Katika pita pita yangu ndani ya maktaba moja kubwa hapa nchini nimekutana na jina la huyu mtoto, Momčilo Gavrić na taarifa kuwa ndiye mtoto au mtu mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kuingia vitani mpaka sasa, huku vita ya kwanza ya dunia WWI iliyoanza Julai 28, 1914 na kutamatika mwezi Novemba 11, 1918.
Momčilo Gavrić inasemekana aliingia vitani akiwa na umri wa miaka nane tu na kuanza majukumu ya kupambania taifa la Serbia. Nimekuja huku ili nipate kufahamu je ni kweli kuwa Momčilo Gavrić alipata kujiunga na jeshi akiwa na umri huu wa miaka nane?