JamiiCheck - Tanzania

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Nimepokea hivi karibuni voice note kutoka kwa Mtanzania anayeishi Afrika Kusini. Sauti hiyo ya Dudula Master ambaye ni mhamasishaji mkubwa wa Xhenophobia ametoa onyo dhidi ya wageni wote kuondoka Afrika ya Kusini kuanzia tarehe 02 Septemba 2022 hadi Machi 2023. Nchi zetu hususan Tanzania zinapaswa kuhakikisha usalama kwa raia wao wanaoishi kule kihalali na ikiwezekana kuweka utaratibu wa kuwaondoa raia wake Afrika ya Kusini. Matishio haya yamekuwa yakifanyika bila hatua zozote kuchukuliwa, hivyo inawezekana baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola vya Afrika ya Kusini ni wahusika wa hizi operesheni dhidi ya wageni. Hatulipi ubaya kwa ubaya bali kumtenga mtu mbaya ni sehemu ya kumpa fundisho dhidi ya mtenda ubaya. Ni wakati sasa wa Nchi...
Ushiriki wa mazoezi ni jambo muhimu kwa afya. Husaidia kuongeza utimamu wa mwili pamoja na kuupa kinga ya kutosha dhidi ya magonjwa, hasa yale yasiyoambukizwa kama kisukari, shinikizo kubwa la damu na viribatumbo. Pamoja na faida hizi, watu wengine hushiriki mazoezi mbalimbali ya Gym kwa lengo la kuboresha muonekano wa miili yao, tunaweza kusema kwa sababu za urembo au utanashati. Miongoni mwa mazoezi yanayofanyika sana siku hizi hasa kwa wanawake ni kupiga vibao sehemu ya chini ya tumbo ili kubana misuli. Je, ni kweli kuwa mazoezi haya husaidia kubana misuli ya tumbo?
Taarifa ya kusikitisha kidogo kutoka Kata ya Mwana-Mutombo Kijiji cha Mwasinasi Tarafa ya Nkololo Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, Diwani kwa jina la Rambo Kidiga anatuhumiwa kuozesha wanafunzi wawili wa kidato cha pili na pia yeye binafsi kufunga ndoa na mabinti wawili wakisadikika kuwa ni Wanafunzi mmoja wa kidato cha pili na mwingine wa kidato cha tatu (majina yamehifadhiwa). Halikadhalika mtendaji wake wa kijiji alifahamika Kwa jina la Bw. Magobeko mwenye umri wa miaka 50 ameozesha binti wa kidato cha pili na vilevile Mwenyekiti wa kijiji afahamikaye kwa jina la Madereke Ngoro anatuhumiwa kuoa binti wa darasa la nne na kuachishwa masomo yake Katika Hali ya kusikitisha tumepokea malalamiko Kwa mama mzazi (Mama Nkwabi) wa binti...
Mdau wa JamiiForums ametoa hoja yake kuwa watu wanaokula dagaa hupata faida kubwa zaidi kuliko wale wanaokula samaki wakubwa. Amedai kuwa tofauti na samaki wakubwa, mtu anayekula dagaa anakula hadi mifupa yake yenye madini mengi ya calcium hivyo kuwafanya wawe na mifupa imara kuliko alaye samaki wakubwa, hasa kwa watoto ambao wanakua. Amewashauri watu kutumia dagaa kwa wingi, ikiwezekana wawepo kwenye kila mlo. Madai haya ni sahihi?
Mdau mmoja wa JamiiForums ameelezea kuwa watu wanaokunywa pombe kupita kiasi (Ulevi uliopindukia) wakiacha ghafla matumizi ya pombe wanaweza kufa. Mdau huyu anaeleza kuwa pombe hupunguza utendaji wa akili kama yalivyo madawa mengine ya kulevya, pia huleta uraibu na utegemezi. Amewashauri walevi sugu kuacha pombe taratibu ili wasipatwe na athari kubwa kwenye afya, ikiwemo kifo kutokana na kifafa. Madai haya ni sahihi?
Zipo taarifa zinadai kuwa Jeshi la Tanzania katika wilaya ya Nangade, Cabo Delgado waliingia kwenye mtego wa Magaidi katika kijiji cha Vondanhar, eneo la Palma. Aidha inadaiwa Jeshi la Tanzania lilikuwa likisafiri kwa magari ya kivita sambamba na jeshi la Msumbiji. Magari matatu ya jeshi la Tanzania yamechomwa moto na baadhi ya Silaha kuharibiwa. Taarifa iliyotolewa na kikundi cha Kigaidi cha IS, imedai wamekamata baadhi ya Silaha ikiwemo Chinese Type 81-1 assault rifle pamoja na 12.7x108mm Type 54 HMG ya kwenye gari. Zaidi inaelezwa kuwa haya ni magari ya JWTZ yapo chini ya himaya ya magaidi.
Back
Top Bottom