Uchaguzi 2020 Yanayotokea Tanzania Leo yalitokea Indonesia 1998

Uchaguzi 2020 Yanayotokea Tanzania Leo yalitokea Indonesia 1998

Mfano wako ni irrelevant, hao Pepsi wanafanya matangazo kwakuwa wako kwenye ushindani wa soko huria, ambapo mteja ananunua bidhaa kwa ridhaa yake. Umewahi kuwaona Pepsi wamezuia Cocacola kuuzwa mahali kisa wao pepsi walitangulia kufungua tawi eneo hilo? Huu mfano wako inaonyesha kabisa umeishiwa na hoja, ndio maana unatoa mifano isiyoendana na hali ya kisiasa tunayoijadili hapa.
Sawa naheshimu mawazo yako.
 
Hii ndiyo tunaita kujifariji au kukariri.
Media maarufu zenye subscribers wengi karibu zote zinapiga safari hadi miakoani kuonesha miradi iliyofanywa na jamaa kisha wanarusha kila kitu kila kona. Wanarusha hadi miradi ya choo au jiko la shule au zahanati.
Unafikiri mtu anaye fanya hivyo ametishwa?
Fedha za hizo safari anatoa wapi?

Media zote zinafanya live coverage ya matukio ya zinduzi zote za wale wa ngazi za juu kila kona ya nchi, unataka kusema wanafanya hivyo sababu wametishwa?

Hujaliona hilo jambo toka miaka angalau mitatu iliyopita? Watu wanakula mahindi, madafu, mapapai kule forodhani ufukweni, watu wanakaa chini na walemavu wajane, wazee, migogoro ya ardhi inatolewa maamuzi papo hapo kwenye misafara, teuzi katikati ya mikutano au hotuba.

Watu wanaongeza umiliki wa media za chama kama 'Channel Kumi', n.k. wewe bado unahisi vitisho tu?

Je ninyi upinzani mmewekeza angalau redio moja ya chama ya kurusha live matangazo hadi vijijini ambako wengi hawana smart phones hawaingii mitandaoni? Msifikiri watanzania wengi wana vifaa vya kuingia na kuona matangazo mitandaoni.
Kuna mikoa maskini huko wengi hawana simu wala computer.

Hiyo ya media kutorusha mambo ya chama chenu kwenye media inaweza kuwa hoja yako na mimi naikubali huenda ni vitisho, lakini tujiulize swali.
Hivi kama media flani ina mkataba wa ku-brand chama flani na mgombea wake, na katika Terms za mkataba wao wamekubaliana ili tukupe dau hili basi usitangaze brand ya mpinzani wetu hiyo ni kosa kibiashara?
Ukumbuke media nyingi binafsi zinaendeshwa kibiashara kama biashara zingine. Ni kama vile Emirates wanafadhili Arsenal wanaweka mashariti uwanja wenu na jezi zenu marufuku kuweka au kutangaza wapinzani wetu kama Qatar au KLM, n.k.
Je, utawalaumu Arsenal kwa kutoweka matangazo ya brand hizo zingine uwanjani kwao na kwenye vipindi vya TV zao?

MY TAKE: Kutangazwa na media flani siyo hisani bali ni biashara ambayo lazima uingie gharama kubwa kushinda dau la mshindani wako.
Media zinajipendekeza tu hakuna lolote. Kwa taarifa yako, media nyingi ziko hoi kwa sababu umma umepoteza imani nazo.
 
Kama wakoloni waliweza kubadili mind set zetu na kukubali ku slimu na kubatizwa na kuacha kutambikia mizimu. Tulianza kwenda hospitali tukiugua badala ya kuchemsha mizizi.

Tena siku hizi kuna mass media kuelimisha wananchi inawezekana.
Ndiyo hivyo jiwe anawabadili watu tabia lakini itachukua muda kufanikisha hilo.
Kelele 'mingi' sana, na usaliti mwingi mno.
 
