Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Wananchi waamke na kudai uwajibikaji wa viongozi.

Serikali ina matumizi makubwa ya anasa

Uchumi umedorora kwa wananchi, Coronavirus imeathiri uchumi. Hivyo serikali ilipaswa kuacha matumizi ya anasa, na kunyonya masikini
Nani kakwambia Royal Tour inagharamiwa na Serikali?
 
Ni kama maajabu mapya ndani ya taifa , Rais anakazana kuibrand nchi na kuacha mamlaka husika kufanya kazi zake , serikali ina wizara yenye dhamana , wizara ina Bodi maalum ya Kutangaza Utalii ndani na nje ya nchi , serikali ina mabalozi karibia asilimia 80 ya mataifa duniani , taifa lilipata Uhuru mwaka 1961 ambapo ikifika disemba mwaka huu wa 2021 taifa litakuwa na miaka 60 ya Uhuru wake wa kupeperusha Bendera , umri wa miaka 60 sio umri mdogo duniani ,Rais kadanganywa na wapiga dili eti anaibrand nchi kama vile nchi haijulikani kuanzia jiografia yake mpaka uhuru wake , utamduni wake, yani ukisikia nchi imekamatwa na wapiga dili ndio sasa.

Hivi wenzetu wa nchi ya Rwanda ndio wanaibrand nchi yao hivyo jamani , kwanini majasusi wetu wa uchumi wasiige hata hapo Rwanda jamani , mbona Rwanda wametoka katika taswira mbaya ya nchi yao lakini leo branding yao ni kimataifa duniani kote , mfano juzi hapa wakati mchezaji maarufu duniani Leon Messi alipoamia timu nyingine Rwanda walifanya ujasusi wao mbele ya dunia na ile kaulimbiu yao ambayo ni fupi tu inasema "VISIT RWANDA" yaani dunia ilisimama kuangalia Messi kapewa jezi namba ngapi katika kikosi kipya alipogeuka tu wakakuta maneno ya VISIT RWANDA, jamani hizi vitu zinatengenezwa na wazalendo , tatizo la watanzania tunawaza ujinga tu kuanzia ngazi Usalama wa Taifa mpaka chini hakuna cha uzalendo zaidi ya dili tu.

Sasa mtu unajiuliza hivi hili taifa tangu lianze kushiriki katika mambo mbalimbali ya duniani tangu lilipozaliwa bado tu haina special branding yoyote , mabalozi wanafanya nini sasa ? wizara ya utalii inafanya nini sasa? Bodi ya Utalii inayotumia mamilioni ya kodi za watanzania inafanya nini sasa? hivi ni kweli katika juhudi zote zilizofanyika hapo awali ni sawa na zero na tunaamini kuwa hiyo documentary ya mama Samia ndio itafanya branding ya taifa , hivi kweli watanzania tumefikia upeo huo wa kufikiri?

Nauliza tena hivi ni kweli kuwa Mama Samia akitoa hiyo Movie yake taifa ndio litajulikana na uchumi wa taifa kuongezeka na wawekezaji wataongezeka? huu ushauri kapewa na nani jamani ? alafu watu wanaoitwa Usalama wa Taifa wapo tu kuangalia ni kama hawajijui kuwa nao wanamajukumu ya kuangalia mikakati na dira ya kitaifa , ukisikia hovyo ndio hii , wale think tanker wa taifa nao wameafiki kuwa Movie ya Mama itatutoa kiuchumi na kimataifa... eee mungu tusaidie ... hii style ya branding inatokea wapi ...
Janga la CORONA limesababisha tupate bilioni 500 tu Kati ya malengo ya TRILIONI 5.....

Katika hali hii ,mh.Rais wetu SSH halaumiki KUUTANGAZA UTALII kwa nguvu hizo ili pale tu DUNIA itakapovuka hivi vikwazo watalii wamiminike vya kutosha......

#LawamaHazilisaidiiTaifa
#SiempreJMT
 
Rais Samia anaongea kwa mipasho Mambo muhimu ya nchi.

Eti "ukifanya watasema, usipofanya watasema. Sasa acha tufanye"
Kwako maneno ya UKWELI ni mipasho bwasheee eee?!!!

