Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Chama cha ACT Wazalendo kimesema kuwa kimeshafanya mazungumzo na vyama vingine vya upinzani kwa lengo la kuungana na kuikabili Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi ujao.

Kauli hiyo imetolewa Februari 9, 2025, na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu, alipokuwa kwenye mkutano katika Jimbo la Kibiti, wakati akiendelea na ziara yake ya siku tatu katika majimbo matatu ya Mkoa wa Kichama wa Mwambao.

Soma: Ado Shaibu: ACT Wazalendo, CHADEMA na vyama vingine makini vya upinzani tuungane kuing'oa CCM madarakani

Ado Shaibu amesema tayari ACT Wazalendo kimezungumza na vyama vyenye nguvu vya upinzani, vikiwemo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Chama cha Wananchi (CUF) na NCCR- Mageuzi

Amesema vyama hivyo vina historia ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024, ambao walidai ulikumbwa na dhuluma.
Your browser is not able to display this video.
 
Waende mozambiq wakaongeze podems hawawezi hiyo Act ina nguvu visiwani bara mdebwedo chadema wana nguvu bara na ukristo wao visiwani kwetu hawana nguvu hata ya kura moja!
 
Ado hajasema hivyo, amesema ameviandikia barua kuomba ndoa na vyama hivyo.

Kuungana ni jambo jema. Lkn je, chadema watawezana na unafiki wa ACT (ccm B) watakapoanza uchawa wao?
 
Shida cuf bara Lipumba ameiua kwa tamaa, kwa sasa hata uwezo wa kuongoza hana ila among'ang'ania kiti mwanzo mwisho ati
 
Siwezi kuwaamini hawa ACT, wametumwa. Kule Visawani wana kipato cha kutosha. Kwanza wakiachie hicho kipato tuone.
 
Hapo
Hapo kwenye cuf
 
Waende mozambiq wakaongeze podems hawawezi hiyo Act ina nguvu visiwani bara mdebwedo chadema wana nguvu bara na ukristo wao visiwani kwetu hawana nguvu hata ya kura moja!
Huhitaji hata kura moja kutoka Znz kuwa rais wa JMT, kaa na hilo.
 
Lipumba hana kabisa mvuto wa kisiasa kwa sasa. Arudi tu kwao Tabora kulina asali.
 
CUF na NCCR ya sasa nina wasiwasi navyo
Chama pekee ninachokiamini hapo ni CHAUMMA, japo hakina ushawishi wowote. ACT ni mashaka matupu, CUF na NCCR cdm wasithubutu kuungana nao hata kwa bahati mbaya, hasa kwenye hizi chaguzi za kihuni. Hawa ndio watahongwa kupotosha matokeo na kuleta migogoro isiyo na lazima.
 
Kidogo ACT baada ya Zito kukaa pembeni inaweza kuwa na manufaa
 
HARUNA asiwepo kwenye hilo kolabo....mpuuzi sana
 
Kwani vipi utakwenda kupiga kura!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…