Yanga ndiyo club ya kwanza duniani yenye mkopo na bado ikapata faida ya million 500

Hapo number 2 deni si linalipwa mda wa marejesho ukifika? hio 500M ni sehemu ya mtaji
mkuu, kiuendeshaji Yanga hajapata faida, ila ana hasara ya bil 4.3+....

mapato yote ya yanga kibiashara (yaliyotokana na biashara wanayofanya) ni bil 13,
matumizi kwa mwaka husika ni bil 17.3......

sasa, baada ya kuona matumizi ni makubwa kuliko mapato, wamekopa bil 4.8... ili kufidia nakisi ya hio hesabu,......

haya, niambie, kibiashara kuna faida hapo?
 
thamani ya simba leo sio bil 40 (maana MO alilipa 20b kwa 49% ya hisa, na hii ilikua mwaka 2016 huko).....
utaona mwaka 2016 huku thamani ya Simba ilikua 40b,......

fast foward miaka 6 mbele, thamani ya Simba bado imebaki ni ile ile? tupe jibu....

ukitaka kulinganisha thamani ya timu vs bajeti, itakua sahihi ukilinganisha thamani ya simba 2016 vs bajeti ya simba 2016.........
 
Mkuu kwani ni lazima kutumia faida yote kulipa deni mpaka limalizike ndio uanze kuhesabu faida, si unaweza kutumia sehemu ndogo tu ya faida kulipunguza kidogo kidogo?.......Kuna mikopo ya kulipwa kwa kipindi kirefu tena kidogo kidogo tu.
Mkuu, mkopo una process za kulipwa mpaka uite faida? Mkopo apo ni 4B na hakuna hatua yoyote ile inayoonesha linalipwa.
 
Kwani hisa zimenunuliwa lini na Mo,maana kumbukumbu zangu zinaniambia ni 2021.

Hiyo 2016 sijui labda hizo ni behind the scene.
 
20bil 2021 for 49% then 23bil per year in 23/24 bajeti ya timu,sijui labda kwako ina make sense kwako.
Haina tatizo kabisa, thamani ya hisa kipindi hicho ilikuwa 20b kwa sasa haziwezi kuwa na thamani hiyo, hata bajeti ya uendeshaji ilikuwa chini ......ila kwa Sasa bajeti ya uendeshaji imepanda.

Thamani ya hisa 49% kipindi hicho na gharama za kuendesha timu kwa sasa hazina uhusiano wowote.
 
So kampuni yenye haki ya kutangaza faida ni ile tu isiyokua na mkopo?
hapana, hata yenye mkopo inaweza kutangaza faida.......
ni hivi mkopo huwa unakua na muda wa kulipa
mfano, nimekopa mil 100, natakiwa kulipa kwa miaka 5.... kwa riba ya 10% per annual,

kwaio, riba itakua ni 100 (principal) x0.1 (10% riba) x 5 (umri wa mkopo) = 50,

kwaio sasa marejesho itakua 100 (principal) + 50 (riba) =150....

kila mwaka nitatakiwa kulipa 150÷5 =30mil,

sasa katika hesabu zangu kila mwaka kwenye matumizi kutakua na loan repayment ya 30mil,.... kinachobaki baada ya kuondoa matumizi yote ikiwemo kulipa mkopo kitakua ni faida....
 
Baada ya Yanga kusema bajeti yao ya msimu ni bln 20 makolo now jana wakabidilisha gia angani wao bajeti yao ni b 23
 
Sijakataa thamani kupanda ila hata iweje thamani ya hisa alizo nazo Mo hazizidi 25bil tukisema tuinclude na faida,then bajet per Yr 23bil labda kwetu bongo. Ila kwa wenzetu welio anza mapema na maswala ya hisa ukiwaambia hiki wataona ni kituko.

Yaani bajeti ya club ya mwaka approx ni sawa na nusu ya thamani ya club,haya maajabu ujue na inawezekana Simba ikawa ya kwanza duniani.
 
uwezo wako wa kuelwa hesabu ni mdogo,kuwa na deni hakukufanyi usipaye faida,na faida haikokotolewi kutoka kwenye mkopo,faida ni faida na mkopo ni mkopo,ndio maana unaweza kukuta una mkopo wa miaka 30 au 40 na utakuwa na loan repayment kutokana na mkataba wako,so kama hujui kitu kaa kimya
 
1.Kwanza tukubaliane kuwa taasisi inaweza kupata faida licha ya kuwa na mkopo

2. Pia tukubaliane kuwa kiasi kinachobaki mkononi mwishoni mwa mwaka baada ya matumizi yote sio lazima kiwe faida au hasara.

3. Pia ningependa kupata kujua ni wapi Rais wa Yanga alisema taasisi imepata faida ya kiasi hicho cha pesa. Hapa Tutofautishe faida/hasara mwishoni mwa mwaka na salio la mwishoni mwa mwaka.

4. Tuweke akilini hesabu za taasisi hazifanywi kwa mfumo wa hesabu za mauzo ya mafungu ya nyanya.


5. Tukijua nature ya CASHFLOW STATEMENT na Financing activities zinakuwa treated vipi kwenye kwenye Cashflow statement wala hatutajisumbua na huu mjadala.
 
2
So kutoka 2021 mpaka 2023 ndio imedouble?
thamani ya simba aliyolipa MO hizo 20b kwa 49% share sio ya mwaka 2021 mkuu......
rudi ufuatilie tathmini ya thamani ya simba ilifanyika lini, na MO aliingia makubaliano ya uwekezaji na Simba kipindi hiko hiko, ndio maana akawa anaweka pesa yake pale Simba......

wakati MO anaingia pale Simba kama mwekezaji walikua hawajawahi kanyaga CAF QF, ni kipindi ambacho Simba ilikua ombaomba,..... alipoingia yeye na tathmini kufanyika ndio wakaanza kupata mafanikio (hayo wanayojivunia), wakaanza kuboresha uwanja wao kule bunju.....etc,

kiufupi thaman ya Simba leo inaweza kuwa ni mara tatu au zaidi...

NB/ mwekezaji atakayeenda Yanga leo akitaka kununua hisa 49% za Yanga hii ya leo, usishangae akaambiwa alipe bili 40 au 50 kabisa.......,

Metl na GSM wapongezwe kwa kuinua thaman ya hivi vilabu...... wameweka pesa zao nyingi hapo (japo wameiba pia maana hizo timu ni kubwa ila zilikuwa na viongozi mbumbumbu)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…