Anayofanya Christina Shusho ni matokeo ya Wanaume wengi kuoa Wanawake Watumwa wasio huru. Siku wakipata Uhuru wao hayo ndio hutokeaga

Anayofanya Christina Shusho ni matokeo ya Wanaume wengi kuoa Wanawake Watumwa wasio huru. Siku wakipata Uhuru wao hayo ndio hutokeaga

Mkuu?
Concept ya uhuru nadhan kuna mengi nahitaji kujifunza.

Ngoja niweke kambi hapa nione wengine wanasemaje?

Uhuru bila kufanya uhalifu wala dhambi ndio huitwa Uhuru.

Sasa mwanamke kuwa huru kwa nini baadhi ya Watu huona shida? Nîni wanafaidika wanawake wanapoteseka kihisia, kiakili, kiroho na kimwili?

Najua wapo wanaume pia wanateseka kwa kasumba na dhana potofu kwa kisingizio cha uanaume.

Mfano, umenyeke na kuteseka kutafuta pesa ili umhudumie Mwanamke ambaye sio mkeo na huishi naye. Huo ni unyanyasaji
 
Classes uliyo itathmini siyo aliyoimaanisha MUNGU..wewe umeitathmini classes kama uwezo wa kifedha/kiupeo/kielimu/kimwonekano nk. kutokana na thread yako lakini hapo kilichomaanishwa zaidi ni sifa za nafsi zaidi zinazobeba Character ya mtu kama upole,utu,hekima,kupenda ibada,utii,unyenyekevu nk...

Na ndio maana kwa Wanaume ambao wamekuwa waaminifu kwa Mungu na kujenga naye mahusiano mazuri Mungu huwa anawapa wake wanaofanana nao usije kutegemea wewe malaya ukapewa mwanamke anajitunza na mtii NEVER labda huyo mwanaume aje akengeuke mwenyewe badae kwa kumuacha MUNGU.

Hio ndiyo maana yake halisi na si kama wewe ulivomaanisha.
Kwa nyuzi zake na reply inaonyesha bado ni mtoto anayeongozwa na fantasy
 
Jalali akuongoze.
Watu tuwaze tunavyowaza, tuhubiri tunayoyaamini ila kwenye hii dunia UHALISIA NDIO CHUJIO na muda unatosha kabisa kuthibitisha hilo.
Ni wachache sana wameweza kutenganisha hisia zao kwenye kufanya maamuzi,na hao ndio wanaofuzu.
Maadamu andiko lako linaishi,na Christina tunamtumia kama sampuli....tuache uhalisia uamue.
ULIMWENGU NDIO MAMA
 
Inaonyesha alikuwa na tamaa zake binafsi kwa huyo mume wake akamua kuishi naye kinafiki kwa miaka yote ambao baada ya kuzipata anaona Hana maana Tena kwake
Neno “inaonyesha” ni tafsiri yako wewe binafsi ili ku-justify point yako.

Yeye amesema alilazimishwa Halafu wewe umetafuta neno la kusadikika kwa upeo wa akili yako ili upate hoja

Kama alilazimishwa na wazazi sisi hatujui, mapito aliyokuwa akipitia ndani ya ndoa yake vilevile hatuyajui.
 
Mpinga kristo ni wale wasiotaka ukweli na wanaopinga Haki.
Huyo Christina keshakuambia Ndoa alilazimishwa sasa wewe unataka kusemaje?

Hakuna hoja yoyote ya kumtetea Christina Shusho yenye mashiko...

Wewe una uhakika Gani kuwa mke wako anakupenda?

Haya twende..., kuna uhusiano Gani kati ya kuolewa na mume asiyempenda na Yeye kumuacha Mungu aliyemuimbia Mtetezi wangu yu hai na akaungana na Mungu wa mtu mwingine?

Ni kwamba hiyo ndiyo rangi yake halisi. Unamtetea!!! Unajua Kwa matendo yake anaziangamiza nafasi ngapi?

Binafsi yangu nilimpenda sana Shusho hata isingeweza kupita wiki sijaskiza nyimbo zake kadhaa, zilikuwa zinahuisha...

Sasa nioneshe huyo Mwanaume Yeye anampenda na akaolewa nae.

