Mtambo hauonyeshi Kuwa Simu ni Feki au Original

Mangula: Kitu gani Kinaonyesha kuwa Simu ni Feki au Original

Shahidi: Kitu nilichosema Kuna Kama zile Simu za Kichina, Mtambo una Operate kwa OS

Mangula: Kwa hiyo nini Kina onyesha ni FEKI Au ORIGINAL?

Shahidi: Nilichosema naomba Unisikie Vizuri, Mtambo una Option ya Kufanya Kazi hata Kwa kutumia Chip

Mangula: Mheshimiwa Jaji naomba NIISHIE Hapo

Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji NAOMBA KWENDA WASHROOM (CHOONI)....

Shahidi anatoka na kuelekea katika vyoo vya nje..

Mahakama Ipo kimya inasubiri arejee kizimbani.

Shahidi amerejea kizimbani kutokea kwa fasii ya chooni.

Kihwelo: Shahidi Nilisikia Unazungumzia Kuhusu Celebrite Physical analyser Je ni Software Au.?

Shahidi: Ni software

Kiwhelo: nani alifanya Development ya Software

Shahidi: Celebrite Wenyewe

Kiwhelo: Nilisikia Umesomea Kuhusu Penetration Test

Shahidi: Ndiyo

Kihwelo: Je Penetration Testing, Ni sawa na Fazzing

Shahidi: Sifahamu

Kiwhelo: Je Wakati Unafundishwa Kuhusu Penetration Testing, Walikufundisha Kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao (High Tech Cyber Attack)

Shahidi: Sijafundishwa hiyo

Kiwhelo: kwakuwa Ujafundisshwa kuhusu Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao, Ni sahihi Celebrite Ingeweza Kuingiliwa

Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa

Kiwhelo: pale Ofisini kwenu ni nani Network Provider

shahidi: ni TTCL

Kiwhelo: Ni sahihi Kuwa Network Services Provider anaweza Kuingilia Data Zako

Shahidi: Hawezi

Kiwhelo: Nyinyi Kama Jeshi la Polisi Mnatumia Nini Kujilinda na Mashambulizi ya Hali ya Juu ya Kimtandao

Shahidi: Naomba nisijibu sababu za Kimtandao

Kiwhelo: Nilisikia Kuwa unazungumzia kuhusu DECORDING

Shahidi: Ndiyo

Kiwhelo: Shahidi Pegasus Technology ni Moja ya Technology mnayotumia?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji naomba Nisijibu Sababu za Kiusalama

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba anijibu sababu Baadae Nitataka kujua Intergrity ya Technology Wanayotumia

Jaji: Shahidi ame raise suala la Security, Au mnasemaje Upande wa Serikali?

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi amesha Sema kuwa awezi Kusema Sababu za Kiusalama, Sisi tunaona Sababu hizo ni Valid, lakini siyo kutulazimisha

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Shahidi Wakati Shahidi anataka Ushahidi Wake Jana Alitaja Hapa Kuhusu Microsoft na Celebrite, alitaja hizo Mbili Maana yake ameshataja

Jaji: Sasa Shahidi Kaja na suala la Security kwa hii Uliyotaja

Kiwhelo: Basi Ngoja Niendelee na Kingine, Shahidi Wakati Una Extract Data Kwenye Celebrite Ulihifadhi Kwenye nini

Shahidi: Nili hifadhi Kwenye Computer

Kiwhelo: Vipi kuhusiana na Usalama wa computer yenyewe

Shahidi: Kimya

Kiwhelo: Uliandika Taarifa ya Simu Nne..?

Shahidi: Simu zote Nane

Kiwhelo: Siku ya Tarehe 09 July 2020 Uliingia Saa ngapi

Shahidi: Niliingia Saa 1 na Nusu Asubuhi

Kiwhelo: na Ulitoka Muda gani

Shahidi: Unatoka Muda wowote, hupangiwi kwa Sababu tunafanya Kazi Masaa 24

Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji ulikuwa unaandika summary kisha unafuata extraction

Shahidi: Siyo sahihi

Kiwhelo: Soma hapo kwenye report yako

Shahidi: Inaanza na summary kisha extraction

Kiwhelo: Kwa hiyo imeanza na summary

Shahidi: Ni sawa, imeanza na Summary

Kiwhelo: Tuzungumze Kidogo Kuhusu Kampuni ya CELEBRITE Ukasema Kuwa Ni Moja ya Kampuni inayodevelop Software

Je unafahamu Celebrite Ni Kampuni Ya Kijasusi wa Kidigitali ya Nchi Israel

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kiwhelo: Je Unafahamu Kuwa Hiyo Kampuni inahusishwa na Unyanyasaji wa Waandishi Wa Habari na Wana Harakati Duniani

Shahidi: Sifahamu

Kiwhelo: na Je Unafahamu Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa.?

