Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

asalaaam aleykum kandambili wote.... ninawapa pole kwa kuwakosa wakongo lakini nategemea yule beki wa malawi hamtampanga tena..

Mimi sina huruma na Yebo yebo kabisa. Hawana moyo wa kiuana michezo kabisa. Walivyoona timu yao mdebwedo inakamuliwa wakaamu ku-hack JF ilitusiwashushue. Belo na Balatanda acheni kushabikia maradhi. Wachezaji wana njaa watacheza vipi?

Wachezaji Yanga walia njaa Monday, 15 February 2010 04:16
*Uongozi kujadili kipigo leo

Na Mwandishi Wetu

BAADHI ya wachezaji wa timu ya Yanga, wameulalamikia uongozi wa klabu hiyo kwa kuwacheleweshea mishahara yao ya Januari, huku wakiwa hawana taarifa zozote juu ya mishahara hiyo ambayo wao wanaitegemea kwa matumizi mbalimbali.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Dar es Salaam jana na kuomba majina yao yahifadhiwe, wachezaji hao walisema wanashangaa kuona mpaka wanacheza mchezo wao wa kwanza katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika, bila kulipwa mshahara wa Januari jambo ambalo linawatia wasiwasi na kuwavunja moyo.

''Huwezi kuamini mpaka sasa, hatujalipwa mishahara yetu ya Januari, alafu jambo la kushangaza viongozi wanachozungumza hatukielewi, sasa mimi naona ni bora watuambie moja hatma ya fedha zetu, kama kukopa tuanze kukopa,'' alilalamika mmoja wa wachezaji hao.

Aliendelea kusema kwamba licha ya kuwa walituambia wangetupa kabla ya kuanza kwa michuano hiyo ya kimataifa, lakini wanashangaa siku zinakwenda bila kupewa taarifa zozote, kitu kinachowanyima raha kila wakirudi nyumbani kwani wao wanafamilia zinazowategemea.

Akizungumzia sakata hilo Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Lawrance Mwalusako alikiri kwamba ni kweli mshahara wa Januari, hawajawapa wachezaji wao lakini tayari kila kitu kipo vizuri na kuanzia leo huo mchakato wa kuwalipa fedha zao utaanza.

''Ni kweli mshahara wa Januari hatujawalipa wachezaji wetu hadi sasa, lakini tulikubaliana kwamba tutawapa mishahara hiyo baada ya kumalizika kwa mchezo wetu dhidi ya Lupopo ambao tayari tumeshacheza, hivyo kuanzia kesho (leo) tutaanza kuwapa mishahara yao,'' alisema Mwalusako.

Wakati huo huo, Mwalusako alisema leo Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, inatarajia kukutana na benchi la ufundi, kujadili na kupanga mikakati ya mchezo wao wa marudiano dhidi ya FC Lupopo, utakaopigwa wiki mbili zijazo nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).

Alisema watakutana kujadili ni vipi walipoteza mchezo huo wa kwanza kwa kuangalia makosa yao na kujipanga upya, pamoja na kupanga mikakati ya kuaminika katika kuhakikisha wanaingia hatua ya pili ya michuano hiyo.
 
Wachezaji Yanga walia njaa Monday, 15 February 2010 04:16
*Uongozi kujadili kipigo leo

Na Mwandishi Wetu

BAADHI ya wachezaji wa timu ya Yanga, wameulalamikia uongozi wa klabu hiyo kwa kuwacheleweshea mishahara yao ya Januari, huku wakiwa hawana taarifa zozote juu ya mishahara hiyo ambayo wao wanaitegemea kwa matumizi mbalimbali.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Dar es Salaam jana na kuomba majina yao yahifadhiwe, wachezaji hao walisema wanashangaa kuona mpaka wanacheza mchezo wao wa kwanza katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika, bila kulipwa mshahara wa Januari jambo ambalo linawatia wasiwasi na kuwavunja moyo.

''Huwezi kuamini mpaka sasa, hatujalipwa mishahara yetu ya Januari, alafu jambo la kushangaza viongozi wanachozungumza hatukielewi, sasa mimi naona ni bora watuambie moja hatma ya fedha zetu, kama kukopa tuanze kukopa,'' alilalamika mmoja wa wachezaji hao.

Aliendelea kusema kwamba licha ya kuwa walituambia wangetupa kabla ya kuanza kwa michuano hiyo ya kimataifa, lakini wanashangaa siku zinakwenda bila kupewa taarifa zozote, kitu kinachowanyima raha kila wakirudi nyumbani kwani wao wanafamilia zinazowategemea.

Akizungumzia sakata hilo Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Lawrance Mwalusako alikiri kwamba ni kweli mshahara wa Januari, hawajawapa wachezaji wao lakini tayari kila kitu kipo vizuri na kuanzia leo huo mchakato wa kuwalipa fedha zao utaanza.

''Ni kweli mshahara wa Januari hatujawalipa wachezaji wetu hadi sasa, lakini tulikubaliana kwamba tutawapa mishahara hiyo baada ya kumalizika kwa mchezo wetu dhidi ya Lupopo ambao tayari tumeshacheza, hivyo kuanzia kesho (leo) tutaanza kuwapa mishahara yao,'' alisema Mwalusako.

