Yanga kwenda kucheza CAF champions Zanzibar, JKU na UHAMIAJI wamekataa kuchezea Zanzibar, Kuna nini?

Yanga kwenda kucheza CAF champions Zanzibar, JKU na UHAMIAJI wamekataa kuchezea Zanzibar, Kuna nini?

Kwanini Karume asaidie jengo la Yanga kama sio mshabiki/ mwanachama wa Yanga? Yanga ni timu ya wanachama na hao wanachama wapo hadi Zanzibar unalinganisha vipi na Man united?
Kuna kosa gani wanachama wa Yanga waliopo Zanzibar kuona timu yao ya Yanga? Akili yako inawaza kama vile Yanga ni timu ya jamii fulani ya watu wakati Yanga ni timu ya wanachama na mmoja ya mjumbe wa baraza la wadhamini anatokea Zanzibar. Hauna hata moja ya maana
Karume alisaidia hata Simba kupata jengo lao lile. Mzee karume alikuwa na fedha nyingi sana zilizoachwa na Sultani baada ya mapinduzi, hakujua afanye nini nazo wakati ule. Alijenga viwanja vizuri vya mpira, kituo ghali cha television ya rangi, maghorofa yenye kila kitu ndani kila sehemu watu wake wakae bure, kuoa wake wazuri, kuoa na maeneleo mengine. Hivyo kujenga jengo la Yanga haikumaanisha kitu kikubwa sana kama tunachokiona sasa kwenye uongozi wa Hersi. Hata hivyo ni jambo zuri kama Yanga sasa itakuwa taasisi ya muungano, lazima katiba ya yanga iseme hivyo huko baadae.
 
Michezo siku zote ina imarisha udugu
Ni kweli kabisa, kama Yanga itavuna wanachama wengi kutoka Zanzibar pia hilo ni jambo la kuigwa na timu zote. Ni vizuri ifikirie kujitanua hata East Afrika, Kenya, Uganda, Burundi, DRC na Rwanda ili mechi siku nyingine zipelekwe kuchezwa Rwanda au Kenya pia.
 
Haiwezi kuwa hivyo, unataka kusema Iko siku Man U wanawezakupeleka mechi zao Afrika kwakuwa Wana wapenzi wengi pia?

Kwenye mechi kama hizi Kuna vitu ambavyo ni zaidi ya mpira. Kuna watu wanafanyabiashara, kunawatu wanaenda kufurahi na Kuna taasisi zinapata makusanyo kutokana na mechi hizi, sio maswala ya kuhamisha mechi TU. JKU na UHAMIAJI hawakuona faida ya kiuchumi kwa wageni kuja Zanzibar kulala, kula, kusafiri, viingilio na furaha kwa watanzania hasa wa Zanzibar wenzao, badala yake wanataka kazi hiyo kuiachia Yanga timu ya Tanzania bara. Hii haiwezi kuwa sawa . Yaani unamtuma mwanangu kwenda kulinda mpunga wako wakati mwanao kaenda beach kuogelea. Yanga ni timu ya dar es salaam ya watu wa dar es salaam kwa maslahi ya watu wa dar es Salaam.
Screenshot_20240919-090722_Chrome.jpg
Screenshot_20240919-090722_Chrome.jpg
 
Wakati 5imba na Yanga zinaenda kucheza dabi uwanja wa Tanganyika, Kigoma, kuna aliyeuliza? Wakati Yanga na Coast wanacheza Sheikh Amri Abeid, Arusha, kuna aliyeuliza? Wakati 5imba na Azam wanacheza pale Nangwanda Sijaona, Mtwara, kuna aliyeuliza? Wakati 5imba na Yanga wanacheza Mkwakwani Tanga kuna aliyeuliza? etc. Hizo timu zote tajwa hapo juu zilicheza nje ya 'nyumbani' kwao..!! Kwanini hii leo iwe nongwa hao ambao nyumbani kwao ni ZENJI kucheza nje ya ZENJI..!!??
Unaongea kana kwamba hujui nini tofauti kati ya TFF na ZFF. ZFF iko level moja na TFF, FUFA, FKF, nk.
 
Unaongea kana kwamba hujui nini tofauti kati ya TFF na ZFF. ZFF iko level moja na TFF, FUFA, FKF, nk.
Ok, then, kwanini Mudathir, Baka na Fei Toto wapo taifa stars? Kwani mashindano haya hayana Zanzibar Heroes? Inawezekana mimi sijui, naomba unifafanulie.
 
