Zitto: Hata kesi ya Mbowe ni jumba bovu kwa awamu ya 6. IFUTWE!

Zitto: Hata kesi ya Mbowe ni jumba bovu kwa awamu ya 6. IFUTWE!

View attachment 2032644

Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana ! Leo Mtukufu Rais kwa kinywa chake mwenyewe ametamka kwamba ameona mambo ya hovyo ambayo amebambikiwa na awamu zilizopita , ameongea mengi na kukemea vikali kundi la watu waliomuangushia gari bovu kwenye awamu yake kwa lengo la kumchafua .

Mh Samia hakuwataja wapinzani , bali amewataja wanaccm wenzake na viongozi waliomo kwenye serikali yake mwenyewe , hawa watu wa hovyo ndio walewale waliokuwemo kwenye awamu ya 5 , hawa ndio waliomuangushia gari bovu mama na kumlisha maneno ya uongo ya kwamba Freeman Mbowe ni Gaidi , Njama zote za kumbambika kesi ya Uongo ya Ugaidi Mbowe zilipangwa kwenye awamu ya 5 na hawa hawa watu wa hovyo waliotajwa leo

Kesi ya uongo iliyofunguliwa kishamba sana bila hata ushahidi wa kuthibitisha ugaidi wa Mbowe , sasa inadhalilisha Nchi kila mahali duniani , mliyoyasikia huko EU ni ushahidi wa kwamba hili ni gari bovu aliloangushiwa mama na utawala uliopita kwa msaada wa vyombo vya dola , ANAPASWA KUTOONA AIBU KUIFUTA KESI HII ILI KULINDA HESHIMA YA UTAWALA WAKE , na baada ya kufuta uchafu huu unaoleta harufu kali na mbaya duniani kote , tunaamini atafanya mabadiliko kwenye uongozi wa vyombo vya dola nchini , Ili kuondoa watu wa hovyo wanamuangushia gari bovu

KUANZA UPYA SI UJINGA .
Kweli wewe ni mtu wa Propaganda wa hali ya juu. Kila kitu unakibadili kwa faida yako.
 
Ama Mikwara ya EU imezaa matunda wanajinyofoa ki aina? Hiyo yani tanguliza kujisafisha ili wamtoe Mbowe kwamba alishikwa na awamu iliyopita tu baada ya kusema katiba.
 
Back
Top Bottom