Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Hao TFF na Ally Kamwe ni binadamu kama wewe je hawawezi kukosea? Basi ili wawe wamepatia kauli zao basi niambie hao Stella walicheza caf super cup dhidi ya nani katika ufunguzi wa pazia jipya la msimu wa 1994? Nina uhakika asilimia 100 USM anaenda kucheza caf super cup dhidi ya Al Ahly. Basi njoo na uthibitisho au ushahidi kuwa Stella walicheza caf super cup kama ambavyo leo hii USM Alger anavyocheza caf super cup dhidi ya Al Ahly. Kumbe unaonesha ni mtu wa kufuata mkumbo tu kichwani utaki kujishughulisha.
Kwani Caf super cup hicho kipindi ilikuwa imeanzishwa na kama ilikuwepo ilichezwa kati ya timu ipi na ipi na mshindi ilikuwa timu ipi
 
Kwani Caf super cup hicho kipindi ilikuwa imeanzishwa na kama ilikuwepo ilichezwa kati ya timu ipi na ipi na mshindi ilikuwa timu ipi
.
IMG_20230426_074839.jpg
 
Kwani wewe Mkuu sio binadamu?

Umekomalia hapo kwenye Super Cup, kwani haiwezekani sheria zilizotumiwa kipindi hicho ni tofauti?
Kumbe unabisha halafu hujui unachokibishia ni kipi. Tunalinganisha je kati ya CAF cup na Africa cup winner's cup ni ipi ilikuwa ni mashindano sawasawa na Caf confederation cup iliyopo sasa. Sawa unaposema sheria zilizotumiwa kipindi hiko ni tofauti sio hoja kwasababu sheria hizo hizo ulizodai ni tofauti ndio hizo hizo zinafanana na wanaoshiriki caf confederation cup kwa hivi sasa.

Kuna vigezo viwili vikuu katika huo ulinganifu
1) je kati ya Caf cup na Africa cup winner's cup ni timu ipi inaenda kucheza na timu inayobeba ubingwa wa klabu bingwa (sheria hii ipo sawasawa na caf confederation cup)

2)Je kati ya CAF cup na Africa cup winner's cup, ni mashindano yapi yalikuwa ni kwaajili ya washindi wa kombe la FA ( caf confederation cup ni mashindano kwaajili ya wanaobeba kombe la FA) na ndio maana kila association member wa CAF ni lazima awe na mashindano ya FA.

Sheria za caf confederation cup ilikuwa ni sawasawa na Africa cup winner's cup
 
Basi wangetumia neno "limefutwa" badala ya mashindano hayo mawili "yameunganishwa". Maneno yana maana, hatuyatumii tu.
Haujaelewa nilichokimaanisha ni kipi. Nilichomaanisha ni kwamba jina tu ndio limebadilishwa kuwa caf confederation cup lakini sheria na utaratibu ni ule ule kama ilivyokuwa zamani Africa cup winner's cup.
 
Kwani Caf super cup hicho kipindi ilikuwa imeanzishwa na kama ilikuwepo ilichezwa kati ya timu ipi na ipi na mshindi ilikuwa timu ipi
Super cup ilichezwa kati ya Zamalek vs Al Ahly ( mshindi wa Africa cup of champions club VS Africa cup winner's cup)
IMG_20230616_081151.jpg
 
TFF waje waweke hili sawa...
Issue ya takwimu mbona jambo la a msingi tu na jepesi?
 
Kwahiyo Mtibwa sugar hajawahi kubeba hii ndoo ya TPL? ZAKA ZA KAZI nae tapeli tu
 
Haujaelewa nilichokimaanisha ni kipi. Nilichomaanisha ni kwamba jina tu ndio limebadilishwa kuwa caf confederation cup lakini sheria na utaratibu ni ule ule kama ilivyokuwa zamani Africa cup winner's cup.
Kwani CCM ikivyoweka neno "Mapinduzi" katika jina lake, inamaanisha ASP ndiyo kama iligeuzwa kuwa CCM na TANU ikafutwa tu?
 
Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...

Soma sehemu ya pili hapa

Soma sehemu ya tatu hapa

Soma sehemu ya nne hapa
KMKM, Malindi zinatoka wapi kwenye ligi yetu ya bara. Anaweka na mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania badala ya Tanzania Bara.

