ilikuwaje Goodluck Jonathan alishinda kwenye mazingira kama hayo?
Hakushinda. Mwaka 2010 alipata urais baada ya Rais kufa, yeye akiwa makamu. Mwaka 2011 ukafanyika uchaguzi. Akaiba kura na vurugu kali zolilitokea. Mwaka 2015 akakubali kushindwa maana angeiba tena hali ingekuwa si hali.ilikuwaje Goodluck Jonathan alishinda kwenye mazingira kama hayo?
Babu yako tunamjua ni Magufuli sio Abacha.President SHONEKAN ambaye alikaa kwa miezi michache akaja BABU yangu mimi SANI ABACHA ambaye ndio kiongozi aliyeipa maendeleo zaidi NIGERIA ingawa pia alikuwa katili sana.
Huyo Tinubu hachukui round anarudisha mpira kwa kipa,uchaguzi unaitishwa tena,Uzee wote huo unang'ang'ania madarakaNgoja maisha yaendelee state capture
Ila kwa huyu Tinubu, Buhari ataonekana alikuwa bora sana, kwa huku Africa kuwa rais kwa umri huo wa Tinubu hasa kwa nchi kama Nigeria yenye matatizo lukuki ni vigumu mno kuwa na matokeo mazuri.....Muda utakuwa shahidi mzuri.Kwangu mimi Buhari ni failed president kwa muda mrefu. Ukianza kumfuatilia Buhari miaka miwili hii kabla ya uchaguzi ambapo yeye na genge lake walishtuka wanaweza poteza urais ndio utaona anafaa ila ni hafai kabisa.
Buhari ni retired General, alishaongoza nchi baada ya kufanya mapinduzi miaka ya 1980s akafanya transformation kwa civilian leadership. Alishindwa nini kupambana na Boko Haram na jeshi la Nigeria lote na uzoefu wake serikalini na jeshini?
Buhari na Boko Haram ni kabila moja la Fulani. Hao ndio tuseme Wamasai + Wakurya wa Nigeria ila wana fujo sana na wengi Waislamu kama walivyo raia wengi wa Kaskazini. Buhari na Boko Haram waliongea lugha moja wakaelewana, magaidi hawakupigwa na hawakufanya mashambulizi wakati Goodluck Jonathan alivyokuwepo mara nyingi tu wanateka wanafunzi na kuwaficha Sambisa forest. Boko Haram ilitumika kuidestabilize Nigeria GJ aonekane hawezi. Btw alikuwa mnyonge kama ilivyo kwa makamu wa Rais wa Kiafrika, alikuwa makamu wa Umaru Yar'Adua ambaye asingekufa Nigeria walikuwa wamepata the best president mgumu kupatikana.
Niliandika humu siku moja, ukitaka kujua Nigeria ni wapuuzi huyo Abubakar Shekau katafutwa na jeshi miaka sijui mingapi eti hawajui alipo, kila wakifanya operation anajua kabla. Wakaja ISWAP baada ya ISIS kupigwa pale Syria na Iraq, ISWAP hawakuwa zaidi ya 2000 kipindi wanamuua Shekau. Yani kundi halikukaa zaidi ya mwaka likamuua wakati jeshi lenye maelfu, silaha nzito na bajeti halikuweza muda wote huo. ISWAP walipigana na Boko Haram baada ya kutofautiana kwenye msimamo mkali, BH ni wahuni tu wanalipwa hela na ni biashara ya watu kwa namna fulani. Kuna maeneo ya Nigeria hawajawahi kanyaga.
Chad inazidiwa uchumi na Tanzania, inazidiwa na Nigeria zaidi ya mara kumi na imewapiga magaidi. Cameroon ilikuwa na performance nzuri kuliko Nigeria inaowazidi kila kitu. Ghafla mwaka jana mashambulizi dhidi ya Boko Haram yakawa makubwa, ghafla jeshi likawa na performance nzuri dhidi ya magaidi. Sasa ngoja uchaguzi uishe hizo nguvu za jeshi utashangaa zimeishia wapi.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Babu yako tunamjua ni Magufuli sio Abacha.
Muslim 54%Kwahiyo waislamu ni asilimia ngapi ya wanaijeria?
Vyama Tawala Barani Afrika having'olewi hovyo hovyo bali kwa Mikakati thabiti na Uthubutu bila ya kuwa Muoga wa Kufa au Kufungwa Jela.
Heading na content haviendani. Anyway kwani ni lazima kutwiti kumpongeza?
Eti mwamsheni....., ni lugha isiyokuwa na staha. All in all umeandika rubbish ndugu, ungempongeza huyo mnaijeria bila kuandika vitu visivyo na ulazima. Purely talented my foot!
Moderators wametumia busara kuunganisha iwe ni kama comment. Hapo sawa, comment iko vizuri maana haiwezi kuwa thread hiyo ni komenti tu..Imeshapenya hiyo.....!!!!!!
