Ziara ya Rais Samia nchini Kenya, Mama anakosea

Ziara ya Rais Samia nchini Kenya, Mama anakosea

Napenda kuandika kidogo tu kulingana na uwelewa wangu juu ya Ziara ya Mama nchi Kenya na mikataba mlio tiana sign.

1. Ujenzi wa bomba la gas kutoka Tanzania kwenda Mombasa kwa ajili ya matumizi ya viwanda nchini Kenya,hapa mama unefail pakubwa sana maana yake nikwamba bidhaa za Kenya zitakuwa zinazalishwa kwa gharama nafuu zaidi na kuteka soko la Africa Mashariki kuliko Tanzania. Tutarudi miaka ya nyuma tena kila kitu Made in Kenya.

a. Hii sera yetu ya viwanda itakufa maana hatuweza kushindana tena na product kutoka Kenya na vijana wetu watazidi kuwa wachuuzi wa bidhaa kutoka nje.

b. Kenya itatumia mwanya huu kuvutia wawekezaji kutoka nje kuwekeza Kenya kuliko kuja kuwekeza Tanzania.

c. Tunasafirisha gas kama kuna surplus ya viwanda vyetu na matumizi yetu kama Taifa.Viwanda vyetu bado vinahitaji nishati ya gas lakini bado upatikanaji wake umekuwa mgumu na kwa gharama kubwa

d. Kenyatta amecheza karata yake vizuri katika ujenzi wa gas kuliko Mama sijui washauri wake wamekwama wapi natarajia kuona Kenya ikinufaika zaidi katika utawala wa Mama kuliko kipindi chochote kile katika historia ya Tanzania na Kenya.

2. Ushirikiano wa anga..hapa Kenyatta anatafuta namna ya kuisaidia Kenya airways..inakwenda ku dominate soko na anga tena kama huko nyuma.hapa kumbuka faidia kubwa ya Kenya Airways inatokana na safari za Tanzania. Dsm, Zanzibar na Kilimanjaro.

Hapa tutalajie Air Tanzania ikifa kifo cha mende kutokana kutoweza kumudu ushindani na Kenya airways. Otherwise kufanyike changes za haraka katika Management ya Air Tanzania.

3. Soko la utalii hapa Kenyatta amecheza vizuri kama pele.
Tutalajie kuona vijana wetu wakiwa watazamaji kama kipindi cha nyuma na soko la utalii nikirudi mikononi mwa wakenya tena.(hapa kwenye utalii wenye fan zao wanaweza kudadavua kwanini Kenyatta amecheza kama Pela)

4. Biashara sioni jipya ni yale yale, hapa Mama ametoka 0-0

Note: Mama washuri wake wamshauri vizuri kabla yakwenda kufanya mikataba kwa niaba ya Watanganyika. Otherwise akubali kutuachia Tanganyika yetu!
Amesha saini, jinyonge.
 
Hizi ni akili za mataga tu. Hujui hata dhana ya competitive advantage?! Sisi tutapata kuinua uchumi wetu kupitia mauzo ya gesi huko Kenya, wao watapata kuinua uchumi wao kupitia kupunguza gharama za kusindika bidhaa ya viwandani. Kila upande unapata - win-win position.
Mkuu, "competitive advantage" ipo wapi hapa, mbona siioni?
Binafsi naona kama umewahi sanaaa hili la bomba gesi wamekubaliana kutafuta pesa zaa ujenzi wa ilo bomba naa bado hayo mazungumzo hayajaisha...

Ukisemea la gesi kwann una sahau kusemea pia la MW 400, ambazo tayyari project ni on going uwekaj wa njianza kusafirishia huo umeme kwenda kenya na hii ilisainia na mpendwa wetu
Usiwe na shaka mkuu, mengi ya haya uliyosikia hapo ni kulisha upepo tu!

Kama bomba hilo litajengwa, huo si mpango wa leo wala kesho. Huenda hata Samia mwenyewe asilione hilo bomba lina picha gani.

Haya mambo mengine ni ya kupandisha 'pressure' za watu bila ya sababu zozote za maana.
 
1. Nadhani wewe ndiye huelewei alliances za mashirika kuwa ni kwenye codeshare, kwamba abiria mwenye ticket ya shirika moja anaweza kusafirishwa na kampuni nyingine kwenye njia wanazoshirikiana. Vile vile aliance hizo huzuia partners washindanie njia, yaani husitumie njia ambayo partner wakao anatumia. Kwa hali hiyo partnership ya KQ na ATCL itaweza kuifanya ATCL isishindanie njia nyingi ambazo tayari ni za KQ.