Mh.Rais AFANYE TU kwani waswahili wanasema "miluzi mingi humpoteza mbwa"......
 
SASA naelewa Kwa nini kina Polepole walitaka kupindisha Katiba. Mama ni mweupe pee.
Polepole alikuja kwa "kubebwa tu ndani ya CCM"....

Ana kaliba ipi ya SIASA TUNDUIZI ndani ya CHAMA?!!!!

Hivi Polepole unaweza kumfananisha na Komredi Shaka Hamdu Shaka kwa HUDUMA YAKE YA MUDA MREFU NDANI YA CHAMA?!!

CCM INA KANUNI ZAKE

#SiempreCCM
#KaziIendelee
 
😁😁😁
2656558_102011131.jpg
 
Huwenda mama anadanganywa kama unavyosema lakini kwanini tuwaige Rwanda sisi hatuna ubunifu rais ni taswira ya taifa wamebuni wazo zuri sana na huwenda faida yake ikaonekana baadae
Inabidi tuwe wabunifu siyo kuigaiga kila kitu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Heee..huo ndo ubunifu shekhe! Uwiii...kachokaaaaa...to hell
 
Umetolea mfano Rwanda ukiwa hujui kuwa Rwanda ndo nchi ya kwanza kufanya hiyo program ya Royal Tour kwa Africa Mashariki.

Kwa Taarifa yako idea ya Visit Rwanda ilikuja baada ya Kagame kuendesha iyo program ya Royal Tour
afadhali umemjibu, mi sikuwa na mpango hata wa kumjibu; sana sana nikitaka nimuulize tu kuwa kwani ni lazima kufanya kile kinachofanywa na rwanda?!! hatuwezi kuja na ubunifu wetu wenyewe?

mtamtukana matusi yote, lakini huyooooo anaenda zake taratiiibu
 
Ni kama maajabu mapya ndani ya taifa , Rais anakazana kuibrand nchi na kuacha mamlaka husika kufanya kazi zake , serikali ina wizara yenye dhamana , wizara ina Bodi maalum ya Kutangaza Utalii ndani na nje ya nchi , serikali ina mabalozi karibia asilimia 80 ya mataifa duniani , taifa lilipata Uhuru mwaka 1961 ambapo ikifika disemba mwaka huu wa 2021 taifa litakuwa na miaka 60 ya Uhuru wake wa kupeperusha Bendera , umri wa miaka 60 sio umri mdogo duniani ,Rais kadanganywa na wapiga dili eti anaibrand nchi kama vile nchi haijulikani kuanzia jiografia yake mpaka uhuru wake , utamduni wake, yani ukisikia nchi imekamatwa na wapiga dili ndio sasa.

Hivi wenzetu wa nchi ya Rwanda ndio wanaibrand nchi yao hivyo jamani , kwanini majasusi wetu wa uchumi wasiige hata hapo Rwanda jamani , mbona Rwanda wametoka katika taswira mbaya ya nchi yao lakini leo branding yao ni kimataifa duniani kote , mfano juzi hapa wakati mchezaji maarufu duniani Leon Messi alipoamia timu nyingine Rwanda walifanya ujasusi wao mbele ya dunia na ile kaulimbiu yao ambayo ni fupi tu inasema "VISIT RWANDA" yaani dunia ilisimama kuangalia Messi kapewa jezi namba ngapi katika kikosi kipya alipogeuka tu wakakuta maneno ya VISIT RWANDA, jamani hizi vitu zinatengenezwa na wazalendo , tatizo la watanzania tunawaza ujinga tu kuanzia ngazi Usalama wa Taifa mpaka chini hakuna cha uzalendo zaidi ya dili tu.

Sasa mtu unajiuliza hivi hili taifa tangu lianze kushiriki katika mambo mbalimbali ya duniani tangu lilipozaliwa bado tu haina special branding yoyote , mabalozi wanafanya nini sasa ? wizara ya utalii inafanya nini sasa? Bodi ya Utalii inayotumia mamilioni ya kodi za watanzania inafanya nini sasa? hivi ni kweli katika juhudi zote zilizofanyika hapo awali ni sawa na zero na tunaamini kuwa hiyo documentary ya mama Samia ndio itafanya branding ya taifa , hivi kweli watanzania tumefikia upeo huo wa kufikiri?