Ni kweli kabisa, kama Yanga itavuna wanachama wengi kutoka Zanzibar pia hilo ni jambo la kuigwa na timu zote. Ni vizuri ifikirie kujitanua hata East Afrika, Kenya, Uganda, Burundi, DRC na Rwanda ili mechi siku nyingine zipelekwe kuchezwa Rwanda au Kenya pia.
Na wakenya huwa wanakuja kwa Mkapa kucheki DABI. Wakipelekewa huko huko dabi itakuwa kubwa zaidi
 
Ok, then, kwanini Mudathir, Baka na Fei Toto wapo taifa stars? Kwani mashindano haya hayana Zanzibar Heroes? Inawezekana mimi sijui, naomba unifafanulie.
Kakaaa wamelazimishwa kucheza TU baada ya FIFA na CAF kuwanyima uwanachama kamili Zanzibar. Lakini Kuna ada ya uhamisho ili timu ya bara kupata mchezaji wa kiZanzibar.
 
Kakaaa wamelazimishwa kucheza TU baada ya FIFA na CAF kuwanyima uwanachama kamili Zanzibar. Lakini Kuna ada ya uhamisho ili timu ya bara kupata mchezaji wa kiZanzibar.
Kuna sababu yoyote ya Zenji kunyimwa uanachama?
 
Yanga wameenda Zanzibar si Kwa sababu wanawanachama wengi kama baadhi ya watu wanavyoseme lakini ukweli wameenda Zanzibar ili kujipendekeza Kwa mheshimiwa rais.Huu ni ukichaa kabisa
 
Watu hawajui tu lakini iko sheria (nadhani haijafutwa) ya kuilipa serikali ya zanzibar US Dollar 40 kama mtu wa tanganyika ukitaka kumuoa Mzanzibar. Haitumiki, iko dormant lakini ipo.
 
TFF, IDFA
Timu ni ya wanachama, TFF na DFA hawana timu bali ni mashirikisho ya soka ngazi ya taifa na mkoa. Kazi zao ni kusimamia sheria, na kuendesha ligi kwa ngazi mbalimbali. Yanga ni timu ya wanachama na wapo wanachama wengi tu wa kutoka Zanzibar na ndio maana unaona ina mjumbe wa baraza la wadhamini kutoka Zanzibar.
 
Timu za JKU na UHAMIAJI ni timu za Zanzibar kindaki ndaki kuliko Yanga. Hatukuelezwa kwanini JKU na UHAMIAJI hawakutaka mechi zao za mashindano ya CAF wachezee Zanzibar, lakini Yanga wanataka kwenda kucheza CAF championship mzunguuko wa pili Zanzibar. Kuna nini hasa hapo?

Ufafanuzi unahitajika juu ya jambo hili. Michezo ni furaha, uchumi na undugu, kwanini JKU na UHAMIAJI walihamisha furaha, uchumi na undugu unaotokana na michezo kwenda Egypt na Libya na Yanga kupeleka Zanzibar furaha, uchumi na undugu Zanzibar kutoka dar es salaam?

Je, unawaweza kuwa mkatoliki safi kumzidi Pope?; muislam fafi kuliko mufti?
hawana hela za kusupport chakwao hao wazanzibari
 
Watu hawajui tu lakini iko sheria (nadhani haijafutwa) ya kuilipa serikali ya zanzibar US Dollar 40 kama mtu wa tanganyika ukitaka kumuoa Mzanzibar. Haitumiki, iko dormant lakini ipo.
Kumbe hoja yako ipo katika kiubaguzi wa utanganyika na uzanzibar.
 
Yanga wameenda Zanzibar si Kwa sababu wanawanachama wengi kama baadhi ya watu wanavyoseme lakini ukweli wameenda Zanzibar ili kujipendekeza Kwa mheshimiwa rais.Huu ni ukichaa kabisa
Wakijipendekeza kwa raisi ndio watabeba kombe la CAF? au ndio watafanya vizuri mashindano ya CAF? Kichaa ni wewe unayewaza visivyohusiana. Au kuna kiongozi wa Yanga anataka kuwa waziri?
 
Timu ni ya wanachama, TFF na DFA hawana timu bali ni mashirikisho ya soka ngazi ya taifa na mkoa. Kazi zao ni kusimamia sheria, na kuendesha ligi kwa ngazi mbalimbali. Yanga ni timu ya wanachama na wapo wanachama wengi tu wa kutoka Zanzibar na ndio maana unaona ina mjumbe wa baraza la wadhamini kutoka Zanzibar.
Yanga inapocheza mechi pale Benjamin Mkapa niambie ni akina nani wanaopata gawio kwenye gate collections, na kwanini wanapata gawio? Je, Yanga inapopeleka mechi zake Zanzibar ni akina nani kati ya hao hawatapata sehemu ya gate collections na kwanini?

Yule mjumbe unaesema yumo ni kwasababu tu hati ya jengo ilikuwa kabatini kwake, la sivyo ondokeni tuchukue jengo letu..
 
Back
Top Bottom