Nyota wa zamani wa Real Madrid, Roberto Carlos anadaiwa kuingia kwenye mgogoro na mkewe hali iliyopelea atumia majengo ya uwanja wa mazoezi wa Real Madrid kama makazi wakati akishughulikia suala lake la talaka na mkewe waliodumu kwa miaka 15
Wenzi hao, waliofunga ndoa mwaka 2009, sasa wanakabiliwa na vita vya kisheria kuhusu utajiri mkubwa wa Carlos, unaoripotiwa kuwa na thamani ya pauni milioni 133 (Tsh410,091,550,000)