zitto junior unasema hawa wapalestina wa sasa ndiyo wayahudi orijino,hawa akina Cohen,Alhel etc tunaowajua ni fake.
Unaendelea kusema ..
Hata Adof Hitler aliua wayahudi fake,wayahudi orijino walibaki mashariki ya kati hapo hapo.
Akina mahamudu abba(hammas fighters)ndiyo kizazi cha yakobo.
It might be true some how..ila siku moja uje utufafanunulie kwanini humo ndani ya hammas hakuna weusi uzao Sheba?.
Na why hawaendi kuungana na hammas(wayahudi orijino kwa mjibu wako)badala yake wanakwenda kuungana na wayahudi fake?.
Ama wao pia hawaujui ujuzi huu unaoujua wewe kuwa hao wanaojiita wayahudi wenzao ni fake na wayahudi wenzeo(the legit ones) ni hammas?.
Ukiwa miongoni mwa wasomi ninaowakubali hapa Jf ninamini majibu unayo kama ambavyo hukoswi majibu mengine ya historia ya mashariki ya kati.
Nilivyojaribu kuelewa mafafanuzu yako kuhusu Israel na wayahudi ni kwamba hawa akina mahamudu abbas(wayahudi orijino kwa mjibu wako) uislamu ulipowafikia walislim nakuamua kuachana Iman yao ya Kiyahudi,wakaenda mbali hadi kubadili hadi Majina ya Miji yao kutoka majina ya kiebrania hadi Majina ya Kiarabu.
Mfn;- Yeruselm wayahudi wakaibadili jina na kuuita Al-qudus.
Katika history ya Israel imewai kaliwa na Mataifa ya Kigen zaidi ya mara 18 na mara zote hizo hawakuwai kuacha Dini yao,mila zao hata kubadili majina ya miji za ili kukumbatia tamaduni za kigeni..
Sasa nini kilikuja kuwapata baada ya kufikwa na Uislamu?.
Kwamba tamaduni na imani za Wagriki hazikuwa na nguvu kwao?.
Warumi na tamaduni zao ziliendekea kubaki za kipagani machoni pa wayahudi.
Persians nao waliwatawala ila Dini na Tamaduni zao hazikufua dafu machoni pa wayahudi ila tamaduni za waarabu na Dini yao mpya ilipowafikia Wayahudi wakaona Tamaduni na Dini yao ya kiyahudi hazina maana ila tamaduni na Dini ya Makka ndiyo sahihi?.
Alafu,hapo katikati (baada ya kifo cha Muhammad)kulitokea nini hasa maana mwanzoni kabisa ya uislamu Muhammad aliwapelekea Mafunuo yake wayahudi,wakayapambanua wakayakataa kabisa kuwa hakuna mkono wa MUNGU katika Mafunuo hayo,hali iliyofanya Mtume Muhammad(PBUH) atangaze uadui nao..
Sasa ilikuwaje baadae wayahudi wayakubali?.
Nini hasa kilitokea hapo katikati?.
Mfn; Wayahudi hawakumkubali Yesu hata kabla hajaja.
Akaja, hawakumkubali.
Hadi kaondoka,bado hajamkubali. Sasa Maalim wangu Zitto unajua nini hasa kilichopeleka wayahudi kuyakubali mafunuo ya Muhammad wakati mwanzoni waliyakataa hadi ukawa uadui baina ya Muhammad na wayahudi?.
Mwisho kabisa narudi kukuuliza swali langu la siku ile.
Q'uran kitabu chako cha Iman.
Inasema;-
Moja ya Dalili ya kiama ni waislamu kuwapiga wayahudi hadi watakuwa wanajificha nyuma mawe,na mawe yatakuwa yanawaambia Waislamu; huyu hapa myahudi kajificha nyuma yangu,njooni mmuue...
Sasa ikiwa akina Jonathan netanyau ni Mayahudi fake ila dunia medanganywa kinyume chake ila wayahudi orijino ni hawa Hammas(wapalestina) so,tutegemee siku moja waislamu kuji- mobilise na kuanza kuua Wapalestina(Wayahudi Orijino)ili kutimiza ili andiko?.
Maana binadamu tumedanganywa kuwa wanaojiita wayahudi ni orijino kumbe sio ila Allah hawezi danganywa.
alipotoa ilo andiko alikusudia Wayahudi Orijino, akina mahamudu abbas si akina Netanyau.
Andiko lazima litimie kwa namna yoyote ile.
Sasa nifafanulie.. ipo siku nyie waislamu mtawapiga Wapalestina ili kutimiza ili andiko?. Ama nini kitafanyika hapo ilikutimiza ili andiko?.
zitto junior wewe ni Miongoni mwa Maguru hapa ebu nifafanulie japo kidogo ili nielewe na nikubaliane totally na Dai lako kuhusu wayahudi.
Picha chini ndiyo waisrael halisi kwa mjibu wa zitto.