Shahidi: Haiwezi Kuingiliwa

Kiwhelo: Je Nitakuwa Sahihi Nikisema Kuwa Celebrite Mashine Inaweza Kuingiliwa na Kubadili Taarifa Zilizotamgukia na zilizopo

Shahidi: Hapana Siyo Sahihi

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji naomba nimkabidhi Shahidi Nyaraka asome Kuhusiana na Celebrite

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba wakili azuiwe Kusoma hiyo Nyaraka

Kiwhelo: Mheshimiwa Jaji Kwa ajili ya Muda nitaomba Kuachana na hiyo

Naomba nipatiwe P23 na P35

Naomba Sasa Nimkabidhi Shahidi

Kiwhelo: naomba Unisomee description hapo Juu

Shahidi: Imeanza Neno Station, Date 05 August 2020, CF imeandikwa. Simu Imeandikwa Tecno IMEI imefutika, Ilipatikana Maungoni (Mwilini)

Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Wewe Umetoa wapi Namba kwa Mujibu wa IMEI namba ambayo Imefutika

Shahidi: Inawezekana Physically Isionekane ila akuna Namna unaweza Kuona, au Kwenye Barua

Kiwhelo: hiyo Barua Ipo Hapa Mahakamani

Shahidi: Haipo Mahakamani

Kiwhelo: Ulizungumzia Kuwa IMEI namba ulitoa Kwenye Barua.?

Shahidi: Nili zungumza Kwa Ujumla

Adv. @FrederickWakili
: Mheshimiwa Jaji nimeishia hapo na naomba kurudisha vielelezo

Anasimama Wakili Msomi Peter Kibatala.

Kibatala: Inspector Ndowo Mambo Vipi

Shahidi: Salama

Kibatala: Siku ya Kwanza Uliomba Kusitisha Ushahidi Kwa sababu uliumwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: na Ulipitia Hospitali.?

Shahidi: Nilienda Ofisini, nikarudisha Vielelezo

Kibatala: Kwa hiyo Baada ya Kutoka Hapa Hukwenda Hospitali Moja kwa Moja

Shahidi: Si kwenda Hospitali Moja Kwa Moja

Kibatala: Ulisema Kichwa Kilikuwa Kinafanya nini Vile

Shahidi: Kilikuwa Kinaniuma Kadri nilivyokuwa natoa Ushahidi

Kibatala: Na Kwa hiyo Ofisi Yako Ilikuwa wapi Vile

Shahidi: Posta

Kibatala: na Baada ya Hapo Ukaenda Hospitali Wapi

Shahidi: Kilwa Road

Kibatala: Twende Kwingine, Shahidi Je Uliwahi Kufanyiwa Training na Watu wa CELEBRITE

Shahidi: Yes Wawakilishi Wao

Kibatala: Unakumbuka Kozi Mbalimbali Ulizo taja Siku ya Kwanza Ukiwa unataja Mafunzo mbalimbali uliyopata.

Kibatala: Je kwa Kumbukumbu yako Ulitaja Mafunzo Yaliyo endeshwa na Celebrite au Wawakilishi wao

Shahidi: Jibu Lina hitaji Maelezo, Nilitaja Kozi Mbalimbali na Baadhi walitoka Nairobi.

Kibatala: Maelezo Ambayo Umeyatoa, Kuna Mahali Umesema Kuna watu Walitoka Nairobi Kuja Kuku train Kuhusu Celebrite.%?

Shahidi: Nilipata Kozi Mbalimbali, sikudadavua

Jaji: Swali Lake Ulisema Kuwa Kuna Wataalamu Kutoka Nairobi Kuja Kuku Fundisha Kuhusiana na Celebrite.

