Arusha: Atobolewa Jicho na kung'olewa meno mawili kisa wivu wa mapenzi

Arusha: Atobolewa Jicho na kung'olewa meno mawili kisa wivu wa mapenzi

Mwalimu anakwenda jela kipumbavu kabisa. Aende akaonyeshe umwamba wake kwa wanaume og.
hawezi kufungwa , NI ugomvi wa familia , ni kesi ndogo Sana hii. mwisho wa siku familia zitaingilia Kati na wataombana msamaha , yanaisha .
 
Duhh! Matai kumbe ni mjomba wa huyo dada? Matai alikuwa rafiki yangu kipindi niko meatu Simiyu.

Ni katibu wa wazazi CCM wilaya ya meatu.
 

Attachments

  • Screenshot_20230526-205612.jpg
    Screenshot_20230526-205612.jpg
    57.8 KB · Views: 2
  • Screenshot_20230526-205634.jpg
    Screenshot_20230526-205634.jpg
    127 KB · Views: 2
Hata iwejeeee hata iweje nasema...this is unacceptable....
Jiweke kwny position ya huyo dada utobolewe jicho na kutolewa meno bila ganzi hivi mmefikiria kweli??? Uwiiiiiii
huyo jamaa yake atakuwa na matatizo ya Akili
 
Aliolewa na kichaa,ukishaona mume kakasirika hivo angejifungia chumban asingetoka,ngoja mpwayungu aje
 
Yes sura ya upole,sauti ya upole ila ukizingua tutaoneshana kweli labla nife vinginevyo hakuna namna 🤷🏼‍♀️
Omba amani , na kisasi hakijawahi mwacha mtu salama.. Ukipigwa we ondoka hujui utakapotokea.. Ni ushauri
 
Angempiga ngumi meno yakatoka sawa, ila hiyo ya kuchukua plaiz na kupunguza meno asipofungwa na kama huyo dada ndugu zake wasipolipiza basi huyo mwanamke atakuwa hapendwi kabisa na jamii hata ndugu zake.
Hatafungwa
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Yule jamaa wa Mwanza ambaye aliamua kumaliza magazine nzima

Magazine ya risasi 10
 
Kwa sheria gani?
Chukua nyundo nenda kamvunje meno mpenzi wako halafu chukua kisu mtoboe macho halafu useme kwa sheria gani, hatutaki kujua alikcheat hilo halijustify kumtoboa macho na kumngo'a meno huyo ni muuaji kama wauaji wengine
 
Mmmmmmhmn watu tunakuwaga na mikwara hapa ila kuna wanaume wenzetu wapo kivitendo zaidi. Mmmmmm hadi nimeogopa aisee.

Huyu mwamba ni katili balaa. Halafu hii inaonekana si mara ya kwanza kwa huyu dada kupewa kipigo. Maana wana watoto wawili hao so it means wameshakuwa pamoja muda mrefu.

Halafu nihoji, mwanaume anaishi vipi Rombo mkewe akabakia Arusha?! Hapa si ni kumpa majaribu huyo dada wa watu?!

Anyways, turudi kwenye mada, hiki sio kipigo cha kumpa mwanamke wako especially mama watoto. Najua hawa viumbe muda mwingine huwa wanatia hasira kupita kiwango hadi unaishiwa maneno unatamani hata ulie ili akuelewe.

But ni vema kuwa na subira na kuwaepuka zile nyakati wanapokengeuka na kutufanya tujiskie kupata kichaa. Dawa ya mwanamke. Mkorofi ni kumtafutia mwanamke mwenzake ambaye atafanya kile unachotaka yeye akufanyie halafu akakataa kwa jeuri tu za kike mradi kisiwe Haram.

Jamaa amepitiliza sana kwenye hili, dada yake au mdogo wake wa kike angepigwa hivi yeye angejisikia namna ipi?

Tuheshimu Ndoa zetu, tuepuke sababu za kijinga zinazoweza wafanya wenza wetu kurukwa akili na kufanya matukio ya kikatili.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom