JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Inadaiwa huyu jamaa bhana enzi za utumwa, alitumika na masta wake kama mbegu ya kuzalisha watumwa wenye nguvu. Inadaiwa kutokana na kuwa na nguvu, umbo maridadi na urefu wa futi 7 hivyo masta wake alimpa upendeleo wa kipekee wa kumpunguzia majukumu mengi huku kazi yake kubwa ilikiwa ni kulala na kuwapa mimba wanawake mbalimbali ili waweze kumzalia masta wao watoto wenye nguvu ambao wangetumika katika shughuli za kitumwa. Roque Jose Florêncio aliacha idadi kubwa sana ya watoto.
Je, ni kweli kuna Samaki mtu? Maana huku mtaani kuna watu huwa wanatuhadithia namna walikutana na Samaki watu au kuhadithiwa na wengine stori kama waliona mwanamke Mrembo mweupe kama Mwarabu ila amekaa juu ya jiwe au ufukweni au anaogelea kwenye bahara au ziwa. Mwanamke huyo wanaeleza anakuwa na nywele ndefu na chini umbile la samaki wa kawaida ila kuanzia kiunoni ndio binadamu, na wasimuliaji husimulia kuwa ukitaka kumkamata unaona analia na anaomba usimkamate wengine wakidai wana watoto wadogo wananyonyesha, au wana familia hivyo kuomba waachwe huru waondoke. Stori ni nyingi sana huku wakidai samaki watu hao hukamatwa na kuliwa kama samaki wengine huku viwiliwili vyao vikizikwa au kutupwa tena majini. Je, ukweli ni upi JamiiCheck...
Tizama hi video kwa makini kabla ya ku-comment. Kiongozi wa Korea kasikazini amelegeza mashariti kwa dini moja tu uko nchini kwake baada ya kushuhudia great miracle en Wisdom katika kitabu cha Qur"an tukufu, wakati anaingia madarakani 2011 Uislamu kama dini zingine zilikua marufuku nchini mwake, mwaka 2015 waislamu kwa kujificha ficha walifika 3000 tu kwasasa waislamu ni 30,000. Adhana ya kila swala kwa kutumia vipaza sauti misikitini imeruhusiwa katika hiyo nchi kali ya kicommunist kuna hofu kubwa kwamba Uislamu ndani ya miaka 10 watagawana hiyo nchi na wa Buddha.
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limeeleza masikitiko yake na kulaani vitendo vya upendeleo vinavyodaiwa kufanywa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC). TEF limezitaka taasisi zote zinazojihusisha na haki za binadamu, kama LHRC, kulaani vitendo vya ukiukwaji wa haki bila kuegemea upande wowote. TEF imetoa wito kwa LHRC kutoa kauli ya wazi dhidi ya mauaji, utekaji, na vitendo vya ukiukwaji wa haki kwa watu wasio na hatia. Pia, TEF imeshauri LHRC kufanya maboresho ya kimkakati ili kuepuka upendeleo wa aina yoyote unaoweza kudhoofisha lengo lake la kutetea haki kwa uwazi na usawa. TEF inaamini kuwa hatua hii ni muhimu katika kujenga jamii yenye misingi bora ya haki na usawa kwa wote.
Back
Top Bottom