2024 Africa Cup Of Nations (AFCON) | Special Thread. Mechi ya fainali, FT: Nigeria 1 - 2 Ivory Coast. Ivory coast abeba ubingwa. 11.02. 2024

B... hapana bwana. DRC walistahili ushindi, bahati haikuwa tu upande wao.
Kwa majumuisho ya mwenendo wao katika michuano yote, utaona kama kila mtu kapata alichostahili hapo.

Ujue DRC wameshinda mechi moja tu kwenye michuano hii. Moja tu basi.

Ova
 
Kwa majumuisho ya mwenendo wao katika michuano yote, utaona kama kila mtu kapata alichostahili hapo.

Ujue DRC wameshinda mechi moja tu kwenye michuano hii. Moja tu basi.

Ova
Najua hilo b… Ila tukiongelea mechi ya leo ni kama mwanafunzi aliyefeli test za kawaida ila akapiga msuli kwenye mtihani wa mwisho.

Katika mechi zote hii ya leo wamecheza vizuri sana, kila idara walikuwa bora.
Kuliko hata ile ya robo fainali.
 
Penati anapiga utadhani hajakula chakula
Angepiga Mayele tujue moja tu kuwa inapaa hadi juu kwa mashabiki.
Itakuwa ameng'ang'ania apige yeye ndio maana kakosa.

Hii michuano ndio ya Mwisho kwa kwao.
Wangepata ushindi waingie walau kwenye history ya CAF .
 
Halafu na leo umewashabikia wamefungwa, kaogee chumvi ya mawe.

Sijapanga timu ya kushabikia kesho ila niachie Nigeria please πŸ˜†πŸ˜†
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Nimewatia gundu

Nilisema mimi nikichagua timu lazima ifungweπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Kiukweli nimekuwa mzalendo kwa Africa mashariki japo mahaba yangu yalikuwa kwa wasouth,, namzimikia Williams.

Mechi ya leo sijaicheck kwa presha kabisa.

Kesho sina timu
Wote siwapendi
Matapeli Nigeria waliwatoa wangoni wangu lolote liwapate
Janjajanja Ivory Coast mbio za sakafuni huishia ukingoni wachawi hawa wamezindika viwanja vyao.
 
πŸ€£πŸ˜‚πŸ˜‚Leo umetupa gundu my
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…