Shahidi: Sikutaja Mheshimiwa

Kibatala: Katika Maelezo yako, Ulisema Ulienda Training Mahala Mbalimbali, Je Ulisema Kuwa ulienda Israeli.?

Shahidi: Israel Sikutaja

Kibatala: Unafahamu Kuwa Makao Makuu ya CELEBRITE Yapo Nchini Israel

Shahidi: Nafahamu Yapo Israel

Kibatala: Je Unafahamu Kuwa Israel Kwa Wivu na Technology yao Hawaja Outsource kwa Mtu Kuhusiana na Training wala Technology?

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kibatala: Unafahamu Kuwa Nairobi Hakuna Wakala Wa CELEBRITE?

Shahidi: Hapana Sifahamu

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Misamiati Migumu ya Technology shahidi anaweza asijue ni nini Kinaongelewa.

Kibatala: Mheshimiwa Jaji hakuna hoja hapo, Mbona shahidi anajibu, Eti ndugu shahidi, ni kweli huelewi Kitu?

Shahidi: Ndiyo sielewi

Kibatala Kwanini sasa ulikuwa unajibu?

Shahidi wa Jamhuri: Kimya

Kibatala: unafahamu sababu ya Wivu Wa Technology, Israel Hawana Mwakilishi wa CELEBRITE Duniani katika Nchi yoyote

Shahidi: Yupo Nairobi

Kibatala: Anaitwa Nani

Shahidi: SAM

Kibatala: Unafahamu Kuwa Technology ya Pegasus ni Technology ya Israel Pia

Shahidi: Hapana Sifahamu

Kibatala: una Cornfirm kwetu bila kwenda kwenye details kuwa Jeshi la Polisi mnatumia pegasus?

Shahidi: Naomba nisijibu hilo swali kwa sababu za Kiusalama

Kibatala: Baadae Nitakuja hapo na nitakutaka kwa lazima ujibu hilo swali, kwa sasa ngoja niende kwingine.

Kibatala: Ni sahihi Kwamba Celebrite unatumia Software Mbili UFET na physical analyser?

Shahidi: Ndiyo ni baadhi ya product za kwake

Kibatala: UFEN kazi yake I naingia katika Simu au Computer kisha Inatengeneza Back up

Shahidi: Inategemea na level ya Extraction Unayofanya

Kibatala: Ni sahihi Kuwa katika kazi Uliyo kuwa unafanya unaunganisha Simu Kwa Kutumia Cable kisha Celebrite inachofanya Kwa kutumia UFEN Kutengeneza Back up

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Ni sahihi Kuwa physical analyser Inafanya kazi Kwa Ku arrange Taarifa In Chronological Order

Shahidi: Sahihi ila inategemea Level

Kibatala: Jaji akimaliza Ku Rekodi Mwambie Kuwa Kazi ya Physical Analyser Kama Software Ni kuyapanga Mafaili Kwa Mchunguzi ili Ku Make Sense na hiyo Process inaitwa PASSING

Shahidi: Naomba nijibu kwa Maelezo Kuwa Physical analyser, Inafanya kazi 3 ila Kwa Ujumla Ndiyo PASSING

Kibatala: Katika Report Yako Kuna Item Ya PASSING

Shahidi: Kama Software Include hizo Taarifa zake, Basi itaonekana

Kibatala: Basically Physical analyser haina Jipya Zaidi ya kupanga Mafaili

Shahidi: Hapana Physical analyser ni zaidi ya hapo

Kibatala: Tofauti Yake nini, Kama Unaingia Kwenye simu yangu ya Telegram na kisha unapamga Mafaili

Shahidi: Ni zaidi ya hapo kwa sababu ina Uwezo Kuwa Kufanya Back Up Kwa Vitu Vilivyofutwa

Kibatala: Physical ANALYSER inaweza za KubadiliSha Chochote

Shahidi: Hapana

Kibatala Physical analyser Ina extract

Shahidi: Hapana

Kibatala: unapokuwa na Kifaa kama Simu Kutoka Kwa DCI Nini Kilianza Kati ya kutumia UFEN Kufanya Extraction au Physical Analyser Kupamga kazi yako