Sasa Robert tuelewane kitu kimoja, usije hata siku 1 ukafikiri kwamba mkeo kuchepuka ni ishara ya kutokukupenda.

Kijana wewe bado sana hujaizunguka Dunia, bado tena nasema bado.

Nisitoe maelezo mengi ila kuna mtu akikuamulia huyo Mwanamke wako ni ndani ya nusu saa anabebwa.

Na una hakika Gani huchapiwi?

Isije ikawa umelishwa malimbwata tunaongea na malimbwata ndo maana hata nyuzi hazieleweki...

(Mimi nachoelewa ni Shusho amepata shambulio la kiroho akashindwa kujinasua)
(Mimi nachoelewa ni Shusho amepata shambulio la kiroho akashindwa kujinasua)

Hapa naunga mkono kiuhalisi wakristo ambao wako karibu sana na MUNGU ndio wanapigwa vita kubwa sana coz wengi huwa wanajikuta wamedondoka kwa kusema wamesikia sauti ya roho ya mtakatifu ikiwaambia this and this kumbe ni Bwana DEVIL huwa wanashindwa kutofautisha Is this the Voice of GOD/SATAN? na kama hulijui neno vizuri UNAENDA NA MAJI.
 
NAkubaliana na ww kwa asilimia 100% juu uhuru huo uloeleza kwan mm pia naheshimu haki na utu wa mwanamke duniani.
Lakini tatizo lako haliapply kwa shusho hata kidogo.
Mkuu shusho aliolewa akiwa na miaka 19 ambayo kwa mtu ambae hakwenda shule ni mmama .mm by 19 mama yangu alikuwa na 2 kids.
Pili ndoa ni mkataba wenye maadili yake.kinachotokea ni ulimbukeni wa exposure baada ya mafanikio.ntatoa mfano wa wakinga kariakoo.
Wanawake wakinga huwa sio wazuri ni wafupi na shapeless na wanasura za babu.
Sasa wakinga wakiwa kwao huwa hawana exposure wanajikuta wanachagua mke out of love na limited expoure .wanaoa kikristo na wanaanza saka mali na mkewe .
Sababu ni wapiganaji na wabahili wanajikuta wanapata mtaji mkubwa ndani ya 2 to 5yrs .ndo kwa konekshen ya ndugu zao wanaingia kariakoo.
Hapo wanajuana waaminifu sana kuna mkinga nlimlipa milion nkatega kwa kuongeza elfu kumi asee alipiga na simu kabisa .
Sasa wanakopeshana mzigo zana unakuta ndani ya miaka miaka 10 anakuwa bilionaire ashanunua mahotel na migorofa kama yote.
Tatizo sasa anguko la wakinga limepatikana vyema .ni walaini kwa pisi kali unakuta wanaacha wake zao ili waoe mislay qeen.yaan wakinga ndo madanga wa makahaba dar.
Hapo wamejikuta wanajiingiza kwenye starehe na wengi nawajua wameachana na ndoa na wamefilisika.
Nini point yangu? Ndoa ukiifunga hususan ya kikristo ni mkataba na Mungu .biblia haiatoa takwa la mwanamke kumpenda mume limeagiza kumuheshimu.kupenda ni jambo la wanaume .mara ngapi mwanamke asie kupenda ukilala nae tu anabadilika ? Mwanaume kwa manamke asiempenda hata atoe tigo haisaidii.
Ukiingia na mtu ndoa ya kikristo kama ulikosea au uliingia kwa dhiki kaa na ndoa yako kuheshimu mungu sio mume.
Shusho aliolewa akiwa na umri wa kufanya maaamuzi 19 akamuapia mume kwa mungu .leo ametenda dhambi isiyo na msamaha inaitwa KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU.Yaan kusema mungu alimuonesha avunje ndoa akamtumikie .dhambi ya kumsingizia mungu uongo
 
ANAYOFANYA CHRISTINA SHUSHO NI MATOKEO YA WANAUME WENGI KUOA WANAWAKE WATUMWA "WASIOHURU. SIKU WAKIPATA UHURU WAO HAYO NDIO HUTOKEAGA.

