Zombe aachiwa huru, Mshirika wake ahukumiwa kunyongwa hadi kufa

Zombe aachiwa huru, Mshirika wake ahukumiwa kunyongwa hadi kufa

nataka kujua tu kama zombe atarudishwa kazini na kulipwa stahiki zake zote au la....maana kuna kamanda naye alikutwa na kesi ya kasusura enzi hizo alikua mkuu wa upelelezi wa mkoa wa tanga anaitwa mushongi sasa ni rpc pwanii
 
Wanajamvi
naona hisia zimetawala kiasi kwamba hoja za msingi zinaachwa

1. Kuna Christopher Bageni
2. Abdallah Zombe

Kosa la msingi ni mauaji ambalo mahakama kuu haikuona hatia kwa wahusika

Kesi imefikia tamati mahakama ya rufani, Bageni amepatikana na kosa la kuua na hivyo anyongwe hadi afe.

Mahakama haikuona Zombe kama 'accomplice' kwa namna yoyote
Mwendeaha mashtaka hakuweza ku associate mauaji na Zombe

Kumbuka hapa ni mauaji kwanza, kabla ya habari nyingine

Kilichokatiwa rufaa kwa Zombe ni kuhusu cover up aliyofanya

Kimahakama, mwenye jukumu la kuthibitisha tuhuma ni mshtaki.
''The onus is on the complainant to prove guilty''

Inaonekana wameshindwa kwa hilo, Zombe yupo huru

Hata kama tunajua alifanya hivyo, kama haikuthibitishwa mahakamani, mahakama haiwezi kutoa hukumu hisia.
 
Hii itakuwa fundisho kwa Polisi wanaofanya kazi kwa remote badala ya kufanya kwa mujibu wa sheria.
 
Wanaukumbi.

Kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini watatu na dereva teksi mmoja: Christopher Bageni ahukumiwa kunyongwa hadi kufa, zombe na wenzie wawili waachiwa huru.

Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Ilala Christopher Bageni amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kutengua hukumu iliyomwachia huru na kumtia hatiani kwa kosa la mauaji ya wafanyabiashara wa madini watatu na dereva teksi mmoja.

Kadhalika mahakama hiyo imewaachia huru Mkuu wa Upelelezi wa zamani (wakati huo Mkoa wa Dar es Salaam) (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi mstaafu Abdallah Zombe na wenzake wawili baada ya ushahidi wa rufaa hiyo kushindwa kuwatia hatiani.Mara baada ya hukumu kusomwa, ghafla Bageni aliduwaa wakati wenzake wakimkumbatia huku wakibubujikwa na machozi wakiwa kizimbani.

Wanaodaiwa kuwa wanafamilia wa washtakiwa hao waliangua vilio huku washtakiwa wenzake walisikika wakieleza masikitiko yao. Wengine walisikika wakisema angejua asingekuja mahakamani kusikiliza hukumu hiyo.“Namshukuru Mungu...Lakini nasikitika kwa Bageni kukutwa na hatia sina raha kabisa....” alisema ASP Makele wakati akitoka katika ukumbi namba moja wa mahakama hiyo. Akizungumza baada ya hukumu hiyo, ACP mstaafu Zombe alisema anamshukuru Mungu na kuhusu Bageni alisema hana cha kuzungumzia.

Hukumu hiyo imesomwa leo na Msajili wa mahakama hiyo Mhe. John Kahyoza baada ya rufani iliyokatwa na upande wa Jamhuri kusikilizwa na jopo la majaji watatu likiongozwa na Mwenyekiti, Jaji Bernard Luanda, Jaji Sauda Mjasiri na Jaji Semistocles Kaijage.

Msajili alisema awali Mahakama Kuu iliyoketi chini ya Jaji Salum Massati (wakati huo kabla ya kupanda kuwa jaji wa rufani), ilimuona Zombe na wenzake hawana hatia na kwamba haiwezi kuwahukumu kwa kosa la kusaidia kufanyika mauaji hayo.Alisema Mahakama ya Rufani inakubaliana na Jaji Massati kwamba mtuhumiwa hawezi kutiwa hatiani bila kuthibitisha mtu aliyetenda kosa hajashtakiwa na kutiwa hatiani.
 
Kwa kuwa walishinda Mahakama Kuu walikuwa huru na hivyo siyo wafungwa wa kukaa gerezani.
Kwa mtu yoyote aliyefuatia lile tukio la mauaji atakubaliana na mimi kuwa hapa mahakama imetoa hukumu halali. Huyu jamaa aliyehukumiwa kunyongwa kweli ndie mhusika mkuu kwani marehemu wote walichukuliwa chini ya usimamizi wake na wafikwa na umauti chini ya usimamizi wake. Zombe ni lazima angepona kwa sababu hakuwepo kwenye tukio na hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa alitoa amri wauawe.
 
Ila kwenye hii issue ilikuwa tamaa zao tuu, hasa huyo Zombe, na sijui amechomokaje aisee.

Sheria za polisi hautakiwi kuact kwenye order inayokinzana na taaluma ya upolisi
 
Ivi Hukumu ya kunyongwa kwa Tanzania huyu Rais wetu ameshasain?
Maana nahisi utekelezaji wake utakuwa ni Politics mwisho wa siku jamaa atafungwa kifungo cha maisha
 
Wanajamvi
naona hisia zimetawala kiasi kwamba hoja za msingi zinaachwa

1. Kuna Christopher Bageni
2. Abdallah Zombe

Kosa la msingi ni mauaji ambalo mahakama kuu haikuona hatia kwa wahusika

Kesi imefikia tamati mahakama ya rufani, Bageni amepatikana na kosa la kuua na hivyo anyongwe hadi afe.