Ana kura million 6 mshindi ana 8 million unasemaje hawezi kuwa mshindi chaguzi zijazo??Acha uongo mzee, sijui kama hata hapo Nigeria unapajua. OBI kwanza hata ATIKU hamfikii kwa umaarufu na hata ubora. Huko kwao Anambra kwenye masikini sana.
OBI hawezi kuwa Rais wa NIGERIA hata iweje, na hivi ametumia makanisa kuomba kura, vijana wengi wameamua kumwaga mboga, hiyo 2027 watu wanarudi kwenye UDINI na UKABILA.
OBI kabila lake limeonekana wao ni LABOUR PART tu, yaan IGBO wao wamechagua kutokana na KABILA lao na sio MTU. Hali tofauti na makabila makubwa kama HAUSA na YORUBA ambayo kura zao ziliegemea kwa watu na ndio maana kuna mgawanyo mahsusi, kwa LP, APC, NNNP, PDP nk.
Kwa siasa za Nigeria miaka ya karibuni hii hasa uchaguzi wa 2011, 2015 na 2019 haukuzingatia sana suala la Kabila au Dini zaidi ya hali ya kiuchumi na Siasa.
OBI hawezi kuwa Rais wa Nigeria.
Dah!...kati ya wapiga kura million 93 mshindi kapata kura million 8.8 tu yaani asilimia 37...na bado hitilafu za uchaguzi zipo za kutosha huu mtindo wa mshindi kukomba kila kitu peke yake hata kama ushindi ni tofauti kiduchu hauna afya...Ana kura million 6 mshindi ana 8 million unasemaje hawezi kuwa mshindi chaguzi zijazo??
Naamini kama uchaguzi ukiwa huru na haki matokeo yangeshangaza wengi. Ila hizi analysis ilihali uchaguzi una kasoro haziwezi kuwa objective.
Mfano kama wangeungana Obi na Atiku unadhani chances za BAT kushinda zingekuwepo?
Hicho kikundi ni akina nani mkuuObi Mkristo angeshinda magaidi wangefanya mashambulizi mengi kwa miaka ya kwanza ila wangepigwa. Tinubu Mwislamu akikubaliwa kuwa Rais magaidi hawatofanya mashambulizi kupitiliza na serikali haitoshughulika nao. Nigeria inakuwaga hivyo, Goodluck Jonathan alivyoondoka tu Boko Haram wakaacha kuteka wanafunzi.
Huyu Buhari alikuwa anawachekea Boko Haram ambao ni kabila lake, nao hawakuwa wanafanya matukio sana. Baadae ISWAP walivyoanza kupambana na Boko Haram na kufanya matukio na wananchi wakachukia to the maximum ndipo Nigeria ikanunua silaha na kufanya missions kali kabla ya uchaguzi. Uchaguzi ukiisha hutoona operations za kuwapiga waasi endapo chama tawala kitaendelea. Ila silaha za jeshi la Nigeria zimenunuliwa nyingi kwa gharama kubwa miaka miwili hii.
BAT hata uwezo wa kusimama vizuri hana, elimu yake haijulikani, umri wake kadanganya miaka zaidi ya kumi kwa sababu mwanamama mmoja aliyekuwa deputy wake na mdogo kiumri alishastaafu miaka kibao nyuma uko. Na classmates wa Tinubu elimu za kwanza walishastaafu na kusahaulika ila wa elimu za juu hawajulikani kwani hakufika uko. Then ni muuza madawa ya kulevya mstaafu.
Hawezi ongea bila kusoma speech mzee wa agbado. Ukijichaganya ukamuuliza maswali anasahau alichojibu.
Obi na obidients wake ni kama woke community. Ni jamii fulani king'ang'anizi ambayo haipendi kuambiwa ukweli kwamba kushinda kwa mazingira ya Nigeria hakupo, na ni jamii ya vijana wanaotumia sana media na hype kufanya kampeni. Obi ametumia makanisa na wachungaji wamempigia kampeni mno. Yeye binafsi nina imani anajua haya ila mashabiki zake hawataki kuelewa. Obidients watakuwa wapinzani wazuri na ni basis nzuri ya uchaguzi ujao kama Obi atabaki relevant. Maana najua lazima Tinubu awe kilaza kupindukia, we uliona wapi mgombea hata jimbo aliloongoza na alikozaliwa linamkataa wakati Nigeria ni nchi ya ubaguzi wa majimbo?
Yani Samia agombee alafu Unguja alikozaliwa wasimpigie kura.
Obi ndio ana unafuu kati ya wagombea wote ila hana connection kubwa na uzoefu. Akikaa calm hivihivi uchaguzi ujao atawakimbiza. Hata hivyo kaleta sense ya uwajibikaji kwa viongozi, Nigeria wanaoamua Rais awe nani na kakundi kadogo tu wala hakana kelele machoni mwa watu. Marais walikuwa wanafanya lolote as long as kale kakundi kanatimiza malengo mwananchi anadharauliwa ndio maana hiyo nchi huwa ina mambo ya ajabu sana yanatokea.
Mkono mtupu haulambwi mkuuuKila raisi Nigeria ni bilionea mungu afanye yake ⛔🙄