2. Kuhusu hasara uanikuza hasara ya ATCL kupita kiasi. CAG alikuwambia sehemu kubwa za kinachoitwa hsara siyo hasara itokanayo kuendesha biashara vibaya bali ni mlundikano wa madeni ya zamani na tozo za serikali, ambazo rais SSH ameahdii kuzindoa. Sasa wewe kudai kuwa ni kutokana na volume ya capitala pia huenda hujsaoma mahesabu ila unatafuta ama kuhalalisha hasara za KQ au kuzidi kudharau operations za ATCL.

ATCL ilipata hasara ya TSh 150b kwa mwaka ambazo ni sawa na US$ 64.7m ambao ni wastani wa USD5.9m kwa kila ndege (fleet ya ATCl ni ndege 11); KQ ilipata hasara ya KSh 36.2b ambazo ni sawa na US$338.63m ambao ni wastani wa USD 8.5m kwa kila ndege (fleet ya KQ ni ndege 40). Kwa akili yako ni kampuni gani iliyopata hasara kubwa hasa ukigundua kuwa KQ hawalipii uwanja wa JKIA wakati ATCL inalipia kutumia JNIA.
Hili ni jibu lililofanyiwa kazi.
Hongera.
 
Sio kwa wakenya ninao wajua mimi...... Yaani wao wakuache wewe ukafungue biashara kwao kule..... Labda Uganda sio kenya.....
But kunao waTz weengi wenye biashara kubwa na ndogo pia. Wachaga wamejaa kwenye biashara ya nguo za mtumba. Kama hujui Kenya ni a country where you can own land ukiwa foreigner. No one can take that from you. Hata serikari haiwezi kuichukua. Fanya utafiti wako.
 
Mtoa Mada naona hajatizama hili jambo kwa upana. Kwanza anasema unauza Gas bidhaa zao zitakuwa rahisi sasa viwanda vyetu wanashindwa nini kutumia hiyo Gas na bidhaa zao ziwe rahisi na pia sisi tunauza Gas sio kutoa msaada. Mambo ya ndege Air Tanzania haishindani na Kenya soko ni kubwa na kila mtu anashindana kama unaona Kenya huiwezi sasa hao kina Qatar, Emirates, Flydubai na Ethiopia ukiondoa Emirates wote wanatua kilimanjaro ila ameona Kenya airways tu, hawa wanaleta watalii kama humtaki Kenya wakatae na wengine. Dubai wana mandege kibao lakini ndege za nchi nyingine zote zinatua kwao sijasikia wakisema tunazo ndege za kutosha hatutaki ndege zingine. Tatizo kubwa sisi tunaogopa sana ushindani dunia hii biashara ni ushindani unadhani Fast jet tungewaacha wakashindana na Air Tanzania na bei zingeshuka kwa faida ya mteja ila wakawaondoa ili bei wa control.
Shida inayotusumbua wengi ni mawazo ya inward looking na protectionalism by 100% we need strategically to balance.
 
Hoja zako zote ziko wrong.

Kuhusu gesi.
Hadi sasa hakuna uhaba wa gasi kwa matumizi ya Tanzania. Bomba la kusafirisha gesi toka Mtwara hadi sasa linafanya kazi chini kabisa ya uwezo wake haifikii hata asilimua 50. Hakuna kiwanda cha ndani kinachohitaji gesi ya Mtwara na kinashindwa kupata. Kuuza gesi Kenya kutasaidia bomba la gesi liweze kuwa utilised walau juu ya asilimia 50. Duniani kote walio na gesi nyingi wanaiuza nje ili kupata fedha tena kutokana na gesi kugunduliwa kwa wingi hivi karibuni bei imeanza kushuka rejea eneo la mediteranian. Kosa linaloigharimu Tanzania isinufaike sana na gesi yake ni mikataba mibovu ya uchimbaji na ujenzi wa bomba la Mtwara Dar iliyoingiwa na serikali ya awamu ya nne. Ndio maana umeme wa gesi umekuwa ghali. Hivyo kuiuza Kenya kutaleta unafuu kwa sababu ya economy of scale.

