Zitto Kabwe: Mwambieni Waziri Mkuu "Watu wake hawawezi kumpenda kama wana hofu ya kupigwa na kutekwa"

Zitto Kabwe: Mwambieni Waziri Mkuu "Watu wake hawawezi kumpenda kama wana hofu ya kupigwa na kutekwa"

Kipindi kile cha mwendazake walikuwa hawamtaji PM ni Magu moja kwa moja nini kimetokea mbona mama hatajwi mzigo anaangushiwa PM!!

Hii laana ya unafiki tulio nayo sijui kama kuna siku itakuja kuisha.

Kuna mda nakaa nawaza hivi ile ndege iliyopata ajali bukoba ingekuwa ni hizi alizonunua Magu ukosoaji ungekuwaje!!
 
Mh Waziri Mkuu Kasim Majaliwa lichukulie uzito hili alisemalo Zitto Zubeir Kabwe huyu kuna watu wako nyuma yake wana ajenda ya siri dhidi yako tunaweza tukasema huyu ndiye Ole Sabaya wa awamu ya sita kuwa makini ni hayo tu.
 
Kwahiyo watu wasiojulikana sahizi ni kosa la waziri mkuu sio rais tena kama mlivyokua mnaaminisha umma 2021 kurudi nyuma? Mna nini na Majaliwa? Anakwamisha mambo yenu yepi? Mnadhani mnammudu?
 

“Najua kuna Maafisa wa Usalama wa Taifa hapa kwenye Mkutano wetu Ruangwa, nawatuma wakamwambie Waziri Mkuu kuwa Zitto anasema maliza hofu Ruangwa.

“Watu wako hawawezi kukupenda kama wana hofu ya kupigwa na kutekwa kwa sababu tu wako vyama tofauti na wewe,” - Zitto Kabwe akiwa Jimbo la Ruangwa Mkoani Lindi.

Ameongeza kusema: "Nitamweleza Waziri MKuu Kassim Majaliwa kuwa kiongozi ukitaka kupendwa na kukubalika na watu wako, wasaidie kuwainua hali zao na sio kuwaburuza kwa mabavu na vitisho. Kufanya hivyo, kutakuchora kuwa kiongozi katili, watakuogopa na kukuchukia."
Uongozi wa Hayati utaendelea kuwa mfano mbaya Kwa vizazi vyote hapa Tanzania na dunia
 
Katumwa akamchafue majaliwa ruangwa. Baada ya kuwaambia watu kuhusu tatizo la umeme, tozo na ubadhirifu uliokithiri ye anamchafua Majaliwa.

Majaliwa keshaifungua ruangwa. Kuna mahakama nzuri ya wilaya, hospitali mbili kubwa za wilaya, chuo cha veta, ofisi ya takukuru, magereza ya wilaya, duka la msd, ambulensi kila kituo cha afya, vituo vya afya vya kisasa vyenye vyumba vya operasheni kwa ajili ya wazazi, shule nzuri zenye tiles na madirisha ya aluminium, uwanja wa mpira, barabara za lami, taa za barabarani, benki za nmb na crdb.

NMB wana jengo la ghorofa ruangwa na wenyeji wanakuambia hawakutegemea kama ipo siku ruangwa kutakuwa na ghorofa. Na kuna hotel ya ghorofa tatu imejengwa.

Zitto kama ameenda kujenga chama chake ruangwa aachane na majaliwa ila kama kaagizwa na team msoga kwenda kutest mitambo dhidi ya majaliwa basi aendelee kufanya kazi aliyotumwa.
Majaliwa anachafuliwa na matendo yake mwenyewe hakuna anayemchafua.
 
Kama hujui si ungekaa kimya tu kuliko kuwa mropokaji kama huyo swahiba wako nepi ah nape.
Mropokaji ni Bashiru anayelalamikia serikali aliyotumikia juzi juzi tu hata miaka mitatu bado ameshafilisika.
 
Kalalamika sana[emoji28][emoji28]
Angekuwa amelalamika usingeonana wanaumana huko. Si umeonana uvccm na kina nape wameanza kujitoa akili.

Usiku huu ninapokuambia wapo msoga state house wanajipanga kuwatumia misukule yao kina steve mengele kumjibu dr bashiru.
 
Back
Top Bottom