JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Upungufu wa nguvu za kiume ni tatizo linalokabili wanaume wengi duniani. Kwa mujibu wa tafiti, tatizo hili linazidi kuwa kubwa miaka ya hivi karibuni tofauti na zamani. Katika kutafuta visababishi vyake, Mdau mmoja wa JamiiForums aliweka chapisho lake lenye utafiti unaotaja sigara kuwa miongoni mwa mambo yanayofanya tatizo hili litokee. Ni kweli kuwa sigara inaweza kusababisha tatizo la upungufu wa nguvu za kiume?
Miaka ya 2000s imekumba na mabadiliko mengi ya kiteknolojia ikiwemo uwepo wa safaru za kidigitali ambazo haiziwezi kudhibitiwa na mamlaka za serikali (Benki Kuu). Sarafu za kidigitali zinazotambulika hadi sasa ni pamoja na BitCoins na OneCoin. Sarafu nyingine ya Islamic Coin (ISLM) imeibuka. Hivi karibuni kumeibuka madai kuwa sarafu hiyo imetambuliwa na Fatwa kuwa ni halali kutumika na waislam.
Kumekuwepo na picha inayozunguka mitandaoni ikimuonesha mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akizungumza na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho huku mandhari ya nyuma ya picha hiyo yakiwa na picha yenye chupa ya konyagi. Picha inayodaiwa kuwa na chupa ya Konyagi Ukweli wa picha hii upoje? Picha 1 kati ya 4 zilizowekwa na Tundu Lissu kwenye mtandao wa Twitter
Mdau mmoja wa Jamiiforums ameonesha wasiwasi wake baada ya kwenda hospitalini kupima VVU ambapo tofauti na namna alivyotarajia, daktari wake alimpima kwa kutumia mate yaliyotolewa kwenye fizi ya juu na chini. Jambo hili limemfanya atoe ushauri kwa watu kuwa makini wanapokuwa wanabusiana kwa kuwa tendo hilo linaweza kusababisha maambukizi ya VVU kupitia mate. Ukweli wa jambo hili upoje?
Kuna Taarifa zilizosambaa kwenye Mitandao ya Kijamii, zinazodai Tarehe 31 Januari 2023 wakati Tundu Lissu akifanya Mahojiano ya channel ya YouTube ya Jambo TV, kwamba alimpongeza Rais Samia kwa kuunda Tume mpya ya Kuchunguza Haki Jinai. Taarifa hizo ni Uzushi. Uzushi huo ulidai kuwa Tundu Antipas Lissu alisifia kuundwa kwa Tume ya Haki Jinai, hata hivyo, kwa mujibu wa video iliyorekodiwa wakati wa mahojiano hayo Lissu hakupongeza kuundwa kwa tume ya haki jinai wala hakuzungumzia kundwa kwa tume ya haki jinai bali alizungumzia mfumo wa haki jinai kwa kukosoa mfumo huo. Tarehe 31 Januari 2023 Rais Samia alizindua Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuimarisha Taasisi za Haki Jinai. Rais Samia alisema Tume hiyo imeundwa kutokana na kuvurugika...
Kipindi cha afya hai ya uzazi wa mwanamke hutawaliwa na mizunguko ya hedhi ya kila mwezi ambayo hukoma baada ya kupata ujauzito, muda mchache baada ya kujifungua na pia baaada ya kufikia umri wa ukomo wa hedhi. Kwa maana rahisi, mwanamke hawezi kupata ujauzito ikiwa hapati hedhi. Hata hivyo, tumesikia mara kadhaa baadhi ya wanawake wakitoa madai kuwa wamepata ujauzito muda mfupi tu baada ya kujifungua, kabla hata hedhi yao ya kwanza haijarudi. Madai haya yana ukweli kiasi gani?
Kumekuwepo na madai kuwa Serikali imesitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo baada ya Kushindwana na mwekezaji. Hapo awali Serikali ilifufua mazungumzo na mwekezaji kuhusu ujenzi wa Bandari hiyo ila mazungumzo hayakwenda sawa. Hayo yamesemwa na Waziri Prof. Makame Mbarawa NB. Kwenye suala na negotiation timu ya mama Samia ipo vizuri sana na ipo kwa maslahi ya watanzania wote.
Asali ni chakula kinachotumika kama dawa ya magonjwa mengi. Hutibu vidonda, kikohozi, huondoa sumu mwilini, ni chanzo bora cha nishati pia hutumika kwa kazi nyingi za urembo. Ukipita mtandaoni utaona baadhi ya makala zikiweka marufuku ya kuwapatia watoto wachanga asali. Jambo hili linaleta ukakasi mkubwa wa jamii kwa kuwa asai imekuwepo kwa miaka mingi, na karibia kila jamii huitumia. Katazo hili lina ukweli gani kisayansi?
Inadaiwa kuwa mabehewa 30 na vichwa 2 vya treni za SGR mali ya TRC vinapigwa mnada 25/11/2022, nchini Germany kufuatia mgogoro wa TRC na EUROWAGON Railways Limited (Turkey), iliyopewa kazi ya kukarabati na kutia nakshi. TRC wamelipa Sh. 23 bilioni (35% ya kazi). Inadaiwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa EUROWAGON, Yalçın Aydemir amesema wataanza na mnada wa mabehewa 17 ya awali katika mnada huo (hadi sasa wateja wawili wamepatikana kutoka Serbia), na mabehewa 13 na vichwa 2 vya treni za mwendokasi vitasubiri hadi mteja apatikane na kisha watavipiga mnada. Shirika la Reli Tanzania (TRC) na kampuni ya EUROWAGON ya kutoka Turkey ziliingia makubaliano Oktoba 2020 kwa ajili ya ujenzi (ukarabati na utiaji nakshi) wa vichwa viwili vya treni ya...
Back
Top Bottom