Anaandika Robert Heriel
Mtibeli

Huwezi mfanya Mwanamke mtumwa alafu ukamuita Mkeo.
Unajua Watu wengi wamechukua wanawake na kuwageuza watumwa wa kingono na vijakazi wao alafu hujinasibu kuwa Wameoa. Hakuna ndoa ya hivyo. Sema umemnunua Mwanamke na kumgeuza mtumwa wa ngôno na kijakazi wako hapo sisi Watibeli tutakuelewa.

Mfano, kwenye ndoa hakunaga ndoa ya Wake wengi. Ila kwenye utumwa wanaume huruhusiwa kuchukua wanawake watumwa wengi na kuwaita Wake zao ilhali sio kweli na sio Haki.

Kama ilivyo kwa sisi wanaume tusivyoweza kukubali kuwa na Mwanamke mwenye mahusiano na wanaume wawili. Ndivyo hivyohivyo kwa wanawake.

Wanaume wengi hupenda kuishi na Wanawake watumwa kuliko kuoa Mke. Sio ajabu wanaume wengi hujiamini na kutaka Mwanamke mwenye kipato duni au asiyefanya kazi, na wengi huenda mbali kwa kuchukua vibinti vidogo ili wavitumikishe kitumwa.

Kimantiki huwezi pata kitu kinachoitwa heshima kwa mtumwa. Mtumwa hawezi kukupa heshima. Heshima hutolewa na Watu Huru.
Kupewa heshima na mtu asiyehuru au mtumwa huitwa nidhamu ya woga, unafiki na ulaghai.

Kuoa Mwanamke mdogo kiumri ambaye hana maamuzi sio tuu ukatili bali pia ni dhulma ambayo baadaye lazima iligharimu.

Mimi kama Mtibeli halisi nasema, hasa kwa vijana. Ikiwa unahitaji kuishi na mwanaume ambaye utamuita mke basi yakupasa ûtafute mwanamke aliyehuru.
Namaanisha huru kiakili, kihisia, kimwili na kiroho.

Christina Shusho NI kielelezo cha wanawake wengi walioolewa pasipo uhuru wao kuheshimiwa na kuthaminiwa.

Nilieleza pia, Mke hatolewi Mahari. Ila watumwa hutolewa mahari.
Mwanamke aliyehuru hawezi kukubali kutolewa mahari kwa sababu mahari msingi wake mkuu ni kumdunisha Mwanamke na kumdhalilisha ingawaje kwa umbo la nje waliolianzisha walilifanya kama kumheshimisha.

Mwanaume ni bora ikiwa atajua kusimamia Haki. Na Mwanamke atakuwa bora kama mwanaume ikiwa atajua haki zake na nani wa kuzisimamia.

Usioe Mwanamke asiyehuru(tegemezi) na kama utamuoa basi hakikisha unampatia uhuru wake. Ajitegemee.

Usimuozeshe binti yako kama bado hayupo huru. Huko ni kumkosea binti yako.

Usioe Mwanamke asiyefanyakazi, na kama umemuoa akiwa hana kazi basi hakikisha unampa kazi au anasimamia kazi na miradi ya familia. Nazungumzia kazi za kuzalisha kipato sio kazi za nyumbani. Kazi za nyumbani zitafanywa na mtu yeyote au machine. Baba au mume uwe kiongozi alafu mke au mama awe msaidizi. Hiyo ndio tafsiri ya ndoa kama hamtaki iwe ndoani.

Usioe Mwanamke ambaye hakupendi(moyo wake haupo huru na wewe). Atakusumbua na wewe utamsumbua.

Usimlazimishe Mwanamke kuwa na wewe hata kama mmeishi miaka mingi.
Usiingilie uhuru wa mtu mwingine wa kuchagua na kuutendea mwili wake. Kama ameku-cheat na anataka mwanaume mwingine muache aende.

Elewa, Mwanamke aliyehuru hadanganywi ila anafanya kwa Makusudi.
Ila watumwa hudanganywa kwa sababu wapo kwenye harakati za kutafuta uhuru wao.

Usioe mwanamke asiyeweza kujitunza mwenyewe, wala kujitafutia kipato. Huyo sio mke, huyo ni mtumwa.

Mke mchapakazi haimaanishi kazi za nyumbani pekee bali kazi za uzalishaji mali. Hata siku usipokuwepo unajua kabisa ile ndoto ya familia uitakayo itatimizwa na mkeo. Na sio ukifa basi watoto wako ndio habari imeisha.

Oa Mwanamke anayejua Haki zake kwani mtu kujua haki zake ni tafsiri ya kujua haki zako pia.
Mtu asiyejua haki zake hawezi kujua haki zako.

Elewa, mwanamke anayekubali kuonewa jua naye kuna sehemu ànakuonea au upo wakati unaokuja atakuonea tuu. Kwa sababu hiyo ni HAKI.

Ukijiona wewe ni mwanaume na unathamani kwenye ndoa kuliko Mwanamke elewa hata mwanamke atajiona anathamani kuliko wewe. Haitakuwa ndoa bali ndoano full kuumizana.
Lakini ukijitoa kwa mwenzako naye atajitoa. Ukimtañguliza mwenzako naye atakutanguliza.

Heshima yako kama mwanaume haipo kwa kumfanya Mwanamke mtumwa wako. Ila ipo kwa kumfanya Mwanamke kuwa Mtu na kulinda utu wake.
Yale yote unayotaka kufanyiwa basi mfanyie mwenzako. Na yale yote isiyotaka kufanyiwa basi usimfanyie mwenzako.

Kuwa mwanaume sio tafsiri ya tiketi ya kufanya dhulma na uhalifu wa kijinsia kwa Mwanamke.
Kama nilivyoandikaga, kuwa mzazi sio kigezo cha kufanya dhulma kwa watoto wako kisa uliwazaa.

Ni ruhusa na Haki yako kumuacha(kutoa talaka) Mwanamke ambaye ulimpenda, na ukafanya kila jitihada na kuheshimu na kulinda ûtu na hadhi yake na yako lakini ikashindikana. Vivyohivyo kwa Mwanamke.

Ni yule Mtibeli kutoka nyota ya Tibeli.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama, Shinyanga.

Nimesoma post yako kama nusu tu nikaona huna uelewa wa mambo ya Ndoa hivyo huna sifa ya kuandika mambo yanayo husiana na ushauri wa ndoa; unge endelea na yale mengine ya kisiasa
1. Kudhibitisha kuwa huna sifa ya kuongelea mambo ya Ndoa, umeweza kumsikiliza Christina Shusho na kuamini kila anachosema na kutoa hukumu wakati hujasikiliza upande wa pili wa mUme wake
2. Kwa maelezo yako ni kuwa, mwanamke asiolewe kama hana kazi au niseme wanaume wasije kuoa wanawake wasio na kazi au Kipato; sijui unajua ni asilimia ngapi ya wanawake au niseme vijana wenye kazi?
3. Kama unafikiri mtu akioa mke kwa sababu anataka asifanye dhambi ya kuzini mtaani ananyanyasa mke wake kwani anataka kufanya tendo la ndoa; inabidi ujitafakari upya...
4. Hiyo ya kusema mke asilipiwe mahari sijui umetoa wapi????
5. Kwa wenye maarifa wanajua kuwa, masuala ya ndoa sio mepesi kama kuongelea Siasa au pengine kuongelea mpira wa Yanga & Simba
 
Christina Shusho NI kielelezo cha wanawake wengi walioolewa pasipo uhuru wao kuheshimiwa na kuthaminiwa.

Nilieleza pia, Mke hatolewi Mahari. Ila watumwa hutolewa mahari.
Mwanamke aliyehuru hawezi kukubali kutolewa mahari kwa sababu mahari msingi wake mkuu ni kumdunisha Mwanamke na kumdhalilisha ingawaje kwa umbo la nje waliolianzisha walilifanya kama kumheshimisha.
Tafuta Hela Wewe mke wa Bure Bila mahari hayupo

Mahari unapangiwa kupima uwezo wako moja je una kipato Cha kutunza familia? Ukisema huna Hela ya mahari tu huyo mkeo atakula Mawe akija kwako?

Ndio.maana Hadi wachungaji wafungisha ndoa huuliza kama huyo mwanaume mahari alilipa au la kuwa hawamdai chochote Kabla kufungisha ndoa

Mahari tu inakushinda hiyo familia utatunzaje unataka mke akajiuze au?

