Mr. Sound umetumia neno kali kidogo jaribu kuwa na Adabu na mkuu wa nchi. Mwenzio mch. Msigwa kaitwa polisi kwa tweet tu.
Mimi napenda sana mh. Mkuu wa nchi
Asimamie aliyoiita vibrant democracy kwa kusaidia Swala la la Mbowe.
Matatizo yetu mengi ya kutofuata sheria,kanuni na taratibu watu bila kuwajibishwa yanatatuliwa na Katiba mpya. Ningependa kabla mama hajamaliza miaka yake kumi awe ametuwekea kitabu kipya cha kutuongoza Tanzania sio kisiwa dunia ni kijiji na mbaya zaidi information zina transcend haraka sana yale yaliyotokea Arab spring tujiepushe nayo yanweza kuja kutokea hata hapa kwetu na kwa akili na ufahamu wa watu wetu yanaweza kuwa na outcome mbaya zaidi.
Siamini sana kwenye uwekezaji huu kama wa wachina hawa na wahindi wanaokuja kunyonya wananchi. Serikali iwezeshe zaidi wananchi waweze kuwa na mitaji riba za mikopo zipungue na utalaamu. Sekta zote haswa kilimo. Ikiwa Philipine anauza mchele ulaya mchele wa mbarali sijui unashindwaje kwenda kuuzwa hata Morroco na Tunisia tuu.
Serikali ipunguze watumishi wasio na tija bali wapo kisiasa hii yote ni kupunguza matumizi. Mkoa tulihitaki DEd tu anatosha hawa wakuu wa mikoa,wilaya, katibu sijui wote wangeenda kujiajiri mambo wanayoyahubiri wakiwa majukwaani. Too much chawaz u know.
Fedha ya serikali kuwe na ukali na ufuatiliaji wa kimfumo na kibinadamu isifujwe. Mfano sasa hivi kila siku watumishi wanatoka dodoma kuja dsm bila sababu za msingi. Kipo kisa kimoja mkoa mmoja jengo haliishi huku serikali imetoa fedha lakini mkandarasi fedha halipwi kufauatilia kumbe Mkurugenzi anazungushia hela kkoo kwenye biashara zake.
Waziri wa fedha ame underperform sana simply gharama za vitu vyote kuanzia vyakula, umeme, ujenzi,mbolea, spare,pembejeo,dawa vimependa ghafla kila wiki. Kunahitajia ultimate intervention hata ya ubabe vitu vispande hovyo. Maisha mtaani yanazidi kuwa magumu ili hali mishahara haiendani na bei ya vitu.
Bado tunapenda tusikie mara kwa mara performance ya mabalozi wetu maana wanalipwa na watoto wanasomeshwa lakini output yao bado ni storiii tuu. Na hata watanzania wanapopata matatizo mabalozi huwasikii wakitia jitihada. Kuna dogo kapigwa risasi marekani ikabidi upitishwe mchango wa nauli ya kuja kuzikwa nyumbani hii nia aibu kwa nchi. Wote tu ajua hakuna wawekezaji wazuri wenye manufaa kwenye ajira kama wazungu kuliko wachina na mataifa mengine. Balozi zetu zichangamke zilete wawekezaji. Mfano Hakuna mwekezaji aliinua wafanyakazi kama Barrick, Twiga cement lakini sio wahindi wa Tanzanite one, Sio Dangote mpopo. Wawekezaji kabobo wala wasitupotezee muda tutachosha wanachi wetu bure.