Akili yake ni ya kisoda kama yako.

Asichanganye ligi kuu ya Tanzania Bara na ligi kuu ya (Tanzania) Muungano
 
Tate Mkuu
changaule

Mnalolote la kusema?
Akili za kisoda kama huyo Zakazaka

Hapa chini orodha kamili ya historia ya ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara tangu mwaka 1965:

1965 Sunderland (Simba SC)
1966 Sunderland (Simba SC)
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans Sc
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans Sc
2006 Young Africans Sc
2007 Simba SC
2007-08 Young Africans Sc
2008-09 Young Africans Sc
2009-10 Simba SC
2010-11 Young Africans
2011-12 Simba SC
2012-13 Young Africans
2013-14 Azam FC
2014-15 Young Africans
2015-16 Young Africans
2016-17 Young Africans
2017-18 Simba SC
2018-19 Simba SC
2019-20 Simba SC
2020-21 Simba SC
2021-22 Young Africans SC
2022-23 Young Africans SC

Hii ni LIGI KUU TANZANIA BARA na si LIGI KUU YA TANZANIA (MUUNGANO)
 
Kwa source niliyoisoma mimi inaonesha kuwa mwaka 1988 bingwa wa ligi ya Tanzania bara alikuwa ni Coastal union, na mwaka 1989 na mwaka 1992 kombe la ligi ya Tanzania bara alibeba Yanga. Je ipi ni sahihi?
Uko sahihi
 
Sehemu ya Tano
Screenshot_20230616-101824.png


Ukiwauliza wale jamaa kwamba hayo mataji 43 wanayomiliki kwa pamoja ni ya ubingwa wa mashindano gani, watakujibu kuwa ni ligi ya bara.

Hapa ndipo wanapojifichia kwa kuwa hatuna udadisi na tunakosa vitengo vya rekodi, kumbukumbu na historia kwenye taasisi zetu za mpira.

Kimsingi ni kwamba Ligi ya Bara haikuishi miaka mingi kiasi cha kutoa mataji yote hayo.

Ilianza mwaka 1982 na kuisha mwaka 2003...miaka 21 tu. Yanga mara 11 na Simba mara 6!

Sasa wao wanayahesabu mataji haya na kuyachaganya na yale ya ligi ya kwanza ya 1965 hadi 1981, kisha wanahesabu mataji ya ligi ya sasa, ndiyo wanapata 43!

Iwe kwa kutojua au kwa makusudi, hayo ni makosa makubwa.

Ligi iliyoanza 1965 haikuwa ya Bara, ilikuwa ya Muungano na hata vilabu vya Zanzibar vilishiriki, kama nilivyofafanua kwenye sehemu zilizopita.

Kwa hiyo bingwa wa ile ligi ya zamani hakuwa wa bara, alikuwa wa Muungano.

Wao kama wanataka kuhesabu mataji ya bara pekee, basi wahesabu ya 1982 hadi 2003...kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa ligi ya bara.

Ligi iliyoanza 1965 kama klabu bingwa ya taifa, ilikuwa ya muungano na kuanzia 1982, ikabadishwa jina muundo na mfumo.

Jina la kwanza lilikuwa Klabu Bingwa ya Taifa, jina jipya likawa Ligi ya Muungano.

Muundo wa kwanza ulikuwa kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa, muundo mpya ukawa wa madaraja, la kwanza hadi nne, kutokea pande zote mbili za Muungano.

Mfumo wa kwanza ulikuwa kwa mtoano, muundo mpya ukawa wa mzunguko, nyumbani na ugenini na kuhesabu alama.

Lakini licha ya mabadiliko hayo, bingwa alibaki na hadhi ile ile, yaani kutambuliwa na FIFA na CAF na kupata tiketi ya kushiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika.

Sasa hawa jamaa wanaacha kuhesabia ubingwa wa ligi ya muungano wa kuanzia 1982 hadi 2003, wanahesabu ubingwa ile ligi ya bara ambayo ilikuwa sawa na mtihani wa moko.

Kwa sababu kwenye hiyo ligi ya Muungano hawakupata mataji mengi hivyo haina maana kwao.

