Zitto: IGP amemdhalilisha Waziri Gwajima na Rais Samia

Huoni hatari ya kuwa na undumila kuwili hapo?

Kumbe ili kuepuka kuwajibishwa dawa yake kujifanya wa kubwabwaja?
Ni viongozi wa dini wangapi wanaongea vitu vya kijinga kama Gwajima? Jibu ni kwamba hamna, hajaanza leo kuongea huo upupu wake, mtu kama huyo ni wa kumpuuza!!

Leo hii mambo anayoyaongea yeye wakiongea watu kama Pengo, Kakobe, Gwamanya, Malasusa hapo lazima watu washtuke, lakini siyo huyo jamaa!!

Kama aliweza kuprint matokeo ya Bashite na kuwapa waumini wake wasambaze kama vipeperushi ni nini atashindwa kusema ama kufanya? Hivi mtu anayesema sehemu uliyochanjwa itatokea alama ya 666 ana utimamu hata wa kuhangaika naye?
 
Ni kweli IGP amevunja sheria ya Public Health Na amekaidi agizo la bosi wake. AJIUZULU AU RAIS AMFUKUZE.
Ingawa Waziri alipaswa kuspecify kipengele cha Public Health act kilichovunjwa.

All in all IGP alipaswa kuelewa Waziri wa Afya kuna muda ana mandate ya kumtuma katika kuenforce public health act.

leo Gwajima(boy) akipelekea watu kufa IGP SIRRO anayo kesi ya kujibu
 
Walioungia Mkenge na kuchanja wanatuonea donge tusiochanja!

Zitto hujifanya kutetea uhuru wa kutoa maoni halafu hataki Msemaji wa wasiochanja Baba Askof Josephat Gwajima Mbunge wa Kawe kututetea

Zitto aelewe hata tusiochanja tunalipa kodi kuanzia za VAT, Miamala na mpaka sasa za majengo hata kama huna jengo

Rais Biden kishatangaza waliochanja wajiandae kwa chanjo nyingine kuimarisha ile chanjo ya kwanza wasipate Corona
 
Acha basi. IGP hajagoma ameomba apewe maadishi atekeleze
 
Sahihi kabisa

Rais Samia bado hajasahu jinsi Mtanzania huyu mwenye asili ya Kivu ya Kaskazini akishirikiana na Chama Rafiki kutok Hai alivyomuingiza kingi mwendazake kwenye kesi ya Escrow akawakamata kina Seth na Ruge na baada ya Serikali kushindwa hata namna ya kuendesha hayo mashtaka akarudi tena Mtaani kitangaza Serikali inawaonea Wawekezaji
 
Walioungia Mkenge na kuchanja wanatuonea donge tusiochanja!

Zitto hujifanya kutetea uhuru wa kutoa maoni halafu hataki Msemaji wa wasiochanja Baba Askof Josephat Gwajima Mbunge wa Kawe kututetea...
Waliochanja wanataka tuchanje wote [emoji23] yaani wanataka kama ni mkenge tuuvagae wote! Never [emoji23][emoji23]
 
Zitto bana[emoji3. Ameacha kujadili Mambo ya msingi na kuanza kujadili mtu. Gwajima akikamatwa yeye inamsaidia nini? Au Gwajima anamkwaza nini hadi au kavunja sheria gani hadi apige chapuo kutaka akamatwe! Kweli usiombe kubanwa mbupu,!]
 
Walioungia Mkenge na kuchanja wanatuonea donge tusiochanja!

Zitto hujifanya kutetea uhuru wa kutoa maoni halafu hataki Msemaji wa wasiochanja Baba Askof Josephat Gwajima Mbunge wa Kawe kututetea...
Kweli kabisa mnaonewa wivu na donge juu. Kwa sababu nyie mna akili nyingi, wenye chanjo watakuwa mazombi na kufa na ila nyie mtadunda milele.

Wazungu wamekaa huko wanawafikiria nyie Waafrika muda wote na wanawaonea wivu jinsi mlivyotoboa kimaisha na wanawataka kuwapunguza lakini wameshindwa!

Nadhani mawazo yako ni hivyo. Sasa siku tembelea ICU ukaone binadamu mwenye Covid anavyopambania Oxygen utapata mwanga.
 
Zitto amesema IGP Siro anapaswa kujiuzuru maana amekataa kutii amri ya askari wa mwamvuli wa rais SSH kwa kukataa kumkamata askofu Gwajima.

Na kwa kufanya hivyo Siro amegoma kutii amri toka kwa rais SSH.

Source; StarTV medani za siasa.
Halafu kila siku nyinyi ndio mnaolalanika kuwa jeshi la polisi halifuati sheria. Tunajua chuki ya Zitto dhidi ya JPM ndio inayomsukuma kutaka Gwajima akamatwe.

Hata siku moja jambo jema haliwezi toka kwa wapinzani kwenda kwa serikali ukiona wanashauri kitu basi kuna mtego ndani yake.
 
Chanjo hii inapingwa Dunia nzima hadi huko zilipoanzia Chanjo ndio sababu hii ndio chanjo ya kwanza kuwa unachanjwa halafu unapewa dola mia moja


Pengine moja ya madhara ya chanjo ni huko kuamini waliolazwa kwa Corona ni wale tu wasiochanjwa, tafuta taarifa za walio kwny mitungi ya gas kwa corona huku wakiwa full vaccinated ndio utaelewa kwanini tunatilia mashaka hayo machanjo
 
Zitto siku hizi ni Pro Mama kwa sababu ya imani yetu ya dini ya Kiislam,ni ndugu kwa Imani.
 
Hata hizo ninazo. Wanaopinga hata huko kwao, wengi ndio hao hao wa “mkichanjwa baada ya muda itatokea namba ya 666”.
Kiukweli, kuna watu kiafya hii kitu ikiwapitia hawachomoki.

Sasa kumwambia mtu eti asichanje maana atakufa anakuelewaje?

Uzuri wanaochanja hawapotezi muda kubishana na mtu..Kimya kimya wanaenda kupata Jab yao wanatulia..
 
Halafu Waziri wa Afya Mbona amekanusha kusema hakuagiza J. Gwajima kukamatwa?
Yule mama kama haekeweki vile?!
 
Zitto amesema IGP Siro anapaswa kujiuzuru maana amekataa kutii amri ya askari wa mwamvuli wa rais SSH kwa kukataa kumkamata askofu Gwajima.

Na kwa kufanya hivyo Siro amegoma kutii amri toka kwa rais SSH.

Source; StarTV medani za siasa.
Mbowe siyo gaidi aachwe huru mara moja
 
Zitto amesema IGP Siro anapaswa kujiuzuru maana amekataa kutii amri ya askari wa mwamvuli wa rais SSH kwa kukataa kumkamata askofu Gwajima.

Na kwa kufanya hivyo Siro amegoma kutii amri toka kwa rais SSH.

Source; StarTV medani za siasa.
tatizo hawa viongozi wa kiume kwasasa wanawadharau wanawake waliojuu yao kiutawala kwa sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…