Zanzibar ni nchi huru au ni sehemu ya Tanzania?

Ni nchi Ila unaweza kukusanya watu wote kwa kupiga filimbi


Mzee Aboud “Mmasai”


Khiyana imekuwa kubwa, kubwa sana. Na hii yote, kwa sababu mbili. Sababu ya kwanza, ni ujinga wa Karume.

Yeye alikuwa na khofu na watu walokuwa na ilimu, hata mapinduzi bado.

Aliwahi hata kuhutubia kusema “wakimbieni wenye ilimu.” Na sababu hizo ndo akenda kujiunga moja kwa moja na Nyerere bila ya kumshauri mtu kwamba asipinduliwe na hawa halafu wataleta Waarabu. Mimi nilikuwa sijui habari za muungano. Pia Babu alikuwa na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na yeye alikuwa hajuwi habari hio. Mimi nilikuwa nakwenda kazini, nafika kwa Sapriji, mbele si kuna duka la yule Muhindi anatengeneza radio anaitwa Dawud, nimesikia radio pale inasema juu, habari za muungano. Babu akasema yeye hajuwi habari hizo na yeye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje. Na Nyerere kakubali kwa makusudi kuitawala Zanzibar. Hichi ndicho ninachokiamini. Sababu moja ni hiyo ya Karume, ya pili ya Nyerere kukubali bila ya kuwashauri wananchi.

Halafu Karume Mawaziri wote walosoma kawapeleka bara. Kina Babu, kina Idris, Hasnu Makame. Wote wamepelekwa bara wakawa wanacheza ngoma huko. Na ndivo inavotawaliwa Zanzibar, manake mpaka leo hakuna Bunge la Muungano. Kuna Bunge la Tanganyika. Lina watu mia sita na ngapi, na watu wa Zanzibar wametiwa ndani watu khamsini, watafanya nini ndani yake?

Kinachotawaliwa kwenye muungano si idadi ya watu, bali ni mambo ya nchi za nje na ulinzi.1 Zanzibar ina nguvu yake kama Tanganyika hata kama Tanganyika ina mamilioni ya watu zaidi. Zanzibar ni nchi huru kama weye wa Tanganyika. Ningelikuwa mimi ni mtu wa kisiasa sitokubali. Namshukuru Mungu nalisema, mara tu baada ya kutangazwa muungano ikiwa kuwa hatuna Bunge la Muungano, tena mbele ya Bhoke Munanka, alikuwa ofisi yake Beitlajaibu, Waziri wa Mambo ya Muungano “ikiwa hatuna Union Parliament, Bunge la Muungano hatuwezi kulichukuwa Bunge la Tanganyia tukalifanya ni Bunge la Muungano.”

Udhaifu wa watu wetu wote hawaitetei hii Zanzibar. Nadhani kama Hanga alikuwa akiitetea ilikuwa ndo sababu ya kuuliwa. Mimi sikusikia kama aliwahi kuitetea Zanzibar. Hanga alitaka kufanyisha nishani kwa walioshiriki kwenye mapinduzi kwa sababu ni kujionyesha na kujiaminisha kwa watu. Na watu walopigana wawe na furaha. Mwalimu akamkubalia halafu akamuuwa.



source: Kwaheri uhuru kwaheri ukoloni
 
Aisee! Asante sana kwa mchango mzuri. Nina imani bado tunahitaji kujifunza zaidi kuhusu muungano wetu. Lakini kwaninin malalamiko haya yapo pande zote? Bara wanaona kama Zanzibar inanufaika zaidi na muungano kuliko Tanganyika. Mfano, Mikopo kutoka taasisi za fedha za kimataifa, hukopwa kwa jina la Tanzania na kisha marejesho ya mkopo hufanyika kwa jina la Tanzania. Je, kuna kipengele chochote katika katiba yetu ambacho hutaja asilimia ambazo zanzibar wanatakiwa kuchangia kurudisha mkopo hali kadhalika Tanganyika vile vile? Maana ninavyoelewa, mikopo hii imekuwa ikigawanywa bara na visiwani. Vipi kuhusu mgawanyo wa ajira katika pande zote mbili? vipi kuhusu mgawanyo wa matumizi wa rasilimali asilia za muungano?
 

