arola
JF-Expert Member
- Dec 19, 2013
- 550
- 187
Chadema haina mjinga kama wewe acha kujivalisha ngozi ya kondoo wewe.
Ndio chadema haina wajinga bali ina misukule.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Chadema haina mjinga kama wewe acha kujivalisha ngozi ya kondoo wewe.
Ngoja Lowassa nae ataje alio wapatia pesa ndani ya chadema tuone nani atabaki....
Watoto wa nje ya ndoa mnakazi sijui kama unazo zote kichwani.
Wakati tukisubiri CHADEMA "wajifafanue" kuhusu mtafaruku huu ambao, bila shaka kabisa, umeharibu sana taswira ya chama, Serikali nayo iwe makini. Siku zote tumekuwa tukiamini marehemu Chacha Wange alifariki katika ajali ya kawaida, lakini kwa kauli iliyotoka kwa Mh. ZZK, basi vyombo vya Dola viifanyie kazi. Kwa kuanzia ZZK na Mbowe wahojiwe kikamilifu hadi tuondolewe shaka kabisa kuhusu kifo hicho.
Ni unafiki mkubwa kwa Watanzania kujidai tunajenga taifa la amani huku idadi ya misiba isiyoeleweka au kuelezeka ikizidi kuongezeka. Inawezekana wanasiasa wananufaika kwa kuacha mashaka katika mambo muhimu lakini sisi ni binadamu kwanza kabla hatujajumuika katika jamii zetu mbalimbali ziwe za kiukoo, kikabila, kidini, kisiasa, n.k. CHADEMA inaweza kujiadhiri kiasi chochote na hata kufa ikitaka, lakini haikubaliki katika "michezo ya kisiasa" maisha ya binadamu nayo yachezewe kiasi hiki - hata kama ni kwa kauli za kizushi tu; lazima watu wawajibike. Kama aliuawa, wauaji wachukuliwe hatua; kama ni uzushi, mpayukaji naye achukuliwe hatua. Hiki sio kitu cha kujinasibu nacho.
Kwa HIYO NI KWELI aliuza nafasi za Ubunge kwa Pinda, Mkono na Dewji?
Hakuna kitu hapo wewe usiwe kibajaji mkuu,, inshu ya wangwe haiwezi kufanana na ya ulimboka na mvungi mkuu nafikiri yuanze na hizo kwanza,hayo mengine ni kutapatapa tu wewe na zitto wako wote hamna hoja mnhaha tu kutafuta huruma ya wanachama makini wa chadema .
Zito hanatofauti na Juliana Shonza na mwampamba, walipofukuzwa walizusha, walitoa kila aina ya ujinga.
Chadema inasonga mbele lakini kwa kasi ya ajabu vijana hao wanatoweka katika ulingo wa siasa.
Zito ameshapoteza sasa kachanganyikiwa ilobaki arudi ccm akapewe cheo cha mwigulu nchemba.
Atazusha, ataropoka na kujikanyaga lakini chadema haitateteleka bali inasonga mbele
Nafurahi sana pale ambapo watu wenye akili wanasoma mambo yanayo andikwa humu jf na kuyatafakari. Mtu ukitafakari saana mambo ya humu jf utaona kuwa wengi huenda kwa mihemko zaidi ya halisia.
Mh. Zitto Kabwe, umetuhumiwa na CC ya CDM. Unaacha kujitetea hizo tuhuma ulizo vikwa, unatoka kabisa kwenye somo unaenda kuleta mambo ya mwaka 47!!!Muda wote weye ulikuwa kimyaa. Hasira ni M/kiti wako kamtuma Lisu akuseme. Mjibu basi huyo Lisu. Unapomwacha Lisu ukaleta issue ya Mbowe tena ambayo usingaliisema inaonesha kuwa moyo wako haupo sawa na Mbowe.
Mambo ya kifamilia ya Mh. Mbowe yanahusu nini hongo ulizopokea weye kutoka kwa Mkono? ZZK jibu tu tuhuma zako, tena sio kwenye fb bali fuata the right channel na utajibiwa tu. Kila hatua unayochukua ni hatua mbovu zaidi. Kama ungeandika barua yako ya kujitetea kwa CC na ukaomba msamaha kwa tuhuma hizo, ukaeleza kuwa litakuwa pigo kubwa kwa Wananchi wa Kigoma Kask. wewe kuupoteza ubunge wako, hapo sasa, hata sisi tungeweza kuomba msamaha pamoja na weye kwa CC.
Tungesema umeliona kosa hivyo kurudia hapana na kwamba CC lazima nao wakuamini. Hayo hutaki kwa sababu ulihakikishiwa na hao waliokutuma ambao hujakanusha mpaka sasa. Wao walikuhakikishia kuwa watakuweka CDM kama mwanachama wa Mahakama na ndicho wanakazania kufanya. Sawa, kabisa lakini nadhani CCM ndiyo watalia zaidi siku si nyingi. This is going to be a reference in every court proceedings to come of which am quite sure they will be many from ccm soon and very soon.
Mzanzibari walie mrimua mbona hakwenda mahakamani? Kiburi mnachopewa na hilo lichama kitawaharibu tu. Ungeshuka ukaonwa na umma ndipo ungekaa juu siku zote wala si kwa hizi fitna zako.
Je ZZK katamka neno CHACHA WANGWE!??? Au unaropoka!????
tuko nyuma yako kamanda ZZK,akupigae ngumi ya jicho....we mpge ya ckio
u wil never walk alone ZZK
Soma post vizuri ndio ujibu!