Ajabu na kweli: Padri wa kanisa katoliki kaoa mke na anavuta sigara kali!

Ajabu na kweli: Padri wa kanisa katoliki kaoa mke na anavuta sigara kali!

Igizo
Kama ni halisia mtaje jina na alipo sisi wanasheria tutakulinda
Naogopa kumwagia kitumbua chake mchanga; ana watoto wanamtegemea akifutwa kazi watoto watapata shida.
 
Ukistaajabu ya Musa hujaona ya Firauni. Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo. Haujapita muda mrefu nikakutana na kijana na kumuuliza kama padre yupo akanijibu padre katoka ila mke wake yupo. Nikamuuliza je, mke wake ni yule niliyemuona anafanya usafi pale nyumbani? Akajibu: NDIYO! Nilihisi kushikwa ganzi na kushindwa kusimama wima. Nikajifanya sijisikii vizuri nikawa nimechuchumaa chini nimeinamisha kichwa. Yule kijana kaniuliza: Vipi unaumwa? Nikamjibu najisikia vibaya.

Kwa mshtuko wangu nilihisi kabisa yule kijana ameunganisha hali yangu na tukio la mke wa padre kwa kuwa alikuwa akiniangalia kwa hofu iliyochanganyikana na wasiwasi. Kijana alionesha hofu ya kutoa siri za watu. Nikaanza kujilaumu kimoyomoyo kwanini nilishindwa kujikaza hadi kijana wa watu akahisi labda nitaenda kuvujisha hizi taarifa kwa viongozi wa kanisa. Nami wala sina nia hiyo na sijamwambia mtu yeyote hadi leo ninapoandika kuhusu jambo hili hapa JF.

Siku za nyuma kidogo (takribani miaka 3 iliyopita) niliwahi kumshuhudia padre mwingine wa kanisa katoliki akivuta sigara kali. Nikashangaa sana. Wavutaji wa sigra kali wanafahamu aina hii ya sigara. Hii sio sigara ya kawaida ndio maana ikapewa hili jina la kipekee. Tangu siku hiyo nikagundua kwamba kumbe upadre wakati mwingine ni kazi tu kama kazi nyingine wala haina koneksheni na utakatifu au matendo mema. Kuna mapadre genuine ambao kweli wamejitoa kumtumikia Mungu kwa hali na mali na wengine ni wachumiatumbo tu.

MAONI YANGU
Ifike wakati sasa kanisa litambue umuhimu wa matamanio ya mwili kwa wanadamu na kusitisha mpango wake wa muda mrefu wa kuwazuia mapadri kuoa na kutumia vilevi vingine kama watu wa kawaida ilmradi hawavunji amri 10 za Mungu. Kitendo cha kulazimisha mapadri wasioe na kushiriki matendo mengine mema ya dunia sio jambo zuri.

ANGALIZO
Hii sio mada ya kidini bali ni habari mchanganyiko inayohusu maisha ya binadamu bila kujali imani, dini, rangi, jinsia, kabila au ukanda. Mods msiingie mkenge kuhamisha hii mada kwenda jukwaa la dini tafadhali.

Nawasilisha.


Uko nyuma sana na dunia ya leo
 
.
 

Attachments

  • Screenshot_20230927-171416.png
    Screenshot_20230927-171416.png
    18.9 KB · Views: 4
Na wenyewe wamo humu wanawasoma tuu jinsi mnavyo comment , ila inshot hakuna mfupa mgumu duniani means that , maisha ya useja hakuna anayeweza ishi , hakuna mwanaume duniani aliyekamilika anayeweza ishi bila kukutans kimwili na mwanamke HAKUNA.
s
so ni haki ya uanaume kuto.mba , na ku.nywa bia / kilevi , ILA NI KWA KIASI HATA WAO WANAFUNDISHWA KUFANYA KILA KITU KWA KIASI...........
 
