Anayesema Moshi pagumu kwa wageni, ugumu wake ni nini?

Anayesema Moshi pagumu kwa wageni, ugumu wake ni nini?

Nakubali kwa eneo la ujenzi wanaongoza maeneo makuu mawili ujenzi wa nyumba za makazi ambazo kazi yake kubwa Ni moja kufikia wakati wa Krismasi na pili kufikia waombolezaji waliopeleka msiba

Ujenzi wa pili wasiousahau Ni wa kuzika kwao na kujenga makaburi ya waliowazika

Haya ndio hasa utasokia ohh mchaga lazima ajenge kwao!!!!

Makabila Mengine definition ya kwao Ni pale anapopatia Riziki iwe Dar ,Mwanza au popote .Anaweka kambi hapo.Mchaga Akisema kwao definition kubwa Ni Krismasi na kuzikwa!!! Hamna kingine Cha ziada.Muulize mchaga yeyote ana Nini Cha ziada kafanya kwao zaidi ya kujenga nyumba ya kufikia Krismasi na misiba na kujenga makaburi kwao.Ana Nini Cha ziada? Wengi wao hamna kitu
@YEHODAYA una CHUKI kubwa sana na wachagga kuanzia na chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kumbe hata chuki yako na Chadema ni safu ya chama pale juu kuwa ni ya wacchaga ikiongozwa na Mbowe
 
Nyumba ya kulala tu sio Asset ni liability sababu haiingizi hela linatumia hela tu

Hakuna benki itakupa pesa kisa eti una ghorofa la kufikia Christmas Moshi. Hawataki benki kuchukua kama dhamana unless likiwa na wapangaji hapo Sawa lakini ghorofa tu liko migombani Moshi liimekaa kama mtu anajisaidia haja kubwa wima linasubiri tu watu waje msibani na krismasi eti ukopee benki kama dhamana Hakuna
Una chuki binafsi. Hawaendi Christmas tu wanaenda vipindi vingine vya mwaka sababu sk hizi barabara zimetengenezwa na watu wengi wana magari si kama zamani.
Zile nyumba zinarithishwa kwa hiyo vizazi na vizazi vinaendekea kuishi kwenye makazi bora, sio kunywa supu mjini ukirudi kijijini kwenu unaenda kunya vichakani.
 
Nipo kwenye keyboard just like you

Huna tofauti na mimi,then una audacity ya kuniita "keyboard warrior" wakati na wewe upo kwenye keyboard?

"Mere say" ni Kingereza cha wapi ndugu?

Your English is in ICU,try to polish it up for God'sake!

Ofisa Ardhi usiejua Kingereza sijui ni wa wapi aisee.

Nenda site kashike beacon za kuchimbia!
Umepanic mkuu take a glass of cold water and relax for a bit,we waenda wizarani kutafuta data za land owners in Tanzania,mie nalog in na kukupa hizo data😂👊🏼🙏
 
moshi ndio mkoa pekeee nyumba za msajili huwezi kukuta wamelundikana wahindi kama mikoa mingine kupata duka la muhindi moshi ni sawa na kukuta mhindi bariadi
Wapo wahindi wenye maduka Moshi mjini nenda double road,kina panjwan and the like unasemaje?sio kila aliye if haifahamu Moshi joh,jipange
 
moshi ndio mkoa pekeee nyumba za msajili huwezi kukuta wamelundikana wahindi kama mikoa mingine kupata duka la muhindi moshi ni sawa na kukuta mhindi bariadi
Kijana labda Kama Kuna Moshi nyingine sio hii.

Wap wahindi kibao hapa double road na maeneo mengine ya mjini kati
 
Kijana labda Kama Kuna Moshi nyingine sio hii.

Wap wahindi kibao hapa double road na maeneo mengine ya mjini kati
sio kama hawapo wapo ila sio wengi kama mikoa mingine broo niko moshi pia
 
Fanyeni kazi acheni lawama za kiree. Yani mkiona mchaga amefanikiwa badala muige mfano wa anayofanya mnabaki kuanza kutafuta lawama na maneno yasiokuwa na ukweli.

Kwa attitude hii mliokuwa nayo mtaendelea kuburuzwa na wachaga vizazi vyenu vyote. Sasa sisi wachaga tutanunua ardhi zenu zote mpaka hii nchi yote tuimiliki mbakie nyie wengine kuwa vijakazi wetu tu. Hakuna namna nyingine.

Ulishaona mchaga analalamika kwenye mikoa mingine? Je kwani wachaga hawapati ugumu wa biashara huko walipo nchi nzima? Ulishasikia malalamiko? Akiona mambo magumu hakalii kulialia anainuka anatafuta fursa nyingine mahali pengine.

Sasa mtu kwasababu ameshindwa kufanya biashara Moshi anaanza kulia kwani ni lazima ufanyie Moshi? Fursa zipo kila mahali na sio lazima ufanikiwe kila mahali, nenda tafuta mahali pengine.

