Zaka ya 10% unatoa kwenye faida au kwenye utajiri wako?

Zaka ya 10% unatoa kwenye faida au kwenye utajiri wako?

Yes,wanatunza wasiojuweza
Ht kkkt niliyopo mie pia wanafanya hivyo
Na Kuna mchungaji anawatembelea
KKKT ni tofauti na makanisa wezi ya walokole.
KKKT ..kanisa sio mali binafsi ya askofu na pesa zinajulikana zinapoenda ila ulokoleni kanisa ni mali binafsi ya askofu na familia yake,zaka na sadaka ni pesa zinazoenda kunufaishia mchungaji na familia yake
 
KKKT ni tofauti na makanisa wezi ya walokole.
KKKT ..kanisa sio mali binafsi ya askofu na pesa zinajulikana zinapoenda ila ulokoleni kanisa ni mali binafsi ya askofu na familia yake,zaka na sadaka ni pesa zinazoenda kunufaishia mchungaji na familia yake
Hata hayo ya walokole pia yametofautiana
Kuna yenye mifumo ,km Yale makubwa yenye matawi mpk mikoa,Wana utaratibu pia!

Ila haya ya mtu mmoja mmoja ndo hivyo!
Lkn pia mi nimeenda baadhi ya makanisa,nyie acheni tu sadaka unakuta ht elf 20 haifiki!

Hayo mnayoona watu wanakula na yana watu wengi wenye uwezo,watoaji ni machache sn ukilinganisha na ya kawaida
 
Sadaka zinatosha kuendesha kanisa,fungu la kumi ni kuibia waumini tu
Zaka kwa ulimwengu wa leo ni mishahara ya wachungaji au maaskofu. Na ni sawa kwa misingi ya biblia. Zamani makuhani walikuwa wanakula hekaluni kile kilicholetwa na waumini. sasa leo makuhani ni viongozi wetu. sasa changamoto inatakiwa wawe wamenyooka na huduma, ila kituko ni kwamba tunao wachungaji na maaskofu ambao wanapiga huduma wanakusanya zaka na huku wana miradi mingine. Hapo ndo naona shida
 
Habari. Assume wewe ni mfugaji wa Kiebrania. Umepewa urithi wa ng'ombe 100 na baba yako. Ndani ya mwaka wakazaliwa ngombe 20. Ukawa na ng'ombe 120. Wakati wa kutoa zaka unefika.

Je utatoa ng'ombe wawili kama asilimia kumi ya ng'ombe ishirini walioongezeka au utatoa ng'ombe 12 kama asimilia kumi ya ng'ombe 120 ulionao? Vipi mwaka huo upate majanga na kubakiwa na ng'ombe 80. Utatoa zaka kiasi gani?
Zaka ni kodi na inatolewa kutoka kwenye pato lako ghafi, bahati mbaya watu siku hizi wanakatwa makato mengi sana kwenye mapato yao, hakuna zaka tena, labda kama unataka kujifurahisha na kuwafurahisha watu. Umeshatoa kodi ya mapato kwenda kughalimia huduma ambazo zilikuwa zinaghalimiwa na zaka enzi hizooo wakati dini zinaundwa.
 
Zaka ilikuwa katika mfumo wa mazao,
Katika kila mafungu kumi (moja la kumi ndilo hutolewa kama zaka) ambayo ni sawa na asilimia kumi ya kile ulichokipata wakati wa mavuno,
Same na mshahara ama biashara
Kwahiyo Zaka Ndio fungu la 10?
 
Na nauli ni makato pia, mana hizo ni expenses za kazi,

Halafu jibu swali, Zaka inakatwa on revenue or Profit ?
Hakuna in between
Mi sio mwajiriwa,sijawahi kuwa mwajiriwa
Kwahiyo hata sijui unachouliza mkuu😅
 
Habari. Assume wewe ni mfugaji wa Kiebrania. Umepewa urithi wa ng'ombe 100 na baba yako. Ndani ya mwaka wakazaliwa ngombe 20. Ukawa na ng'ombe 120. Wakati wa kutoa zaka unefika.

Je utatoa ng'ombe wawili kama asilimia kumi ya ng'ombe ishirini walioongezeka au utatoa ng'ombe 12 kama asimilia kumi ya ng'ombe 120 ulionao? Vipi mwaka huo upate majanga na kubakiwa na ng'ombe 80. Utatoa zaka kiasi gani?
Kitendo cha kupewa tu hapo lazima katika hao Mia toa ng'ombe 10 zaka kwanza
 
Kwa kifupi 10% ni kwa kila ulichopata! Umepewa ng'ombe 100 unapaswa kutoa 10% kwa mara ya kwanza.
Baada ya hapo unaanza kutoa 10% ya Faida.
Sasa ukikutana na Wachungaji waliojaa tamaa ya hela,watakwambia ni 10% ya (Mtaji +Faida) kila mwezi! Ukifilisika wanakutimua Kanisani.
Wakitaka kukubana vizuri wanakupa Fomu ya kujaza! Unatakiwa kujaza vyanzo vyako vya mapato yote, kazi, biashara, zawadi, nk harafu wanakukadiria kiwango cha kutoa kila Mwezi.
Sasa kwa mfanya biashara wanakukadiria (Mtaji + Faida)! Sasa bila kujali kuwa biashara yako inaweza kukwama na usipate Faida, hilo hawaangalii.
Usipotoa unaitwa Mwizi, ukikwama zaidi wanakwambia umekufa kizaka!
Shughuli ukisema unajifufua, sikiliza mtiti wake!!
Shalom kaka.. Hahaha eti kujifufua
 
Back
Top Bottom