Zitto: Hata kesi ya Mbowe ni jumba bovu kwa awamu ya 6. IFUTWE!

Zitto: Hata kesi ya Mbowe ni jumba bovu kwa awamu ya 6. IFUTWE!

Ifutwe, tena alipwe kutokana na posho na mishahara za walioitunga, ili liwe fundisho.
 
Samia aliteua DPP wake ndio akamshtaki Mbowe kwa hii kesi, sio DPP wa Magufuli (Biswalo Mganga)
Sasa ni jumba bovu kivipi wakati DPP ni wa Samia?
Hao makomandoo walipokamatwa mwezi wa 8 mwaka 2020, DPP, alikuwa ni wa samia?
 
Mambo yaliyopo mahakamani yataamriwa na Mahakama. Tusiingilie na kujadili masuala yaliyopo mahakamani.
Aliyeshtaki anaweza kuiondoa kesi mahakamani. Ila kwa jinsi kesi hii inavyoendelea kuivua nguo CCM na Serikali yake dhalim wacha iendelee tu ili dunia ione uovu wa Serikali hii dhalim.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Dhamira ya mama inaonesha wazi kuwa hataki maugomvi na kulipiza visasi.Lakini kwakuwa ameshajionea nia ovu ya baadhi ya watu dhidi ya uongozi wake,ni vizuri akatoa maamuzi magumu.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Lakini ana jidikia raha kumuona Mbowe mahakamani kila siku? Mbowe ni baba wa familia kama Mama Samia alivyo mama wa familia. Kesi yenyewe haina kichwa wala miguu. Hadi sasa sio Kingai wala Mahita walio weza kuonyesha ugaidi ulifanyika wapi?
Kwa matendo Ccm inayo mfanyia Mbowe wasidhani hasira za Mungu zita acha kuwa andama.
Mbowe sio gaidi...
 
Rip Magufuli
Una uhakika na hiyo RIP yako ? Unafikiri Mungu ni mjomba wake? Acha kujidanganya hakuna cha RIP
 
Si ulisema Magufur na samia, Hawa watu ni kitu kimoja....? Inabidi tu ukubali mama
Mimi nilisema kuwa msaidizi wa shetani hawezi kuwa Malaika na Samia akaja kuconfirm hili jambo yeye mwenyewe kuwa yeye na Magufuli ni kitu kimoja😁😁😁
 
Hii kesi ni kweli kabisa haina mashiko na doa lakini tusikatae ukweli kwamba Mh. Mbowe naye aliingizwa chaka na waliomwambia aanze kumtunishia misuli mama. Mama alianza vizuri sana kwa kuahidi mambo yaende kwa utaratibu na vikao. From no where mkaanza kumchomekea agenda ya Katiba mpya tena kwa ubabe huku mkijua miezi michache iliyopita mwendazake akiwepo mliufyata. Hii ilimpa picha kuwa mnataka kumpelekesha na kumfanya atoke kwenye agenda zingine. Tujisahihishe.
 
Hii kesi ilianza lini? Awamu ya tano imeingiaje kwenye hii kesi?
Shida Zitto anapenda sana kuonyesha kila tatizo ni tatizo la miaka mitano ya nyuma. Hata kama limeanza leo
 
Injili ya Luka Mtakatifu Mlango wa 3:

2 wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia Yohana, mwana wa Zakaria, jangwani.

14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.
 
Kesi ya kubumba ya Mbowe inaivua nguo serikali na kwa kweli ni hujuma dhidi ya utawala wake. Kesi hii imewaudhi mno na inawakera watanzania wote, wapinzani na wana CCM na inamweka Rais Samia katika mizani sawa na Fashisti Magufuli. Ni kesi inayoharibu tashwira ya Mahakama, Polisi na Majaji. Hoja iliyowasilishwa karibuni katika Bunge la Ulaya ya kuiponda kesi hii imedhihirisha namna kesi ya kijinga hii inavyoligharimu Taifa! Naungana na Mh. Zitto kwamba Kesi hii ni jumba bovu inayolinufaisha na kulifurahisha genge la kihuni la Mwendazake. Kwa vyovyote vile haina maslahi kwa Taifa wala Utawala wa awamu ya Mama Suluhu.
EU wamemshtua mama
 
Injili ya Luka Mtakatifu Mlango wa 3:

2 wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia Yohana, mwana wa Zakaria, jangwani.

14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu.
Amina
 
Back
Top Bottom