Mahari ni interview kupima kama una kipato Cha kutunza familia huna wazazi wanaojielewa watagoma kuwa hatutaki aoe mtoto wetu sababu waweza kuwa mzigo Kwa wakwe wanunue Hadi chakula wakuletee Wewe lofa mkubwa ule na mkeo

Huna Hela ya mahari lofa Wewe nenda kawe padri wa kanisa katoliki ambao Hawaoi achana na ndoto za kuoa bure
 
ANAYOFANYA CHRISTINA SHUSHO NI MATOKEO YA WANAUME WENGI KUOA WANAWAKE WATUMWA "WASIOHURU. SIKU WAKIPATA UHURU WAO HAYO NDIO HUTOKEAGA.

Anaandika Robert Heriel
Mtibeli

Huwezi mfanya Mwanamke mtumwa alafu ukamuita Mkeo.
Unajua Watu wengi wamechukua wanawake na kuwageuza watumwa wa kingono na vijakazi wao alafu hujinasibu kuwa Wameoa. Hakuna ndoa ya hivyo. Sema umemnunua Mwanamke na kumgeuza mtumwa wa ngôno na kijakazi wako hapo sisi Watibeli tutakuelewa.

Mfano, kwenye ndoa hakunaga ndoa ya Wake wengi. Ila kwenye utumwa wanaume huruhusiwa kuchukua wanawake watumwa wengi na kuwaita Wake zao ilhali sio kweli na sio Haki.

Kama ilivyo kwa sisi wanaume tusivyoweza kukubali kuwa na Mwanamke mwenye mahusiano na wanaume wawili. Ndivyo hivyohivyo kwa wanawake.

Wanaume wengi hupenda kuishi na Wanawake watumwa kuliko kuoa Mke. Sio ajabu wanaume wengi hujiamini na kutaka Mwanamke mwenye kipato duni au asiyefanya kazi, na wengi huenda mbali kwa kuchukua vibinti vidogo ili wavitumikishe kitumwa.

Kimantiki huwezi pata kitu kinachoitwa heshima kwa mtumwa. Mtumwa hawezi kukupa heshima. Heshima hutolewa na Watu Huru.
Kupewa heshima na mtu asiyehuru au mtumwa huitwa nidhamu ya woga, unafiki na ulaghai.

Kuoa Mwanamke mdogo kiumri ambaye hana maamuzi sio tuu ukatili bali pia ni dhulma ambayo baadaye lazima iligharimu.

Mimi kama Mtibeli halisi nasema, hasa kwa vijana. Ikiwa unahitaji kuishi na mwanaume ambaye utamuita mke basi yakupasa ûtafute mwanamke aliyehuru.
Namaanisha huru kiakili, kihisia, kimwili na kiroho.

Christina Shusho NI kielelezo cha wanawake wengi walioolewa pasipo uhuru wao kuheshimiwa na kuthaminiwa.

Nilieleza pia, Mke hatolewi Mahari. Ila watumwa hutolewa mahari.
Mwanamke aliyehuru hawezi kukubali kutolewa mahari kwa sababu mahari msingi wake mkuu ni kumdunisha Mwanamke na kumdhalilisha ingawaje kwa umbo la nje waliolianzisha walilifanya kama kumheshimisha.

Mwanaume ni bora ikiwa atajua kusimamia Haki. Na Mwanamke atakuwa bora kama mwanaume ikiwa atajua haki zake na nani wa kuzisimamia.

Usioe Mwanamke asiyehuru(tegemezi) na kama utamuoa basi hakikisha unampatia uhuru wake. Ajitegemee.

Usimuozeshe binti yako kama bado hayupo huru. Huko ni kumkosea binti yako.

Usioe Mwanamke asiyefanyakazi, na kama umemuoa akiwa hana kazi basi hakikisha unampa kazi au anasimamia kazi na miradi ya familia. Nazungumzia kazi za kuzalisha kipato sio kazi za nyumbani. Kazi za nyumbani zitafanywa na mtu yeyote au machine. Baba au mume uwe kiongozi alafu mke au mama awe msaidizi. Hiyo ndio tafsiri ya ndoa kama hamtaki iwe ndoani.

