Anapost wanaume walionunua magari na chattings zao status wakati mimi niko kwenye hali ngumu kiuchumi

Hivi ni mm na ushamba wangu au mwanamke akiolewa anatakiwa achunge anachopost hasa kinachohusu wanaume wengine ambao si ndugu zake!
Naunga mkono hoja, kuna wanawake ni shenzi type kabisa.
Unakuta mke wa mtu anapost kabisa eti "leo nna hamu ya kula kuku nani aninunulie"? Siriazi ?

Mwanamke wa aina hiyo hafai ni wakupiga chini ili aende kwa hao wenye magari aone kama wana muda nae baada ya kuliwa.
 
bahatimbaya hajaolewa nayuko 30+wahuni siowatu wazuri

Comment yangu ni baada ya kusoma comment yake.

Ikiwa simjui undani wake zaidi ya kuona jina lake JF basi sina sababu ya kutaka kujua zaidi ya alichoandika muhisika ama kushuku ukweli wa alichoandika.
Hayo mengine kama yana ukweli basi ni yake mwenyewe, hayanihusu.
 
Ulipokuwa ukiazima magari pindi una mtongoza na kwenye sherehe kwa hisani ya michango ukawa na msafara mreefu wa magari wakati wewe hauna hata side mirror ulitegemea nini?
 
Naona siku za hivi karibuni nyuzi za Wanaume kulalamika kuhusu ndoa zao zimekuwa nyingi sana, why??? Au ni mbinu maalumu ya kufanya kampeni ya "kataa ndoa" huku ajenda zikiletwa hapa jukwaani kwa kupitia mlango wa nyuma?
Hii december ngumu sana kwa wanaume wenye wake/wapenzi wapenda show off na matanuzi.
 
Anaye kebehi na wewe mkebehi na uache life liendelee,hiyo ni dawa mujarabu,kuliko ya kuandikiwa na daktari🤔
 
Miaka 29 bado ni kijana mwenye nguvu na safari ndefu.

Sijajua ilikuwaje ukapata matatizo ya kiuchumi na ni kipi kilijiri.

Lakini fanya uwe na vyanzo vingi vya mapato na usitegemee kimoja.

Mkeo yupo obsessed na magari kwa sababu ndivyo walivyo wanawake huwa wanawaza kwa kutumia moyo(hisia) kwa hiyo anahisi (siyo kweli) kwamba maisha yamekushinda.

Uwezekano upo kwamba yeye ndicho kikwazo cha wewe kutokusonga mbele. Yeye mfano, alitakiwa akutie moyo ili uweze kuinuka, maana ndiyo kanuni ya maisha. Kuanguka ni kwa kila mtu; suala linakuja, je, ni mara ngapi unainuka?

Kwa kawaida simba jike humpa nguvu simba dume ili afanye zaidi. So tulia na uzungumze na huyo msichana, ila ukithibitisha kwamba anakuletea ukichaa badala ya faraja mkanye bila uoga, na akikaidi kaa naye mbali, hata uanze upya.

Mwanaume hazeeki. Kuanza upya siyo ujinga. Kupata ni foleni kila mtu kwa wakati wake.
 
Hoja yake ina mashiko, siyo mawazo dhaifu.
Kumbuka: Vyanzo vikuu vya ugomvi na mauaji kwa wanandoa ni masuala ya namna hii.
Binti wa miaka 20s bado ana mawazo ya chini sana na pengine kampongeza bila kuwa na ujumbe wowote kwa mumewe, na mumewe anamjua huyo jamaa....akiachana na huyo ni wapi atapata aliyekamilika asiye na makwazo?
 
Hakika umepevuka akili
 
Mkuu hapo kwenye "Mens" sema tu "Men". Milenia hii mna changamoto sana yaani sijui tuko kwenye Ruhamo wa Ruwaza (Paradigm Shift)? Na hii ndiyo imekuwa new normal! Vijana mnakimbilia sana kuleta na kuanika matatizo yenu ya ndoa kwenye mitandao! Ina maana siku hamna washenga au Wazazi wa kuwaweka chini na kusuruhisha matatizo yenu? Mnajichoresha! Mwingine juzi kaja kuanika hapa eti amegongewa mke na mke amehama chumba! Karne hii vimama vinawapitisha kwenye tanuru la moto mpaka mseme!
 
Mwamposa huwa anasema tatizo lako litazaa faida.
Mfano hamonizer alivyoachana na kajala(tatizo) likazaa wimbo wa single(faida) ambao umemfanya kupiga hatua.
Usijali,Mungu anakupitisha ili ujue Mkeo NI MTU wa Aina gani.
Tafuta Yatima na Wajane katoe sadaka ya shukrani Mshukuru Mungu kwa yote.Msifu yeye,mtukuze.hasira weka pembeni.
Katafute Sala ya Mt.Rita sali novena siku 12.
Nakupa siku 30 lete mrejesho.
NB:Usimuulize chochote,Wala usionyeshe umekasirika.wewe ongea na Mungu TU.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…