TANZIA Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar, Willson Kabwe afariki dunia

TANZIA Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar, Willson Kabwe afariki dunia

Status
Not open for further replies.
RIP rafiki yangu Mzee Wilson Mbonea Kabwe kweli kila nafsi itaonja mauti.
Jamani tuwe tayari muda wote kwa hatujui siku wala saa
 
Hajajibu mashtaka yapi? Maneno ya Makonda ndio criminal charge sheet?

Tujifunze kuwapa watu due process of law. Ungempeleka akajitetee angeweza labda kukupa majina makubwa zaidi. RAS is a lightweight kwenye utawala na maamuzi ya jiji. Rais kashtukizwa hadharani na maneno ya Makonda akataka kufurahisha umati kwa kum fire RAS. Mbona kamuacha RC Sadick, alikuwa wapi wakati hii mikataba inapitishwa? Kwa nini AG nae hakuihakiki? Pesa iliyoingiwa mkataba ilikuwa north of the threshold which triggers Attorney General mandatory review. Inakuaje mtu mmoja ajiamulie peke yake kuingia mkataba wa mabilioni bila kufuata sheria? Haiwezekani. Basi angeweza kuuza Uwanja wa Taifa peke yake. Your problem here is bigger than just one individual.

Kwameh weye umekurupuka Au Ulikuwa Na Kitwanga.Makonda aliwaambia wahandishi wa habari majanga aliyo yafanya ndungu Kabwe hapo Dar.Kwa sababu Mh Makonda hawezi kumfukuza kazi kisheria alipeleka malalamiko Kwa Mkulu.
Siku ya ufunguzi wa daraja la Nyerere ndio Mkulu akamuuliza Mh Makonda kuhusu hayo malalamiko ndio akayaeleza Ndio JPM akatumbuwa bila ganzi
Halafu umechanganya sana madai yako kwa KiswaNglish haueleweki kabisa
 
Ni msabato. Kumbuka usihukumu ... Anayehukumu sio binadamu.. Unaweza kuhukumu kumbe wewe kifo chako umepangiwa kwenda kufia gesti na mke wa mtu..
Umeelewa nilichoandika?. "Kama aliwekeza kwa mungu basi akale bata"
 
Anayetakiwa kuzingatia masuala ya kisaikolojia na utu wa binadamu ni MTUMBUAJI na siyo MTUMBULIWA. Tukiendelea na style hii ya kudhalilisha viongozi hadharani bila kuzingatia sheria na kanuni za uongozi bora tutapoteza wengi.

Usisahau kila nafsi itaonja mauti. Siku yako ya kufa ikifika hata Kama umetumbuliwa jipu chumbani tena gizani bila mtu mwingine kujua bado utakufa tu.




RIP Kebwe.
 
Ni kweli mtumbuaji anatakiwa aangalie hilo, lkn tutafanyaje ikiwa watu sio waadilifu? mimi nadhani mtumbuaji akianza kufikiria masuala ya saikolojia kwa watuliwaji na viongozi wa chini nao wafikirie uadili pia! nchi yetu hii viongozi walijisahau!
 
Anayetakiwa kuzingatia masuala ya kisaikolojia na utu wa binadamu ni MTUMBUAJI na siyo MTUMBULIWA. Tukiendelea na style hii ya kudhalilisha viongozi hadharani bila kuzingatia sheria na kanuni za uongozi bora tutapoteza wengi.
Jamani tusikuze sana haya mambo maana kufa kupo na probability ya kutokea ni 1 (100%), mind mh. alishaenda India hata kabla ya kutumbuliwa kielelezo kwamba alikuwa mgonjwa.
Kwani jamani makaburi yote yaliyojaa nchi hii na dunia hii mauti yao yalisababishwa na kutumbiliwa au kudhalilishwa!?
 
Mimi Sitasema R.I.P hadi pale pesa za watanzania alizokula azirudishe hata kama ni familia yake
 
Tabia ya Watanzania kusifia Marehemu, Badala ya ku-appriciate walio hai wakitahidi.

Mnatoa tuzo makaburini wakati wenzetu wanatoa tuzo majukwaani!

Haya endeleeni
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom