Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Uzuri mi nimeweka chanzo, we umeweka maneno tupu.

Utaaminika na nani?
 
Achana na Google muzeye, ndo maana kuna sehemu ya edit, niambie ni lini Malindi na KMKM alishiriki Ligi ya Bara, tuanzie hapo.
Si ndio hoja ya Zakazakazi ilipo, kuwa kuna washindi wa ligi ya Muungano ambao walihesabu ubingwa huo kama ligi kuu.
 
Ukihesabu hapa unaona kabisa Yanga kachukua ubingwa mara 24View attachment 2658337

Hizi data sio za kweli

Majimaji,Mtibwa,Prison,Coastal ,Azam zimechukua ubingwa mara moja moja tu na hakuna timu ya Zanzibar iliyochukua ubingwa wa bara 1993 Yanga ndio alikuwa Bingwa akaenda Uganda kuchukua kombe la Africa Mashariki
 
Hicho sio kitu alicho maanisha Zakazakazi.

Hata Gongowazi wenzio wanapinga ligi ya Muungano kuihesabia kama ligi kuu.
 
Zinaweza zikawa hazina manufaa kwasababu upande mmoja utaenda kuonekana ni inferior kwakua utakuwa downgraded

Ila kwanini tuache kusema ukweli ili kuzuia takwimu za uongo zisiendelee kumea?
Hivi wewe tunavyokuheshimu humu kumbe tunafanya kazi bure? Hivi unawezaje kuleta takwimu za Tanzania Prisons kubeba ubingwa wa Tanzania 1999 halafu tukae tukusikilize? Mrudishie takwimu zake zitamsaidia ligi ya Mapinduzi.
 
Hivi wewe tunavyokuheshimu humu kumbe tunafanya kazi bure? Hivi unawezaje kuleta takwimu za Tanzania Prisons kubeba ubingwa wa Tanzania 1999 halafu tukae tukusikilize? Mrudishie takwimu zake zitamsaidia ligi ya Mapinduzi.
Msiwe mnakosoa kienyeji, hiyo ni Wikipedia na tunafahamu kuwa haiwezi kuwa 100% hivyo tunafahamu uwezekano wa taarifa kuwa ndivyo sivyo, ila critics mnapaswa kuja na hoja kutoka trustable sources sio kubeza.

Na kama utakumbuka hadi website ya Yanga iliwahi kutumia hizihizi data na picha mpaka leo tunazo.



Soma hapo juu hiyo ilikuwa ni screenshot ya 2022 ambapo Yanga alikuwa bingwa, na kwenye rekodi ikaonekana ni bingwa mara 27.

Hesabu hiyo miaka hapo kama inatimia 27

Kipindi ligi yetu inaanza hakukuwa na mfumo mzuri wa kutunza data tofauti na wenzetu, sasa linapokuja swala kama hili ukifika muda wa kupendekeza source ya kuaminika inakuwa vigumu.

Kwasababu historia haikuhifadhiwa kwenye mfumo rasmi unaotambulika bali zilikuwa local recorded.
 
Mara nyingi na ignore replies zako ili nijilindie heshima ila leo nakublock rasmi, usihangaike kujibu post zangu maku wee.

Kama mnafuata standard za Ulaya, na hiyo treble ya juzi mliyofanyia gwaride na tamasha nayo inafuata standard za Ulaya?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Inaonekana mwaka 1993 Simba anapofika fainali ya CAF, kulikuwa na mashindano mengine ya Abiora.

Ulikuwa ni mwaka ambao una mashindano mengi sana

Asante kwa kunijuza ndio naskia kwako.
Mshindi wa hilo kombe alicheza super cup?
 
Kutuambia kwamba African sport na Pamba fc zilishawahi kuwa mabingwa wa ligi yetu ya bara ni uongo mkuu. Wala binafsi sihitaji kuendelea kuona na makala zake za upotoshaji.
Ana kijiji chake cha wajinga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…