Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Inasikitisha sana Kimbukiko
 
We jamaa fala kweli. Unadhan hesabu hiyo mm siijui?. Mshahara unasoma tarehe 30 net! Ukianza kazi tarehe 10 unakuja kupokea mshahara tarehe 10 wa siku 20 tu.

Kakojoe ukalale
 
Duh rushwa ni tatizo.Sufuria zina dhuru nn?
 
Hali sio nzuri... Sio viwandani tu... Waoneni Hawa sales officers wanaozunguka barabaran muwaulize wanachopata.. kiufupi wengi tunafanya kazi ili kukamilisha kilichosemwa na kilichopo kwamba ufanye kazi ili ule. Na kula kwenyewe usipoangalia dah hutoboi kukuta mshahara mwingine
 
Hii nchi ngumu sana sema kweli viongozi awako seriously na maisha ya watu wanao waongoza kiujumla. Kwa maana aiwezekana maisha ya wanachi wanayajua vizuri kabsa iwe umesoma au ujasoma. Nachotaka kusema ni kuweka utaratibu juu ya malipo ya wafanya kazi viwandani ni kazi ngumu sana kama ulishawahi kufanya hiyo kazi alafu isitoshe unafanya kazi Masaa kumi na mbili, sijui mnaelewa kazi ya Masaa kumi na mbili non stop. Alafu Mtu analipwa 7000.


Nizungmzie pia kwa watu waliosomeshwa kwa mkopo na serikali alafu Mtu anamaliza mpaka chuo kikuu anabahatika kupata sehemu ya kazi analipwa hela hiyo hiyo kama kibarua na serikali inaona hilo na inakaaa kimya. Alafu mwisho wa siku Mtu huyo huyo anaanza kukatwa kwenye huo huo mshahara wa laki tatu kwa mwezi. Mnategemea kwa mshahara huo Mtu kama huyo atamaliza kulipa si chini ya miaka 20. Mnakaa kwenye vyombo vya habari mnasema mmeongoza ajira kwa kumlipa Mtu 4000 kwa siku na makato juu.

Cha muhimu kama serikali inabidi itoe maelekezo yanayo eleweka juu ya malipo ya wafanya kazi viwandani. Kwa watu wote.
 
Hawa watu wa chama cha wafanyakazi na wakaguzi kutoka serikalini walikuwa wakifika kiwandani nilikokuwa nafanya kazi, lakini hawakuwa wanaonana na wafanyakazi badala yake walikuwa wanaishia ofisi ya HR wanapiga stori na muhindi kisha wanasepa huku sisi tukiendelea kupigika. Mbaya zaidi kile kiwanda kilianza na tabia ya kunyonya malipo ya nssf ya wafanyakazi, na ikiwa mtu akienda kudai kule nssf basi anabambikiwa kesi na hakuna anachopata.
 
Kima cha chini ni 346000TSh, hiyo 5000 kwa siku ni nyingi Sana,
Wabaya wako ni ccm, mbunge analipwa milioni 11 kwa mwezi, posho kwa siku 350K, baada ya miaka 5,anakula mafao yake, wakatunga kikokotoo, "kizuuuri" Kwa ajili ya "kutunza" Pesa za, wastaafu, ili wastaafu vzr,cha ajabu wao wabunge, wamejitoa kwenye uzuri wa kikokotoo,! Wao sio, watumishi wa umma! Mpunga wao wanauvuta mapeeemaaa! Kwenye hili la maokoto, si chadema, act wala ccm, anayeweza kusema kitu!
 
Tajiri Kuuona Ufalme Wa Mbingu Ni Sawa Na Ngamia Kupita Kwenye Tundu La Sindano.
Tajiri ndio anautumia mfanano wake na Mungu, anatoa ajira, Kodi za kusaidia serikali kulipa mishahara, maskini ye ye ni kunya na kuvuta pumzi tu!
 
Acha kupotosha watu kwa Zanzibar gani labour analipwa zaidi ya 20,000?
Zanzibar kuna unyanyasaji mkubwa sana tena hata zaid ya bongo na kuna ukabila mkubwa sana kati ya mzanbari na mbongo huku tunaitwa Wanyamwezi
 
Kusoma sio suluhishobkwa maisha ya sasa maana wasomi wapo na hawana hata pa kushika kikubwa ni kukituma na ubunifu katika kazi
 
Inabidi uchunguzi ufanyike vyakutosha na serikali ichukue hatua za kisheria, japokuwa Sheria wakati mwingine inaruuhusu pale ambapo mmiliki wa kiwanda ataomba asijumuishe kwenye employment standards na hapa ndipo tatizo lilipo kifungu Cha Sheria 100, "The Employment and Labour Relations Act [CAP. 366 R.E. 2019]" kifungu Cha Sheria hiyo kinasema kwamba "100.-(1) The Minister may exempt any employer or class of employers from any employment standard contained in sections 19, 20, 23 to 25, 27,31 to 34, 41, 42 and 43." sasa tatizo kubwa lipo hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…