Zitto Kabwe: Membe alitupigania dhidi ya tabia Mbaya ya Watu wenye Mamkala kutumia Wahuni kutukana Viongozi wenzao

CCM ukweli upo wazi na haupingiki mmemfanya vibaya kwenye historia ya marehemu Benard Membe kipengele cha siasa ,mmeshindwa kuelezea alihama CCM na kugombea Urais kupitia Act wazalendo, hivyo hivyo pia kwa msemaji wa familia

Zitto kabwe umefanya vizuri kuwakumbusha waweke record vizuri ya historia ya marehemu kupitia siasa , lakini kwangu mimi Zitto kabwe atabaki kuwa mwanasiasa mnafiki.
 
Nafuatilia kuaga mwili wa Hayati Bernard Membe kwenye runinga. Nimeipenda hotuba ya Zitto Kabwe maana hajamng'unya maneno katema nyongo kwa kusema ukweli. Tuwe wakweli kwa kusema ukweli na siyo kurembaremba hata pale ambapo mambo hayakwenda vizuri.
Acheni umbea
 
CCM hatataki kusikia

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Salamu za Zito kabwe zimelenga kumsimanga hayati Magufuli na kuonyesha kwamba,Membe alikuwa bora kuliko Magufuli ikiwemo kuendekeza mtifuano kwenye taifa hili ,inahitaji akili kubwa kulitambua hilo alilifanya Zito kabwe
 
Namuona Zito hapa na vazi lake jeupe tayari kwenda kuzikwa na Maembe. Kipara nae hatulii kila saa kugeuka nyuma tu kwa kina Lukuvi anafosi tabasamu na kucheka kwingi, hivi hajui kama the next ni dingi yake?
Ikiwa next ni "dingi yake" wewe ni lini ?!!!
 
Kuna shida mbili tu hapo;

Moja, kasema ukweli na kwa kawaida ulweli haupendwi.

Pili, amepitiliza dakika!
 
Kabla ya Magufuli Zitto alikuwa milionea kwa kulipwa na serikali ili aisaliti CHADEMA na upinzani. Magufuli aliifuta ile ajira. Je Zitto angempenda Magu aliyekata mrija wake? Na bahati mbaya kule Chadema alishafukuzwa akadhani uenyekiti wa PAC ni wake wa kudumu. Waulize wakuu wa mashirika watakueleza Zitto alikuwa anapewa nini ili awaongee vizuri bungeni. Kuna mmoja alimnyima kabisa Zitto akatumia madaraka ambayo hakuwa nayo akaita polisi wamweke ndani. Sasa wakati wa Magufuli Zitto hata huo uenyekiti wa PAC ukafutika. Zitto akarudi kuwa mbunge wa kawaida halipwi kwa usaliti wala kwenye PAC. Adui namba moja wa Zitto akawa JPM. Ila sasa naona mambo yameanza kumwendea poa. Atasema sana.
 
Kwa hiyo ni kuamua kuununua ugomvi wa hao wanasiasa?. Safari bado ni ndefu kwetu sisi watanzania.
Wana siasa wana wafuasi. Mimi binafsi sioni logic ya kucheka mtu aliyekufa, maana ntakufa pia
Lakini wanasiasa wajinga, wanathubutu kusema maneno ambayo ni kufuru kabisa, kama wao wataishi milele.
Wanachekwa sababu, yanawafika siku sio nyingi baada ya maneno yao yenye mbwembwe nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…