Ajira Serikalini iwe miaka 10 tu, baada ya hapo watu wastaafishwe

Mnaongea kitu ambacho hamkijui kabisaa
 
Na huu utaratibu wa Interview ndio unaenda kuwa Mwarubaini
China/ India zina watu zaidi ya 1.8B
Kupata ajira mpaka uwe na IQ kubwa sana ( Survival for fittest)
Na kuna watu kumbuka wanafanya kazi na Kuacha wanavyotaka ( Salary & oher Benefits Negotiations) Wakitaka Maslahi makubwa kwa kuwa Skills zao ni very demanded hata hapa nchini
 
Pension ya nini mtoto kaajiriwa na 23 akifika 28 anaachia ofisi hapo unalipwa penshen gani na bado umri mdogo? Kwani wanaopiga kazi kwenye NGO wanalipwaga pension wale baada ya contract ya miaka 5
NGO inayo endesha shughuli zake kisheria ni lazima ifuate matakwa yote ya sheria za kimataifa za ajira na sheria za kitaifa, hivyo ni lazima watumishi wake wawe pensionable na wawe na mikataba inayo tambuliwa kisheria ,wawe walipa kodi nk . Ukiona NGO inaendesha shughuli zake na haifuati huo utaratibu basi ujue ni ya kitapeli
 
Sina takwimu sahihi lakini kuhusu auditing and performance test zinafanyika katika ofisi za umma na kwa watumishi pia

Kuhusu production nadhani umewaza tofauti.Hizi ofisi za umma zingekuwa hovyo kama unavyodhani nadhani impact ingekuwa-felt katika maisha ya kila siku. Lakini unaona kabisa mambo kwa ground yapo sawa, mapambio ya mama yupo kazini mengi(hii inatosha kuonyesha public offices nyingi zinafanya kazi kwa ufanisi)
 
Najua huwezi rudia kusoma ulichoandika hapa🤣🤣🤣 sababu unajua kuwa ni porojo
 
Huko vyuoni watakuwa wanajitolea?
 
We unalipwaje pension kwa miaka 5 ya kazi?😂
Pension wanalipwa waliozeekea kazini
 
Pension ya nini mtoto kaajiriwa na 23 akifika 28 anaachia ofisi hapo unalipwa penshen gani na bado umri mdogo? Kwani wanaopiga kazi kwenye NGO wanalipwaga pension wale baada ya contract ya miaka 5
Hizo pension funds Ndio zinazorotesha bongo za waajiriwa wengi maana wako almost 1000% guaranteed na matokeo yake maendeleo na mipango mikakati ya nchi haiendi inavyopaswa.

Aliepewa kazi, vision yake na mission yake ni mbingu na ardhi na aliempa hiyo kazi!!

Mtu yupo radhi afie ofisini kisa anafukuzia pension na sio Kwa sababu ana mchango husiozibika kwenye department yake!

System ya malipo na mafao yaweza kufuatwa ya private sector.

PPP inaweza kuwa Ndio mfunguzi wa njia pia.
 
Kujiajiri ni kugumu na ni kipaji pia; ndio maana wengi wanategemea kuajiriwa mpaka wanakufa.

Mtaji unaweza usiwe sababu, sababu wapo wanaolipwa pesa nyingi kwenye kuajiriwa lakini hawawezi kujiajiri.​
Kwahio point yako ya kwamba wameshafanya kazi na kupata mitaji ni VOID ab INITIO wala ilikuwa haina maana kuiweka hapa sababu hata wewe unapingana nayo...

Kuhusu sera, unategemea alie ajiriwa akutengenezee wewe sera ya kujiajiri wakati yeye mwenyewe amefeli kujiajiri?​
Kuhusu Sera sio kwamba aliyeajiriwa..., Kuhusu Sera ni kwamba tuliyemuajiri sisi ndio mabosi wake na anakula Kodi zetu hivyo ni kazi yake kutengeneza Sera wala sio Hisani..., Hao ndio kazi ya kutunga Sera..., wanacholipwa ndio wanatakiwa kukifanya..., Na hizo ndoto kwamba 100 percent ya watu wanaweza kujiajiri ndio nimekwambia ni Utopian Idea ambayo umekubaliana nayo paragraph ya kwanza naona tena unaileta hapa....
 
Mnajua kweli kuongea ,ukisema hakuna kinacho fanyika maana yake serikali imesimama ,au tafsiri yako ni ipi? Hali ingekuwa hivyo unavyo sema basi mchi hii isinge kuwa hapa ilipo, kikubwa ni nchi kuwa na utamaduni wa kuwajibisha viongozi wakubwa wa serikali na sio kulindana , huku chini watu wanafanya kazi bwana mdogo ndio maana nchi imefikia hapa ilipo, huwezi fananisha tanzania ya miaka 20 au 30 iliyo pita na ya sasa.
 
Ukweli ndio huu, serikalini kila mtu anajivunia security ambayo ndio hio pensheni. Wala focus sio ku deliver wengi wanaenda makazini kwa sababu watalipwa mshahara mwisho wa mwezi na posho za katikati ya mwezi🤣 ndio maana ukiwaambia habari ya kuwa na ajira za mikataba wengi wanang'aka hawataki kusikia hilo na wanalipinga vikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…