Usioe Mwanamke ambaye hakupendi(moyo wake haupo huru na wewe). Atakusumbua na wewe utamsumbua.

Usimlazimishe Mwanamke kuwa na wewe hata kama mmeishi miaka mingi.
Usiingilie uhuru wa mtu mwingine wa kuchagua na kuutendea mwili wake. Kama ameku-cheat na anataka mwanaume mwingine muache aende.

Elewa, Mwanamke aliyehuru hadanganywi ila anafanya kwa Makusudi.
Ila watumwa hudanganywa kwa sababu wapo kwenye harakati za kutafuta uhuru wao.

Usioe mwanamke asiyeweza kujitunza mwenyewe, wala kujitafutia kipato. Huyo sio mke, huyo ni mtumwa.

Mke mchapakazi haimaanishi kazi za nyumbani pekee bali kazi za uzalishaji mali. Hata siku usipokuwepo unajua kabisa ile ndoto ya familia uitakayo itatimizwa na mkeo. Na sio ukifa basi watoto wako ndio habari imeisha.

Oa Mwanamke anayejua Haki zake kwani mtu kujua haki zake ni tafsiri ya kujua haki zako pia.
Mtu asiyejua haki zake hawezi kujua haki zako.

Elewa, mwanamke anayekubali kuonewa jua naye kuna sehemu ànakuonea au upo wakati unaokuja atakuonea tuu. Kwa sababu hiyo ni HAKI.

Ukijiona wewe ni mwanaume na unathamani kwenye ndoa kuliko Mwanamke elewa hata mwanamke atajiona anathamani kuliko wewe. Haitakuwa ndoa bali ndoano full kuumizana.
Lakini ukijitoa kwa mwenzako naye atajitoa. Ukimtañguliza mwenzako naye atakutanguliza.

Heshima yako kama mwanaume haipo kwa kumfanya Mwanamke mtumwa wako. Ila ipo kwa kumfanya Mwanamke kuwa Mtu na kulinda utu wake.
Yale yote unayotaka kufanyiwa basi mfanyie mwenzako. Na yale yote isiyotaka kufanyiwa basi usimfanyie mwenzako.

Kuwa mwanaume sio tafsiri ya tiketi ya kufanya dhulma na uhalifu wa kijinsia kwa Mwanamke.
Kama nilivyoandikaga, kuwa mzazi sio kigezo cha kufanya dhulma kwa watoto wako kisa uliwazaa.

Ni ruhusa na Haki yako kumuacha(kutoa talaka) Mwanamke ambaye ulimpenda, na ukafanya kila jitihada na kuheshimu na kulinda ûtu na hadhi yake na yako lakini ikashindikana. Vivyohivyo kwa Mwanamke.

Ni yule Mtibeli kutoka nyota ya Tibeli.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama, Shinyanga.
Mkuu kabla sijadandia naomba unijuze unaposema kuolewa kama mtumwa unamaanisha nini?
Ina maana tina ameolewa kabla ya kutimiza miaka 18?
Namkumbuka alikuwa maarufu kwa wimbo wake wa UNIKUMBUKE
Je wakati anaibuka kuwa maarufu alikuwa ameolewa au alikuwa kwa wazazi wake?
 
Hakuna hoja yoyote ya kumtetea Christina Shusho yenye mashiko...

Wewe una uhakika Gani kuwa mke wako anakupenda?

Haya twende..., kuna uhusiano Gani kati ya kuolewa na mume asiyempenda na Yeye kumuacha Mungu aliyemuimbia Mtetezi wangu yu hai na akaungana na Mungu wa mtu mwingine?

Ni kwamba hiyo ndiyo rangi yake halisi. Unamtetea!!! Unajua Kwa matendo yake anaziangamiza nafasi ngapi?

Binafsi yangu nilimpenda sana Shusho hata isingeweza kupita wiki sijaskiza nyimbo zake kadhaa, zilikuwa zinahuisha...

Sasa nioneshe huyo Mwanaume Yeye anampenda na akaolewa nae.

Sasa Robert tuelewane kitu kimoja, usije hata siku 1 ukafikiri kwamba mkeo kuchepuka ni ishara ya kutokukupenda.

