Yanga bado ni wa moto, wanakwenda kuanzia walipoishia msimu uliopita

Mzize bado mchanga tumpe muda mkuu.
Mzize ni mzito sana ,Denis nkhane kwa kasi na talent yake angekuwa na nguvu za mzize angekuwa top scorer
Nimemkubali coach na bench lake lote siku chache tu tangu aanze Kazi lakini timu inamuunganiko hakika yanga wamempata guardiola .
Nafasi kadhaa za kufunga zimetengenezwa
Skudu na max wAna talent za kutosha
 
Uko sahihi kabisa, mimi ni kolo ila Yanga hii ya leo ikipata team chemistry vizuri, wanabeba ndoo ya 30 hawa 😂🙌🏿
Kama ni kubeba ndoo ya kimba sawa, lakini ya nbc, sahau
 
Bila makasiliko kushoto akikaa ngushi kulia skudu striker akipatikana km mayele,Musonda 8,imeisha hiyo
 
Upo sahihi.Hajuagi anataka nn uwanjan
Kunahitajika tu mbadala wa Mayele, tena ikibidi wasajiliwe mastraika wawili hata kama mmoja atakuwa wa ndani. Huyu Mzize huwa ananitibuaga sana anayofanya uwanjani.
 
Naiona yanga ikifanya vizuri zaidi klabu bingwa barani afrika msimu huu,...
Hayo mengine yote nimeyavumilia tu, ila hapa kwenye kipengele cha CAFCL nimeshindwa kuvumilia aiseee. Yani mechi moja tu, tena na KC imetosha kukupa hiyo picha ya Yanga kufanya vizuri zaidi. Hebu fafanua zaidi ilitupate hiyo ulopata wewe.
 
Hayo mengine yote nimeyavumilia tu, ila hapa kwenye kipengele cha CAFCL nimeshindwa kuvumilia aiseee. Yani mechi moja tu, tena na KC imetosha kukupa hiyo picha ya Yanga kufanya vizuri zaidi. Hebu fafanua zaidi ilitupate hiyo ulopata wewe.
Uwezi kuvumilia maana maumivu ni makali tofauti na mlivyotegemea, wengi mlitegemea kiwango kibovu baada ya kocha Nabi kuondoka bila kuelewa kuwa yanga aikutengenezwa kumzunguka mtu mmoja, bali yanga inaongozwa na team work kuanzia viongozi mpaka chini kwa mashabiki,
Ninaposema yanga atafanya vizuri klabu bingwa licha ya mechi moja ya kujipima waliyocheza kama utakuwa unaujua mpira kiufundi nafikiri usingeuliza ilo swali
Angalia maingizo mapya yaliyoingia namna walivyokuwa wanacheza kana kwamba wamekaa pamoja mda mrefu kutengeneza muunganiko, angalia kikosi kilichoanza na kilichoingia kipindi cha pili wote wako timamu kiakili na kimwili, klabu bingwa yanga anakwenda kukutana na timu zenye ubora unaoshabihiana na kaizer chiefs ambayo ishacheza fainali ya klabu bingwa barani Africa,
Nafikiri nimekujibu swali lako
 
Tabu bado ipo pale pale ,wanadhani mayele kuondoka ndiyo watapata unafuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…