Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

MAMBO MENGINE SIO RAIS NI NDALICHAKO NA UMMY MWALIMU.

MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI.
Wanamchafua bure Raisi wa NCHI. Hiyo tabia waache kabisa. Ipo siku hawa mawaziri watataka kujaribu walimu wa shule ya msingi kwenda kufundisha vyuo vikuu kwa kisingizio kuwa na wao ni walimu wanahaki sawa. Niombe Rais wa NCHI amuondoe Ndalichako hapo wizarani haraka sana.
 
Ukiwa Rais pamoja na kuwa na Washauri, lakini unatakiwa kuwa na uwezo wako binafsi, lakini huyu ana uwezo mdogo mno, hasa kwa cheo alicho nacho.
Uwezo wake labda angekuwa mkuu wa shirika au Taasisi fulani hivi.
 
Alipokwenda UN, Marais hata wale walioleta kaptula za mdomoni hawakuvaa, alibaki amevaa pekee yake bila aibu.
 
Mbowe siyo Gaidi ila anafanya vitendo vya kigaidi.

Ni kweli wakati ule wenzake wanataka wajipange kupanga mipango ya kiuongozi unaanza kuleta kelele ili wapoteze direction lazima hata angekua yeye angefanya Jambo ambalo litakupa utulivu wa kupanga malengo yako.

Mfano upo wazi wakati wanafanya malbano na Polisi,mahakama huku wenzao wanaendelea na ujenzi wa nchi wakimaliza angalau tutakuwa tumefika mbali.

Mama piga KAZI sisi hatuoni kosa lako na tupo kimya tunaangalia tukiwa imara na vichinjio.
 
Mpuuzi weye hadi keshokutwa asubuhi.
 
Tozo, kubambika kesi ya ugaidi kwa mbowe na kukandamiza democracy na mwisho huwa hafuatilii utendaji wa mawaziri na watumishi wengine, Hii italeta upigaji mkubwa ktk serikali yake na miradi mingi itakwama,and this will bring her failures sooner than later,and In free, fair,competitive democratic election she can only win the heart of Jakaya,
 

(1)Mahakama haijatoa hukumu mpaka sasa wewe unasemaje amebambikiwa? Na ukifuatila mwenendo wa kesi inaoneka uchunguzi wa mashtaka yake ulianza kabla ya Samia kuingia madarakani sasa Rais Samia anausikaje hapo?

(2)Embu tutajie walau bidhaa tano muhimu unazozijua wakati Rais Samia anaingia madarakani zilikuwa zinauzwa tsh ngapi na sasa ni tsh ngapi?

Kwa sasa Uhuru wa Wananchi kujieleza na kuwa na furaha mitaani kimeongezeka kuliko mwanzo sasa sijui ni kipimo gani ulichochukua kuonyesha kwamba demekrasia imebanwa kama kipindi cha Magufuli?

Ili la mwisho sijalielewa yeye ni mwana CCM na anajipambanua kuwa yeye ni CCM sasa sijui wewe ulitaka ajipambanue vipi embu hapo tufafanulie kidogo
 
😍
 
1.Tozo
2.Tozooo
3.Tozoooooo
4.Appointed Jan Makamba for Tanesco shittt!!!
 
1)Mahakama haijatoa hukumu mpaka sasa wewe unasemaje amebambikiwa? Na ukifuatila mwenendo wa kesi inaoneka uchunguzi wa mashtaka yake ulianza kabla ya Samia kuingia madarakani sasa Rais Samia anausikaje hapo?
Acha kutetea ujinga, unaelewa maana ya ile interview yake na Kikeke?? Unakumbuka alichokisema? Unaelewa impact ya maneno yake?
 
Kupandishwa MADARAJA WATUMISHI WA UMMA......

Haiwezekani hawa WATUMISHI wa umma wapandishwe madaraja....bora wangebaki vilevile tu kama miaka 5 iliyopita.....

HAPA MH.RAIS SSH "ameniangusha mnoooo"

NDIMI PINGA PINGA FC MEMBA
kufanya hayo katimiza wajibu wake lakini ukishapuuza mambo ya msingi lazima watu timamu nao watakupuuza na utabaki kuungwa mkono na oya oya wasojua haki zao/wanaonufaika kupitia wewe
 
we jamaa sijui kama upo sawa kichwani, rais alipohojiwa bbc alidai wenzake mbowe walishahukumiwa na yeye alikimbilia kenya kuepuka kukamatwa
 
Ninasikitika leo hii mwananchi anauziwa bati moja 25,000 cement na nodo Bei hazishikiki lililo mbaya zaidi sahivi pembe jeo za kilimo Bei imepanda marudufu hususan mbegu za mahindi toka 11,000/12,000 kwa mfuko wa kilo mbili Hadi kufikia 15,000.kwa maisha haya cjui tunakoelekea
 
we jamaa sijui kama upo sawa kichwani, rais alipohojiwa bbc alidai wenzake mbowe walishahukumiwa na yeye alikimbilia kenya kuepuka kukamatwa
Kwa hiyo kwa kauli hiyo ndio majibu ya hoja zako? Angalia isije ikawa wewe ndio haupo sawa kichwani badala ya mimi
 
Kwa hiyo kwa kauli hiyo ndio majibu ya hoja zako? Angalia isije ikawa wewe ndio haupo sawa kichwani badala ya mimi
kwako wewe rais kusema uongo wa wazi unaona ni jambo dogo? unadhani akiitwa mahakamani kuthibitisha hilo itakuwaje?
 
Acha kutetea ujinga, unaelewa maana ya ile interview yake na Kikeke?? Unakumbuka alichokisema? Unaelewa impact ya maneno yake?
Subiri hukumu au uiamini Mahakama? Rais ni binaadamu kama wengine tu anaweza kusema neno na ulimi ukateleza(kukosea) alisema kuna magaidi wamefungwa Tanzania je tunamfungwa walau mmoja wa ugaidi katika Nchi hii?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…