Kijana wewe bado sana hujaizunguka Dunia, bado tena nasema bado.

Nisitoe maelezo mengi ila kuna mtu akikuamulia huyo Mwanamke wako ni ndani ya nusu saa anabebwa.

Na una hakika Gani huchapiwi?

Isije ikawa umelishwa malimbwata tunaongea na malimbwata ndo maana hata nyuzi hazieleweki...

(Mimi nachoelewa ni Shusho amepata shambulio la kiroho akashindwa kujinasua)

Mkuu, mada imetolewa kulingana na maelezo ya shusho mwenyewe. Kuhusu uhakika hilo sio juu yetu. Tunajadili kile ambacho amekifanya na kile ambacho ndani ya jamii tunakuomba.

Shusho ametoa hoja zake. Hoja kuu ni hizi za kuachana na mumewe;
1. Alilazimishwa kuolewa na wazazi
2. Kutimiza ndoto yake ya kumtumikia Mungu.

Mada yangu imejikita katika hoja yake ya kwanza kuwa uhuru wake wa kuchagua mwenza uliingiliwa.
Na hiki anachokifanya ni matokeo tuu ya kile alichotaka ni siku nyingi ajikomboe apate uhuru wake.

Kuhusu Mungu wake hilo silijui. Sijui anamtumikia mungu yupi na kama amebadili Mungu pia huyo mungu wake mpya simjui. Hapa ninajadili vitu vilivyowazi na dhahiri.

Hoja ya uhakika wa kupendwa au kutokupendwa hilo wala sio jambo gumu. Kujua mtu anayekupenda ni rahisi mno.

Kuhusu kuchapiwa hiyo haipo ndani ya uhuru wangu. Kila mtu anahaki ya kutumia mwili wake atakavyo. Hiyo ni Haki. Lakini kama nikijua mke wangu anachapwa yaani ametumia uhuru wake kutumia mwili wake kula na mtu mwingine mimi nami nitafanya maamuzi yangu ambayo hayataingilia uhuru wa mtu mwingine na wala kuvunja sheria za nchi na Mungu ninayemuamini.
 
Huwezi panga kumpenda mtu inakuja automatic
Tunaongelea upendo wa kwenye mahusiano na sio wa baba kwa mtoto
Unatakiwa ujue kuna aina nyingi za upendo
Watoto ndiyo wanadhani upendo wa mwanamke na mwanaume huja automatically. Ukiwa mtu mzima utajua watu wanapendeana, pesa, sura, matako, elimu, tabia, macho, swaga, umaarufu, nk nk. Na anayempendea mtu pesa na anayempendea mwingine matako hawana tofauti. Hakuna mwenye upendo wa kweli zaidi ya mwingine.
 
Mwanamke kuna mda inabidi akubali kuolewa na mwanaume flani sababu ndo aliyekuja na yuko tayari kumuoa sasa unavyosema mwanamke awe na uhuru ni kichekesho kwakweli
Kama alikubali bila kulazimishwa hilo halina Tatizo, ikiwa ni kinyume na hapo huo ni utumwa.

Umeelewa mada lakini mkuu?
 
Ndoa inatakiwa ije na version mpya jamani hii ya zamani ipo outdated sana....haikidhi wala kuendana na nyakati za sasa.
 
Watoto ndiyo wanadhani upendo wa mwanamke na mwanaume huja automatically. Ukiwa mtu mzima utajua watu wanapendeana, pesa, sura, matako, elimu, tabia, macho, swaga, umaarufu, nk nk. Na anayempendea mtu pesa na anayempendea mwingine matako hawana tofauti. Hakuna mwenye upendo wa kweli zaidi ya mwingine.
Mkuu kabla sijadandia naomba unijuze unaposema kuolewa kama mtumwa unamaanisha nini?
Ina maana tina ameolewa kabla ya kutimiza miaka 18?
Namkumbuka alikuwa maarufu kwa wimbo wake wa UNIKUMBUKE
Je wakati anaibuka kuwa maarufu alikuwa ameolewa au alikuwa kwa wazazi wake?

Kulazimishwa
 
Back
Top Bottom