Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

China sio mwekezaji tu ni mnyonyaji kama wanyonyaji rasilimali wengine.
Mwekezaji gani hajengi viwanda badala yake anachukua tu tenda za kujenga kila kitu hapa barani Africa na kuchota rasilimali zetu??
Mbona kwenye ujenzi wa Chuo cha siasa cha CCM na vyama vya ukombozi hatukusikia hizi figisu. Tulichodikia ni kwamba Wachina na marafiki zetu.

Kitu ambacho sielewi ni wapi Mchina anakuwa rafiki na ni wapi ambapo anakuwa siyo rafiki.... In short. Je China ni rafiki au siyo rafiki!!?
 
Unaelewa mtu akikuuliza maana ya kwa gharama ipi?
Mfano wewe ukitaka kujenga nyumba mfano ya 80m na kulipa na riba ikafika 40m jumla 120m
Na mwingine aje akwambie nitakujengea nyumba lakini nitaka nayo hadi nipate 200m.
Utachukua uamuzi upi
Gharama ni dola bil 10,ambazo wao wanatakiwa wazipate pamoja na faida katika hicho kipindi cha muda wa concession ambayo ni miaka 50 au chini ya hiyo kulingana na umahiri wetu kwenye negotiation.

Ni kama wawekezaji kwenye mradi wa Mlimani City wanavyofanya. Baada ya muda wa mkataba,majengo yote ya Mlimani City yatakuwa mali ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Kumbe ni fursa ya kuona mameli makubwa!!?
Mi nilijua ni fursa ya kupata mradi wenye manufaa kwa Taifa.
 
Wangetuwekea tu Conditions za huo mkata tuzipitie na sie wananchi isije ikawa ndo washakubali mchina aje kumiliki ardhi yetu huko Bagamoyo kwa miaka 99!!!
 
Details zinadai kwamba Wachina wangeleta management team yote kwa miaka 100 ijayo na pia mapato yote ya hiyo bandari kwa miaka 100 ni yao ili kurudisha mkopo wao, Tanzania haipati hata senti.


Ngoja wauweke tuone kama ni mzuri au mbaya kama ni mbaya kwa vipengele vinaweza kujadiliwa ili win win situation ipatikane ,miradi kama ile ndio inakuza uchumi.
 
Hizi kelele zenu za bandari ya bagamoyo dawa hii hapa

Biashara ya duka, mtu huwa huingii mkataba wowote na serikali .Unaenda tu kuomba leseni yaliyobaki ya kwako.

Sasa serikali kama inaona kuna uhitaji wa biashara ya bandari itangaze tu kuwa tunahotaji biashara ya bandari hata mia anayehitaji aje aombe leseni ajenge.Mengine yote yake kuanzia kununua ardhi kufidia nk yanabaki kama ambavyo investor wengine wote hufanyiwa

Hii itakomesha huu utapeli wa watu kutaka kuuza nchi kwa mikataba ya kipuuzi .Bandati ni godown tu la mizigo ya nje inayoingia au kutoka hufikia kwenye hilo godown linaloitwa bandari haihitaji mikataba ya ajabu ajabu na serikali kujenga hilo godown la bagamoyo linaloitwa bandari ya bagamoyo

Ajenge godown lake na magodown mengine yataendelea kama yalivyo .Ndio maana ya biashara huria yenye ushindani

Madalali nendeni mkawaambie wajenge kwa pesa zao tutakuwa tu tunakutana nao TRA

Wawekeze tu kama wawekezaji wengine tu .Walete mitaji yao wajenge tukutane TRA lakini kidiwrko kikaratasi chochote cha mkataba kati yao na serikali waje tu kama wafanyabiashara wawekezaji full stop.

Si sahihi kuuza nchi kwa sababu ya magodown yanayopigiwa debe kujengwa bagamoyo

Quote R
 
Details zinadai kwamba Wachina wangeleta management team yote kwa miaka 100 ijayo na pia mapato yote ya hiyo bandari kwa miaka 100 ni yao ili kurudisha mkopo wao, Tanzania haipati hata senti.

Mkuu siamini kama ni kweli inawezekana ilikuwa kama propaganda kama wahenga wanavyosema ukitaka kumuua mbwa mpe jina baya.

I don't think wachumi wa enzi ya JK kuingia mkataba kama huo ambao hauna maslahi hata chembe kwa TZ.
 
Mbona kwenye ujenzi wa Chuo cha siasa cha CCM na vyama vya ukombozi hatukusikia hizi figisu. Tulichodikia ni kwamba Wachina na marafiki zetu.

Kitu ambacho sielewi ni wapi Mchina anakuwa rafiki na ni wapi ambapo anakuwa siyo rafiki.... In short. Je China ni rafiki au siyo rafiki!!?
Ni mambo ya kushangaza kabisa!

Wachina wamekuwa na sisi kama marafiki kwa muda mrefu tangu tupate uhuru. Wamejenga miradi mingi kwa mikopo,mingine hatujamaliza hata kuwalipa kama Tazara na Urafiki. Lakini pia wao ndio wametujengea uwanja wa kisasa wa Mkapa na ukumbi wa mikutano wa kisasa wa Julius Nyerere.

Hata huu mradi wa bomba la mafuta uliosainiwa juzi, wachina wanamiliki hisa nyingi tu.
 
Hawa wametumwa! Hii campaign itakuwa chini ya uratibu wa timu ile ile inayomchafua JPM.
Usichanganye mada hapa, Magufuli alijichafua mwenyewe. Alikuwa na nafasi ya kuwa Rais bora kabisa lakini akachagua kuwa Dikteta. Mimi simkubali na sitamkubali kwa namna yake ya kuendesha nchi kama familia yake, lakini bado sikubaliani na mradi wowote ulioasisiwa na Kikwete baada ya Ridhiwan kukamatwa China.
 
KC wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema kitu ambacho wabunge wengi hawakijui ni kwamba Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa makubwa kutoka huko duniani ambazo hatujawahi kuziona hapa Tanzania..
Stupid statement! Hayo mameli makubwa yataleta nini? Ni statement inayostahili kutolewa na vijana wa kivukoni wakisubili kuzamia meli. Yaani meli kubwa zinaweza kuja bila sababu.
 
Kwa gharama ipi , ya kuuza hiyo Bandari kwa wawekezaji.
Shida mnaochangia hamkumsikiliza. Kasema waliona plan ya huo mradi lakini mkataba haukueahi kupelekwa bungeni wala hawakuwahi uona uko ikulu tu, kaomba badala yake uwekwe wazi watu wajue kilichokuwemo kuliko tu mtu kusema tu kwanini usiwekwe wazi.

Pia kasema huo mradi ulikuwa utekelezwe na wachina wakishirikiana na nchi ya Oman ambapo sasa Oman serikali ya raisi Mwinyi washaingia nayo makubaliano ya kujenga bandari.

Yani ile bandari ya bagamoyo anasema masterplan yake haikuwa ni bandari ya hii iliyopo, ile ilikuwa ni ya meli kubwa kuja kushusha mizigo halafu hizi meli tulizozoea znachukua pale na kusambaza kwenye bandari nyingine za afrika.

Akaendelea kusema kuwa ingemalizika ndiyo ingekuwa bandari ya tatu kwa ukubwa duniani. Ila shida kasisitiza ikulu haikiwahi kuweka huo mkataba hadharani wala kuupeleka bungeni zaidi ya kuambia tulichosikia.
 
Back
Top Bottom