Uchaguzi 2020 ACT-Wazalendo wamuunga mkono Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu

Tujadili kwa hoja ndugu zangu, tuache matusi na zaidi sana tusiwabeze viongozi kwa kuwatamkia maneno mabaya.

Binafsi sijapenda kabisa kudhalilishwa kwa maumbile ya mgombea kwani hii inaamsha hasira na kufanya watu waandike mambo yasiyoandikika.

Tuwapigie debe wagombea wetu bila kudhalilisha wagombea wengine
 
Unapofanyia wanadamu uharifu utegemee mawili - Wakuvumilie au wapambane nawe kwa kuvunja haki zao, ukiona watu wamepambana nawe usianze tafuta au kumpa lawama aliyewashitua na kuwapa mbinu ya kukuchabanga, unatakiwa kutofanya uharifu utochabangwa, usitegemee kuvumiliwa tu
 
Kuna mtu ikifika tarehe 28 October ndo atajua kua maendeleo hayana vyama au yana vyama.
 
BREAKING NEWS: Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo taifa, Seif Sharif Hamad amemuidhinisha mgombea wa Chadema Tundu A Lissu kuwa mgombea wao wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa zaidi kufuata baadaye
Source: EATV
Msumari mgumu kwa janaa wale waliotunga njama mbaya kwamba hakuna muungano wa vyama.

Sasa muungano umekuja kwa namna ambayo hawakuwahi kufikiri na madhara yake ni mabaya kuliko yale waliyotaka kuyadhibiti.

Maneno ya Mungu Muumba yanasema, 'adai atakujia katika njia moja lakini Mungu atamtawanya kwa hofu kwa njia saba'
Hili neno linawadhihirikia sisiem kwa sasa.
 
Kwahiyo huu muungano ni zaidi ya uke wa ukawa?

Huu wenyewe mnauitaje?

Membe jina lake halikuwewepo kwenye orodha ya wapigiwa kura?
 
Strategy ya Chadema kutoanza kampeni Mikoani ya kusini kumbe waliona mbali... Sasa kusini Lissu akifika itakuwa kivumbi..
 
Kwahiyo huu muungano ni zaidi ya uke wa ukawa?

Huu wenyewe mnauitaje?

Membe jina lake halikuwewepo kwenye orodha ya wapigiwa kura?
Ule wa namna ya ukawa ndio wali utungia sheria za kuusiriba wasijui wasijui kuwa maji ya mafuriko hayazuiliwi kwa kuukinga mkondo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…