Ndio maana Mkapa aliwaita wapinzani marofa na wapumbavu, huo mfumo unaotaka utaongozwa na maroboti, ndg mifumo ipo mzuri tu ila tulikuwa akuna msimamizi sahihi kusimamia, na ndio tatizo la Tanzania, mfno hapo juzi wakati Rais anatoka mtwara anafika kibiti anakutana na watu wanasema hawana choo zaidi ya miaka huku wanakusanya bilion 1.8, gari la kubeba wagonjwa limepaki Kwa kukosa tairi, naili nalo linaitaji mfumo Hipi? Ungesema tunaitaji viongozi wenye uthubutu maana hata kama kutakuwa na mfumo mzuri nanma hipi kama kiongozi atakuwa hana utashi mfumo utakwama maana haujiongozi
Kamsalimie che nkapa huko aliko
 
Media zinajipendekeza tu hakuna lolote. Kwa taarifa yako, media nyingi ziko hoi kwa sababu umma umepoteza imani nazo.
Kwa sababu mabadiliko ya kiteknolojia kwa dunia nzima, na hapa kwetu kuna tatizo la ziada la kuhamishia zabuni za miradi mbali mbali na matangazo kwenye taasisi za umma.
Lakini siyo vitisho. Kwanini uogope kuandika au kurusha matangazo kama kinachotangazwa ni sahihi hakivunji sheria?

Mdororo wa vyombo vya habari ni knock-off effect ya zabauni zote kupewa taasisi za umma.
 
Wanakijiji huko siku wakiona vyombo vya ulinzi wafugaji washafanya yao kwenye mashamba na jamaa wanaenda kutuliza hali au wanataka ardhi isiyoendelezwa kinguvu polisi wanaenda kuweka mambo shwari.

Siku zingine zote shida zao zote zilizobaki wanazipeleka kwa mwenyekiti wa kijiji, diwani au ofisi ya wilaya ivyo vyombo vya ulinzi wala hawana shughuli navyo na wala awakumbani navyo on daily basis. Na hawa ndio watanzania walio wengi.

Halafu wee uende huko uwaambie story zako sijui hawapo huru chini ya serikali ya sasa polisi wananyanyasa raia (vyombo ambavyo wakiviona sababu ni migogoro walioanzishiana wenyewe) sijui habari za vyombo vya habari kufungiwa; watu ambao wanataka ardhi, maji, umeme, barabara, uwatoe wamang’ati kwenye mashamba yao.

Wakati Magufuli amejiandaa kwenda kutatua changamoto zao za kila siku na nyingi tayari keshazifanyia kazi.

CDM wajiandae wanashindwa huu uchaguzi mchana kweupe kwa sera zao wenyewe, wasitunge story tu ya kupeleka kwa mabeberu ikifika November.
Sisi wa vijijini, mnatuchukulia pouwa ee? Unafikiri tunafuraia mipaka kufungwa na bei elekezi ya mazao tuliyo lima kwa gharama zetu!? Jidanganye kwamba sisi wa vijijini ni mtaji wenu! #sasabasi
 
Kwa sababu mabadiliko ya kiteknolojia kwa dunia nzima, na hapa kwetu kuna tatizo la ziada la kuhamishia zabuni za miradi mbali mbali na matangazo kwenye taasisi za umma.
Lakini siyo vitisho. Kwanini uogope kuandika au kurusha matangazo kama kinachotangazwa ni sahihi hakivunji sheria?

Mdororo wa vyombo vya habari ni knock-off effect ya zabauni zote kupewa taasisi za umma.
Mengine sitakomenti. Ila unapoongelea zabuni kupewa taasisi za umma, hapa unaonyesha huna uelewa wa mambo ya kiuchumi wala biashara.
 
Umejiuliza kwanini Lissu mlimpokea hata baada ya katazo la jeshi la polisi na hakuzuiliwa wala kusumbuliwa?
Umejiuliza kwani sasa anaongea mengi ambayo awali alikuwa anaongea anasumbuliwa na vyombo vya kusimamia sheria?

Sasa nakuambia hata kungekuwa na vyombo vya habari vya chama siyo vya mwanachama (e.g. Mbowe) wangeona aibu kuvifungia wakati huu.

Kwahiyo kwa maelezo haya gazeti la Tanzania daima litafunguliwa kwakuwa sasa hivi waliolifungia wanaona aibu! Kwa hiyo hao cdm wangekuwa na vyombo vyao ambavyo vinaweza kufungiwa wakati wowote, lakini vinaweza kurusha matangazo wakati wa uchaguzi kisa kuna kundi la viongozi linaona aibu? Unajua kwanini unakuja na utetezi wa kuokoteza usiokuwa na mashiko, kwakuwa umeamua kutetea tabia binafsi za mtu zisizo kwenye utaratibu wowote.
 