Shahidi: Nilianza Kutumia UFEN

Kibatala: Wewe Umeletewa 8 applications phones, Je zile Data zilizokuwa katika Hizo phones, Je ni Software gani zilikuwezesha Kuingia Kwenye simu na Kusoma Meseji

Shahidi: Ni Physical analyser

Kibatala: Sasa Mbona Mwanzo Ulikataa, Wacha sasa Ikae Hivyo

Kibatala: Jana Ulizungumzia Kuwa huwezi Ku impose Vitu Vyako Kutoka Nje,

Shahidi: Ndiyo WRITE BLOCK

Kibatala: Unafahamu Kuhusu Software ya CELEBRITE Kuhusu Soft Write Block?

Shahidi: Hiyo sifahamu kwa kweli

Kibatala: Ni kweli au siyo Kweli Kuwa Celebrite Soft Write Block Ndiyo inayomzuia Mtu Kuingilia Mashine ya CELEBRITE

Shahidi: Hiyo sifahamu

Shahidi: Na Bado Ukitaka Kutuaminisha Kuwa Mashine zenu zina Intergrity?

Shahidi: Ndiyo Sijataja

Kibatala: Je ulitaja Jana software zaidi ya Mbili

Shahidi: Sikutaja

Kibatala: Ulizungumzia Forensic Cables,

Shahidi: Sawasawa

Kibatala: Ni Cables kama za USB tuh au Kuna tofauti

Shahidi: Ni Tofauti Kabisa

Kibatala: Inasifa gani Kitaalamu ambayo ni zaidi za USB

Shahidi: Ni Cable Zenye namba pembeni

Kibatala: Je Hapa Umetaja Namba za Cables

Shahidi: Hapana

Kibatala: Hizi Simu ambazo wewe Ulifanyia Extraction, Makers ni Tofauti

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Jana Nilisikia Unasema wewe siyo Mpelelezi ni Mchunguzi?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ni wapi au Kwenye Instrument ipi Inatofautisha Mpelelezi na Mchunguzi?

Shahidi: Ukija Ofisini Utajua

Kibatala: Mpaka Nije Ofisini kwenu, Vipi PGO Inatambua?

Shahidi: Sijui

Kibatala: PGO ya 8 Sehemu Ndogo ya 4 inasema Kuwa Ofisi Ya DCI inagawanywa katika Divisheni Nne, Mmoja wapo ndiyo hiyo ya Forensic Beaural

Shahidi: Sijui ni PGO gani

Kibatala: zote mbili

Shahidi: Mimi ninachojua Forensic Beaural ni Imtependent Beaural

Kibatala: na Ndiyo Maana ni Kuuliza Unapata wapi Mgawanyo huo

Shahidi: Ukienda Ofisini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi au Dodoma

Kibatala: Mhe Jaji naomba Kielelezo 6,7,

Kibatala: angalia Maneno ya DCI Katika hiyo Barua. Unafahamu Kirefu chake?

Shahidi: nimesahau kidogo

Kibatala: Mimi nikikwambia kwamba kirefu cha hayo maneno uliyoandika wewe kwenye barua yako ni DIRECTOR OF CRIMINAL INVESTIGATION?

Shahidi: Sijui mpaka Nipate Mwongozo Wa Wakubwa zangu

Kibatala: Juu pia maneno ya DFSI kuwa ni DIRECTORATE OF FORENSIC SCIENCE INVESTIGATION?

Shahidi: Sifahamu mpaka Nikumbushwe na wakubwa zangu

Kibatala: Na Bado wewe Unasema ni inspector wa Jeshi la polisi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala Mheshimiwa Jaji muda wetu wa kupumzika umefika, labda nipate mawazo kutoka kwa wenzetu nina maswali mengi bado

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tu' break dakika 45

Wakili Peter Kibatala Saa Saba na Dakika 45

Jaji: Tuna break kwa dakika 45 tutarudi saa saba na dakika 45
Shahidi anajibu swali halafu anasema halielewi swali alilojibu!
 
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Misamiati Migumu ya Technology shahidi anaweza asijue ni nini Kinaongelewa.

