Yupi bora, mwanaume anayeacha pesa au anayenunua mahitaji yote mwenyewe?

Yupi bora, mwanaume anayeacha pesa au anayenunua mahitaji yote mwenyewe?

Mimi ninachofanya naenda sokoni nanunua mchele unga na kila kitu cha ndani kiwemo kisha naacha na pesa ya kununua chipsi pale anapotamani au vitu vidogo vidogo hivi.

Lakini sitokuja kukaa n pesa ya matumizi ya ndani hata siku moja,pesa inayohusu mambo ya kula namuachia wife.

Nikikaa nazo mara natumia
Mko wachache sana wenye hii tabia wenzio sikuizi wanataka wabane kila sehemu
 
Binafsi ingawa sina mke lakini naona ni bora mke awe na uhuru na sehemu yake.

Pangeni budget, ukishajua matumizi yote ya chakula nyumbani ni kiasi gani unatenga fungu unampa. Mwanamume kuanza kudeal na mambo ya jikoni directly ni kukosa kazi.

Mwanamume unapaswa kuwaza mambo makubwa kama ujenzi, ada za WATOTO, kuongeza kipato n.k

Ikitokea emergency mnakaa mnajadili mtatatua vipi.

Hakuna kitu sikipendi kama uko busy umekaa tena sometimes na mgeni unaanza tena kuambiwa mboga ya jana iliisha, au kiberiti kiliisha.
Una nafasi yako peponi 👊
 
Mimi kila kitu nanunua .

Na pia nitampa Pesa kwaajili ya Mambo mengine ambayo sio lazima aniambie.



Haya mambo ya kuacha Pesa mezan kila siku , yanafanya Mwanamke aweke akilin Pesa sana,kuliko kukuweka wewe akilini.
[emoji38][emoji38][emoji38] mkuu unafanya vyema wenye mkono wa birika wanapigiwa tu wake zao
 
Mm nanunua mahitaji ya mwezi kama mchele, unga ngano/mahidi, maharage, mafuta ya kula, chunvi, na sukari baada ya hapo nampa kiasi cha pesa ya mboga ya mwezi mzima, pia ni jukumu langu kuleta kuleta nyanya na mboga mboga kila jmosi, haya ndio makubaliano yetu na imenisaidia sana huu mwaka wa nne kwenye familia.

Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
Natamani wanaume wengine wajifunze kutoka kwako
 
Wapo hao watu ,tena wengi anaweza akashindia mihogo ya kukaanga na maji ya kudownload na watoto wakashindia uji ili mradi a_make akanunue kijora.
Kama kijola unamnunulia hiyo ela nyingine anafanyia nini
 
Habari za saizi wakuu,

Poleni kwa majukumu ya kila siku moja kwa moja niende kwenye point.

Kati ya hawa ni yupi mzuri zaidi, mwanaume anaeacha pesa ya matumizi nyumbani na mwanamke ndio anaepanga matumizi au mwanaume anaenunua kila kitu cha ndani na kama kuna matumizi ya ziada yakubidi uombe pesa kwa kutolea maelezo.
Tafuta kazi ya kufanya utakuwa huru wala hautakuwa unawaza kuanzisha uzi wa namna hii.
 
Mko wachache sana wenye hii tabia wenzio sikuizi wanataka wabane kila sehemu
Kuna siku wife nlimuambia kuwa hata kama hii pesa ya gesi nikikaa nayo mimi lazima niitoe tu pale ambapo gesi itaisha hivyo hakuna faida ya kukaa nayo mimi wakati ina matumizi yake ambayo lazima itumike,sasa kukaa nayo nafaidika nini ?

Ingekuwa ukikaa nayo na matumizi yanapungua hapo sawa

Alafu kitu kingine ni kuwa naona inanijazia wallet tu wakati sio yangu ile pesa.

Alafu ukikaa nazo mwanaume pesa za matumizi stress zinazidi unaona unatoa tu pesa,unatoa tu pesa,unatoa tu pesa,unatoa tu pesa,unatoa tu pesa,unatoa tu pesa unatoa tu pesa mpaka unajiuliza heee inakuwaje pesa inaenda hivi,kumbe ungemuachia wife kila kitu wala yasingekuja mawazo hayo
 
Binafsi ingawa sina mke lakini naona ni bora mke awe na uhuru na sehemu yake.

Pangeni budget, ukishajua matumizi yote ya chakula nyumbani ni kiasi gani unatenga fungu unampa. Mwanamume kuanza kudeal na mambo ya jikoni directly ni kukosa kazi.

Mwanamume unapaswa kuwaza mambo makubwa kama ujenzi, ada za WATOTO, kuongeza kipato n.k

Ikitokea emergency mnakaa mnajadili mtatatua vipi.

Hakuna kitu sikipendi kama uko busy umekaa tena sometimes na mgeni unaanza tena kuambiwa mboga ya jana iliisha, au kiberiti kiliisha.
Watu kama wewe ukinitembelea kwangu nakuchinjia mbuzi tunakula huku tukipanga mipango yakuwa watu wenye nguvu zaidi nchini miaka 10 ijayo.

Siyo kujadili mambo ya jikoni huku unakuna kidevu, Kazi ya kike kabisa.
 
Kutoka kwangu mpaka dukani kuna umbali wa 1.5 Km wife hajui kudrive, mwanzo wa mwezi inabidi niende kununua vitu vya jumla vya mwezi mzima!

Kila Jumamosi naenda gulioni namnunulia vitu vya wiki nzima kutokana hivyo hata nikimuachia hela hawezi kudrive kwenda sokoni! Je nakosea!??
1.5km hadi utumie gari?
 
Baadhi ya wanawake unaweza ukaacha pesa na ukapigiwa simu ukirudi njoo na sukari,chumvi na nyanya.

Mimi nanunua vitu vya ndani vya kutumia na pia natoa hela ya emergency mezani.
Ukiona anazingua, unamnunulia mfuko wa sukari kilo 50, unamnunulia mchele kilo 100, unamnunulia chumvi kilo 20, unanunua mafuta lita 50.

Upime tena atamanage vipi
 
Una mawazo ya kizamani sana, sikushauri uoe mchagga au uje uishi huku ughaibuni.
Nadhani huo huenda ni udhaifu wangu. Hata sasa hivi ninakaa na washkaji, huwa sihangaiki na mambo ya manunuzi ya mahitaji ya ndani.

Tulishaona tunakulaje ( chakula common ) tunachanga, mimi nawapa tu hela.

Kama ikitokea tuna hamu ya chakula kingine nje ya budget Mwenye nayo anatoa tu, au tunachanga
 
Back
Top Bottom