Umri wako na upeo wako haukuruhusu kuyajuwa haya.
Simba na Yanga hazitamilikiwa na mtu binafsi wala hiyo mifumo ya kisasa mnayodanganywa haitofanyika.
Mo atauza hisa zake na GSM watafika mwisho watashuka kwenye hilo treni mmiliki wa hizi timu atapachika vikaragosi wengine wa kuwachangamsha.
Sunderland ndio ilikuwa timu ya watu binafsi waarabu, lakini waliponyang'anywa timu Waarabu na timu kukabidhiwa kina Abunuwasi na kupewa jina la Kawawa (Simba wa vita) hiyo timu ikawa imechukuliwa rasmi na yuleyule mmiliki wa Yanga.
Wewe ni dogo tu huna ulijuwalo, wakati Yanga ipo mtaa wa Mafia, Karume akajenga jengo la Simba mtaa wa Msimbazi, the Karume huyohuyo akajenga jengo la Yanga Jangwani, malengo yakawa yametimia, na ndio sababu Simba ilipotaka kushuka daraja mechi ya mwisho ilikuwa inakutana na Yanga, na ilibidi Simba lazima ishinde ili ibaki daraja la kwanza, mmiliki wa hizi timu hawezi kujihujumu akaamrisha timu kuu iachie ushindi kwa Simba, ambayo kwenye mfumo wa kikampuni Yanga ni Mother company na Simba ni sister company.
Kiongozi yeyote aliyeiva kwenye siasa na historia ya Tanzania ni lazima atakuwa Yanga.
Haya ni mambo ambayo mpayukaji domo bwabwaja kama wewe huwezi kuyajuwa na ndio sababu hakuna uwekezaji utakaowezekana Simba wala Yanga mpaka wamiliki halisi wa hizi timu wakubaki kubadili malengo ya uanzishwaji wake, malengo ya hizi timu hayakuwa mpira.