Kwa hiyo wanajifariji kwa kuwa Tanzania One kwenye Moko na kujitangaza walifaulu, kisha wanayaacha matokeo ya mtihani wa taifa kwa sababu walipata Zero!

Itaendelea...
 
Akili za kisoda kama huyo Zakazaka

Hapa chini orodha kamili ya historia ya ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara tangu mwaka 1965:

1965 Sunderland (Simba SC)
1966 Sunderland (Simba SC)
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans Sc
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans Sc
2006 Young Africans Sc
2007 Simba SC
2007-08 Young Africans Sc
2008-09 Young Africans Sc
2009-10 Simba SC
2010-11 Young Africans
2011-12 Simba SC
2012-13 Young Africans
2013-14 Azam FC
2014-15 Young Africans
2015-16 Young Africans
2016-17 Young Africans
2017-18 Simba SC
2018-19 Simba SC
2019-20 Simba SC
2020-21 Simba SC
2021-22 Young Africans SC
2022-23 Young Africans SC

Hii ni LIGI KUU TANZANIA BARA na si LIGI KUU YA TANZANIA (MUUNGANO)
Tupe chanzo tujisomee wenyewe, vinginevyo utakuwa unarudia kile kile alichokifanya Zakazakazi
 
Simba bingwa mara 22.

Ifuatayo ni miaka ambayo simba amechukua ubingwa.

1965,1966, 1973, 1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1993, 1994, 1995, 2001, 2002, 2003, 2004, 2007, 2009–10, 2011–12, 2017–18, 2018–19, 2019–20, 2020–21.

Sources' Trust me bro.
Imekuaje 2002 Simba na Yanga mabigwa
 
Sehemu ya TanoView attachment 2659398

Ukiwauliza wale jamaa kwamba hayo mataji 43 wanayomiliki kwa pamoja ni ya ubingwa wa mashindano gani, watakujibu kuwa ni ligi ya bara.

Hapa ndipo wanapojifichia kwa kuwa hatuna udadisi na tunakosa vitengo vya rekodi, kumbukumbu na historia kwenye taasisi zetu za mpira.

Kimsingi ni kwamba Ligi ya Bara haikuishi miaka mingi kiasi cha kutoa mataji yote hayo.

Ilianza mwaka 1982 na kuisha mwaka 2003...miaka 21 tu. Yanga mara 11 na Simba mara 6!

Sasa wao wanayahesabu mataji haya na kuyachaganya na yale ya ligi ya kwanza ya 1965 hadi 1981, kisha wanahesabu mataji ya ligi ya sasa, ndiyo wanapata 43!

Iwe kwa kutojua au kwa makusudi, hayo ni makosa makubwa.

Ligi iliyoanza 1965 haikuwa ya Bara, ilikuwa ya Muungano na hata vilabu vya Zanzibar vilishiriki, kama nilivyofafanua kwenye sehemu zilizopita.

Kwa hiyo bingwa wa ile ligi ya zamani hakuwa wa bara, alikuwa wa Muungano.

Wao kama wanataka kuhesabu mataji ya bara pekee, basi wahesabu ya 1982 hadi 2003...kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa ligi ya bara.

Ligi iliyoanza 1965 kama klabu bingwa ya taifa, ilikuwa ya muungano na kuanzia 1982, ikabadishwa jina muundo na mfumo.

Jina la kwanza lilikuwa Klabu Bingwa ya Taifa, jina jipya likawa Ligi ya Muungano.

Muundo wa kwanza ulikuwa kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa, muundo mpya ukawa wa madaraja, la kwanza hadi nne, kutokea pande zote mbili za Muungano.

Mfumo wa kwanza ulikuwa kwa mtoano, muundo mpya ukawa wa mzunguko, nyumbani na ugenini na kuhesabu alama.

Lakini licha ya mabadiliko hayo, bingwa alibaki na hadhi ile ile, yaani kutambuliwa na FIFA na CAF na kupata tiketi ya kushiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika.

Sasa hawa jamaa wanaacha kuhesabia ubingwa wa ligi ya muungano wa kuanzia 1982 hadi 2003, wanahesabu ubingwa ile ligi ya bara ambayo ilikuwa sawa na mtihani wa moko.

Kwa sababu kwenye hiyo ligi ya Muungano hawakupata mataji mengi hivyo haina maana kwao.

Kwa hiyo wanajifariji kwa kuwa Tanzania One kwenye Moko na kujitangaza walifaulu, kisha wanayaacha matokeo ya mtihani wa taifa kwa sababu walipata Zero!

Itaendelea...

Upo tayari kujibu maswali ya uthibitisho maana unaweka muendelezo wa ku copy na ku paste maneno ya Zaka Zakazi huku hoja za nyuma umeshindwa kujibu. Haya tuje kwenye muendelezo wako, Zaka Zakazi anasema tokea mwaka 1965 ligi ilikuwa ni ya muungano, naomba njoo na uthibitisho wa hili kwa kuonesha timu za Zanzibar zilizoshiriki ligi ya mwaka 1965
 
Sehemu ya TanoView attachment 2659398

Ukiwauliza wale jamaa kwamba hayo mataji 43 wanayomiliki kwa pamoja ni ya ubingwa wa mashindano gani, watakujibu kuwa ni ligi ya bara.

Hapa ndipo wanapojifichia kwa kuwa hatuna udadisi na tunakosa vitengo vya rekodi, kumbukumbu na historia kwenye taasisi zetu za mpira.

Kimsingi ni kwamba Ligi ya Bara haikuishi miaka mingi kiasi cha kutoa mataji yote hayo.

Ilianza mwaka 1982 na kuisha mwaka 2003...miaka 21 tu. Yanga mara 11 na Simba mara 6!

Sasa wao wanayahesabu mataji haya na kuyachaganya na yale ya ligi ya kwanza ya 1965 hadi 1981, kisha wanahesabu mataji ya ligi ya sasa, ndiyo wanapata 43!

Iwe kwa kutojua au kwa makusudi, hayo ni makosa makubwa.

Ligi iliyoanza 1965 haikuwa ya Bara, ilikuwa ya Muungano na hata vilabu vya Zanzibar vilishiriki, kama nilivyofafanua kwenye sehemu zilizopita.

Kwa hiyo bingwa wa ile ligi ya zamani hakuwa wa bara, alikuwa wa Muungano.

Wao kama wanataka kuhesabu mataji ya bara pekee, basi wahesabu ya 1982 hadi 2003...kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa ligi ya bara.

Ligi iliyoanza 1965 kama klabu bingwa ya taifa, ilikuwa ya muungano na kuanzia 1982, ikabadishwa jina muundo na mfumo.

Jina la kwanza lilikuwa Klabu Bingwa ya Taifa, jina jipya likawa Ligi ya Muungano.

Muundo wa kwanza ulikuwa kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa, muundo mpya ukawa wa madaraja, la kwanza hadi nne, kutokea pande zote mbili za Muungano.

Mfumo wa kwanza ulikuwa kwa mtoano, muundo mpya ukawa wa mzunguko, nyumbani na ugenini na kuhesabu alama.

Lakini licha ya mabadiliko hayo, bingwa alibaki na hadhi ile ile, yaani kutambuliwa na FIFA na CAF na kupata tiketi ya kushiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika.

Sasa hawa jamaa wanaacha kuhesabia ubingwa wa ligi ya muungano wa kuanzia 1982 hadi 2003, wanahesabu ubingwa ile ligi ya bara ambayo ilikuwa sawa na mtihani wa moko.

Kwa sababu kwenye hiyo ligi ya Muungano hawakupata mataji mengi hivyo haina maana kwao.

Kwa hiyo wanajifariji kwa kuwa Tanzania One kwenye Moko na kujitangaza walifaulu, kisha wanayaacha matokeo ya mtihani wa taifa kwa sababu walipata Zero!

Itaendelea...
Hii ni post ya kufunga mjadala. Alichobakisha sasa ni kutandika mkeka rasmi wa mwisho kuonyesha miaka hiyo ambayo kulikuwa na Ligi ya Muungano, Bingwa alikuwa nani, na miaka hiyo ambayo hakukuwa na Ligi ya Muungano, Bingwa wa Bara alikuwa nani. Mahesabu tutapiga wenyewe.

Yanga acheni upotoshaji. Zama zimebadilika hiziii 🤣😂🤣
 
Back
Top Bottom