Uwekezaji wa Kenya
Kenya kana zilivyo nchi zote za dunia wana haki pia ya kuwekeza Tanzania kwa kufuata sheria zetu xa uwekezaji. Kwa nini ulalamike Kenya wakiwekeza lakini hulalamiki US au China wakiwekeza nchini? Hata hoja ya kulalamika kuwa Kenya wamewekeza miradi 500 nchini sisi tumewekeza miradi 30 haina mashiko kwani katika uwekezaji sio lazima mlingane , kinachotakiwa ni sisi kama nchi tuwe na sheria nzuri zinazolinda maslahi ya watu wetu wakati uwekezaji unafanyika. Kuna maeneo tunaweza kuzuia kabisa, mfano kumnyang'anya ardhi ya kilimo mkulima mdogo kisha ardhi hiyo hiyo unampa mkulima mkubwa toka nje alime.

Viwanda
Hoja kwamba viwanda vya Kenya vitaua viwanda vyetu haina mantiki. Katika uchumi sio lazima uzalishe kila kitu hata kama huna comparative advantage. Unachotakiwa kufanya ni kuzalisha vitu ambavyo una comparative advantage na kuwauzia wenzako kisha wewe unanunua vile ambavyo huna comparative advantage. Kama gesi imetoka kwetu ikasafirishwa umbali mrefu kwenda Kenya maana yake kuna gharama kubwa ya kuisafirisha kwa mtumiaji wa Kenya kuliko mtumiaji wa Tanzania hivyo kama bado pamoja na ughali wa gesi bado bidhaa toka Kenya ambayo imesafirishwa kuja Tanzania itauzwa kwa bei nafuu kuliko bidhaa kama hiyo iliyozalishwa Tanzania maana yake ni kuwa kiwanda cha Tanzania ni inefficient producer. Sasa wewe uko tayari kununua bidhaa ya ndani tena isiyo bora kwa gharama kubwa kuliko bidhaa rahisi lakini bora toka nje? pia kumbuka bidhaa toka Kenya ikiuzwa nchini serikali inakusanya kodi ya VAT na kodi ya mapato na wananchi wanapata satisfaction kwa kula bidhaa bora. Viwanda vya ndani Tanzania vinaathiriwa na gharama kubwa za uzalishaji zinazotokana kwanza na ughali wa nishati ya umeme au gesi unaitokana na mikataba ya kufisadi iliyofanyika huko nyuma na sio sababu ya kuelewana na Kenya.

Usafiri wa anga
Kuruhusu Kenya airways kuja nchini maana yake pia ATCL inaruhusiwa kwenda Kenya hivyo pande zite mbili zitanufaika. Hata kana ATCL haiwezi kushindana na Kenya airways, bado Tanzania itapata faida za moja kwa moja na zile zisizo za moja kwa moja. Ndege za kenya zikitua katika viwanja vyetu zitalipa kodi mbali mbali, kuweka mafuta, kununua vyakula vya kwenye ndege, makampuni yetu ya kuhandle mizigo yatapata kazi ya kushusha na kupakia, abiria wanaokuja wanatumia pesa kwa huduma wawapo nchini. Urahisi wa connection kuja nchini tokea hub ya Jomo Kenyatta airport utafanya tupate wageni wengi wakiwemo watalii kwa sababu ni rahisi uwanja wao kupokea wasafiri wanaokuja kwetu kutokana na mashirika mengi ya ndege kufua huko. Kiuchumi manufaa ni mengi mno kwa Tanzania tena pengine kuliko hata kenya yenyewe. Kama ATCL ikishindwa kuperform mchawi wetu sio Kenya ni sisi wenyewe mipango yetu mibovu.

Mazao ya wakulima
Wakulima wetu watapata sako la uhakika hivyo kuchochea bei anayolipwa mkulima kuongezeka kutokana na ushindani. Kumbuka hivi karibuni walipozuia mahindi yasiingie kenya bei ya mahindi kwa mkulima ilishuka sana.

NB: Tuache chuki dhidi ya Kenya bali tujifunze na kuiga toka kwao moyo wa kufanya kazi kwa bidii, uzalendo kwa nchi na kuwa aggressive katika kuchangamkia fursa.
Pengine hofu ni ile ya Tanzania kuwa nchi ya kuzalisha mazao ghafi kwenda kenya na kutokuwa na viwanda vya ndani vya kuchakata mazao au kuzalisha finished products na hivyo kubana ajira ya ndani. Kwa hilo tujipange na sera yetu ya viwanda ndiyo itakuwa na comparative adv.
 
