Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Zitto Kabwe: Bandari ya Bagamoyo itapokea mameli makubwa ambayo hamjawahi kuyaona, tusipoteze hii fursa jamani

Here we come 'China Bay'….hizo meli kubwa kubwa zisiwe nazo zina mzigo wa Gold Dust.
 
Stupid statement! Hayo mameli makubwa yataleta nini? Ni statement inayostahili kutolewa na vijana wa kivukoni wakisubili kuzamia meli. Yaani meli kubwa zinaweza kuja bila sababu.
Kasema ni bandari iliyolenga kupokea mizigo toka kwenye meli kubwa zaidi halafu hizi meli tulizozoea zinachukua pale na kusambaza sehemu mbalimbali za Africa.

Shida kasema mkataba hata Wabunge hawakuwahi kuuona hivyo zaidi ya kuambiwa sote tulichosikia wao kama wao hakuna aliyewahi kuona kilichomo. Hivyo kashauri bora uwekwe wazi ujadiliwe tujue kilichomo kuliko kuambiwa ambiwa tu.
 
Mbona kwenye ujenzi wa Chuo cha siasa cha CCM na vyama vya ukombozi hatukusikia hizi figisu. Tulichodikia ni kwamba Wachina na marafiki zetu.

Kitu ambacho sielewi ni wapi Mchina anakuwa rafiki na ni wapi ambapo anakuwa siyo rafiki.... In short. Je China ni rafiki au siyo rafiki!!?
China ni Nafiki siyo Rafiki.
 
Here we come 'China Bay'….hizo meli kubwa kubwa zisiwe nazo zina mzigo wa Gold Dust.
Kwanza kasema mradi haukuwa unatekelezwa na china peke yake bali ilikuwa china na oman na ile mizigo haikuwa kwa ajili ya tz pekee bali ilikuwa ni kama kituo ambapo meli kubwa zaidi zinateremsha mizigo halafu hizi meli tulizozea zinaichukua pake na kuisambaza sehemu nyingine za Afrika na dunia.

Amesema ingemaliza ndiyo ingekuwa bandari ya 3 kwa ukubwa duniani. Shida kasema mkataba hata yeye hakuwahi kuona ikulu haikuwahi kuuweka wazi ila angetamani wauweke wazi ujadiliwe zaidi ya kutuambia kama tulivyosikia tu
 
Sasa kwanini waliukataa? Tuliwahi kusaini mkataba wowote wenye maslahi kwa Taifa letu? Kumbuka IPTL, Richmond, Dowans, dhahabu, gesi, Escrow etc waweke hadharani details.
Mkuu siamini kama ni kweli inawezekana ilikuwa kama propaganda kama wahenga wanavyosema ukitaka kumuua mbwa mpe jina baya.

I don't think wachumi wa enzi ya JK kuingia mkataba kama huo ambao hauna maslahi hata chembe kwa TZ.
 
Gharama ni dola bil 10,ambazo wao wanatakiwa wazipate pamoja na faida katika hicho kipindi cha muda wa concession ambayo ni miaka 50 au chini ya hiyo kulingana na umahiri wetu kwenye negotiation.

Ni kama wawekezaji kwenye mradi wa Mlimani City wanavyofanya. Baada ya muda wa mkataba,majengo yote ya Mlimani City yatakuwa mali ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Bado unakuwa mgumu kuelewa, miradi mingi muda wa kurudisha pesa ni miaka 8 au chini ya hapo.

Jingine kwanini tusi chukue mkopo wa hiyo 10bn tukajenga wenyewe. Na tulipe hilo deni sisi wenyewe kwa kuendesha huo mradi.

Au wao nani atakuwa anahakikisha kuwa wamewekwa hizo 10bn, na pia kama hawajapata Mapato ya kuzidi 10bn kwa muda mfupi zaidi
Je, umesikia kuhusu port ya Sri Lanka ambayo imeshindwa kurejesha deni kwa wachoma.
 
Wachawi wote wameamua kujianika nje hadharani kwa ajili umma mzima kuwatambua.
 
Hawa wanasiasa hawaaa, wao wakishaashiba haijalishi ni shibe ya halali ama haram kwakua majina makubwa wataauza hata Mlima Kilimanjaro, ila mjue mbeba dhamana na mjue kwa Haqika mtaulizwa siku ya Qiyama
 
Zitto huwaga mpiga debe wa mabeberu tu hata sinshangai, hii meli kubwa kiasi gani istue dar? Muongo sana huyo. Na yeye kaiona wapi?
Siyo mtu wa kumuamini

Ova
 
Kasema ni bandari iliyolenga kupokea mizigo toka kwenye meli kubwa zaidi halafu hizi meli tulizozoea zinachukua pale na kusambaza sehemu mbali mbali za Africa. Shida kasema mkataba hata wabunhe hawakuwahi kuuona hivyo zaidi ya kuambiwa sote tulichosikia wao kama wao hakuna aliyewahi kuona kilichomo. Hivyo kashauri bora uwekwe wazi ujadiliwe tujue kilichomo kuliko kuambiwa ambiwa tu
Hapo nitamuelewa, bila mkataba kuwekwa wazi watu wakaujua No.
 
Sijui kwa nini tu huyu jamaa huwa siamini ayasemayo....
Tuna tofauti nyingi baina yangu mimi na wewe lakini linapokuja suala la Zitto yuko pamoja sana. Sijawahi kumwamini Zitto hata siku moja labda lile Kanisa la Askofu Rashid wanifanyie maombi ya nguvu.
 
Hawa wanasiasa hawaaa, wao wakishaashiba haijalishi ni shibe ya halali ama haram kwakua majina makubwa wataauza hata Mlima Kilimanjaro, ila mjue mbeba dhamana na mjue kwa Haqika mtaulizwa siku ya Qiyama
Ungemskiliza ungeelewa alichosema ila nina hakika hukusikia interview yake. Kaeleza vizuri tu yeye alichoona ni masterplan ya bandari ila mkataba bunge halikuwahi kuuona na ikulu haijawahi kuuweka wazi, hivyo tunaambiwa tu yeyw kapendekeza kwanini wasiuweke wazi.

Maana kasema kutokana na masterplan ile bandari ingemalizika ingekuwa ndiyo ya 3 kwa ukubwa duniani na lengo ilikuwa ipokee mizigo toka meli kubwa zaidi halafu hizi meli tulizozizoea znaichukua pale na kuisambaza huko sehemu mbambali Africa na duniani ikibidi.

Ila shida serikali haikuwahi kuweka huo mkataba wazi. Na pia kasema ni China na Oman ndiyo walikuwa wajenge hiyo bandari na Mwinyi keshawahi Oman wanajenga bandari zanzibar.
 
Back
Top Bottom