Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Afu eti 2025 anataka aendelee kugombea,Nafikiri ule wakati wa TZ kufanya kweli utakua umewadia.
Huyu mama jinsi alivyo hapendwi na WaTZ Zaid ya vimtu vichache vyenye maslahi/matumbo njaa,Ataaibika.
 
Unaandika kama mtu asie na akili. Sasa kama yule alikua anaua watu wewe mbona hukuuawa.

Uhuru gani alitunyima, huku JF tumekua tukiandika kila siku, toka lini JF ilifungwa tusitoe maoni?

Huyo mama ametoa uhuru gani wa maoni ambao hatukua nao?.

Taniri gani analipa kodi ya haki?
 
Huo ni kwa mujibu wa uoni wako hafifu,wetu tunaiona Tanzania Mpya inayozidi kuimarika zaidi na zaidi kitaifa na kimataifa.
 
Frankl speaking ,Sijawahi shuhudia Tanzania hii Rais hapendwi na wananchi kiasi hiki.
Yan hapendwi haswaaaa,hata tukisema wanaume tukae pembeni tumuache na hao wanawake wenzie anaoamini ndo wanamuunga mkono,Hapati hata 30% ya uungwaji mkono,Huyu Urais umemkataaa na unaendelea kukamkataa kabisa
 
Hapendwi na nani? Hapendwi na machadema na wazee wa legacy mbona sisi tunampenda?

Utaacha kumpenda Rais anayefanya haya 👇





 

Sema CCM Imechokwa Wala sio mtu,leo ukimchukua SSH akaja chadema utashangaa Sana NDANI ya wiki yani, huko ccm mtu akishaona tumbo lake limebonyea ,kelele zake sio za Dunia hii,

CCM inafanya viongonzi wake wasipendwe, laki pia niseme hata mwendazake alichukiwa Sana na tena Sana kuliko huyu
 
Kama hujafa wewe siyo kwamba hakuua. Magufuli kaua Ben Saanane, Azory Gwanda na wengine zaidi ya 300 wa Mkuranga, Kibiti na Rufiji.

Akina Tito Magoti na Eric Kabendera walibambikiwa kesi kwa sababu ya maoni yao.

Matajiri wanalipa kodi. Kama hawalipi, kuna Mahakama ya TRA Tribunal wapelekwe pale. Kama mfumo wa nchi ni dhaifu katika ukusanyaji, hilo ni suala jingine.

Kama unabisha na hii mifano itakuwa siyo mtu makini yaani kama wale wa darasa la 7. Sintokuwa na msaada zaidi
 
Jumla 3000 hv mkuu sio 8000 hiyo namba siyo ya kwel mkuu.
 
Nani aliiambia IMF kuwa damage ya korona Tanzania unaweza kuwa covered na Hizo tirioni walizokopesha?
Tanzania ambayo Raia wake wamegomea (wamechanjwa 350k tu kwa watu zaidi ya 60M) chanjo hiyo korona imewaathiri vipi?
Tanzania ambayo korona imechukua watu wasio fikia hata 500 imekuwa na adhari gani kulinganjsha na magonjwa na majanga mengine yanayotukabili?
Kwanini badala ya kutoa mkopo IMF hawakuona njia nyingine kama kusamee madeni tuliyonayo ili tupunguze kiasi tunachowalipa badala yake wameongeza deni ambalo (japo wanadai ni la masharti nafuu) linaongeza mzigo kwa taifa hapa ukiwa na fikra hafifu utaona ni ahueni eti ajira ooh madaraja yamepanda na mishahara inapandishwa yaani tushabikie inchi kuongeza uwezo wa kufanya matumizi bila kufikiria mapato yake ni hii mikopo ya IMF ambayo ina subject vizazi vijavyo kwenye utegemezi na umasikini wa milele!!
 
Mkuu Sasa umeisha nichefua sema hapendwi na machadema , Mimi ni kada mtiifu wa chama changu CHADEMA, sikia sie tunamchukia shindwa simamia haki Basi Wala hatuna ugonvi nae, ila nikwambie asilimia ,50% ya wanaomchukia ni ccm nae hashutuki
Hiyo asilimia 50% umeipataje mkuu? tuwekee data hapa za hiyo research yako.
 
Mkuu Sasa umeisha nichefua sema hapendwi na machadema , Mimi ni kada mtiifu wa chama changu CHADEMA, sikia sie tunamchukia shindwa simamia haki Basi Wala hatuna ugonvi nae, ila nikwambie asilimia ,50% ya wanaomchukia ni ccm nae hashutuki
Ccm wa legacy wakimchukia kuna shida gani? Ulitegemea wampende au? Hadharani hawawezi kuongea wataishia kunong'ona na yupo hapa hadi 2030..

Inaitwa usiyempenda kaja,sisi kitaani tunamkubali anatatua kero zetu kama hutaki subiria uchaguzi.
 
Wewe nae ni kiazi hizo,kwa hiyo uchumi ukiathirika na Serikali ikapata fedha za kupunguza makali iache kukopa au? Huna akili aisee,mda huo hutaki pesa mahitaji yanakusubiria ukipange au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…