Kiongozi wa dini ni muwakilishi wa dini yake anapaswa kufanya mazuri..
Lakini pia sisi tunapaswa kujua wale ni binadamu wanaweza kukosea, so kukosea kwao hakuifanyi ile dini iwe ya kichizi, ni muhimu kujua sheria ya dini husika, akikosea kiongozi ujue kakosea yeye na sio dini
 
Enzi zetu mapadri ilikuwa ni wazungu wengi toka nchi za italia, hispania, ubelgiji, ureno, canada na ujerumani. Waafrika walikuwa wachache, parokia nzima ni mmoja tu. Padri wa kizungu akifanya misa kigangoni waumini hujaa kanisani, wa kiafrika hawajai. Padri wa kizungu huja na zawadi kama pipi, maziwa ya ngamia, juisi na biskuti, wa kiafrika haji na zawadi. Siku hizi mapadri wengi ni waafrika, hawapendwi kama wazungu. Mapadri wa kiafrika ni wagumu kutoa zawadi. Hawana sauti za huruma
 
Bora hata huyo padre kaoa mke kuliko kudanga kwa siri...bora na huyo anayevuta sigara kali kuliko wanavuta mpaka bangi
 
Ukistaajabu ya Musa hujaona ya Firauni. Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo. Haujapita muda mrefu nikakutana na kijana na kumuuliza kama padre yupo akanijibu padre katoka ila mke wake yupo. Nikamuuliza je, mke wake ni yule niliyemuona anafanya usafi pale nyumbani? Akajibu: NDIYO! Nilihisi kushikwa ganzi na kushindwa kusimama wima. Nikajifanya sijisikii vizuri nikawa nimechuchumaa chini nimeinamisha kichwa. Yule kijana kaniuliza: Vipi unaumwa? Nikamjibu najisikia vibaya.

Kwa mshtuko wangu nilihisi kabisa yule kijana ameunganisha hali yangu na tukio la mke wa padre kwa kuwa alikuwa akiniangalia kwa hofu iliyochanganyikana na wasiwasi. Kijana alionesha hofu ya kutoa siri za watu. Nikaanza kujilaumu kimoyomoyo kwanini nilishindwa kujikaza hadi kijana wa watu akahisi labda nitaenda kuvujisha hizi taarifa kwa viongozi wa kanisa. Nami wala sina nia hiyo na sijamwambia mtu yeyote hadi leo ninapoandika kuhusu jambo hili hapa JF.

Siku za nyuma kidogo (takribani miaka 3 iliyopita) niliwahi kumshuhudia padre mwingine wa kanisa katoliki akivuta sigara kali. Nikashangaa sana. Wavutaji wa sigra kali wanafahamu aina hii ya sigara. Hii sio sigara ya kawaida ndio maana ikapewa hili jina la kipekee. Tangu siku hiyo nikagundua kwamba kumbe upadre wakati mwingine ni kazi tu kama kazi nyingine wala haina koneksheni na utakatifu au matendo mema. Kuna mapadre genuine ambao kweli wamejitoa kumtumikia Mungu kwa hali na mali na wengine ni wachumiatumbo tu.

MAONI YANGU
Ifike wakati sasa kanisa litambue umuhimu wa matamanio ya mwili kwa wanadamu na kusitisha mpango wake wa muda mrefu wa kuwazuia mapadri kuoa na kutumia vilevi vingine kama watu wa kawaida ilmradi hawavunji amri 10 za Mungu. Kitendo cha kulazimisha mapadri wasioe na kushiriki matendo mengine mema ya dunia sio jambo zuri.

ANGALIZO
Hii sio mada ya kidini bali ni habari mchanganyiko inayohusu maisha ya binadamu bila kujali imani, dini, rangi, jinsia, kabila au ukanda. Mods msiingie mkenge kuhamisha hii mada kwenda jukwaa la dini tafadhali.

Nawasilisha.
wanasema binaadamu hawezi kuacha tabia zake za asili
 
Pumba tupu, mapadr lazma wakae kwenye majengo ya dayosisi si vinginevyo
 
Back
Top Bottom