Nikweli but just think Lisu Kuwa Rais? Or Member? Nadhan nibora tuongozwe na Jiwe Tu. Tunasafari ndefu Sana bado vyama vya upinzani Kuwa vyenye uwezo kutuongoza. Tutakuwa tumepoteza
Sijui kwa nini unaona waliopo ccm wataweza au unavyosema Magufuli afadhali aendelee kuliko upinzani?
Kwani wao wana nini
Huyo unayemtetea amewahi kuzungumza nini cha maana
Lissu/Membe sio walipa visasi ndio maana mahubiri yao hayawavutii
Huyu alivyoingia si wengi walisema haya
Safari bado ni ndefu lakini tunahitaji chama tawala kiwe upinzani hata kwa 5yrs Tutarekebishana ndipo tutaenda sawa
Usiwadharau waliojitoa kuleta mabadiliko kwani wana haki kikatiba
Au mna mpango wa kupoteza wengine kama Ben Saanane

Kuweni na utu kidogo mnazingua sana mjue
 
Kwahiyo kwa maelezo haya gazeti la Tanzania daima litafunguliwa kwakuwa sasa hivi waliolifungia wanaona aibu! Kwa hiyo hao cdm wangekuwa na vyombo vyao ambavyo vinaweza kufungiwa wakati wowote, lakini vinaweza kurusha matangazo wakati wa uchaguzi kisa kuna kundi la viongozi linaona aibu? Unajua kwanini unakuja na utetezi wa kuokoteza usiokuwa na mashiko, kwakuwa umeamua kutetea tabia binafsi za mtu zisizo kwenye utaratibu wowote.
Nadhani hukusoma maelezo " vyombo vya habari vya chama siyo vya mwanachama "
Pia ningependa nikuambie hilo neno aibu limetumika kukwepa neno flani.
Nakuachia kitendawili.

Mwisho wa siku haya ni maoni tu siyo kusema nisemacho ndiyo sahihi.
Naheshimu maoni yako pia kwa leo niishie hapa mjadala huu.
 
Sisi wa vijijini, mnatuchukulia pouwa ee? Unafikiri tunafuraia mipaka kufungwa na bei elekezi ya mazao tuliyo lima kwa gharama zetu!? Jidanganye kwamba sisi wa vijijini ni mtaji wenu! #sasabasi
Bei elekezi umepewa na nani wakati kila siku Bashe amekuwa muumini wa soko huria, tena kaenda mbele zaidi na kupendekeza ‘price floor’ ikibidi serikali kufidia deficit pale ambapo bei za soko zikishuka sana yote hayo mkulima alindwe.

Wewe utakuwa sio mkulima wala mwanakijiji vinginevyo ungeona jitihada za serikali nina wasiwasi ni mkazi wa Dar maana ata hujui kinachoendelea mashambani.
 
Sijui kwa nini unaona waliopo ccm wataweza au unavyosema Magufuli afadhali aendelee kuliko upinzani?
Kwani wao wana nini
Huyo unayemtetea amewahi kuzungumza nini cha maana
Lissu/Membe sio walipa visasi ndio maana mahubiri yao hayawavutii
Huyu alivyoingia si wengi walisema haya
Safari bado ni ndefu lakini tunahitaji chama tawala kiwe upinzani hata kwa 5yrs Tutarekebishana ndipo tutaenda sawa
Usiwadharau waliojitoa kuleta mabadiliko kwani wana haki kikatiba
Au mna mpango wa kupoteza wengine kama Ben Saanane

Kuweni na utu kidogo mnazingua sana mjue
Mkuu huyo ukimtajia Ben Saa8 tu, umemaliza!
 
Wanakijiji huko siku wakiona vyombo vya ulinzi wafugaji washafanya yao kwenye mashamba na jamaa wanaenda kutuliza hali au wanataka ardhi isiyoendelezwa kinguvu polisi wanaenda kuweka mambo shwari.

Siku zingine zote shida zao zote zilizobaki wanazipeleka kwa mwenyekiti wa kijiji, diwani au ofisi ya wilaya ivyo vyombo vya ulinzi wala hawana shughuli navyo na wala awakumbani navyo on daily basis. Na hawa ndio watanzania walio wengi.

Halafu wee uende huko uwaambie story zako sijui hawapo huru chini ya serikali ya sasa polisi wananyanyasa raia (vyombo ambavyo wakiviona sababu ni migogoro walioanzishiana wenyewe) sijui habari za vyombo vya habari kufungiwa; watu ambao wanataka ardhi, maji, umeme, barabara, uwatoe wamang’ati kwenye mashamba yao.