Kibatala: Mheshimiwa Jaji hakuna hoja hapo, Mbona shahidi anajibu, Eti ndugu shahidi, ni kweli huelewi Kitu?

Shahidi: Ndiyo sielewi

Kibatala Kwanini sasa ulikuwa unajibu?

Shahidi wa Jamhuri: Kimya

Shahidi haelewi kitu ndugu zangu,huyu kawekewa kikaratasi chooni sasa kila alidesa anakuta maswali ni tofauti,ndio maana anaomba kwenda chooni sana[emoji3]
 

Make Your Investigations Smarter, Faster and More Efficient​

Cellebrite's end-to-end Digital Intelligence Investigative Platform and Services are trusted by over 6,700 federal, state and local public safety agencies and enterprises in over 140 countries and is used in millions of cases each year.

Mbowe kapambana na serikali iliyojiandaa kiteknolojia
Tatizo hakuna kitu relevant walichokikuta zaidi ya mawasiliano ya kawaida!
 

Hongera Jeshi la polisi kwa kwenda na wakati wa kidigital- watu kama Mbowe wamesumbua sana nchi hii sasa wanashikwa kirahisi​

Accelerate Justice​

From the field to the lab and the courtroom… solve cases faster.

CELLEBRITE
Huoni aibu kuandika huu upuuzi?? Au hata huwahurumii Wazazi wako ambao waliacha kula wakakupeleka shule?
 
Ukichukua tahadhari kupita kiasi kwenye maneno unayoongea mahakamani Ni lazima uonekane hujui kitu (boya) hata Kama unajua na kuonekana huaminiki hata Kama ulipaswa uonekane unaaminika.
******
Kibatala: angalia Maneno ya DCI Katika hiyo Barua. Unafahamu Kirefu chake?

Shahidi: nimesahau kidogo

Kibatala: Mimi nikikwambia kwamba kirefu cha hayo maneno uliyoandika wewe kwenye barua yako ni DIRECTOR OF CRIMINAL INVESTIGATION?

Shahidi: Sijui mpaka Nipate Mwongozo Wa Wakubwa zangu

Kibatala: Juu pia maneno ya DFSI kuwa ni DIRECTORATE OF FORENSIC SCIENCE INVESTIGATION?

Shahidi: Sifahamu mpaka Nikumbushwe na wakubwa zangu

Kibatala: Na Bado wewe Unasema ni inspector wa Jeshi la polisi

Shahidi: Ndiyo
Shahidi ni VERY SMART. Kibatala asimchukulie poa. Maswali ya kipuuzi yanajibiwa kipuuzi. Ask Henry Ford alipokuwa akiwaguyuguza washtakiwa wake mahakamani.
 
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Wakili anataka Misamiati Migumu ya Technology shahidi anaweza asijue ni nini Kinaongelewa.

Kibatala: Mheshimiwa Jaji hakuna hoja hapo, Mbona shahidi anajibu, Eti ndugu shahidi, ni kweli huelewi Kitu?

Shahidi: Ndiyo sielewi

Kibatala Kwanini sasa ulikuwa unajibu?

Shahidi wa Jamhuri: Kimya

Shahidi haelewi kitu ndugu zangu,huyu kawekewa kikaratasi chooni sasa kila alidesa anakuta maswali ni tofauti,ndio maana anaomba kwenda chooni sana[emoji3]
Wakati mwingine mjinga unamjibu kijinga
Rejea Yesu na Pilato
Pilato- wewe ni mwana wa Mungu
Yesu- WEWE WASEMA
 
Shahidi ni VERY SMART. Kibatala asimchukulie poa. Maswali ya kipuuzi yanajibiwa kipuuzi. Ask Henry Ford alipokuwa akiwaguyuguza washtakiwa wake mahakamani.
Mkuu shida ya akina Kibatala wanadhani polisi kuna wajinga wajinga tu- safari hii imekula kwao
 
Sawa- mwisho wa siku ya leo jaji atasema hivi
Nairisha kesi mpaka kesho washitakiwa wote akiwemo Mbowe watarudi rumande ya Magereza
Unashangaa mbowe kurudishwa gerezani. Hushangai yule kibaka aliyepewa KISONGO???
Wewe na mashetani wenzio mkimsifia hapa
 
Back
Top Bottom