Nauliza tena hivi ni kweli kuwa Mama Samia akitoa hiyo Movie yake taifa ndio litajulikana na uchumi wa taifa kuongezeka na wawekezaji wataongezeka? huu ushauri kapewa na nani jamani ? alafu watu wanaoitwa Usalama wa Taifa wapo tu kuangalia ni kama hawajijui kuwa nao wanamajukumu ya kuangalia mikakati na dira ya kitaifa , ukisikia hovyo ndio hii , wale think tanker wa taifa nao wameafiki kuwa Movie ya Mama itatutoa kiuchumi na kimataifa... eee mungu tusaidie ... hii style ya branding inatokea wapi ...

Povu jingi hamna la maana hata moja la maana
Akili yenye afya nzuri inaelewa kuwa mtu wa kwanza kabisa kuibrand nchi huwa ni RAISI wa nchi ktk angle yeyote atakayo ibuka nayo. enzi za MWENDA ZAKE aliibrand Tanzania katika ushupavu wa maamuzi na misimamo.tulifahamika sana Afrika mapaka ulaya walikua wanatuimba Tanzania na Magufuli wetu. Lakini brand hiyo ilikua haina tija ya kipato kwa kipofu hakuyaona hayo.
Na Raisi Samia mama yeye ndio nembo ya kwanza ya nchi nae ataka kuibrand Tz katika Utalii na vivutio vya Tanzania hili litaingiza tija kubwa kwa kumiminika watalii nchini na huo mfano wa Visit Rwanda ni hatua changa sana kwa nchi kama vile Tanzania
 
Mama anafanya uzuri.
Baada ya kungana Tanganyika na Zanzibar Library za huko duniani zilibaki na lundo la vitabu vinavyojisomo kuwa Tanganyika ipo East Afrika kumbe ilishapoteza jina na kuitwa Tanzania.

Tanzania ina rasilimali nyingi lakini haijjlikani.
Huko nje watu wa Kawaida hawaijui Tanzania.
Zanzibar inajulikana mana historia yake haikuchakachuliwa sana.

Acheni mama aitangaze nchi.

Matumizi mabaya hata Magufuli na ukali wake alipigwa changa la macho.
Watu wakanunua mpaka nguo hewa kwenye wizara ya mambo ya ndani chini ya Kangi Lugola.

Magari ya milioni 400 yananunuliwa na yale ya mil. 180 yanauzwa mil. 5.

Magari yaliyonunuliwa mil. 80- 100 yapo juu ya mawe yanapewa bajeti ya mafuta kila mwezi watu wanakwenda kula bata.
Mama amekuta maadili ya watanzania bara ambao wengi wao ni zao la vyeti feki na wizi wa mitihani yapo chini sana. Wengi wa Watanzania Bara wanaibia nchi wapate pesa za ngono na ulevi.

Nchi ina watumishi 90 % wasio na maadili mazuri kuanzia kwenye familia siasa mpaka kwenye dini.
 
Wananchi waamke na kudai uwajibikaji wa viongozi.

Serikali ina matumizi makubwa ya anasa

Uchumi umedorora kwa wananchi, Coronavirus imeathiri uchumi. Hivyo serikali ilipaswa kuacha matumizi ya anasa, na kunyonya masikini
wananchi gani unawaongelea? hawa hawa wabongo waoga na wanafki?
sana sana wataishia kulalamika kwenye social media
 
Umetolea mfano Rwanda ukiwa hujui kuwa Rwanda ndo nchi ya kwanza kufanya hiyo program ya Royal Tour kwa Africa Mashariki.

Kwa Taarifa yako idea ya Visit Rwanda ilikuja baada ya Kagame kuendesha iyo program ya Royal Tour




Alisikika mmoja na aliyoongea ni Kweli



Kipindi hichi Mr Slim alihusika
 
Rais Samia anaongea kwa mipasho Mambo muhimu ya nchi.

Eti "ukifanya watasema, usipofanya watasema. Sasa acha tufanye"
maybe alivyowasilisha si powa but she is right. na hii inaanzia kwenye jamii na familia ndani kabisa.
kuna mambo usipofanya watakusema.. ukifanya watakusema pia.
 
Back
Top Bottom