Msikilize huyu Mwinyi , hii ni miezi miwili tu iliyopita, Zanzibar haipati chochote kwenye mikopo inayokopa Tanganyika / Tanzania

 
Uamsho walishtakiwa ila hawakufungwa.
 
Zanzibar siyo dola huru kwa sababu:

Haina kiti UN na haitambuliki Kimataifa kama dola yaani state. Vigezo vingine vya kuwa dola vipo ila kimojawapo pekee cha uhuru wa Kimataifa yaani external sovereignty haina.
Mkuu, bado unaendelea na huu msimamo, au umebadilika ?
 
Mkuu, bado unaendelea na huu msimamo, au umebadilika ?
Siyo msimamo wangu. Ni msimamo wa Sheria za Tanzania na zile za Kimataifa. Rejea pia case ya Machano Hamis Machano iliyoamuliwa na Mahakama ya Rufaa ya Tanzania
 
Zanzibar ni chawa wa Tanganyika.
Kama Zanzibar ni Chawa wa Tanganyika basi huyo chawa ni mkubwa kiasi kwamba humfunika Tanganyika kwa kiasi kikubwa saana,

Kifupi ni kwamba Tanganyika lilikuwa koloni la wa Oman, muda wote walipokuwa Zanzibar, Hivyo kabla ya uhuru kwa chini chini kulikuwa mapatano ya kuipa uhuru Tanganyika but Not Zanzibar ili waoman waendelee kutawala remotely, and this has been accomplished.

Sent from my TA-1004 using JamiiForums mobile app
 
Kasome Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema hivi endapo itatungwa sheria yoyote inayokwenda kinyume na Katiba hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hiyo sheria ni batili kwa hiyo ile sheria iliyotungwa na baraza la Wawakilishi kwamba Zanzinzibar ni nchi ni batili.
 
Ndiyo maana Tanganyika hulazimisha kumweka kibaraka wao kila unapokuja Huo unaoitwa uchaguzi
 
Unaweza kutuletea ushahidi wa ulichokiandika
 
Hapo mwisho umejijibu mwenyewe. Sera ya Ccm ni Serekali mbili kuelekea moja. Yaani nia na madhumuni ya CCM ni kuona siku moja Zanzibar inamezwa na kua mkoa. Haya unayoyaona sana ni kama peremende tu tumepewa Wazanzibari na in fact ni small price Tanganyika paid to swallow Zanzibar.
 
Msikilize huyu Mwinyi , hii ni miezi miwili tu iliyopita, Zanzibar haipati chochote kwenye mikopo inayokopa Tanganyika / Tanzania

mwanzo nlikuwa na hasira sana nkidhan wanapata mgao na walipaji ni bara lkn baada ya kuona hii clip kidg afadhal acha wanyonywe tu kama bara ndo anakopa na wanalipa wao wenyewe kuna shida gani na ili haya yaishe zanzibar ifanywe mkoa tu lakini kilichopo sasa lawama hazitakuj isha wabara tunalaum kama kote ni tanzania kwann tuingie kwa vibal zenji na kwann haturuhusiwi kumiliki ardhi wakat huo wazanzibar bara wamejaa na wanamiliki ardhi ,kuwe na rais mmoja, bunge moja na mamlaka moja kama ilivyo kwenye jeshi hapa ndo kelele zitaisha unless otherwise Muungano ufe maan kila mmoja ataona ananyonywa na mwenzie
 
Ndiyo maana Tanganyika hulazimisha kumweka kibaraka wao kila unapokuja Huo unaoitwa uchaguzi
Hata ungekuwa ni wewe kutoka huko unakodhani wanakandamizwa ni lazima uitii Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali anayekandamizwa ni nani kinyume na hapo utakandamizwa wewe.
 
Hata ungekuwa ni wewe kutoka huko unakodhani wanakandamizwa ni lazima uitii Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali anayekandamizwa ni nani kinyume na hapo utakandamizwa wewe.
Hiyo Katiba ianze kufuatwa na hao walioiandika . Chaguzi zote zinafanywa kwa kuzivunja katiba na kanuni Za uchaguzi. Tuanzie hapo kwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…