Wakati huo huo, Mwalusako alisema leo Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, inatarajia kukutana na benchi la ufundi, kujadili na kupanga mikakati ya mchezo wao wa marudiano dhidi ya FC Lupopo, utakaopigwa wiki mbili zijazo nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).

Alisema watakutana kujadili ni vipi walipoteza mchezo huo wa kwanza kwa kuangalia makosa yao na kujipanga upya, pamoja na kupanga mikakati ya kuaminika katika kuhakikisha wanaingia hatua ya pili ya michuano hiyo.
basi mimi nilijua simba tu ndio njaa.... sijui GC yuko wapi awalipie wenzake mishahara
 
katika hili naushukuru uongozi wa JF kwa kuunganisha na kuziweka habari za YANGA IMARA katika sehemu moja tuluvu kama hii. idumu JF, idumu YANGA! Mnyama, ziiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!
 
basi mimi nilijua simba tu ndio njaa.... sijui GC yuko wapi awalipie wenzake mishahara

Achana na huo ushuzi ulioandikwa '''na mwandishi wetu'''
We ukitaka habari za Yanga tuulize wenye timu.

Hao waandishi wako wa magazeti yako ya shilingi mia mbili wanakupotosha.

Yanga imara
Daima mbele nyuma mwiko.
 
Wadau wa Club ya Yanga ingawa tulifungwa na Lupopo, tunaomba mwenye matokeo ya mechi ya leo kati ya timu yetu ya Yanga na Toto Africa mtuletee ili tujue timu yetu imefanya nini katika mechi ya leo
 
duh bado unafuatilia soka la simba na yanga!
 
Ndio soccer letu ilo lazima tulifuatilie nyie mnaopenda vya huko hongereni
 
duh bado unafuatilia soka la simba na yanga!
Kwa nini asifuatilia na kuna ndugu zake watanzania wanapata ajira na kujikimu kimaisha? pia bado ni burudani kwa wengi. Wale wanaoenda pale uwanjani wote unawaona wehu ila wewe ndio mjanja?
Acheni hizo!
 
Wadau wa Club ya Yanga ingawa tulifungwa na Lupopo, tunaomba mwenye matokeo ya mechi ya leo kati ya timu yetu ya Yanga na Kagera Sugar mtuletee ili tujue timu yetu imefanya nini katika mechi ya leo

he... nawaombea ushindi..... ila unganisheni kwenye jukwaa lenu moja!! au hamna klabu nini kila mtu anajisemea kama Manure?
 
Ndio soccer letu ilo lazima tulifuatilie nyie mnaopenda vya huko hongereni

Kwa nini asifuatilia na kuna ndugu zake watanzania wanapata ajira na kujikimu kimaisha? pia bado ni burudani kwa wengi. Wale wanaoenda pale uwanjani wote unawaona wehu ila wewe ndio mjanja?
Acheni hizo!
Kushabikia soka la bongo ni kupoteza muda!​
 
Kushabikia soka la bongo ni kupoteza muda!​

wewe pape acha kuwa na utumwa wa fikra.....england wanaangalia ligi ya italia,serie A na hata copa..lakini ..lazima wapende ya kwao....

vile vile hata uende japan ..ni vichaa wa ligi ya uingereza kuliko sisi lakini ...hawaaachi ligi yao..

ukija afrika hivyo hivyo...nchi kama afrika ya kusini au hata congo....wanafuailia mipir yao....

sasa sisi maskini .... basi kuona ligi za nje basi ...tunaanza kuona kuangalia ligi zetu ni kupoteza muda..... hatujuwi kuwa hizi ligi pia ni IMPERIALIST INTRUMENTS..za kuteka akili za baadhi ya waafrika wajinga...wasahau na kudharau kwa..

nyumbani ni nyumbani mazee!!
 
wewe pape acha kuwa na utumwa wa fikra.....england wanaangalia ligi ya italia,serie A na hata copa..lakini ..lazima wapende ya kwao....

vile vile hata uende japan ..ni vichaa wa ligi ya uingereza kuliko sisi lakini ...hawaaachi ligi yao..

ukija afrika hivyo hivyo...nchi kama afrika ya kusini au hata congo....wanafuailia mipir yao....

sasa sisi maskini .... basi kuona ligi za nje basi ...tunaanza kuona kuangalia ligi zetu ni kupoteza muda..... hatujuwi kuwa hizi ligi pia ni IMPERIALIST INTRUMENTS..za kuteka akili za baadhi ya waafrika wajinga...wasahau na kudharau kwa..

nyumbani ni nyumbani mazee!!
Umetwanga mzee, hata hizo za huko zilihitaji support ili kukua kwa kiasi hicho. Mwanao kama kila siku mchafu na mjinga utamsusa na kupenda wa jirani eti ni msafi na anatunzwa vizuri?
 
......kumpendezesha mkeo ni kupoteza muda. How does that sound?
wakuu philemon na NL.... utumwa sio pingu!!! kuna mwimbo wa vijana jazz zamani waliimba
mwacheni mwenyewe ye yoyo
mwacheni yeye azuzuke na mji
ngoma ulipoingia daresalama
hukupaka wanja ngoma weee

mwacheni mwenyewe....azuzuke na EPL, winter Olympic na cricket
 
Back
Top Bottom