Wakati Magufuli amejiandaa kwenda kutatua changamoto zao za kila siku na nyingi tayari keshazifanyia kazi.

CDM wajiandae wanashindwa huu uchaguzi mchana kweupe kwa sera zao wenyewe, wasitunge story tu ya kupeleka kwa mabeberu ikifika November.

Hapa naona unjivunia wanakijiji kwasababu ni rahisi kuwadhibiti wasipaze sauti zao kutokana na umasikini wao. Huko vijijini inajengwa taswira kuwa wanaikubali ccm, kwakuwa mifumo na mazingira haiwaruhusu kuweka hisia zao hadharani. Huku mjini kuna watu wengi wenye uelewa wa mambo, ndio maana ccm haijivunii, maana sio rahisi kuuongopea umma kuwa wanakubalika, hiyo ndio inayopelekea matumizi makubwa ya nguvu, ushenzi na uhayawani wa wazi ili ccm watangazwe washindi maeneo ya mijini.

Laiti mazingira yangekuwa rafiki huko vijijini,hisia za wanakijiji zingekuwa wazi, lakini mazingira yaliyopo ni ngumu kwa wanakijiji kuweka hisia zao hadharani, zaidi ya wao kujifanya wanaikubali ccm kwa shingo upande. Na hata hiyo kuwa wanavijiji wanaokubali ccm sio kweli, maana wapinzani wakifika huko na kuwaamsha wote hujikuta hawaitaki ccm. Kisa cha Magufuli kupiga marufuku vyama vya siasa kuzunguka nchi nzima, ni kuhakikisha watu wa vijijini hawatoki kwenye gereza la ccm, ambalo huwa wanawatumia bila ridhaa yao.
 
Bei elekezi umepewa na nani wakati kila siku Bashe amekuwa muumini wa soko huria, tena kaenda mbele zaidi na kupendekeza floor price ikibidi serikali kufidia deficit pale ambapo bei za soko zikishuka yote mkulima alindwe.

Wewe utakuwa sio mkulima wala mwanakijiji vinginevyo ungeona jitihada za serikali nina wasiwasi ni mkazi wa Dar maana ata hujui kinachoendelea mashambani.
Bei elekezi umepewa na nani wakati kila siku Bashe amekuwa muumini wa soko huria, tena kaenda mbele zaidi na kupendekeza floor price ikibidi serikali kufidia deficit pale ambapo bei za soko zikishuka yote hayo mkulima alindwe.

Wewe utakuwa sio mkulima wala mwanakijiji vinginevyo ungeona jitihada za serikali nina wasiwasi ni mkazi wa Dar maana ata hujui kinachoendelea mashambani.
😂😂😂😂 !! As you wish, ila ujue huku kijiji tuna akili pia!
 
Nadhani hukusoma maelezo " vyombo vya habari vya chama siyo vya mwanachama "
Pia ningependa nikuambie hilo neno aibu limetumika kukwepa neno flani.
Nakuachia kitendawili.

Mwisho wa siku haya ni maoni tu siyo kusema nisemacho ndiyo sahihi.
Naheshimu maoni yako pia kwa leo niishie hapa mjadala huu.

Inaonekana una majibu yako mfukoni, nimekuambia iwapo vyama haviruhusiwi kufanya mikutano, wala kuzunguka nchi nzima, hivyo vyombo vyake vya habari ndio vitaruhusiwa kutangaza bila kufanyiwa figisu? Nakutakia mchana mwema baada ya kuishiwa hoja.
 
saivi acha kwanza tumalize na huyu alieshushwa kukomboa waja wake. BTW tunafikilia atawale milele.
 
Kwa upinzani wa GIA ZA ANGANI,KUZUNGUSHA MIKONO NA KUHAMAHAMA VYAMA HOVYO.


MTATOA MIFANO MPAKA YA MAIGIZO YA BONGO MOVIES
 
Inaonekana una majibu yako mfukoni, nimekuambia iwapo vyama haviruhusiwi kufanya mikutano, wala kuzunguka nchi nzima, hivyo vyombo vyake vya habari ndio vitaruhusiwa kutangaza bila kufanyiwa figisu? Nakutakia mchana mwema baada ya kuishiwa hoja.
Nakubali nimeishiwa hoja mkuu.
Mchana mwema pia.
 
Back
Top Bottom