Yaliyojiri: Mapokezi ya Tundu Lissu Jijini Arusha - Ijumaa 14 Agosti, 2020

Yaliyojiri: Mapokezi ya Tundu Lissu Jijini Arusha - Ijumaa 14 Agosti, 2020

Jana wameleta treni lao bovu ili kuzima mziki wa TL but Raia wa Chuga wamewapotezea na mgari moshi wao.
[/Q
Acha utoto upenz wa mtu usikufanye ukawa mjinga... Kuongea ongea ovyo tuu... Kama bovu mbona limafika.... Appreciate juhudi....
 
Ni Ijumaa tulivu.

Kama kawaida jiji la Arusha Kuna ubaridi asubuhi hii.Jiji likiwa katika hekaheka tangu Jana za Maandalizi ya mapokezi ya Mgombea Urais wa Chadema Tundu Lissu.

Kanda ya Kaskazini hususan Jiji la Arusha ni ngome Kuu ya Chadema na akitoa salaam za kunikaribisha jijini humo Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini Godbless Lema alisema mapokezi ya Mgombea wao wa Urais yatazidi Kanda nyingine zote alizokwishatembelea.

Tayari Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe akiongozana na Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu hapo Jana walimlaki Lissu maeneo ya mkoani Manyara tayari kuongozana naye kuingia Arusha leo.

He kweli jiji la Arusha litavunja rekodi leo? Tusubiri tuone.

Molemo Media imekwishawasili jijini Arusha kuwaletea moja kwa moja kitakachojiri katika mapokezi hayo ya kihistoria.

Karibuni...

Taarifa za hivi Punde

Ofisi za Chadema Kanda zachomwa Moto.

Kuna taarifa zilizotujia hivi Punde kwamba ofisi za Chadema Kanda ya Kaskazini zimechomwa Moto usiku wa kuamkia Leo na watu wasiojulikana.Hapa ndipo mgombea wa Urais Tundu Lissu alipaswa kupokelewa kwa ajili ya kudhaminiwa.Tunatarajia kupata taarifa kwa kina zaidi asubuhi hii kutoka kwa viongozi wa chama.
KARATU Hwaendi
 
pale kuna yule chawa MKAMUFANYIE FINISHING CHAP
 
Mpaka anaota kukifuta ila anashindwa atuie mbinu ipi kitu ambacho hawakijui ni kuwa upinzani ni imani na watu wameweka imani yao kwa chadema hivyo siyo rahisi kuiua chadema sana sana watakufa wao kama alivyokufa Wasira...
Hapo kampeni bado kampeni bado kabisa CDM IMESHASEPA na mikoa Kumi
 
Hivi Lema atakuwepo kweli?
Nasikia yuko kizuizini,sijajua kwanini.
 
Thread imeanza mapema ili ifikishe page nyingi.Huyo jamaa hauziki
Usitupangie muda wa kuanzisha thread, na utasaidia kufikisha page nyingi, utake usitake. Ni quote basi page ziongezeke.
 
Watu wa Arusha si wakuwa amini kihivyo. Wakati ule wa EL 2015 walimchanganya Mzee hayati Kingunge akaona umati mkubwa akajikuta anamuita atakaye kuwa Rais bora kabisa wa JMT kuwa ni nyapara barabara. Matokeo yake mzee wa watu akajifutia heshima yake yote aliyojijengea miongo kadhaa mbele ya jamaii ya Watanzamia.
 
Kati ya makosa makubwa CCM watajilaumu kumuacha akazuia Shughuli za Vyama vya siasa na kudhulumu uchaguzi wa Serikali za mitaaa mwaka jana ndio matokeo yake tunayaona leo
WANANCHI KOTE NCHINI BARA NA VISIWANI WAMEKUA NA SHAUKU KUBWA SANA YA KUWASIKILIZA WAPINZANI KINYUME KABISA NA MAWAZO KUWA WANGEKATA TAMAA

Kiukweli kupitia hili ccm wajifunze ;ingekua wapinzani wanapata muda wa kusema miaka mitaano hii bila kunyanyaswa leo hawangekua na la kuwaambia watu

Binadamu huna jipya la kuwafanyia au kuwapa ; WAPE KILA KITU ILA USIWANYIME MDOMO KUSEMA NA MASIKIO KUSIKIA ......Dola na Vyama vyenye Nguvu duniani zilifanya Maendeleo makubwa Lakini zilianguka kwa sababu tu waliziba watu midomo ...

Leo CCM haipo kwa watu kabisa zaidi ya kwenye Dola tena kwenye dola sio wote bali wale wenye mamlaka

Wanamikakati wa CCM wamempotosha Sana Mwenyekiti

Mwaka Huu ni maeneo machache Sana ccm inaweza kushinda kihalali Hii ni tofauti kabisa na miaka mitano nyuma Pamoja na kazi nzuri iliyofanywa

SEKRETARIET ya CCM imeuwa Chama kwenye mioyo ya watu !!!!!

Baada ya uchaguzi Huu lazima mabadiliko makubwa yafanyike kwenye sekretariet ya CCM ile ya kina Kinana na Nape was far better kwakua ilikua na approach ya kutumia siasa zaidi kuliko kutegemea kubebwa na Dola nzima .
 
Back
Top Bottom