Mngekuwa mnataka viwanda mngeweka sheria na kanuni nzuri za uwekezaji sio kuzuia gesi kwenda nje ya nchi.
 
Bomba la gesi linatumika chini ya asilimia 10 tu
Shida sio kuuza nje..Tunauza nje kwa faida ipi je sisi wenyewe imetutosheleza kwanza?

Kama uwekejazi wa gas ulitokana na kodi za watanzania basi watanzania hao hao kwanza ndio wafaidike na kodi zao.

Tuuze gas baada ya sisi kuwa imetutosheleza kile kinachozidi (surplus)ndio kiuuzwe.

Viwanda vyetu wenyewe vinahitaji gas lakini gas hiyo hiyo hawapewi..inakuwaje unakwenda kumpa jirani yako!
 
Viwanda vya ndani vilianza kunyimwa gesi lini??
Kinacholalamikiwa ni viwanda vya ndani kunyimwa gesi halafu unaenda kumpa mtu wa nje, kwani ukatumia hata 1% tu ya ubongo wako, utapungukiwa na nini?
 
1. nikwamba bidhaa za Kenya zitakuwa zinazalishwa kwa gharama nafuu zaidi na kuteka soko la Africa Mashariki kuliko Tanzania. Tutarudi miaka ya nyuma tena kila kitu Made in Kenya. hii fikra ya namna gani? kwa hiyo gesi ibaki huko tusiiuze kwa kuwa tu Kenya watafaidika?

a. Hii sera yetu ya viwanda itakufa maana hatuweza kushindana tena na product kutoka Kenya na vijana wetu watazidi kuwa wachuuzi wa bidhaa kutoka nje. Yaani viwanda vyetu vitakufa kwa kuwa kenya itapata gesi na kukuza vyao? Kwanza viwanda vipi hivyo ambavyo vitakufa, vife mara ngapi maana na hii gesi tuliyo nayo vinakufa na vimekuwa vikifa. Hoja mfu sana na imekaa ki wivu wivu tu. Ni kama unauza vitabu then unaamua kuto muuzia mtoto wa jirani kisa eti atafaulu kuliko wako - ujinga sana huo.

b. Kenya itatumia mwanya huu kuvutia wawekezaji kutoka nje kuwekeza Kenya kuliko kuja kuwekeza Tanzania. Dah hizi akili hizi

c. Tunasafirisha gas kama kuna surplus ya viwanda vyetu na matumizi yetu kama Taifa.Viwanda vyetu bado vinahitaji nishati ya gas lakini bado upatikanaji wake umekuwa mgumu na kwa gharama kubwa. hii ndio ikufanye usiuze kenya gas?

d. Kenyatta amecheza karata yake vizuri katika ujenzi wa gas kuliko Mama sijui washauri wake wamekwama wapi natarajia kuona Kenya ikinufaika zaidi katika utawala wa Mama kuliko kipindi chochote kile katika historia ya Tanzania na Kenya. Ulitaka Kenya isinufaike na ujirani ulitaka indoofike, kila nchi inapambana kutumia fursa na Tanzania haijanyimwa kupambana kutumia fursa zilizopo

2. Ushirikiano wa anga..hapa Kenyatta anatafuta namna ya kuisaidia Kenya airways..inakwenda ku dominate soko na anga tena kama huko nyuma.hapa kumbuka faidia kubwa ya Kenya Airways inatokana na safari za Tanzania. Dsm, Zanzibar na Kilimanjaro. Hamna kitu umeandika hapa

Hapa tutalajie Air Tanzania ikifa kifo cha mende kutokana kutoweza kumudu ushindani na Kenya airways. Otherwise kufanyike changes za haraka katika Management ya Air Tanzania. Kwani Air Tanzania kwa sasa iko hai?



Hebu tujaribu kufungua akili zetu na kuacha mambo ya kijinga ya wivu. Pambana na ushindani kwa mbinu za kisayansi na kishawishi sio ujinga ujinga wa wivu wivu tu
Mahindi na dengu tunauza Kenya gesi eti hapana?hii imekaaje?
 
