Ni Ijumaa tulivu.
Kama kawaida jiji la Arusha Kuna ubaridi asubuhi hii.Jiji likiwa katika hekaheka tangu Jana za Maandalizi ya mapokezi ya Mgombea Urais wa Chadema Tundu Lissu.
Kanda ya Kaskazini hususan Jiji la Arusha ni ngome Kuu ya Chadema na akitoa salaam za kunikaribisha jijini humo Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini Godbless Lema alisema mapokezi ya Mgombea wao wa Urais yatazidi Kanda nyingine zote alizokwishatembelea.
Tayari Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe akiongozana na Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu hapo Jana walimlaki Lissu maeneo ya mkoani Manyara tayari kuongozana naye kuingia Arusha leo.
He kweli jiji la Arusha litavunja rekodi leo? Tusubiri tuone.
Molemo Media imekwishawasili jijini Arusha kuwaletea moja kwa moja kitakachojiri katika mapokezi hayo ya kihistoria.
Karibuni...
Taarifa za hivi Punde
Ofisi za Chadema Kanda zachomwa Moto.
Kuna taarifa zilizotujia hivi Punde kwamba ofisi za Chadema Kanda ya Kaskazini zimechomwa Moto usiku wa kuamkia Leo na watu wasiojulikana.Hapa ndipo mgombea wa Urais Tundu Lissu alipaswa kupokelewa kwa ajili ya kudhaminiwa.Tunatarajia kupata taarifa kwa kina zaidi asubuhi hii kutoka kwa viongozi wa chama.