Mahakama haikuona Zombe kama 'accomplice' kwa namna yoyote
Mwendeaha mashtaka hakuweza ku associate mauaji na Zombe

Kumbuka hapa ni mauaji kwanza, kabla ya habari nyingine

Kilichokatiwa rufaa kwa Zombe ni kuhusu cover up aliyofanya

Kimahakama, mwenye jukumu la kuthibitisha tuhuma ni mshtaki.
''The onus is on the complainant to prove guilty''

Inaonekana wameshindwa kwa hilo, Zombe yupo huru

Hata kama tunajua alifanya hivyo, kama haikuthibitishwa mahakamani, mahakama haiwezi kutoa hukumu hisia.

Mkuu, umehitimisha vizuri.

Pia ukisoma hii sehemu ya Bageni kujitetea utaona wapi alipatwa na hatia.

Utetezi wa bageni;

Jaji: Mshitakiwa, hebu kwanza nikuulize, hii ripoti ya daktari hapa mimi bado inanisumbua kidogo, Kwanza umesema ulipokwenda katika ukuta wa Posta ulipopelekwa na James hamkukuta damu

Bageni: Ni kweli

Jaji: Jana yake siku mliyokwenda ama asubuhi yake kulikuwa na mvua?


Bageni: Hapana hapakuwa na mvua.

Jaji:Umesema ukutani uliona matundu sita yalidaiwa kuwa ni ya risasi, lakini hawa marehemu walikuwa ni wanne je hizi risasi sita zilitoka wapi au baada ya kupigwa waliendelea kupanda ukuta?


Bageni:Mtukufu Jaji. mimi sikuwepo lakini mapambano mengine zinaweza kupigwa risasi nyingi zikajeruhi chache tu.

Jaji:Na kwa nini hapakuwa na damu?


Bageni: Mtukufu Jaji,hata mimi sijui kuwa ilikuwaje.

Jaji:Umesema matundu yale jinsi yalivyokuwa ukutani inaonekana yalipigwa kutokea pembeni, je katika hali hiyo inawezekanaje kumpiga mtu kisogoni? Alihoji Jaji na kumuelekeza Bageni aegemee ukuta na kisha kumtaka eleze mtu akipiga risasi kutokea upande wa kushoto kwake ni jinsi gani inaweza kumpata kisogoni.


Bageni: Mtukufu Jaji hapa zitampiga hapa,alisema Bageni akionyesha sehemu za begani.

Jaji:Umesema ulipelekewa maganda ya risasi baada ya siku tatu, nne je uliuliza kuwa maganda hayo waliyapata wapi?

Bageni: Niliuliza wakasema waliyatoa Sinza eneo la tukio.

Jaji:Waliya-collect siku hiyohiyo?


Bageni: Nadhani maana askari akipiga risasi lazima a-collect maganda.

Jaji:Kama pale ukutani kulikuwa na matundu sita na walikuletea maganda tisa je haya matatu uliuliza waliyatoa wapi?


Bageni: Ni kawaida Mtukufu Jaji kuwa unaweza kulenga risasi ikapita juu ya kitu ulichokusudia.

Jaji:Kwa maelezo ya James (mkuu wa upelelezi kituo cha Urafiki) ni askari wangapi waliopiga risasi siku hiyo?

Bageni: Hakunieleza ni wangapi.

Jaji:Balistic (Mtaalamu wa masuala ya silaha na milipuko) alisema ni silaha mbili tu ndizo zilizopia ya Saad na ya mshtakiwa wa 12 ,una ‘comment’ yoyote kwa hilo?


Bageni: Mtukufu Jaji, yeye ndiye mtaalamu.

Jaji:Umeeleza kuwa mshtakiwa wa kwanza alikushauri lini mbadili taarifa ya kwenda kwenye Tume ya Kipenka?


Bageni: Mtukufu Jaji, sikuwa specific katika tarehe ila rekodi isomeke siku ambayo alikuwa ‘summoned’ kwenye tume.

Jaji:Kwa nini alikwambia uandike nyingine wakati ulikwishaandika taarifa ya kwako?


Bageni:Aliniambai ifanyiwe marekebisho kidogo ili mambo yawe sawa.

Jaji:Mshtakiwa wa kwanza alisema hapa kuwa polisi hutii amri halali tu je hiyo ilikuwa ni amri halali?


Bageni:Ni halali sababu yeye ni mkubwa wangu

NB: Kuna sehemu kama hapo penye rangi nyekundu ndio palikuwa panatayarisha kabisa jeneza la Bageni.
 
Kwa mtu yoyote aliyefuatia lile tukio la mauaji atakubaliana na mimi kuwa hapa mahakama imetoa hukumu halali. Huyu jamaa aliyehukumiwa kunyongwa kweli ndie mhusika mkuu kwani marehemu wote walichukuliwa chini ya usimamizi wake na wafikwa na umauti chini ya usimamizi wake. Zombe ni lazima angepona kwa sababu hakuwepo kwenye tukio na hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa alitoa amri wauawe.

Of course watu kwa vile walimfahamu Zombe na mabaya yake walitamani akutwe na hatia bila kujua kuwa this time around hakukuwa na ushahidi wa kumgusa na mara zote alikuwa smart kutoguswa na ushahidi. Yes, Bageni alikuwa katika mazingira ya kuguswa na ushahidi.
 
Dah, Nikimkumbuka Bageni!!!
Hakika jamaa ana damu za watu za kutosha mikononi mwake.
Ilikua ukiingia anga zake anachofanya ni kukuchagulia kosa lokote kama siyo kukupoteza kabisa
Una criminal behavior kumbe?
 
Dah angepigwa kifungo cha maisha tu.....mambo ya kuhukumiana kifo sio kabisa
 
Back
Top Bottom