Mnasumbuliwa na inferiority complex.
Watuache na Moshi yetu. Pumbavu hawa watu, wanasumbulia na chuki
 
wachaga wamechanganyikana na makabila mengi hapa Tanzania. naweza kusema hakuna kabila lililooleana na makabila mengine kuliko wachaga. pia hakuna kabila ambalo watu wake wametawanyika maeneo mengi ya Tanzania kuliko wachaga.

shida iliyoko katika mji wa Moshi mpaka ukaonekana ni mgumu kwa watu wanaoanza biashara ni uchache wa fursa zilizopo. pia ni mji ambao hauna mzunguko wa fedha mkubwa kulinganisha na miji mingine. Moshi ni mji wa zamani na hakuna biashara mpya au fursa mpya zilizojitokeza kwa miongo kadhaa kuvutia jamii mbalimbali kuhamia huko.

Kwa mfano, Moshi hakuna biashara ya madini kama Arusha, Kahama, na kwingineko. Moshi pia hakuna biashara ya mazao kama mahindi, mpunga, etc ambayo yatavutia watu kutoka nje. Moshi na Kilimanjaro kwa ujumla hakuna maeneo mapya yenye rutuba ambayo yanavutia watu wengi kuhamia huko.

lakini pia ishara ya wazi kabisa kwamba Moshi / kilimanjaro kuna fursa chache ni idadi ya wenyeji wa huko ambao wamelazimika kuhamia maeneo mengine ya Tanzania kutafuta maisha. kwa hapa Tanzania ukiona eneo fulani linakimbiwa hata na wenyeji uwezekano mkubwa ni kwamba hata mgeni akihamia huko hatofanikiwa.

kwa upande mwingine mimi nawafahamu jamaa wa kipare wako maeneo mbalimbali uchagani na wamefanikiwa kibiashara. lakini jamaa hao walihamia huko miaka ya 80 na 90 na walianza kama wafanyabiashara wadogo na sasa wamekuwa vigogo.
Mkuu umeeleza kinaga ubaga na umeeleweka kabisa. Kumbe inaweza kua nisababu pia ya wachaga kutapakaa nchini si ajabu moshi ingekua kama arusha labda wangejikalia zao huko kula mema ya huko kwao.
 
Btw nimezaliwa na kukulia Moshi mjini Soweto pale na tuna bonge la mji plus shamba pale,sitishwina ndezi Kama wewe.Afu ni wakuja tu,sikuzote wanajikomba niwe mchaga Kama wait,nawajibu Noh mie mtu wa mbeya baba🙏
 
Ardhi waipate wapi. Ni maskini wa kutupwa hao
Nenda wizara ya ardhi pale,pitia majina ya land owners in Tanzania

Wachagga are the biggest land owners in Tanzania,na Im talking about real land yenye documents rasmi na zinafanya uzalishaji wa ajabu

Wewe jidanganye na kirobo heka kule Marangu ukadhani ni kweli
 
Mkuu umeeleza kinaga ubaga na umeeleweka kabisa. Kumbe inaweza kua nisababu pia ya wachaga kutapakaa nchini si ajabu moshi ingekua kama arusha labda wangejikalia zao huko kula mema ya huko kwao.
uhaba wa ardhi ulipelekea wachaga wengi kuhama toka kilimanjaro. wakati wa utawala wa mwalimu nyerere kuna wachaga walihamishiwa maeneo ya morogoro na kutokana na uhaba wa ardhi kilimanjaro.

miaka ya 70 na 80 kulitokea changamoto ktk kilimo cha zao la kahawa na hiyo ikasababisha wachaga wengi kukimbilia mijini. jamii ya kwanza kufanya umachinga dar es salaam, kwa mfano, kushona na kupiga rangi viatu, kukaanga chips, na gereji bubu, ni wachaga na hiyo ilikuwa miaka ya 80. ilipofika miaka ya 90 ndipo wakaja wamachinga toka mikoa ya kusini ambao walijishughulisha zaidi na uuzaji wa nguo.

hivi majuzi mbunge wa vunjo dr.kimei aliiomba serikali ifikirie kuwapatia wapigakura wake maeneo ya kulima sehemu mbalimbali za tanzania. sasa inabidi watu wajiulize ni mbunge gani mwingine amewahi kutoa ombi la namna hiyo kwa serikali? mchango huo wa mbunge ni kielelezo cha tatizo kubwa la ardhi na ukosefu wa fursa unaowakabili wananchi wa kilimanjaro.

moshi ingekuwa na fursa mpya kama arusha tusingewaona wachaga wengi maeneo mengine ya tanzania. pia wasingekuwa na tatizo la ardhi wasingetapakaa tanzania nzima. na wasingebahatika kupata elimu wasingehamia maeneo mengine kikazi na kuweza kuziona fursa zilizoko nje ya uchagani.

mwisho, wachaga wanapaswa kuwekeza ktk mji wao wa moshi ambao kwa sasa hivi umedumaa. wako wengi wenye mitaji mikubwa ambao wangeweza kuichangamsha moshi kwa kuwekeza kwenye viwanda. hii habari ya kujisifia kujenga majumba ya kifahari migombani naamini imepitwa na wakati. wachaga wa karne ya 21 wanatakiwa wajisifu kwa kuwekeza ktk viwanda ktk mkoa wa kilimanjaro.
 
Back
Top Bottom