Ni kwel mafegi yalinikwaza sanaa
Ila sio official office kama anavyotangaza hapa hata kama atakuajiri inawezekana ikawa kakuajiri kama housegirl ni sehemu ambayo hamna mfumo wowote ... Hapo anapokuambia mnafanya orietation week hapo ndo anapokufukuza kwani
1. Jamaa ni mjuaji balaa kila kitu anajua halafu halafu apo yy sio kila kitu kuna mfadhil msomali mwenziwe yupo njee yy ndo ana support
2. Mshikaj ana Gubu balaa kias kwamba mkipishana kidogo anakutoa
Halafu anavyoongea kama na fustrustion hiv
Sidhani kama ashajiri mfanyakaz akadum hata mwaka mmoja
Alikuvutisha?
Duniani watu ndio kwanza wanaruhusu bangi, wewe eti "mafegi" yake yalikukwaza.
Ukwazike wewe, anaevuta yeye halafu umlaumu yeye? Hujioni kuwa u poyoyo? Labda ungesema alikulazimisha uvute fegi. Lakini, hola.
Waambie serikali basi wasiuze na wasitishe kilimo cha tumbaku. Abdul anachoma mafegi yake kwa raha zake, wewe yanakuhusu nini?
Halafu hilo la kusema "mkipishana Kidogo basi anakutoa". Hilo ni uongo mkubwa usio na mfano. Hivi wewe haswaa, una nini cha "kupishana" na Abdul? Mwenyewe kila siku anasema yeye anawapenda zaidi wasiojua ili apate kuwafundisha kwa vitendo na anawapenda wanaojuwa ili wafundishe wengine. Sijawahi kusikia mtu kapishana nae, labda uwe umeshakaa kwake zaidi ya miezi sita halafu uwasaliti wanafunzi wake. Hapo atakuambia "straight forward" kwaheri. Lakini hiyo ya kwenda tu mara moja au mbili, atakupa ukweli tu, ambao kama huupendi ukweli, mwenyewe utatafuta pakutokea.
Wadanganye wasiomjuwa.
Tena wewe labda ulienda hujamkuta katoka kula, maana akitoka kula tu, utamkuta na cigar na black cofee yake, sio "mafegi", anaipuliza taratiiibu kama Fidel Castro, huku anamezea na kahawa yake. Tena ukimshangaa anakwambia" usishangae, ukija usiku utanikuta napiga Nduum". Utajaza mwenyewe.
Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?