But kunao waTz weengi wenye biashara kubwa na ndogo pia. Wachaga wamejaa kwenye biashara ya nguo za mtumba. Kama hujui Kenya ni a country where you can own land ukiwa foreigner. No one can take that from you. Hata serikari haiwezi kuichukua. Fanya utafiti wako.
Mmmmmmhmn mbona ngumu kumeza
 
H
Mkuu ninakiunga mkono asilimia 200. Wakenya hawajawahi kutupenda watanzania na wanasema waziwazi. Tanzania ni dumping place ya Kenya
Tena mbaya zaidi bidhaa unayouzwa Tanzania hiyo hiyo ubora wake ni tofauti na inayopelekwa nchi nyinginezo. Huo mkataba wa gas ni mbovu kabisa. Yaani Tanzania bado watu wanapikia kuni halafu unapeleka gas kwa jirani? Viwanda vyetu umeme unaumiza. Gas majumbani hakuna wengi wanaomudu maana ni gharama kubwa. Huyo Economi Advisor aliyeteua ninaomba atizame upya.

Critical Economic analysis was very much needed ahead of the contract signing. Wakenya wanatembelea brains zao at 200% na sisi 50%. Tujipime.
Ii project ya kupeleka gesi Kenya ni ya muda mrefu watu walichelewesha kufanya maamuzi. Bora uamue kuliko kukaa kimya na kuchelewesha mambo.
 
Shida sio kuuza nje..Tunauza nje kwa faida ipi je sisi wenyewe imetutosheleza kwanza?

Kama uwekejazi wa gas ulitokana na kodi za watanzania basi watanzania hao hao kwanza ndio wafaidike na kodi zao.

Tuuze gas baada ya sisi kuwa imetutosheleza kile kinachozidi (surplus)ndio kiuuzwe.

Viwanda vyetu wenyewe vinahitaji gas lakini gas hiyo hiyo hawapewi..inakuwaje unakwenda kumpa jirani yako!
Maza ni zaifu?
 
Kwani ulisikia Samia katoka Kolomije? Naye ni wa mjini kuliko Kenyatta kwahiyo ngoma droo. Aliyekuwa wa shamba now anaongoza malaika huko nchi ipo kwa mtoto wa mjini sasa hivi.
Kenyata mtoto wa mjini kwa kutafuta hela Na kuweka mbele maslah ya Kenya. Wa kwetu anaonekana mtoto wa mjini kwa kiswahili kizuri Na misemo mizuri
 
Kunawakati tunapaswa kujadili maswala ya kitaalaam kwa utulivu na weredi ,hadi nimetamani Jf ingelikuwa na kipengele cha mtu kuruhusiwa kujadili hoja kutokana na TAALUMA yake , hapa unakuta mtu kwakuwa tu anajua kusoma na kuandika anajikuta anajadili kilimo huku akiwa hata hajui utofauti wa aina za mbolea ,eneo la Uchumi ni pana Sana na siyo kila mbinu nilazima ianze chino ,zingine ukija kwenye kuwagawia wa NDANI unakuta tayari ushafanya mlipuko mkubwa na wenye tija .

Tanzania iko hapa ilipo kwa makosa mengi yakiwemo tunayojihubiria hapa.

Watu wenye fikra za aina wzeeka ndiyo huwa mnakuwaga wachawi tu [emoji12] , ukiona mtoto wa yuko smart kuliko wa kwako unaona the best option ni kumdedisha tu au umnyime baadhi ya mahitaji ambayo yqtamfanya asongembele zaidi kwakuhisi wakakwako watapoteza u ora nakudharilika which is not true badala ya kufurahia uwepo wake na huku ukiangalia namna nzuri ya kuutumia uwepo wake ili na wa wajamii yako wawe bora hata kumpita .

Hii tabia yakukumbatia tulivyonavyo haiajawahi kuleta matokeo chanya zaidi ya kutudumaza tu kifikra .

Kanuni ya Biashara inatutaka tuuze tulivyonavyo huku tukizielekeza faida kwenye vitu vitakavyotuzidishia faida maradufu .

Kwa wasiyojua sera yetu ya Uchumi haiwezi kutatuliwa kwa uwepo wa gas bali maboresho mazito ya sera yetu ya elimu (kutoka kwenye elimu ya kukarili kwenda kwenye elimu ya utambuzi (creming education to cognitive education) elimu itakayohakikisha haizalishi wategemezi kwa Taifa kama ilivyo sasa kundi la kuanzia darasa la saba kuwa mzigo tu kwa Taifa , wahitimu wa kidato cha nne kutokuwa na sifa siyo tu za kuajirika lakini hata tu wenyewe wakawa hawana uwezo wakujiajiri nje ya kuwa na sifa za nyongeza achilia mbali cheti cha muhitimu wa chuo kikuu kukosa thamani ya kutumika kama collateral [emoji12] itakayomuwezesha walau kukopesheka na kupata mtaji wa kuanzishia ile taaluma ambayo serikali imemuidhinishia ufaulu (refer to China).

