Uchaguzi 2020 ACT-Wazalendo wamuunga mkono Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 ACT-Wazalendo wamuunga mkono Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu

Mambo hadharani. Kura za ACT Wazalendo zote sasa kwa Tundu Lissu baada ya mwenyekiti wa ACT Wazalendo Maalim Seif kutamka rasmi kumuunga mkono.

Hii ngoma bado mbichi sana.

On top of this latest support from the Maalim himself, tumekuwa tukishuhudia maelfu ya wapiga kura wa hata vijijini swekeni huko jinsi wanavyomlaki Tundu Lissu kwenye campaign rallies zake.

Kwa kweli CCM tutahitajika kufanya rigging ya kutoka sayari ya Mars ili mgombea wetu ashinde!



Huu ni mwendelezo wa kuruka mitego.

Wale wa mboga mboga walidhani walikuwa na miliki ya infiltration. Zama hizi ni tofauti sana.

Viva BKM!
 
Nimeshiriki figisu figusu za uchaguzi mkuu kuanzia mwaka 2000 hadi 2010, sikuwahi kupiga kura.

Lakini mwaka huu, nikijaaliwa afya njema nitampigia Lissu, siwezi kuishi na mateso haya ya Magufuli kwa miaka 5 mingine. Eeh mwenyezi Mungu nisaidie.
Aaamin...✌✌
 
Dah yaani kimchezomchezo tu CCM inaenda kuachia madaraka.

Ngwe hii ya pili tutashuhudia mengi. CHADEMA ikijihakikishia kura za kutosha za waislamu, huu mchezo umekwisha. Hapo bado jeshi la wanawake halijaachiwa lianze mashambulizi yake!
Nashauri awamu ya pili chadema warushe helikopta, baadhi ya majimbo wapige hata Mara mbilimbili has a hai, kawe, tarime, mbeya mjini na hata iringa mjini
 
JP Magufuli hatoachia urais kupitia sanduku la kura. Hivyo hivyo Zanzibar. Maalim Seif hatopewa urais.

Humu jamvini tunajifariji tu. Mwaka 1995 na 2015 bila shaka Wapinzani walishinda (Mrema & Lowassa) lakini hawakupewa Nchi. Maalim anashinda kila uchaguzi. Kwa wenye kumbukumbu kiduchu tu wanakumbuka walichofanya jeshi/TISS mwaka 2015 pale Zenji.... mchana kweupe!

Hii comment ntairudia early November 2020 baada ya NEC & ZEC kufanya yao
jamaa yako aliwatosa na kuwadharau wale waliokuwa wapanga mikakati ya wizi wa kura.. akawanyang'anya chama akawadhihaki, akawatukana, akawatenga wakati wao ndo walimpigia kampeni mpaka wakavunjikia huko na mikono, wakakesha kwenye vyumba huko kubadili matokeo ya kura lakin baada ya jamaa kuapishwa akawatenga kama wakoma, chama akakikabidhi kwa kina sloo sloo wasiokijua chama, akawachukua na wale wale wapinzani akawalundikia vyeo kwa nguvu huku kina februari maropu kinana na napi wakafanywa vidampa.

ccm asilia hawatampa kura hata moja jamaa yako bali atapata tukura tuchache twa ccm mpya(ambayo kimsingi ni "ccm isiyo ccm"), kura za ccm asilia zote ni kwa tundu lisu..ccm asilia wanajua na wameshaamua ni kheri usu shari kuliko shari kamili...kuliko kumpa jamaa miaka mitano tena ya kuwanyamyasa ni heri tu nchi akabidhiwe Lisu ufunguliwe ukurasa mpya...bushiru hata akitishia nyau haisaidii kwanza haijui ccm huyo na ccm si yake, yeye ni wakuja tu ndani ya chama..

na wanachokifanya CCM Asilia wala si cha ajabu, wao kama wenye CCM Asili wanatunza heshima ya chama na kutimiza maono ya muasisi wa chama kuwa Upinzani wa kweli utatoka Ndani ya CCM na kuwa CCM si baba yangu wala si mama yangu...by JK Nyerere.
 
Membe Ana kazi ya kuwashawishi makachero, vipeyo na ... Ili Kumpa Kura lissu, JWTz officers tayari wamekubali bado polisi officers ambao huwa tunawaita wanawake, yo

samahani mi ni mfumo dume

Likely, una data fulani hivi za kushtua,

Embu fafanua mkuu
 
CCM uchaguzi huu inashinda ushindi mnono sana kupita chaguzi zote.
 
Nimeshiriki figisu figusu za uchaguzi mkuu kuanzia mwaka 2000 hadi 2010, sikuwahi kupiga kura.

Lakini mwaka huu, nikijaaliwa afya njema nitampigia Lissu, siwezi kuishi na mateso haya ya Magufuli kwa miaka 5 mingine. Eeh mwenyezi Mungu nisaidie.

Mimi pia
 
Wapi nimemdhihaki?
mkuu tiyar unalo wewe, unamdhihaki mtu aliyevunjwavunjwa kwa makusudi wakati na wewe bado upo hai na ni ama una watoto na wajukuu au utajakuwa na watoto na wajukuu!! utakuta wenzio waliomvunjavunja walilipwa kwa hiyo hata laana zikiwafika watakuwa walishafaidi. sasa wee mwenzetu unajichumia laana kwa buku 7 tu na pengine hata hiyo buku 7 hupewagi mkuu!!! dah...haya wee endelea ila jua laana itatembea hadi kizazi chako cha nne
 
Maalim Seif Sharif Hamad ametangaza leo kuwa chama hicho kinamuunga mkono Tundu Lissu katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano huku akimuacha Bernard Membe kwenye mataa.
Ww ndio umeachwa kwenye mataa....
pole sana.....
msalimie mkeo
 
Kwa hiyo Membe amebaki na mamluki wake zitto?
 
mkuu tiyar unalo wewe, unamdhihaki mtu aliyevunjwavunjwa kwa makusudi wakati na wewe bado upo hai na ni ama una watoto na wajukuu au utajakuwa na watoto na wajukuu!! utakuta wenzio waliomvunjavunja walilipwa kwa hiyo hata laana zikiwafika watakuwa walishafaidi. sasa wee mwenzetu unajichumia laana kwa buku 7 tu na pengine hata hiyo buku 7 hupewagi mkuu!!! dah...haya wee endelea ila jua laana itatembea hadi kizazi chako cha nne
Kwani mimi ndio nilimvunja vunja? Hebu niondolee imani zako za kishirikina hapa.
 
Back
Top Bottom