Mama anaendelea kufanya vizuri sana hebu tujipe utulivu na tumpe muda .

Tusiishi kwa kukarili ,Dunia inakwenda kasi sana .
Hoja ni kwamba utampaje jirani gesi akaendeshee viwanda vyake wakati viwanda Vya ndani vinapata shida kuipata hiyo hiyo gesi?
 
Shida sio kuuza nje..Tunauza nje kwa faida ipi je sisi wenyewe imetutosheleza kwanza?

Kama uwekejazi wa gas ulitokana na kodi za watanzania basi watanzania hao hao kwanza ndio wafaidike na kodi zao.

Tuuze gas baada ya sisi kuwa imetutosheleza kile kinachozidi (surplus)ndio kiuuzwe.

Viwanda vyetu wenyewe vinahitaji gas lakini gas hiyo hiyo hawapewi..inakuwaje unakwenda kumpa jirani yako!
Dust, mbona ndugu yenu alizuia kuingiza sukari nchini, kwa kufunga mipaka mwisho wa siku imepanda bei kutokana na kuadimika na kukosa ushindani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napenda kuandika kidogo tu kulingana na uwelewa wangu juu ya Ziara ya Mama nchi Kenya na mikataba mlio tiana sign.

1. Ujenzi wa bomba la gas kutoka Tanzania kwenda Mombasa kwa ajili ya matumizi ya viwanda nchini Kenya,hapa mama unefail pakubwa sana maana yake nikwamba bidhaa za Kenya zitakuwa zinazalishwa kwa gharama nafuu zaidi na kuteka soko la Africa Mashariki kuliko Tanzania. Tutarudi miaka ya nyuma tena kila kitu Made in Kenya.

a. Hii sera yetu ya viwanda itakufa maana hatuweza kushindana tena na product kutoka Kenya na vijana wetu watazidi kuwa wachuuzi wa bidhaa kutoka nje.

b. Kenya itatumia mwanya huu kuvutia wawekezaji kutoka nje kuwekeza Kenya kuliko kuja kuwekeza Tanzania.

c. Tunasafirisha gas kama kuna surplus ya viwanda vyetu na matumizi yetu kama Taifa.Viwanda vyetu bado vinahitaji nishati ya gas lakini bado upatikanaji wake umekuwa mgumu na kwa gharama kubwa

d. Kenyatta amecheza karata yake vizuri katika ujenzi wa gas kuliko Mama sijui washauri wake wamekwama wapi natarajia kuona Kenya ikinufaika zaidi katika utawala wa Mama kuliko kipindi chochote kile katika historia ya Tanzania na Kenya.

2. Ushirikiano wa anga..hapa Kenyatta anatafuta namna ya kuisaidia Kenya airways..inakwenda ku dominate soko na anga tena kama huko nyuma.hapa kumbuka faidia kubwa ya Kenya Airways inatokana na safari za Tanzania. Dsm, Zanzibar na Kilimanjaro.

Hapa tutalajie Air Tanzania ikifa kifo cha mende kutokana kutoweza kumudu ushindani na Kenya airways. Otherwise kufanyike changes za haraka katika Management ya Air Tanzania.

3. Soko la utalii hapa Kenyatta amecheza vizuri kama pele.
Tutalajie kuona vijana wetu wakiwa watazamaji kama kipindi cha nyuma na soko la utalii nikirudi mikononi mwa wakenya tena.(hapa kwenye utalii wenye fan zao wanaweza kudadavua kwanini Kenyatta amecheza kama Pela)

4. Biashara sioni jipya ni yale yale, hapa Mama ametoka 0-0

Note: Mama washuri wake wamshauri vizuri kabla yakwenda kufanya mikataba kwa niaba ya Watanganyika. Otherwise akubali kutuachia Tanganyika yetu!
Uelewa wako ni mdogo mnno. Kenya na Tanzania zinategemeana sana kibiashara. Hakuna haja ya kuwekeana figisu. Fungua fursa watu wademke.

Badala ya kulalamika, sisi inatakiwa tuangalie fursa na kuzichangamkia.
 
Back
Top Bottom